Professional Documents
Culture Documents
UTANGULIZI
Kumekuwepo na taarifa zilizotolewa kwenye mitandao ya kijamii na vyombo
vya habari, hasa gazeti la Jamboleo toleo namba 2541 la 23 Agosti, 2016
kuhusu Bodi ya Mikopo kuwadai wasionufaika na mikopo. Taarifa hizi
zinalenga kuleta hofu na mkanganyiko usiokuwa wa lazima kwa wadau.
Kufuatia hatua hiyo Bodi ya Mikopo inapenda kutoa ufafanuzi wa suala hili
kama ifuatavyo:-
2.0
2.1 Kwa mtu anayedai kwamba hajasoma elimu ya juu kwa ufadhili
wa serikali au Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu;
mtu huyu awasilishe vielelezo vinavyodhihirisha kuwa hakusomeshwa
kwa ufadhili wa serikali.
2.2 Kwa mtu anayedai amekatwa mshahara ingawa hajawahi
kufikia kiwango cha elimu ya juu; mtu huyo anapaswa kuwasilisha
vielelezo vya kiwango cha elimu yake.
2.3 Iwapo kuna mnufaika wa mkopo anadai amekatwa zaidi ya
kiwango cha mkopo anaodaiwa; mnufaika huyo anapaswa
kuwasilisha vielelezo vinavyothibitisha kumaliza kurejesha deni lake.
Itakapothibitika kuwa kuna makato zaidi yalifanyika, basi kiasi
kilichozidi kitarejeshwa kwa mhusika.
3.0
HITIMISHO
Bodi inapenda kuwahakikishia wadau wake kuwa imetunza vizuri taarifa zote
muhimu za wanufaika wa mikopo ambazo ndizo zinazotumika kwenye zoezi
la urejeshaji wa mikopo. Kasoro ndogo ndogo zinazojitokeza zinatatuliwa
kwa kufanya rejea kwenye kumbukumbu zilizopo.
Aidha, Bodi inaendelea kuwahimiza wanufaika wote wa mikopo ambao
hawajaanza kurejesha mikopo yao kuhakikisha wanawasilisha taaifa zao ofisi
za Bodi au wanajaza taarifa zao kweye fomu Loan Inquiry Form iliyopo
kwenye tovuti ya Bodi na kuituma kwa anuani ya barua pepe
info@heslb.go.tz ili kila mmoja ajulishwe deni lake na kuanza kurejesha.
Kwa mnufaika anayetaka kuanza kurejesha mkopo wake baada ya kuwa
amepata taarifa ya deni lake; aweke fedha kwenye akaunti za Benki
zifuatazo na kisha kuwasilisha hati ya malipo:
A/C No. 2011100205 NMB
A/C No. 01J1028467503 CRDB
A/C No. CCA0240000032 TPB
Imetolewa na:
KITENGO CHA HABARI, ELIMU NA MAWASILIANO
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
Agosti 24, 2016