Professional Documents
Culture Documents
WIZARA YA UCHUKUZI
S. L. P 3056,
DAR ES SALAAM.
29 Oktoba, 2015
Maeneo yanayopata mvua mara moja kwa mwaka Mikoa ya Dodoma, Singinda, Ruvuma,
Lindi, Mtwara, Songea, Mbeya, Iringa, Njombe, Tabora, Kigoma Rukwa na Katavi mvua
zinatarajiwa kuanza kati ya wiki ya pili na ya nne ya mwezi Novemba, 2015. Ambapo mvua
hizo zimeanza kujiimarisha katika mikoa ya Kigoma, Tabora na Katavi na zinatarajiwa
kusambaa katika maeneo mengine mwezi huu wa Novemba 2015. Hata hivyo, Wilaya za
Kondoa, Kongwa na Singida Vijijini katika mikoa ya Dodoma na Singida zinatarajiwa pia
kupata vipindi vya mvua mapema mwanzoni mwa mwezi Novemba, 2015.
USHAURI
Mamlaka ya Hali ya Hewa inawashauri watumiaji wa taarifa za hali ya hewa ikiwa ni
pamoja na wakulima, wafugaji, Mamlaka za Wanyamapori, Mamlaka za Maji na Afya
waendelee kutafuta, kupata na kufuata ushauri wa wataalamu katika sekta husika katika
kutekeleza
mipango
inayoweza
kuathiriwa
na
mwelekeo
wa
hali
ya
hewa
Mwelekeo wa mvua uliotolewa hapa umezingatia zaidi viashiria vya mvua katika kipindi cha
msimu(miezi mitatu) na hali ya mvua katika maeneo makubwa. Hivyo, viashiria
vinavyochangia mwenendo wa mifumo ya mvua na mabadiliko ya muda mfupi katika
maeneo madogo utazingatiwa katika
Watumiaji wa taarifa za utabiri huu wanashauriwa pia kufuatilia tabiri za saa 24, siku 10
pamoja na wa mwezi kama zinavyotolewa na Mamlaka ya hali ya Hewa Tanzania.
Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania Itaendelea kufuatilia mwenendo wa mifumo ya hali
ya hewa na kutoa taarifa za mwelekeo wa mvua nchini.
Dkt. Ladislaus B. Changa
KAIMU MKURUGENZI MKUU