Professional Documents
Culture Documents
www.islamicftz.org
muswada wa habari
ke wa Sheikh mmoja
mashuhuri wa kisunnah
hapa jijini Dar es Salaam
amenyimwa kitambulisho cha uraia kwa kuhisiwa kuwa sio
raia kwa sababu ya asili yake ya uarabu.
Mama huyo ambaye ni mtanzania
halisi alinyimwa kitambulisho yeye na
mtoto wake mmoja huku maafisa wa
Mamlaka ya Vitambulisho ya Taifa
(NIDA) wakimwambia itabidi aanze
mchakato upya.
Mama huyo ambaye asili yake ni
Tanga aliambiwa na afisa mmoja wa
NIDA kuwa kita- inaendelea Uk 5
Uk. 3
Head office, Lumumba Street, Opp: Viwanja vya Mnazi Mmoja, P. O Box 779 Dar es Salaam, Tanzania
Tell: 255 22 2182482/ 255 222184419, Fax: 255 22 2181424, E-mail: info@Binslum.com
habari / tangazo
www.islamicftz.org
TOLEO MAALUM:
Gazeti lako la Imaan, Ijumaa ya Juni 12,
2015 litachapisha toleo maalum la Mwezi
Mtukufu wa Ramadhan litakalochambua
mafundisho na masuala mbali mbali
kuhusiana na Ramadhan.
Ili kufanikisha
toleo hilo maalum, tunakaribisha ushiriki
wa watu binafsi, taasisi, kampuni, balozi na
misikiti
mbalimbali
kwa kutoa
makala na matangazo.
Na Khalid Omary
yombo vya habari vya Kiislam
vimezidi kuongezeka baada ya
kuzinduliwa kwa gazeti jipya la
Iqra, (Hoja kwanza), Ijumaa iliyopita katika msikiti wa Mtambani, Kinondoni jijini Dar es salaam.
Wakizungumza katika uzinduzi huo
Imam wa msikiti wa Mtambani, Sheikh
Suleiman Abdallah aliishukuru bodi ya Iqra
Media kwa kufanya uzinduzi katika msikiti
wake na kusema, kwa sasa Waislam wataendelea kupata habari na elimu kupitia vyombo vya Kiislam vinavyoongezeka kwa kasi.
Tulikuwa na kilio katika suala la elimu,
tunafurahi tumepiga hatua kubwa kwa
kuzinduliwa kwa gazeti hili (Iqra). Tunatumai tutapata elimu kubwa, alisema Sheikh
Abdallah.
Naye, Mwenyekiti wa bodi ya Iqra Media, Bilal Abdul-aziz amewataka Waislam
waweze kuviunga mkono vyombo vya Kiislam, kwani hakuna asiyekuwa Muislam
atakaeweza kutoa msaada zaidi ya wao
wenyewe.
Abul-aziz alisema: Vyombo vya habari
vya Kiislam vimekuwa na muamko
mkubwa hasa baada ya kujitokeza kwa redio Imaan, tunahitaji ushirikiano kutoka
kwa Waislam ili tuweze kufika mbali.
Kwa upande wake, Sheikh Nurdin Kishk,
mdau mwingine wa gazeti hilo, amewataka
Waislam wasome fani ya habari, kwa sababu wengi wa wanaosoma fani hiyo si Waislam na ndiyo maana Uislam unachafuliwa
na vyombo vya habari ulimwenguni.
Gazeti la Iqra linatolewa na Iqra Media,
litakuwa likitoka kila Ijumaa kwa bei ya
shilingi 800 likisheheni habari na makala
za dini ya Kiislam na jamii kwa ujumla zinazoandaliwa na masheikh mbalimbali pamoja na wanahabari wenye uzoefu.
Na bahati chume
miri wa Jukwaa la Vijana wa Kiislamu Mkoa wa Kilimanjaro, Abdalah Muhammed amewakumbusha Waislamu Mkoani Kilimanjaro kujitokeza kwa wingi kujiandisha
kwenye daftari la kudumu la wapiga kura
pindi muda utakapo wadia.
Akizungumza na waandishi wa habari,
nyakati za swala
ISHA
1:25
1:26
1:32
1:32
1:20
1:44
1:39
1:47
2:05
1:57
2:03
1:53
1:55
1:46
1:38
habari
www.islamicftz.org
NA MWANDISHI WETU
www.islamicftz.org
tujikumbushe
NA YUSUFU AHMADI
basi wakapendekeza EAMWS ifungiwe. Nyerere aliwaunga mkono, lakini Bibi Titi akasimama kishujaa dhidi yao.
Biti Titi aliwaambia Diwani, Kitundu na
Nyerere hakuna kati yao aliyekuwa na haki ya
kuifungia EAMWS, kwani taasisi hiyo ilikuwepo kabla ya TANU ikitoa huduma kwa Waislamu, na kuongeza kuwa, kama walikuwepo
watu ndani ya EAMWS walikuwa wanakwenda kinyume na sheria basi wapelekwe mahakamani na sheria ichukue mkondo wake.
Inasemekana hasira zilipanda na kukawa
na kutoleana maneno kati ya Bibi Titi na Nyerere. Bibi Titi akamwambia Nyerere yeye hamuogopi yeyote ila Allah. Haya ni kwa mujibu
wa kitabu Maisha na Nyakati za Abdulwahid
Sykes - 1998 cha Mohammed Saidi.
Inadaiwa kuanzia hapo Mwalimu Nyerere
akajenga chuki dhidi ya Bibi Titi Muhammed
na mwaka 1965, yeye na Tewa Said Tewa wakapoteza viti vyao vya ubunge, hali ambayo inaaminika Mwalimu Nyerere alihusika pakubwa.
Hali hiyo haikumkatisha tamaa marehemu
Bibi Titi na mwenzake Tewa Said, kwani mwaka 1968, wakati njama za kuiua EAMWS zikiendelea kushika kasi, walimfuata Mwalimu
Nyerere ili kuonesha masikitiko yao ya namna
radio ya Serikali na magazeti ya TANU yalivyokuwa yakiishambulia jumuiya hiyo ya Kiislamu.
Wakati Bibi Titi na wenzake wakimtahadharisha Nyerere kwa kuacha vyombo vya serikali kuchochea mgogoro ndani ya EAMWS,
Nyerere aliwachukulia akina Bibi Titi kama
maadui na kuwaambia uso kwa uso Mmeamua kunipiga vita, jiandaeni. (Rejea kitabu cha
Historia ya Kuhuisha Uislamu Tanzania kilichoandikwa na Islamic Propagation Centre).
Vita dhidi ya EAMWS ilinoga zaidi baada
ya Makamu wa Rais wa Tanzania, Abeid Amani Karume, kukiita chombo hicho kuwa ni cha
kinyonyaji. Ikikabiliwa na mashambulizi kutoka kila upande, hatimaye mnamo mwaka 1968
EAMWS ilipigwa marufuku kwa amri ya Nyerere na mali zake zote kukabidhiwa BAKWATA iliyoundwa na serikali, ambayo imekuwa
ikidai siku zote kuwa haina dini. Tangu hapo
BAKWATA imeendelea kuwapo na kuwa
chanzo cha madhila na udhalili wa Waislamu
Tanzania.
Katika kumuelezea Bibi Titi, katika makala
yake aliyoiita, Biti Titi Mohammed and The
Historical Context of the Time in Tanzania iliyotoka katika Awaaz Magazine toleo 3, juzuu
ya 11; Joseph Lwannia alimsifu kuwa alikuwa
Muislamu mwenye muono, kiongozi shupavu,
mwenye muelekeo uliodhahiri na aliyejali
mustakabali wa nchi yake, huku akiwa mfuasi
wa demokrasia yenye ladha ya ubepari.
Mwandishi huyo anaendelea kuandika
kuwa, tofauti za kiimani na kisiasa baina ya
Mwalimu Nyerere aliyekuwa mfuasi mkubwa
wa Ukatoliki na Ujamaa, na Bibi Titi mfuasi
wa Uislamu zilileta mapambano makubwa
katika chama cha TANU na hivyo kutishia
kukigawa chama.
Bibi Titi kupotea katika ramani ya Tanzania:
Mwaka 1969 Bibi Titi Mohammed
alikamatwa na mwaka uliofuata alifikishwa
mahakamani kwa madai ya kupanga njama ya
kutaka kuipindua serikali ya Mwalimu Nyerere
kwa kushirikiana na wenzake sita, akiwemo
Michael Kamaliza aliyekuwa Waziri wa Ulinzi.
Katika kesi hiyo, Bibi Titi alikuwa ni mwanamke pekee na hatimaye alipatikana na hatia
na kuhukumiwa kifungo cha maisha. Mwaka
1972 alipata msamaha wa rais Julius Nyerere.
Baada ya kutolewa jela, Bibi Titi Mohammed
aliishi maisha ya upweke. Mume wake alimtelekeza wakati wa kesi, huku marafiki zake
wengi wakimkimbia.
Mnamo mwaka wa 1991, wakati Tanzania
ikisherekea miaka 30 ya uhuru, Bibi Titi alitajwa kwenye makaratasi ya chama tawala kama
Shujaa wa kike aliyepigania uhuru wa Tanganyika. Na Novemba 5,
2000 Bibi Titi Mohammed alifariki katika
hospitali ya Net Care Hospital mjini Johannesburg ambapo alikuwa akitibiwa.
kutoka misikitini
Uislam. Alisema, ulimwengu wa sasa unakua kwa
kutegemea vyombo vya habari, kwani vinaweza
kufanya uongo kuwa kweli na kweli kuwa uongo, na
hata kama Mtume angekuwepo angetumia njia ya
vyombo vya habari kufikisha ujumbe wa Mwenyezi
Mungu. Sheikh Kishk aliongeza kuwa, kwa sasa
vyombo vya habari ndio silaha muhimu ya kuendeleza jambo lako na kama hutoitumia vizuri silaha
hiyo utakuwa ni mwenye kupata hasara. (KHALID
OMARY)
Vyombo vya habari vya Kiislam vimetakiwa kuwa nyenzo ya kwanza ya kuuendeleza na
kuutangaza Uislam na sio kuwa chanzo cha malumbano miongoni mwao.
Hayo yalisemwa na Sheikh Nurdin Kishk wakati akitoa khutba ya swala ya Ijumaa katika
msikiti wa Mtambani uliopo Kinondoni jijini Dar es salaam. Sheikh Kishk alisema, endapo
kama vyombo vya Kiislam vitatumika katika njia hiyo, basi Uislam utasonga mbele. Hata
hivyo, badala ya kuutangaza Uislam, vyombo hivyo vimekuwa viwanja vya kuushambulia
habari / tangazo
www.islamicftz.org
Uamsho waendeleza
daawah Segerea
Mwingine aliyesilimishwa asimulia
Alikuwa Gift Robert, sasa ni Issa Robert
Na Mwandishi wetu
wa gereza.
Hata hivyo, kwa uwezo wa Allah
masheikh hao wamekuwa wakitumia
muda mfupi kufikisha ujumbe wa dini ya
Kiislamu na kupata kundi kubwa la watu
wanaosilimu, ambapo kwa mujibu wa kijana Nassor aliyesilimu majuma kadhaa
yaliyopita, mpaka sasa wameshasilimisha
zaidi ya watu 15, wakiwemo watu wazima,
vijana na watoto.
Hata hivyo, Nassor alisema, mara nyingi wanaosilimu wanachukiwa na wenzao.
Watu wengi wanaosilimu huitwa majina
mabaya na kuhusishwa na tuhuma za
ugaidi na vile vile kunyimwa fursa ya kufanya ibada ya swala, alibainisha Nassor.
Akielezea sababu za kusilimu kwake,
kijana Issa Robert amesema, ukarimu na
ustaarabu uliooneshwa na masheikh kwa
mwezi mmoja aliokuwa mahabusu ulipelekea kutaka kuifahamu dini hiyo kiundani.
Alisema, baada ya kuvutiwa na tabia
nzuri za masheikh hao aliwafuata na
wakamlingania kwa njia ya kuoanisha vitabu vya Quran na Biblia, na hapo ndipo
alipogundua ukweli.
Afyais natural
source of sweet
drinking water
from underground stream
which is blended
with essential
minerals to support and aid perfect metabolism.
WATERCOM LIMITED
P.o. Box 20409, Plot N.4005, Kisarawe11 area
Temeke,Daresalaam, Tanzania
www.watercomtz.com, E-mail:info@watercomtz.com
hutolewa na kuchapishwa
tahariri / uchambuzi
wishoni mwa juma lililopita umma wa waislamu wa Tanzania ulipata mgeni katika sekta
ya habari baada ya ujio wa gazeti
jipya la Iqra hatua inayofanya idadi
ya vyombo vya habari vya kiislamu
kwa upande wa magazeti kufikia zaidi ya matano (5) ukijumuisha yale ya
awali ambayo ni Annur,Alhudaa,Kisiwa na Imaan.Hiyo ni hatua ya kupongezwa na ni faraja kwa
umma wa kiislamu.
Kama inavyofahamika suala la
upashaji habari ni moja kati ya nyenzo muhimu katika kukabiliana na
propaganda chafu halikadhalika
ubunifu wa ajenda hasi zinazolenga
kuuchafua uislamu ambazo zimekuwepo tangu na tangu tokea enzi za
manabii na mitume.
Ukilinganisha na vyombo visivyo
vya kiislamu hali ya mambo haiko
tofauti sana hata katika vyombo vya
nasaha za wiki
SELEMANI MAGALI
wa na kuishia kuchagua mtu ambaye atakatisha tamaa zaidi wananchi ambao tayari wanaonekana wamekata tamaa na wamepoteza matumaini kutokana na
changamoto za maisha.
Kundi hili linaamini kuwa inawezekana hatua ya uchujaji
itakuwa ngumu kiasi kwamba
maamuzi magumu itabidi yafanyike ili kukinusuru chama kisigawanyike.
Maamuzi magumu ni kama
yale ya 2010 ambapo iliamriwa
nafasi ya uspika ikamatwe na
mwanamke. Maamuzi magumu
ya namna hii sio muda wote
yanaweza kuwa mazuri na yanaweza kuacha wagombea wazuri.
Pia, ugumu wa kupata kiongozi
mzuri unaweza kutokana na ghilba
ya baadhi ya wagombea ambao
tayari baadhi yao inasemekana
wameanza kununua watu ili wa
washangilie na kuonekana kuwa
wanapendwa na kukubalika.
Wagombea wa aina hii, inasemekana, wameanza kununua hata
wanahabari. Ingawa ushahidi sina,
waswahili wanasema lisemwalo
lipo na kama halipo laja.
Lakini wapo pia watu wanaoona utitiri huu wa wagombea kama
jambo zuri, na ni ishara njema kwa
awamu ijayo.
Walio na matumaini kutokana
na utitiri wa wagombea wanaamini katika demokrasia, ambapo wagombea wengi inamaanisha una idadi kubwa ya watu ambao utapata fursa ya kuwapima na
kuchagua mgombea mzuri.
Katika orodha ya wana CCM
waliojitokeza kuna maprofesa,
madaktari, vijana, wazee, matajiri
na masikini, wenye uzoefu na
wachanga, wanadiplomasia na
kadhalika.
Ni mgombea mwenye elimu,
uzoefu na falsafa gani ataweza kuli-
www.islamicftz.org
NA YUSUFU AHMADI
ngoma (beni)
na pia
uzushi kuhusu mambo ya sherehe
za Maulid.(Kitabu cha Sheikh Alamin-Kutizamia, uk 10)
Kwa maneno mengine, Sheikh
Al-Amin ni muasisi wa harakati za
kisunnah Afrika Mashariki ndiyo
maana wanafunzi wake kama
Sheikh Abdallah Saleh Farsy walikuja kuendeleza harakati hizo.
Lakini tofauti na masheikh
wengi wa kisunnah leo, Sheikh AlAmin hakujiona tofauti na waislamu wengine hata kama walikuwa
wakiyafanya yale aliyokuwa akiyapinga kwa mujibu wa Quran na
Sunnah. Kuhusiana na elimu ya
kimagharibi (Western education),
Sheikh Al-Amin aliwahimiza
Waislamu kujifunza elimu ya sayansi na teknolojia ya Magharibi ili
waweze kupata maendeleo huku
akisema kuwa, dini ya Kiislamu ni
dini ya kisayansi na inayotumia
tafakuri (Rationality).
Katika kuonesha kuwa ndani
ya Uislamu kuna mambo ya kisayansi, Sheikh Al-Amin alitolea
mfano wa nchi ya Misri iliyokuwa
ya kiislamu ambapo Waislamu
waliweza kufanya mapinduzi
makubwa katika maendeleo ya
gazeti lake la lugha ya kiswahili lililojulikana kama Sahifa na kufuatiwa na gazeti jingine lililojulikana kama Al-Islah hapo mwaka
1932. Magazeti yote hayo mawili
yalikuwa yakichapisha habari zilizokuwa na lengo la kuufanya
umma kupokea mawazo mapya
ya kimaendeleo katika elimu huku
yakisisitiza watu kufuata misingi
sahihi ya Kiislamu.
Ukiachia mbali kutumia magazeti katika kuhakikisha Uislamu
unaimarika katika mji wa Mombasa, Sheikh Al-Amin alianzisha
Jeshi la Upotovu (Going astray
Army) dhidi ya ushawishi mbaya
wa chini kwa chini uliokuwa ukifanywa na jeshi la Uokovu (Salvation Army).
Maandishi na wanafunzi wake
heikh Al-Amin aliandika
vitabu vingi vya dini ya
Kiislamu katika lugha ya
kiswahili na kiarabu,
ikiwemo kutafsiri Suratul AlBaqara, Suratul Al- Imran na Suratul An-Nisaa. Pia alikuwa akiandika makala katika jarida la AlManar la Chuo Kikuu cha AlAzhar cha nchini Misri.
Katika uhai wake, Sheikh AlAmin alifundisha wanafunzi wengi, ambao baadhi yao walitoa
mchango mkubwa katika maendeleo ya dini ya Kiislamu. Baadhi
ya wanafunzi wake wakubwa ni
pamoja na Sheikh Muhammad
Kassim na Sheikh Abdullah Saleh
Al-farsy, ambao wote wamewahi
kushika nafasi ya Kadhi Mkuu wa
Kenya. Mwanafunzi wake
mwingine mahiri ni Maalim
Ghazali ambae nae alianzisha Madrasa ya Ghazali iliyokuja kujulikana kama Shule ya msingi ya
Mbaraki huko Kenya.
Sheikh Al-Amin atakumbukwa
kwa utabiri wake aliouita khatari
nyeusi uliosema: Jamaa wa bara
watazitupa fagio na kuwa mabwana kwa sababu ya elimu na vitabu,
na sisi tulio mabwana leo ndio tutakaotupa vitabu tukaokota fagio.
Sheikh Al-Amin pia alikuwa
mtetezi mkubwa wa elimu ya wanawake, ambayo haikuwa ikitolewa kwa kiasi kikubwa kwao na
alizihimiza familia nyingi kuwafunza elimu mabinti zao.
Sheikh Al-Amin alifariki dunia
mwaka 1947 baada ya kuugua kifua kikuu kwa muda mrefu. Siku
aliyokata roho, Sheikh Al-Amin
alimuuliza mkewe, sasa ni saa
ngapi? Akajibiwa ni alasiri.
Akamwambia mkewe mkubwa,
Bi Swafia bint Suleiman, amtawadhishe. Kisha, akainuliwa, akasali.
Akatoa salamu kumaliza swala.
Punde, Allah akachukua roho yake
akiwa amezungukwa na wakeze
wawili, wanawe na wanafunzi
wake.
Allah amrehemu
www.islamicftz.org
Na Selemani Magali
Ushindi hauteremki kutoka katika ombwe wala hauji bila kutarajiwa. Kushinda au kushindwa
kupo na kunatawaliwa na kanuni
na njia ambazo zimenukuliwa na
Allah katika Quran ili waumini
waweze kuzijua kwa yakini, elimu
ya uhakika na kwa upeo mkubwa
zaidi. Kanuni hizi hazibadiliki kwa
kiasi kikubwa.
Allah anasema yafuatayo kuhusu kanuni hizi: Kabla yenu
zimepita nyendo nyingi; basi tembeeni katika ulimwengu muangalie vipi ulikuwa mwisho wa wanaokanusha (3: 137).
Na pia, Hii ni ada ya Allah iliyokuwa kwa wale waliopita zamani.
Wala hutapata mabadiliko katika
ada ya Allah (33: 62). Na Anasema tena Allah aliyetukuka: Huo
ndio mwendo wa Allah uliokwishapita zamani, wala hutapata
mabadiliko katika mwendo wa Allah (48: 23).
Kupotoka katika njia iliyonyooka na kusahau ujumbe wetu
ni moja kati ya sababu kubwa zinazotufanya Waislamu tushindwe.
Miaka 20 ya LHRC:
www.islamicftz.org
ncha ya kalamu
Sheikh Muhammad Issa
hiyo wabaguane?
Sababu kubwa ni baadhi ya
wanasunnah kuwaona wengine si
masalafi wa kweli, hata kuthubutu kuwaita watu wa bida na
kuwakufurisha (Mungu atuepushe) kwa kuwa tu wanatofautiana nao mitazamo.
Ni wazi masalafi wa zama hizi
kama zamani wanatofautiana katika jinsi ya kuziendea dalili za
kisharia. Masheikh wakubwa wa
kisalafi duniani wanatofautiana,
lakini hawakufurishani.
Uelewa wetu wa usalafi unajumuisha masuala mengi ya msingi
ambayo hayapewi kipaumbele na
makundi ya kisalafi ya leo,
ikiwemo msimamo kuhusu masuala ya kisasa ambayo watu wema
waliotangulia (Salaf Swaalih)
wenyewe hawakukumbana nayo.
Mambo hayo ni kama kupiga
picha, uraia na kujinasibu kwa
makala maalum
10
www.islamicftz.org
11
www.islamicftz.org
makala maalum
NA IDDI JENGO
Ramadhan ni
katika kambi
maalum za
mafunzo
zinazo
funguliwa
kila mwaka,
kisha
zinafungwa.
Kutokana na
Ramadhan,
mwenye
kutaka
kupata faida
hupata faida
ndani yake na
hula hasara
mwenye
kutaka kula
hasara.
walikuwa hawajui hata kuvaa hijabu, basi
utawaona wanaanza kununua mitandio ya
kujitanda huku soko la kanga nalo likikua.
Wale wanaojitahidi zaidi hununua baibui.
Ndani ya baadhi ya nyumba za Waislam
utaanza kusikia Quran zikisomwa kwenye
redio na runinga na miziki ikipungua.
Hayo yote yanafanyika kama heshima
na taadhima kwa mwezi huu. Ila walichoghafilika ndugu zetu hawa, ni kuwa
uelewa huo unamaanisha kuwa katika
miezi iliyobaki hawapaswi kufanya hayo.
Ina maana kwamba, uwepo wa Mungu,
uwezo wake, nguvu zake na amri zake hazina uzito wowote ila Ramadhan tu. Nayo ni
dhana potofu. Mungu atuepushe nayo.
Ijulikane kuwa ni wajibu wa kila mwanajamii linapoonekana jambo lolote ovu
na baya kulizuia, kulikemea au kulikasirikia, ingawa hili la mwisho la kukasirika tu
ni katika udhaifu wa imani.
Alah Taala anasema:Na waumini wanaume na waumini wanawake wao kwa
wao ni marafiki walinzi. Huamrisha mema
na hukataza maovu, na hushika swalah, na
hutoa zakaah, na humtii Mwenyezi Mungu na Mtume Wake. Hao Mwenyezi Mungu atawarehemu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mtukufu, Mwenye nguvu, Mwenye
hekima (9: 71).
Vile vile hadith kutoka kwa Mtume
wetu mpenzi (Rehma na amani ziwe juu
yake) iliyosimuliwa na AbuSaiyd AlKhudriy(Radhi za Allah zimshukie)ambaye amesema:Nilimsikia Mtume(Rehma na amani zimshukie)amesema:
Yeyote yule atakayeona kitendo kiovu
basi akiondoe (akibadilishe) kwa mkono
wake, ikiwa hawezi basi kwa ulimi wake
(alikemee au kukataza), na ikiwa hawezi
basi kwa moyo wake (achukie) na huo
(yaani kuona baya na kunyamaza) ni udhaifu wa Imani(Muslim).
Jengokeya5@gmail.com 0714 135 201
12
www.islamicftz.org
afya yako
Mlinganiaji
Pazi Mwinyimvua
MLO BORA
KWA MFUNGAJI
SWAUMU YA
RAMADHAN 2
uonesha uzito wa
wajibu wa kufanya
kazi ya dawah kwa
Waislamu, Allah
ametahadharisha wasioifanya
kazi hii kupata laana kama alivyosema katika Quran; Hakika wale wafichao yale tuliyoyateremsha katika ubainifu, baada ya kuyabainisha kwa watu
katika kitabu, hao ndio waliolaaniwa na Allah na wamelaaniwa na kila chenye kulaani
(2:159).
Na maana ya laana ni kufukuzwa au kuwekwa mbali na
rehma za Allah (Subhaanahuu
wa taala). Matokeo ya kuwekwa
mbali na rehma za Allah ni kudhihiri kwa maovu na uharibifu
katika bara na baharini.
Mtume (Rehma na amani
ziwe juu yake) akaweka wazi
uzito wa kosa la kutokufanyika
dawah; Yeyote afichaye elimu
ambayo Allah hunufaisha watu
kwao katika mambo ya dini, Allah atamfunga makongwa ya
moto siku ya Qiyama (Ibn Majah).
Kuwa na Ilmu juu ya Uislamu kisha usiifikishe kwa wanadamu ni sawa na kuificha
elimu hiyo. Hivyo, mtu mwenye
elimu anawajibika kuifikisha
kwa watu kwa kufanya kazi ya
dawah.
Ni Waislamu wangapi wanaishi na wanadamu wenzao
nyumba moja, wanafanya kazi
nao ofisi moja, wanauza nao
soko moja kisha wasiwafikishie
ujumbe wa Allah, lakini wakawafikishia mambo waliyoyaona
katika runinga zao, au waliyoyasoma katika magazeti au
kusikia katika radio zao yasiyokuwa na manufaa nao? Kufanya hivyo ni sawa na kuificha
elimu ya Allah kwa viumbe
wake, ni khiyana ambayo Allah
huilipa kwa kumlaani mtendaji
(Allah atukinge na laana).
Nguzo za dawah:
Nguzo za dawah ni tatu:
Ujumbe unaolinganiwa, Mlinganiaji (Daai) na wenye kulinganiwa. Kila moja kati ya nguzo
hizi ina sifa zake, masharti yake
na malengo yake.
Ili kufanya kazi ya dawah
ipasavyo yampasa mwenye kutaka kuifanya kazi ya dawah
kuwa na elimu ya kutosha
kuhusu kila nguzo ya dawah.
Lengo la kazi ya dawah ni
kueneza mafundisho ya Uislamu kama yalivyofikishwa na
Mtume Muhammad (Rehma
na amani ziwe juu yake) ili dini
13
www.islamicftz.org
uchumi na biashara
JAMAL ISSA
moja ya
kanuni ya
msingi ya
mfumo wa
fedha wa
Kiislamu
ni kuunga
nisha
fedha na
rasilimali
au bidhaa
badala ya
kufanya
fedha
yenyewe
kuwa
bidhaa.
hukrani na
utukufu ni
wake Mfalme
wa mbingu na
ardhi aliye pekee,
mwenye kustahiki
kuabudiwa kwa haki.
Sala na salam zimfikie
Mtume aliye msifika,
mjumbe wa Allah na rehma kwa walimwengu
wote. Kisha salam kwa
wanaofuata muongozo.
Ndugu mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa
safu hii juu ya uchumi
na biashara katika mtizamo wa Kiislamu karibu tena kwa mara nyingine katika mfululizo
wa makala zetu.
Katika makala zetu
za matoleo yaliyopita
Ijarah: Mkataba wa
kukodishana kwa
malipo ya kodi
tulidurusu aina mbalimbali za ushirika, ikiwa ni
namna ya kufanya biashara na kuwezesha
kujenga uchumi usiojikita katika riba na
wenye kuzingatia
Dkt Idris
Rashid,
mkurugenzi wa
benki ya
Amana.
ni kuunganisha fedha na rasilimali au bidhaa badala ya kufanya fedha yenyewe kuwa bidhaa.
Namna nyingine ya kufanya
biashara katika utaratibu wa
Kiislamu inaitwa Ijarah.
Ijarah ni mkataba wa kukodisha rasilimali fulani kama vile
gari au nyumba kwa malipo ya
kodi, ambapo anaye kodisha
hubakia kuwa mmiliki na
anayekodi hunufaika kwa matumizi ya rasilimali hiyo. Anayekodisha anatakiwa amiliki
kwanza rasilimali hiyo kwa kuinunua au kujenga au kwa namna nyingine inayokubalika
kisharia kabla ya kukodisha.
Pia atawajibika kuihudumia
kwa huduma zinazostahiki kwa
nafasi yake kama mmiliki. Kwa
upande mwingine, anayekodi
anatakiwa kuitumia rasilimali
14
www.islamicftz.org
inatoka Uk 9
ra? Sasa inapotokea wanawazuoni wa kisalafi wa
leo wakatofautiana, kwa nini baadhi
wachukue misimamo ya kuwakufurisha wengine kwa mambo yanayohitaji ijtihaadi za wanawazuoni?
Tatizo kubwa ni kujitakasa nafsi
zetu (Tazkiyatu-nnafsi) kunakopelekea kuwaona wengine si masalafi wa
kweli au hata si masalafi kabisa.
Tatizo jingine, ni kujikita katika
kufukua mabaya ya wengine (Al jarh
wat-tadiyl) kiasi kwamba hakuna
aliyesalimika sasa. Badala ya kujikita
katika kuzitakasa nafsi zetu dhidi ya
makosa yetu wenyewe twajikuta
tukitakasa nafsi zetu na makundi
yetu dhidi ya wengine.
Tatizo letu jingine, ni kuwachukulia Waislamu ambao bado hawajashika mwenendo wa kisalafi
kama makafiri. Mtazamo huu unazalisha kibri na kujiona (Al-ujub),
ila kwa mitume tu. Lakini leo inaibuka misimamo mikali ya tasubi si
za kimadhehebu, bali kwa masheikh
tuwapendao. Hata mtu apewe hoja
yenye mashiko, hakiuki msimamo
wa sheikh wake.
Kibaya zaidi usalafi huu wa sasa
umeshachukua msimamo wa kitaifa, huku baadhi wakifuata wanawazuoni wa Saudia, wengine wa Yemen
nk. Tofauti za kisiasa za nchi za Kiislamu zimeingia hata kwenye misimamo ya kisalafi ya leo.
Jambo jingine, ni hili la masalafi
wa leo kunyamaza kimya kuhusu
watawala. Sheikh Ibn Taymiyyah aliwakosoa sana watawala, kinyume
na masalafi wa leo walioshupalia kukosoa masheikh wa kisunnah tu.
15
www.islamicftz.org
NA YUSUFU AHMADI
akati fulani,
Tanzania ilitaka
kujiunga na
taasisi ya kiislamu ya kimataifa ya OIC, jambo ambalo lilipelekea kampeni kali ya kuzuia jambo hilo
kutoka kwa makanisa. Hili ni
suala la uhusiano wa kimataifa ambalo kama Waislamu
tunapaswa kuwahoji wagombea mbalimbali wa nafasi
za urais wanaojitokeza hivi
sasa.
Katika nchi zilizoendelea,
moja ya mambo muhimu
ambayo wapiga kura wengi
wanayaangalia wanapowapima wagombea waliojitokeza
kuwania nafasi kubwa kama
ya urais au uwaziri mkuu
huwa ni sera zake kuelekea
mataifa ya nje (Foreign policies).
Wengi wa wapiga kura na
wachambuzi humtathmini
kwa kina mgombea na sera
zake jinsi atakavyoshirikiana
na mataifa ya nje, na pia
atakavyokabiliana na
changamoto mbali mbali zilioko nje ya taifa lao ili mradi
tu wanaona zinaathiri maendeleo yao.
Japo kila nchi huwa na
sera zake maalum za nje zilizoandikwa kama ilivyo hapa
nchini kwetu, ila kwa baadhi
ya nchi kubwa za wenzetu,
mgombea nae huwa ananadi
sera zake kuelekea mataifa ya
kigeni.
Mfano, wakati Rais wa
Marekani Barack Obama
anawania nafasi hiyo kwa
mara ya kwanza, moja ya sera
zake kuelekea mataifa ya nje
ilikuwa ni kurejesha uhusiano ulioharibika baina ya
taifa lake na ulimwengu wa
Kiislam.
Jambo ambalo alilifanya
muda mfupi mara baada ya
kushika nafasi ya Urais kwa
kwenda nchini Misri katika
chuo kikuu cha Al-Azhar na
kuhutubia mataifa ya ulimwengu wa Kiislam, japo
maneno ya hotuba hiyo na
matendo ya nchi yake ni sawa
na bure.
Hivyo ndivyo ilivyo desturi
ya wagombea wa mataifa
hayo, kwani bila kueleza kwa
ufasaha sera zako kuelekea
mataifa ya kigeni itakuwa
vigumu sana kushinda nafasi
kubwa kama ya Rais, kwani
sera hizo zina nafasi yake katika maendeleo.
Tuje hapa nchini kwetu,
kwa sasa watanzania wanaendelea kushuhudia
mbwembwe, vituko na vim-
Stephen Wassira
Edward Lowassa
Frederick Sumaye
Watangaza nia
watuambie na
sera zao za Nje
bwanga vya watangaza nia ya
kugombea nafasi adhimu na
kubwa katika Urais kutoka
Chama cha Mapinduzi
(CCM).
Kila mtangaza nia amejaribu kusema kile atakachowafanyia watanzania endapo atapitishwa na chama
chake na kisha kupigiwa kura
katika uchaguzi mkuu wa
hapo Octoba 25 mwaka huu
na kushinda.
Yapo mengi ambayo
yamesemwa na watangaza
nia hao katika sera zao mbali
mbali, lengo likiwa ni kuushawishi umma wa Tanzania
uwapigie kura .
Lakini kwa bahati mbaya
au vinginevyo, takriban watangaza nia hao hakuna hata
mmoja aliewaelezea watan-
Lakini kwa
bahati mbaya
au vinginevyo,
takriban
watangaza
nia hao
hakuna
hata mmoja
aliewaelezea
watanzania
sera zake
kuelekea
mataifa ya
kigeni.
makala
16
www.islamicftz.org
Wanahabari
wa Kiislamu
tufuatilie
siasa za nchi
NA KHALID OMARY
Pichani juu
ni uzinduzi
wa gazeti
jipya la
Kiislamu
(IQRA)
uliofanyika
wiki
iliyopita
katika
msikiti wa
Mtambani
jijini Dar es
Salaam.
Chini,
mhariri wa
redio
Imaan,
Kassim
Lyimo
akiwa
katika moja
ya semina
za mafunzo
ya ndani
kwa
watendaji
Imaan
Media.
zilizopangwa jana.
Inawezekana kama
kungekuwa na chombo kimoja
kinachowaunganisha waendeshaji wa vyombo vya habari vya
Kiislamu kusingekuwa na sintofahamu kama hii.
Hii ni kwa sababu dini ya
Uislamu ina mafundisho yake
ambayo hayaendani na mifumo ya uendeshaji wa vyombo
visivyo vya Kiislamu kwa sababu mbali mbali.
Kwa mfano, vyombo vya Kiislamu haviwezi kutoa picha
inayoonesha maumbile ya
mwanamke katika hali yoyote
ila awe amejisitiri.
Moja ya mambo ambayo
yanaonyesha kuwa baadhi wamiliki ama waendeshaji wa vyombo vyetu vya Kiislamu hawapo makini katika kazi zao na
kusahau kuwa hiyo ni taaluma
nyeti kabisa hapa ulimweguni
ni lile nililokutana nalo katika
kituo kimoja cha redio.
Nilipotembelea chumba
chao cha habari wakati wakiandaa taarifa ya habari ya
mchana, nilikuta watangazaji
na waandishi waliokuwepo
wakinakili habari kutoka
makala ya kimataifa
www.islamicftz.org
17
Btittany Maynard
mwenye umri wa miaka 29
aliamua kuhamia Origon
na kujihudumia vidonge
vya barbiturates alivyopewa na daktari wake na
akafa. Kabla ya kuzuka
kampeni hizi, hilo lingeitwa kosa la kumsaidia mtu
kujiua. Lakini sasa si kosa
tena, bali haki ya mgonjwa
ambayo inapaswa
kulindwa.
In a d a i w a kw a m b a ,
mgonjwa kupewa dawa za
kujiua si kosa, kwa sababu
ni uamuzi wake mwenyewe,
na uamuzi wa mtu juu ya
mwili wake ni jambo lililoruhusiwa kikatiba.
uran inakataza
mtu kujiua pale
Allah Taala aliposema Na
wala msiziue nafsi zenu,
hakika Allah ni mwenye
huruma kwenu (4:29).
Katika hadith ya Mtume
(Rehma na amani ziwe juu
Huko nyuma,
madakatari
walikuwa
wapingaji
wakubwa
wa kusaidia
wagonjwa
kujiua.
Jumuiya ya
madaktari
nchini
Marekani
iliwahi
kutoa tamko:
Daktari
kumsaidia
mgonjwa
kujiua ni
kinyume na
wajibu wake,
ambao ni
kumsaidia
mgonjwa
kupona.
TOVUTI ZA
Na Khalid Omary
ndani yake. Miongoni mwa mada
hizo ni historia ya Uislam, Malengo makuu ya Imaan katika
18
www.islamicftz.org
SECTION B: GRAMMAR:
(a) careful (b) carefully (c) very care (d) care (e)
cares
22. Ramadhani is .. than Juma.
(a) Active (b) activier (c) more activist (d) more
active (e) the most active
23. They help us whenever we get
stuck,..?
(a) Arent they (b) do they (c) dont they (d) arent
us (e) werent they.
24. T hat car belongs to them. It is
..
(a) Theirs (b) theirs (c) they are (d) theres (e)
theres
25.Anita is fond .. Playing in
class.
(a) for (b) of (c) about (d) with (e) to
26. The teacher roared angrily, .
Were making noise?
(a) Why (b) which (c) when (d) who (e) whom
27. Mwalimu Julius kambarage Nyerere was
.. Honest man.
(a) the (b) a (c) an (d) some (e) any.
28. He is as as a bee.
(a) Dangerous (b) brave (c) coward (d) cunning (e)
busy.
SECTION C: COMPOSITION:
11. C
12. B
13. A
14. B
15. B
16. C
17. D
18. B
19. C
20. D
21. B
22. B
23. B
24. C
25. B
26. B
27. B
28. C
29. A
30. B
31.C
32. C
33. B
34. B
35.B
36.B
37.C
38.B
39.A
40.C
41.A
42.D
43.C
44.B
45.B
46.C
47.C
48.D
49.C
50.B
kona ya watoto
ZAHRA EBRAHIM
watoto / tangazo
www.islamicftz.org
Muda
11:00 .11:05
05 min
11:05 .11:30
3
4
19
vipindi TV imaan
Kipindi
S/No:
Wakati
TIME
Adhana ya Alfajir
06:00 06:20
20MINSheikh:
NYIRADI ZA ASUBUHI
RECOR
25 min
Dua
06:20 06:35
15MINSheikh:
NASAHA ZA ASUBUHI
RECOR
11:30 .12:00
30 min
Nyiradi za asubuhi
12:00 .01:00
1 hr
06:35 06:45
10MINSheikh:i.Twaha
KILMA KIZURI
RECOR
01:00 .01:20
20 min
07:00 07:20
20MINSheikh:
DIRA YA HABARI
01:20 .04:00
3 hrs 40 min
07:20 07:30
10MIN
CHACHU YA DIRA
LIVE
04:00 .05:00
1 hr
07:30 08:00
30MIN
SUHUFA ZA MAGAZETI
LIVE
05:00 .05:05
05 min
Mukhtasar wa dira
10
08:00 10:00
2HR
MADA NYETI
LIVE
05:05 .06:00
55 min
Salaam za asubuhi
11
10:00 11:00
1HR
USALAMA BARABARANI
MARU
10
06:00 .06:45
45 min
Ulimwengu wa Kiislaam
13
11:04 11:35
31MIN
MAWAIDHA
RECOR
11
06:45 . 06:50
05 min
Adhana ya Dhuhr
14
11:35 12:00
25MIN
BULUGHULMARAM
RECOR
12
06:50 .07:20
30 min
Tarjuma
18
12:14 12:24
RECOR
13
07:20 .08:00
40 min
Mimbar zetu
20
12:26 12:56
10MINSheikh:
ENGLISH LECTURE
30 MIN
14
08:00 .09:00
1 hr
Mawaidha
22
13:00 13:13
13MINSheikhENGLISH
Nassor LECTURE
Bachu
RECOR
15
09:00 .09:20
20 min
Dira ya habari/matangazo25
14:00 14:45
45MIN
RECOR
16
09:20 09:45
25 min
Tauhiid
26
14:46 14:50
17
09:45 .09:50
05 min
Adhana ya al-asr
27
18
09:50 .10:20
30 min
Tarjuma
29
19
10:20 .11:00
40 min
Kalima
20
11:00 .11:20
20 min
Dira ya habari/
21
11:20 .12:00
40 min
Nasaha za washairi
22
12:00 .12:30
30 min
Adhkarul masaa
23
12:30 .12:35
05 min
Adhana ya Magharib
24
12:35 .01:00
25 min
25
01:00 .01:45
45 min
Nasaha marudio
26
01:45 .01:50
05 min
Adhana ya Ishaa
27
01:50 .02:20
30 min
28
02:20 .03:00
40 min
29
03:00 .03:20
20 min
Dira ya habari/
30
03:20 .04:20
1 hr
31
04:20 .05:00
40 min
32
05:00 .06:00
33
06:00 .11:00
Nasaha za asubhi
Dira ya habari/
Majlis ya tv Imaan
Tafsir ya Qur aan
Muda
DURATION
Kipindi
PROGRAM
ST
RECOR
Ust:Ally Ajran
Sheikh:
NAFASI YA MWANAMKE
KUTOKA SHULENI
RECOR
Hasan
RECOR
14:50 15:50
4MINSheikhPROMO
Mohammed Nduli
1 HRSheikh:
UISLAM NA TIBA
15:52 16:22
30MINSheikh:
BUSATI LA KISWAHILI
RECOR
31
16:24 16:55
30MINSheikhQUR'AN
RECOR
S/No:
TIME
35
17:11 17:33
37
17:45 18:00
38
DURATION
MARU
PROGRAM
STATU
Ly
30MIN
SIMULIZI ZA BIBI ZAINAB Kasim
RECOR
Sheikh Mishari
15MIN
ANNASHEED
RECOR
18:00 18:20
20MIN
NYIRADI ZA JION
RECOR
39
18:20 18:40
20MIN
DUA + ADHANA
RECOR
40
18:40 18:57
17MIN
RECOR
42
19:00 19:30
30MIN
MAWAIDHA
RECOR
44
19:31 20:04
33MIN
MAWAIDHA
RECOR
47
20:10 20:32
22MIN
ALINGANIWE
RECOR
Kipindi maalum
50
20:40 - 21:10
30 MIN
SUHUFA ZA MAGAZETI
MARU
Mawaidha
51
21:10 - 23:10
1 hr
Familia
52
23:15 - 23:30
5 hrs
54
23:30 06:00
Sheikh:
Sheikh:
Sheikh
Sheikh:
Sheikh:
Ust:Othmaan Thabit
2HRSSheikh:
MADA NYETI
MARU
15 MIN
KABLA HUJALALA
Baba Kiruwasha
6:30HRS
USIKU WA QURAN
Sheikh:
RECOR
LIVE
Mwanza
105.6 Mhz
Kigoma
Arusha
104.5 Mhz
Tabora
101.6 Mhz
92.5 Mhz
90.8 Mhz
Dodoma
104.5 Mhz
Moro
102 Mhz
104.5 Mhz
Dsm
Masafa ya Imaan FM
1
2
3
4
5
6
Daresalaam
Morogoro
Arusha
Mwanza
Kigoma
Tabora
104.5 Mhz
96.3 Mhz
90.8 Mhz
105.6 Mhz
92.5 Mhz
101.6 Mhz
7
8
9
10
11
12
Mbeya
Dodoma
Ruvuma
Mtwara
Zanzibar
Pemba
90.3 Mhz
102 Mhz
94.2 Mhz
90.9 Mhz
104.5 Mhz
104.5 Mhz
Mbeya
104.5 Mhz
104.5 Mhz
104.5 Mhz
Ruvuma
Mtwara
94.2 Mhz
90.9 Mhz
20
Wanahabari
www.islamicftz.org
wa Kiislamu
tufuatilie
siasa za
nchi
Uk 16
21 Shaaban 1436, jumatatu Juni 8 - 14, 2015
Ansaar Sunnah
si dhehebu jipya
kama wasiojua
wanavyo
ambiwa, kwa
sababu kila
imam katika
maimam wanne
wa Ahlusunnah
wal Jamaaa
walikubaliana
katika kufuata
sunnah katika
kuyaendea
masuala yote
ya dini ya
Kiislam.
YUSUPH AMIN
BASUTA
Ushabiki wa madhehebu na
ujima ni miongoni mwa mambo
yanayotajwa kusababisha tofauti
(Ikhtlafu) kwa umma wa Waislam
ulimwenguni, japokuwa waanzilis h i w a m a d h e h e b u h ay o
hawakupitiwa na hali hii.
Pia, imeibainika kuwa, tofauti
zinazojitokeza zinatokana na baadhi ya Waislam kuacha kutumia
dalili za Quran na Sunnah katika
kuyaendea mambo, badala yake
kutumia fikra na utashi zaidi au
kufuata kauli za masheikh pasina
dalili.
Uelewa tofauti kuhusu sunnah
baina ya Waislam na watu kujiingiza katika utungaji wa hadith za
uwongo ni baadhi ya changamoto
zilizopelekea wanazuoni wa dini
ya Kiislam Tanzania kuanzisha
hutolewa na kuchapishwa na The Islamic Foundation, P.O.Box 6011 Morogoro, Tanzania E-mail: imaanmedia3@gmail.com