Professional Documents
Culture Documents
-Uk 5
www.islamicftz.org
Sheikh Ibrahim
Sheikh Chembea
Aref Nahdi
Busara itumike
kulinda amani
Ayatollah Ali
Khamenei
Head office, Lumumba Street, Opp: Viwanja vya Mnazi Mmoja, P. O Box 779 Dar es Salaam, Tanzania
Tell: 255 22 2182482/ 255 222184419, Fax: 255 22 2181424, E-mail: info@Binslum.com
Sheikh
Ponda
asubiriwa
kwa hamu
Uk 7
Na Kassim Lyimo
Morogoro
habari / tangazo
DHUHUR ASR MAGHARIB
6:08
09:18 12:17
6:08
09:19 12:16
6:12
09:24 12:19
6:17
09:25 12:27
6:09
09:13 12:21
6:21
09:35 12:27
6:21
09:32 12:29
6:33
09:40 12:43
ISHA
1:23
1:23
1:26
1:34
1:28
1:33
1:36
1:50
ISHA
1:59
1:45
1:56
1:48
1:46
1:41
1:43
TIF yafadhili
yatima masomo
Afrika ya Kusini
Selemani Magali
aasisi ya The Islamic Foundation (TIF) imempeleka mwanafunzi Juma Kapilimbi katika chuo cha kuhifadhisha
Quran kiitwacho Tarteel Quran kilichopo katika mji wa Azadvil mjini Johansburg ikiwa ni jitihada za kumuwezesha kijana huyo kuhifadhi kitabu
kitukufu cha Allah. Akizungumza na
gazeti Imaan, Katibu Mkuu wa taasisi
hiyo, Sheikh Ally Ajirani alisema kijana
huyo ni mwanafunzi ambaye alikuwa
akilelewa katika kituo cha yatima kinachofahamika kwa jina la Darul Imaan
kilichopo Kola hili Mjini Morogoro .
Sheikh Ajirani ameongeza kuwa kijana huyo atakuwa masomoni katika
kipindi cha miaka miwili ambapo baada
ya hapo anatarajiwa kurudi nchini ili
kuendelea na masomo yake ya elimu ya
mazingira katika shule ya Forest Hill
ambayo pia inamilikiwa na TIF.
Katika hatua nyingine, Sheikh Ajirani amebainisha kuwa licha ya kituo cha
Darul Imaan, pia taasisi ya The Islamic
Foundation inamiliki vituo vingine viwili ambavyo vimejikita katika kuwalea
watoto yatima hapa nchini.
Kuanzia tarehe 10, Agost, 2015 kwa watumiaji wa receiver, TV Imaan itahama kutoka MPEG2 na kuwa MPEG4 (HD)
Masafa ya Satellite
Satellite: IntelSat 906 Frequency: 4066.25 Symbol rate: 1613.475 FEC: 2/3 DVBS2
Vile vile unaweza kuangalia TV Imaan kwa njia ya mtandao (online) kupitia
http:// www.ustream.tv/channel/radio-imaan-fm-2
www.islamicftz.org
makala
Mchango wao
Katika
jamii ya
kitanzania,
ustaadh
ni yule
afundishae
dini, Quran,
kiarabu
na masomo
mengine
katika
madrasa,
msikitini au
shule za
Kiislamu
Mazingatio muhimu
www.islamicftz.org
kutoka misikitini
Uongozi ni majuto siku ya
kiyama - Sheikh Kishki
Na Mwandishi Wetu
Mlinganiaji maarufu nchini ambaye pia ni imamu wa msikiti
wa Vetenary uliopo Temeke
jijini Dar es salaam Sheikh
Nurdin Kishki amewaasa wagombea wa nafasi mbalimbali
za uongozi katika uchaguzi
mkuu wa mwaka huu kutambua dhima waliyonao endapo
watachaguliwa kuwaongoza
watu.
Sheikh Kishki ameyasema hayo wakati wa khutba
ya ibada ya swala ya
ijumaa iliyoswaliwa katika
msikiti huo wiki iliyopita
na kuongeza kuwa watu
wengi hupenda uongozi huku wakijifaharisha kwa vyeo na
kusahau kuwa uongozi
ni dhima inayoweza kupelekea majuto ya hali ya
juu mbele ya Allah Taala
siku ya kiyama.
Kama tungelijua dhima
ya mtu kiongozi ni ngumu
kiasi gani siku ya kiyama
sote tungekimbia uongozi
na madaraka kama vile
Punda anavyomkimbia
Simbaalidokeza Sheikh Kishki
huku akiwataka waislamu wazidi
kumuomba Allah kuipitisha salama siku ya uchaguzi na kuepusha
shari zinazoweza kujitokeza.
Kuhusiana na zoezi la uchaguzi
mkuu unaotarajiwa kufanyika
mwishoni mwa juma hili Sheikh
Kishki amesema hivi sasa watanzania wapo katika kipindi kigumu
kutokana na mawazo,fikra na
hamasa zao kuzielekeza katika
uchaguzi jambo linalopelekea
watu kusahau hata kutekeleza
ibada muhimu za dini.
Waislamu wahimizwa
kuamrisha familia zao
kufanya ibada
NA HASSAN NINGA
Waislamu nchini wametakiwa kuadhimisha mwaka mpya wa kiislamu kwa
kuamrisha familia zao kutekeleza mambo
ya kheri ikiwemo swala tano kama sehemu ya jitihada ya dini wakati wanapoingia
katika mwaka mpya wa 1437 Hijriya.
Nasaha hizo zimetolewa na Sheikh Issa
Othman Issa wakati wa ibada ya swala
ya ijumaa iliyoswaliwa katika msikiti wa
Maamuur uliopo Upanga jijini Dar es
salaam na kuwataka waislamu kujenga
mahusiano mema na familia na kwamba
kufanya hivyo ndio kutekeleza mafunzo
ya mtume rehema na amani ya Allah ziwe
juu yake.
Sheikh Othman alinukuliwa
akisema:Tunapoingia kwenye mwaka
mpya wa kiislamu,lazima tufahamu mahusiano yetu na watoto wetu yakoje na je,
mwaka uliopita tulipata nafasi ya kukaa
nao na kuwahimiza kufanya ibada au
tulikaa nao na kuwahimiza kufanya bidii
kwenye masomo tu.
Aidha Sheikh Othman aliwataka wazazi
kutambua kuwa,ni jukumu lao kuwahimiza watoto na familia kwa ujumla kutekeleza ibada mbalimbali na kwamba kama
waliteleza katika kuyaamrisha hayo basi
mwaka mpya wa kiislamu uwe ni fursa ya
kubadilisha mwenendo wa familia zao.
tujikumbushe
Choma moto majahazi. Ilikuwa ni amri kwa Waislamu kutoka kwa kamanda wa majeshi yaliyovuka bahari ya Mediterania kwa lengo la kuiteka Hispania au Andalusia kama inavyojulikana katika historia ya Uislamu.
Hatua hii ilifuatia mapambano ya miaka mingi kati ya majeshi
ya watawala wa Andalusia enzi
hizo na yale ya Waislamu kutoka
Magharibi na Kaskazini mwa Afrika. Waislamu walivuka bahari
kuiteka Andalusia ili kuzuia mashambulizi mapya dhidi yao.
Tariq bin Ziyad alikuwa amefaulu kutia nanga mahali penye
milima paitwapo Jabal Tariq
(Mlima wa Twaariq) hivi leo kwa
kumbukumbu ya jina lake. Kuficha historia hii iliyotukuka ya
Waislamu, wazungu wakapaita
Gilbrater. Huo ulikuwa mwaka
711 Miladia sawa na mwaka wa
92 Hijriya, enzi za utawala wa
bani Umayya uliotawala dola
kubwa ya Kiislamu kutokea Damascus (Dameshqi) nchini Syria.
Kilikuwa ni kipindi cha dola ya
Kiislamu kupanuka hadi China
na India.
Mara tu baada ya majahazi
yaliyowabeba Waislamu kutia
nanga, walijikuta wakikabiliwa
na jeshi kubwa la maadui zao.
Tariq bin Ziyad akaona dalili za
hofu toka kwa wapiganaji wake.
Hapo ndipo Tariq bin Ziyad alipofikia maamuzi yake ya kuchoma moto majahazi waliyotumia
kuvuka bahari na kila kilichomo
ndani yake.
Baada ya hapo, Tariq bin Ziyad
akatoa hutba kali yenye mguso
wa aina yake kwa kusema: Ndugu zangu katika imani, tuko hapa
kulieneza neno la Allah. Maadui
wako mbele yenu na bahari nyuma yenu. Na hamna chakula wala
maji ila kile mtakachokiteka
kutoka kwa maadui zenu kwa
panga zenu. Kwa hiyo hapa ni
aidha ushindi au kufa shahidi.
Allahu akbar! Hiki kilikuwa
kilele cha kumtegemea Allah na
azma ya kupigana kwa ajili yake
kilichooneshwa na Tariq bin Ziyad. Kwa wapiganaji katika jeshi
lake, kuitii amri ya kamanda wao
kuyachoma moto majahazi yenye
kila kitu chao kilikuwa kilele cha
utii.
Tariq bin Ziyad alikuwa mtu
wa kabila la Ulhasa katika waberiberi (Berbers) aliyeingia katika
Uislamu kutoka nchini Algeria.
Awali alikuwa mtumwa na aliposilimu akaachwa huru na bwana
wake. Huyu ndiye mtu aliyeiteka
Andalusia (Hispania) na kuupeleka Uislamu Ulaya.
Watu kama Tariq bin Ziyad,
waliokuwa watu duni kabla ya
Uislamu lakini wakapata hadhi
Athari ya utawala wa
Kiislamu Hispania
ipoonesha kuwahurumia Wayahudi, viongozi wa kanisa walimpindua na kumweka madarakani Mfalme Rodriguez. Wayahudi wanaume wakatiwa
utumwani na wanawake wao kufanywa masuaria majumbani.
Utawala wa haki wa
Waislamu
www.islamicftz.org
makala / tangazo
uchimbaji
wa visima
hivyo
katika
maeneo
mbalimbali
ya wilaya ya
Bagamoyo
umesaidia
kwa kiasi
kikubwa
kuondoa
tatizo
la maji
wilayani
humo
vimechimbwa katika maeneo ya soko, shuleni, kwenye
zahanati, misikitini na maeneo ya wazi ili kila mwananchi aweze kufaidika na
huduma hiyo.
Hata hivyo, Mkurugenzi
huyo wa TIF alisema kuwa
bado kuna maombi mengi
kutoka kwa jamii ya kuchimbiwa visima yaliyowasilishwa na wananchi wa Bagamoyo, na kwamba uchimbaji huo wa visima unaendelea wilayani humo ili kuwafikia wananchi wote wenye
shida ya maji katika maeneo
yao.
Akizungumzia umuhimu
wa maji katika jamii, Sheikh
Twaha alisema Mwenyezi
Mkurugenzi
mtendaji wa TIF
sheikh Ibrahim
Twaha akionja
maji kutoka
katika kisima
kilichochimbwa
Kwenye makazi
ya polisi
Bagamoyo.
Mungu ndani ya Qur ani iongeza kuwa serikali inathtukufu amesema amejaalia amini mchango huo na wakatika kila kitu uhai kutoka- nanchi pia wanapaswa
na na maji. Hivyo basi, TIF
kama taasisi ya kiislamu inazingatia kauli hiyo ya Allah
na kutoa umuhimu wa pekee katika huduma hiyo ya
maji. Kwa upande wao, baadhi ya wananchi wa wilaya
Bagamoyo waliofaidika na
msaada wa TIF wamesema
kuwa wanaishukuru taasisi
ya TIF kwa kuwachimbia visima katika mitaa mbali
mbali ya Bagamoyo na kuwaondolea adha ya ukosefu
au uhaba wa maji.
Nae Mkuu wa Wilaya ya
Bagamoyo, Majid Hemed
Mwanga, ameipongeza Islamic Foundation kwa uchimbaji wa visima wilayani
humo na kuongeza kuwa
serikaliinathaminimchango
wa taasisi hiyo katika kutoa
huduma za kijamii kama
hiyo ya visima. Hemed al-
abii na mitume.
Bila shaka wito wa Alhad
unawalenga Mashia ambao
tangu ajali ilipotokea wamekuwa wakiuandama Utawala wa Kisunni wa Ufalme wa
Saudia kwa tuhuma mbalimbali ambazo hazina msigi na
zimejaa uongo. Kufa Makka
na Madina si sawa na kufa
Manzese na Tandale, watu
wanapaswa kuomba kufa
katika ardhi ile kwa sababu
ni ardhi tukufu iliyobeba
watu maarufu hususan manabii na maswahaba, Alhad
alisema.
Aidha, akizungumzia mahujaji ambao hawajulikani
walipo, Sheikh Alhad alisema ana wasiwasi kuwa huen-
Afyais natural
source of sweet
drinking water
from underground stream
which is blended
with essential
minerals to support and aid perfect metabolism.
WATERCOM LIMITED
P.o. Box 20409, Plot N.4005, Kisarawe11 area
Temeke,Daresalaam, Tanzania
www.watercomtz.com, E-mail:info@watercomtz.com
hutolewa na kuchapishwa
tahariri / nasaha
nasaha za wiki
Selemani Magali
habari
www.islamicftz.org
Selemani Magali
Mwenyekiti
wa The
Islamic
Foundation,
Aref Nahdi.
Katika hatua
nyingine, Nahdi
amewataka
wanasiasa
kuangalia
maeneo wanayo
yazungumza
katika majukwaa
yao ya kisiasa, na
kuacha maneno
ya kuchafua na
kudharauliana
miongoni
mwao, kwani
hali ikichwa
itachangia amani
kupotea.
kuwa ahadi hizo, ambazo hazitekelezeki huchangia uvunjifu wa
amani, na pia aliwataka Waislamu
kuwa mbele katika kusimamia amani
Uislamu ni amani ili watu
waabudu Allahni vizuri suala la
amani lizingatiwe katika jamii,
Sheikh Twaha alisema. Alisema ni
kwa kutambua umuhimu wa amani ndio maana taasisi ya TIF ina
malengo ya kuwajenga watu kiroho.
Kwa hivyo, kuzungumza amani
ni jambo la lazima kwetu kwa sababu Watanzania wengi wanaiamni
Taasisi kwa kuwapa mazuri ya
Waislamu, alisema Sheikh Twaha.
Ni kheri tufe katika kufanya
mambo ya heri wala tusipoteze
maisha yetu katika vurugu za kisiasa kwani lengo la kuletwa duniani
ni kumuabudu Allah Taala, alisema Mkurugenzi huyo wa Taasisi ya
TIF.
Hali kadhalika, Sheikh Twaha
alisema kuwa ni aibu kubwa kwa
Muislamu kuhusika katika uvunjifu wa amani kwani dini ya Kiislamu
ni dini ya amani na wala sio dini ya
vuruga na kusababisha machafuko
katika jamii.
mu. Safari ya Sheikh Ponda ya kukaa gerezani ilianza Agosti 10, 2013
alipokamatwa baada ya kupigwa
risasi na polisi mjini Morogoro
dakika chache tu baada ya kumaliza
kuhutubia Waislamu siku ya Idi katika msikiti wa Dini Moja, Mungu
Mmoja ulioko eneo la Uwanja wa
Ndege.
Hata hivyo, Jeshi la Polisi mkoani Morogoro lilikanusha kumpiga
risasi Sheikh Ponda Issa Ponda. Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro
ACP Faustine Shilogile alisema
polisi walikwenda kumkamata lakini kwa kusaidiwa na wafuasi
wake, Sheikh Ponda aliwatoroka.
Baada ya kujeruhiwa, Sheikh
Ponda alikwenda Hospitali ya Taifa
Muhimbili kwa ajili ya kupatiwa
matibabu yatokanayo na kupigwa
risasi lakini polisi wakamtia nguvuni na kumfungulia mashitaka katika Mahakama ya Hakimu mkazi
mjini Morogoro.
www.islamicftz.org
Adhabu ya kifo
huliwaza wafiwa,
hulinda uhai na
kuleta amani
Mpenzi
msomaji, katika
makala kadhaa
zilizotangulia
tulizungumzia
ubaya wa kuua kwa
mujibu wa Uislamu.
Tuligusia pia kuwa
katika Uislamu
mtu huuwawa kwa
kufanya makosa
maalumu na
adhabu hiyo ya
kifo hufanyika kwa
utaratibu maalumu
wa kisheria.
Miongoni mwa makosa yanayopelekea mtu kuhukumiwa adhabu ya kifo katika Uislamu ni kuua kwa makusudi.
Tena, ili adhabu hii itekelezwe
ni lazima ithibitike pasina shaka yoyote kuwa kweli mtuhumiwa kaua kwa makusudi.
Anasema Allah aliyetukuka
katika Quran Tukufu: Na Tumewaandikia (Sharia) humo
kwamba uhai kwa uhai, na jicho kwa jicho, na pua kwa pua,
na sikio kwa sikio, jino kwa
jino; na majeraha (kulipizana)
kisasi. Lakini atakayetolea
sadaka (haki yake akasemehe)
kwayo, basi itakuwa ni kafara
kwake. Na yeyote asiyehukumu kwa yale aliyoyateremsha
Allah, basi hao ndio mad-
halimu. (5 : 45).
Hii ni simulizi ya Quran juu
ya Sharia ya Taurati kuwa
miongoni mwa hukumu zilizokuwamo katika kitabu hicho
kilichoshushwa kwa Nabii
Musa ni adhabu ya kifo. Kama
adhabu hiyo haiko hivi leo
ndani ya kinachodaiwa kuwa
Kumbukumbu la Taurati, basi
watu wameiondoa, na kwa
Itaendelea (tawaqaljuma@yahoo.com)
www.islamicftz.org
ncha ya kalamu
Marekani
imekuwa ikiahidi
kuisaidia
Nigeria
kukabiliana na
kitisho cha Boko
Haram lakini
wachunguzi
wa mambo
wanashangaa
kama kweli
Marekani ina
nia njema, kwa
nini basi ikatae
kuiuzia silaha
Nigeria?
makala
10
www.islamicftz.org
11
www.islamicftz.org
Misingi ya ufanisi wa
Siku ya Ashura:
uongozi wa Mtume
Yatakiwayo na
yasiyotakiwa
Sheikh Mohammad Issa
Said Rajab
sunna (Bukhari).
Katika upokezi wa Imam Ahmad (Allah amrahamu): Hii ni siku ambayo
Safina (ya Nuh) ilisimama juu ya mlima
Juudiy, kwa hiyo Nuuh akafunga
kumshukuru Allah (Ahmad).
Mayahudi walikuwa wameifanya siku
hii kuwa sikukuu ya kusherehekewa na
wanawake wao wakivaa mapambo mbali
mbali. Mtume (Rehma na amani ziwe
juu yake) akawaamrisha maswahaba wajitofautishe na Mayahudi kwa kufunga
swaumu siku hii ya Ashura.
Siku ya Ashura, Mayahudi walikuwa
waliisherehekea kama sikukuu. Mtume
wa Allah (Rehma na amani ziwe juu
yake) akatufundisha kufunga swaumu ili
tujitofautishe na Mayahudi kuhusu siku
hii ya kihistoria ya ukombozi kwa watu
wa Nabii Musa na Nuh (Amani ya Allah
iwe juu yao).
Swaumu ya Ashura ilitangulia
swaumu ya Ramadhan
Kufunga siku ya Ashura kulikuja kabla ya kufaradhishwa swaumu ya Ramadhani mwaka wa pili baada ya Mtume
(Rehma na amani ziwe juu yake) kuhamia Madina. Hii ni hIkma ya Allah kuwazoesha watu kitu kabla ya kukiamrisha. Mtume wa Allah alipofika Madina,
aliwaagiza Waislamu kufunga siku tatu
kila mwezi (masiku meupe) na siku ya
Ashura. Kisha Allah akaifanya swaumu
faradh (lazima) kwa Waislamu aliposema Enyi mlioamini imefaradhishwa
swaumu kwenu (2:183).
Fadhila ya funga ya Ashura
Imepokewa kutoka kwa Bin Abbas
(Allah awe radhi naye): Sikupata kumuona Mtume wa Allah akiwa na
shauku ya kufunga siku yoyote kwa
umuhimu mkubwa kuliko siku hii, siku
ya Ashura, na mwezi huu (Bukhari).
Shauku na umuhimu huu ni kutokana
na fadhila au faida za kufunga swaumu
ya Ashura kwani Mtume wa Allah (Rehma na amani ziwe juu yake) amesema:
Kwa kufunga siku ya Ashura, nataraji
Allah ataikubali iwe kafara ya madhambi
ya mwaka uliokwisha (Muslim).
Tazama fadhila kubwa ya Allah Taala
juu yetu kwamba kwa kufunga swaumu
ya siku moja tu, unafutiwa madhambi ya
mwaka mzima uliopita. Kweli Allah ni
mwenye fadhila kubwa kabisa. Ni heri iliyoje kwa wenye kukimbilia msamaha wa
Allah?
Ashura ni siku gani?
Imam Nawawi (Allah amrehemu)
anasema siku ya kumi ya Muharram
Msingi wa nne
- Kumgeuza
adui kuwa
rafiki. Mtume
wa Mwenyezi
Mungu mara
kwa mara
alikabiliwa
na vitendo
vya uchokozi
kutoka kwa
makafiri.
Wakati
ule Quran
ilimuelekeza
Mtume
kulipa wema
kwa ubaya
aliotendewa
Q u r a n i l i m u e l e k e z a
Mtume kulipa wema kwa
ubaya aliotendewa:
Mambo mazuri na mabaya hayawi sawa. Ondosha (ubaya unaofanyiwa
kwa wema; tahamaki yule
ambaye baina yako na baina yake kuna uadui
atakuwa kama jamaa
(yako) mwenye kukufia
uchungu(41:34).
Hii ina maana kwamba
jambo jema linalotendwa
kama malipo ya ubaya uliofanywa, lina athari ya
mapigo kwa wale waliofanya ubaya. Na maisha ya
Mtume wa Mwenyezi
Mungu ni ushahidi wa kihistoria kuhusu msingi
huu.
Msingi wa tano - Kubadilisha hasi kuwa chanya. Baada ya vita vya Badr,
zaidi ya makafiri 70 walikamatwa kama mateka
wa vita. Walikuwa ni watu
walioelimika. Mtume wa
Mwenyezi Mungu alitangaza, iwapo kila mmoja
wao atawafundisha Waislamu kumi kusoma na
kuandika ataachiwa huru.
Hii ilikuwa ni shule ya
kwanza katika historia ya
Uislamu, ambapo wanafunzi wote walikuwa
Waislamu, na walimu
wote wakiwa maadui wa
Waislamu. Hapa napenda
kumnukuu mwandishi
mmoja wa Uingereza, ambaye amemueleza Mtume
wa Mwenyezi Mungu,
kama mtu aliyeweza kuona mafanikio kutokana na
hali ya kushindwa - He
was determined to write
success out of failure
Msingi wa sita - Nguvu
ya amani ni imara zaidi
kuliko nguvu ya vurugu.
Wakati Makka ilipokombolewa, wapinzani na
maadui wote wa Mtume
wa Mwenyezi Mungu waliletwa mbele yake. Walikuwa ni wahalifu wa
kivita, kwa maana zote za
neno hilo. Lakini Mtume
hakuagiza wauawe. Badala yake alisema: Nendeni,
mko huru. Matokeo ya kitendo kile cha wema yalikuwa makubwa sana.
Wengi wao walisilimu siku
ile.
Msingi wa saba - Kutokuwa na fikra mgando.
Tusifikiri kwa kutumia
vipimo viwili tu, kwamba
kama jambo haliko hivi,
basi lazima liwe vile. Kuna
jicho la tatu pia. Katika
vita maarufu vya Mutah,
Khalid bin Waliyd (Allah
awe radhi naye), kamanda
w
a inaendelea Uk 12
12
www.islamicftz.org
Misingi ya
uongozi
wa Mtume
afya yako
Pazi Mwinyimvua
Umuhimu wa kula
pamoja kama familia
inatoka Uk 1
majeshi ya Waislamu aliamua kuondoa vikosi
vyake kwenye uwanja wa mapambano, baada ya kugundua
kwamba idadi ya wapiganaji
wake ilikuwa ndogo mno, ikilinganishwa na makafiri.
Walipofika Madina, baadhi ya
Waislamu waliwapokea kwa kejeli wakiwazomea Waoga hao!
(Furrar!). Mtume wa Mwenyezi
Mungu akasema: Hapana, siyo
waoga! (Hao ni Kurrar) wenye
kuona mbali.Watu wale wa Madina walikuwa na akili mgando ama kupigana au kusalimu amri,
lakini siyo kukataa kabisa kupigana, kama alivyofanya Khalid
bin Waliyd.
Mtume ameonyesha kwamba
mara zote kuna option ya tatu,
ambayo ni kuepuka vita na
kutafuta muda wa kujipanga vizuri zaidi. Historia inatuonyesha
kwamba baada ya miaka mitatu
y a m at ay a r i s h o , Wa i s l a m u
walielekea kwenye mpaka wa
Warumi, wakapambana vikali na
kupata ushindi mkubwa.
Msingi wa nane - Kupeleka
vita kwenye uwanja tunaouweza.
Msingi huu unatokana na vita vya
Hudaybiyyah. Katika kipindi kile,
makafiri walidhamiria kuwaingiza vitani Waislamu, kwa sababu
walikuwa katika mazingira mazuri ya kushinda.
Lakini Mtume wa Mwenyezi
Mungu, kwa uangalifu mkubwa,
alikubali masharti ya makafiri na
kuingia nao mkataba. Ulikuwa ni
mkataba wa amani wa miaka
kumi. Kabla ya mkataba huo, mahali pa kukutana kati ya Waislamu na makafiri, ilikuwa ni
kwenye uwanja wa vita tu.
Baada ya mkataba maarufu wa
Hudaybiyyah kusainiwa, eneo la
mapigano likabadilika, na sasa
uwanja mpya wa mapambano
ukawa mdahalo wa kiitikadi.
Ndani ya kipindi cha miaka miwili tu, Uislamu ukashinda kwa
kishindo, kutokana na ubora wa
Itikadi yake.
Msingi wa Tisa - Kuwa yakinifu kwenye masuala yenye utata.
Wakati wa kuandika mkataba wa
Hudaybiyyah, Mtume wa
M w e n y e z i Mu n g u a l i s e m a
yaandikwe maneno haya: Hii ni
kutoka kwa Muhammad, Mtume
wa Mwenyezi Mungu. Mjumbe
wa Maqurayshi akapinga vikali
maneno hayo kuandikwa kwenye
hati ya mkataba.
Haraka sana Mtume alipoona
jambo lile lingeleta mzozo usio
wa lazima, na kukwamisha ajenda ya msingi ya Waislamu kwenye
m k at a b a u l e , a k a b a d i l i s h a
maneno yale na kuagiza iandikwe
tu: Muhammad, mtoto wa Abdullah, na mambo yakaenda
kama yalivyopangwa.
Hii ni baadhi tu ya misingi ambayo Mtume wa Mwenyezi Mungu, aliitumia na kupata mafaniko
makubwa katika harakati zake za
kusimamisha Uislamu, mafanikio ambayo wanahistoria wote
maarufu duniani wameyatambua.
13
www.islamicftz.org
uchumi na biashara
JAMAL ISSA
bima huku kampuni ya bima inakuwa kama wakala wa kusimamia shughuli hiyo.
Pili, katika bima ya kawaida
faida hujumuisha ziada (under
writing surplus) ambayo ni tofauti kati ya jumla ya mishango
(premium) iliyokusanywa kutoka kwa wateja na jumla ya
madai, fidia iliyolipwa.
Hivyo, faida hujumuisha ziada katika bima na faida kutoka
katika uwekezaji. Pia ugawaji
wa faida au ziada unategemea
uamuzi wa uongozi wa kampuni
ya bima. Kwa upande mwingine
katika takaful faida haijumuishi
ziada inayopatikana baada ya
kutoa malipo ya fidia katika
mishango (premium). Pia
mkataba wa takaful ndio unaobainisha wakati na namna ya
bima ni
utaratibu wa
kundi la watu
wenye maslahi
ya pamoja
kudhaminiana
au kujilinda
kwa pamoja
kutokana
na majanga
fulani kwa
kuunda mfuko
maalumu
unaochangiwa
kutoka katika
rasilimali zao
How could a man, from being illiterate, become the most important
author, in terms of literary merits, in the whole of Arabic literature?
How could he then pronounce truths of a scientific nature that no other
human being could possibly have developed at that time?
Tafsiri: Inawezekanaje mwanadamu kutoka hali ya kutokujua kusoma na kuandika awe mwandishi muhimu kuliko wote kwa mujibu wa sifa za kitaaluma katika fasihi yote ya kiarabu? Inawezekanaje wakati huo kutamka hakika za kisayansi ambazo hakuna mwanadamu mwingine angeweza
kuzivumbua zama hizo?. (The Bible, the Quran and Science, 1978, p 125)
14
Sheikh Mohammad Issa
Choma moto
majahazi. Ilikuwa
ni amri kwa
Waislamu kutoka
kwa kamanda
wa majeshi
yaliyovuka
bahari ya
Mediterania kwa
lengo la kuiteka
Hispania au
Andalusia kama
inavyojulikana
katika historia ya
Uislamu.
Hatua hii ilifuatia mapambano
ya miaka mingi kati ya majeshi ya
watawala wa Andalusia enzi hizo
na yale ya Waislamu kutoka Magharibi na Kaskazini mwa Afrika.
Waislamu walivuka bahari kuiteka Andalusia ili kuzuia mashambulizi mapya dhidi yao.
Tariq bin Ziyad alikuwa amefaulu kutia nanga mahali penye
milima paitwapo Jabal Tariq
(Mlima wa Twaariq) hivi leo kwa
kumbukumbu ya jina lake. Kuficha historia hii iliyotukuka ya
Waislamu, wazungu wakapaita
Gilbrater.
Huo ulikuwa mwaka 711 Miladia sawa na mwaka wa 92 Hijriya, enzi za utawala wa bani
Umayya uliotawala dola kubwa ya
Kiislamu kutokea Damascus
(Dameshqi) nchini Syria. Kilikuwa ni kipindi cha dola ya Kiislamu kupanuka hadi China na India.
Mara tu baada ya majahazi yaliyowabeba Waislamu kutia nanga,
walijikuta wakikabiliwa na jeshi
kubwa la maadui zao. Tariq bin
Ziyad akaona dalili za hofu toka
kwa wapiganaji wake. Hapo ndipo
Tariq bin Ziyad alipofikia maamuzi yake ya kuchoma moto majahazi waliyotumia kuvuka bahari
na kila kilichomo ndani yake.
Baada ya hapo, Tariq bin Ziyad
akatoa hutba kali yenye mguso wa
aina yake kwa kusema: Ndugu
zangu katika imani, tuko hapa
kulieneza neno la Allah. Maadui
wako mbele yenu na bahari nyuma yenu. Na hamna chakula wala
maji ila kile mtakachokiteka kutoka kwa maadui zenu kwa panga
zenu. Kwa hiyo hapa ni aidha ushindi au kufa shahidi.
Allahu akbar! Hiki kilikuwa
kilele cha kumtegemea Allah na
azma ya kupigana kwa ajili yake
kilichooneshwa na Tariq bin Ziyad. Kwa wapiganaji katika jeshi
lake, kuitii amri ya kamanda wao
kuyachoma moto majahazi yenye
kila kitu chao kilikuwa kilele cha
utii.
Tariq bin Ziyad alikuwa mtu
wa kabila la Ulhasa katika waberiberi (Berbers) aliyeingia katika
Uislamu kutoka nchini Algeria.
makala
www.islamicftz.org
iliwapa utulivu.
Tariq bin Ziyad akamuomba
Jemadari Musa bin Nusair
nyongeza ya wapiganaji na akamtumia wapiganaji 7,000 chini ya
kamanda Taarif bin Maalik Naqiy
ambaye mji wa Tarifa nchini Hispania leo unabeba jina lake.
Kabla Taarif na jeshi lake
hajafikia Waislamu, vita vikaanza
na Waislamu wakawakabili maadui kishujaa. Majeshi mawili, lile
la Waislamu na lile la makafiri
yakakabiliana katika vita vya
Guadalete ambapo Mfalme Roderic alishindwa na kuuawa mwe-
15
www.islamicftz.org
Hispania
fanikiwa kuikalia kwa miaka 750 inaingia katika historia ya vita duniani zama za kati.
Athari ya utawala wa Kiislamu Hispania
Kabla ya Waislamu kuingia Hispania, watawala
wake walikuwa watu kutoka nchi za Skandnavia waitwao Visigoths. Mnamo karne ya tano Miladiya, hawa
Visigoths waliiteka Hispania na kuweka utawala wao
mji mkuu ukiwa Toledo.
Kwa kuwa hawakuwa wastaarabu wajuzi wa kutawala, walikaribisha Kanisa la Roma mwaka 565
kuendesha mambo ya utawala. Kanisa likapata kibali
cha kueneza Ukristo na kukusanya kodi.
Watu wakawa katika tabu kubwa, wakilipa kodi
mara mbili moja kwa watawala na nyingine kwa kanisa.
Kulikuwa na Wayahudi wengi Hispania, kipindi cha
watawala Waislamu Wayahudi waklipata mateso
makubwa sana.
Kwanza walinyimwa haki ya kumiliki ardhi na pili
walikatazwa kuabudu kwa dini yao ya kiyahudi. Walipojaribu kupinga hali hiyo, kanisa likawapa mateso zaidi.
Mwaka 707 Mfalme Vietza alipoonesha kuwahurumia Wayahudi, viongozi wa kanisa walimpindua na
kumweka madarakani Mfalme Rodriguez. Wayahudi
wanaume wakatiwa utumwani na wanawake wao kufanywa masuaria majumbani.
Utawala wa haki wa Waislamu
Mara baada ya Waislamu kuiteka Andalusia (Hispania), haki ikatawala. Hakuna mali ya wenyeji iliyotaifishwa. Waislamu waliwatendea watu wote kwa haki,
wakiwemo Wayahudi, isipokuwa waliweka mfumo wa
kodi wenye uadilifu ambapo waliolipa ni wenye uwezo
tu.
Wakiongozwa na Quran na Sunna ya Mtume (Rehma na amani iwe juu yake), Waislamu waliingiza ustaarabu wa Kiislamu Ulaya na popote majeshi ya Waislamu yalipokwenda yalipokelewa kwa mikono miwili
na wakazi wa maeneo hayo.
Utawala wa Waislamu ukafanya Hispania kuwa nchi
ya kistaarabu iliyojaa haki, uadilifu na elimu. Mtumwa
yeyote aliyeingia katika Uislamu aliachwa huru mara
moja. Idadi kubwa ya wahispani awakaingia katika dini
ya Uislamu. Watu wa dini mbali mbali wakiwemo Waislamu na Wayahudi waliruhusiwa uhuru wa kuabudu
kwa mujibu wa dini zao. Siyo hivyo tu kila mwenye
elimu, ujuzi na maarifa aliruhusiwa kupata ajira katika
kuhudumia jamii.
Vituo na vyuo vya elimu vikafunguliwa huko Toledo
na Cordoba na yeyote aliruhusiwa kuchukua elimu
bure. Magwiji wa elimu za hisabati, jiografia, kemia,
baiolojia na unajimu wakazalishwa kutoka vyuo vikuu
huko Toledo na Cordoba.
Chini ya Waislamu, Hispania ikawa alama ya sayansi, utamaduni na ustaarabu katikati ya Ulaya iliyokuwa
katika zama zijulikanazo kama zama za giza. Mirefeji ya
maji ilichimbwa, mazao mapya yakaingizwa na kuinua
uchumi wa Hispania.
Miji ikakuwa na idadi ya wakazi kuongezeka. Mji wa
Cordoba ukawa kitovu cha elimu Ulaya nzima na hadi
kufikia karne ya 10 Miladiya, mji huo ulikuwa na wakazi
wapatao Milioni moja yaani Manispaa.
Mwanahistoria mmoja Mkristo anaandika: Waislamu walianzisha ufalme ule wa Cordoba uliokuwa fahari
ya enzi za zama za kati, zama ambazo wakati Ulaya nzima ilikuwa imezama katika ujinga na vurugu, mji huo
ulikuwa nuru ya elimu na ustaarabu ikiuangazia ulimwengu wa magharibi.
Khalifa Walid bin bin Marwaan aliwaalika Jemadari
Musa bin Nusair na Tariq bin Ziyad mjini Damascus.
Lakini walipofika walimkuta akiwa mahututi. Aliwashukuru na kuwapa sehemu ya mali waliyoileta
kutoka katika mapato waliyokusanya.
Khalifa Walid alipofariki, Suleiman bin Abdulmalik
akamfuatia katika utawala. Tariq bin Ziyad alifariki
mwaka 720 Miladia. Historia ya Uislamu na ulimwengu haiwezi kamwe kumsahau Tariq bin Ziyad.
Kuaminiana na 2015
kuepuka khiana
Na Iddi Jengo
16
makala
www.islamicftz.org
Na Yusuph Amin
ugha ya vitendo ina nguvu zaidi kuliko maneno. Maana yake ni kwamba
vitendo vina nguvu zaidi ya maneno.
Na hii ni njia bora zaidi ya ulinganiaji
dini kwani Mtume Muhammad (Rehma na
amani ya Allah ziwe juu yake alikuwa mbora
wa tabia (Husnul Khuluuq).
Tabia njema ni kati ya sifa muhimu zaidi
ambazo hupelekea kuibuka mahaba katika
mahusiano ya kijamii.Tabia njema pia ndio
silaha aliyoitumia Mtume (Rehma na amani
ya Allah ziwe juu yake) katika kulingania
jambo lililopekea hata wasiokuwa Waislamu
kuvutiwa na mwenendo wake na hatimae
kusilimu.
Kulithibisha hilo ni pale Allah Taala anaposema: Basi ni kwa sababu ya rehema
itokayo kwa Mwenyezi Mungu ndio umekuwa laini kwao. Na lau ungelikuwa mkali,
mwenye moyo mgumu, bila ya shaka wangelikukimbia (3:159).
Hata hivyo jambo linalosikikitisha katika
zama tulizonazo ni kushuhudia baadhi ya
Waislamu kutosheka kwa kuwa na majina
mazuri ya Kiislamu na kudhani majina yao
yatawapa mafanikio pasipo kutendea kazi
mambo yaliyoamrishwa na dini na mbaya
zaidi ni kujenga matumaini ya kupata malipo
mema akhera bila kufanya kheri yeyote hapa
duniani.
Kimsingi, mafanikio na ubora wa mwanadamu hutokana na maadili na tabia njema
na kinyume chake ni kwamba, jamii ambayo
huwa haina maadili na kuwa mbali na mafundisho ya dini huwa katika mkondo wa
kuangamia kimaadili.
Tafiti mbalimbali zinaonesha kuporomoka na kuangamia kwa mataifa mengi
duniani hakutokani tu na migogoro ya
kijeshi, kisiasa au kiuchumi bali hutokana na
kutoweka kwa maadili bora. Kwa maana nyingine naweza kusema misukosuko katika
misingi ya kimaadili ni mambo ambayo
huangamiza jamii kuliko uharibifu unaosababishwa na majanga ya asili kama vile matetemeko ya ardhi.
Samuel Smiles, mwandishi maarufu wa
Uingereza aliwahi kuandika: Ustawi na upungufu wowote katika maisha unatokana na
nguvu za dhati na uwezo wa kifikra au kimaumbile wa mwanaadamu. Ukweli ni
kuwa mafanikio na ufanisi wa mtu kwa kiasi
kikubwa hutegemea maadili bora na ukarimu wao kwa wengine.
Kutokana na Uislamu kutofautiana na
dini nyingine katika kipengele cha maadili na
tabia njema, taarifa za miaka ya hivi karibuni
zinaonesha idadi isiyowahi kutokea ya
Waingereza, takribani wote wakiwa ni wanawake, wanaingia kwa wingi katika Uislamu katika kipindi ambacho kuna migawanyiko mikubwa kabisa ndani ya makanisa ya
Anglikana na Katoliki.
Tathmini ya mabadiliko haya imesababisha kutabiriwa kuwa Uislamu utakuwa kwa
haraka sana na kuja kuwa dini kubwa yenye
nguvu katika nchi hii ya Uingereza.
Katika kipindi cha miaka 20 ijayo, idadi
ya Waingereza watakaosilimu italingana au
itashinda idadi ya jamii ya wahamiaji wa Kiislamu walioleta dini hii hapa nchini, alisemaRose Kendrick, ambaye ni mwalimu wa
mafunzo ya dini katika shule maalum ya Hull
na mtunzi wa kitabu cha kiada cha muongozo wa Quran.
Anasema: Uislamu ni dini kubwa duniani kama ilivyo kwa kanisa la Katoliki. Hakuna mtu anayeweza kudai kuwa dini husika ni
mali yake. Uislam pia unaenea kwa kasi
kubwa katika bara hili na Amerika kwa
ujumla.
Katika makala hii nitaangazia jinsi Uislamu unavyomtaka Muislamu kujikita na tabia
njema ambayo ni nguzo muhimu katika
kuendeleza Uislamu kwani Quran inatueleza
jinsi tabia ya mtume rehema na amani ya Al-
Ulinganiaji bora ni
hiyo kwa upole na lugha ya laini. Shughuli nyingi za kilinganiaji hazina budi kufungamana
na tabia njema kwa walinganiaji wake na
ndio maana nasema vitendo vina nguvu zaidi
kuliko maneno. Bahati mbaya wengi tumekosa hili. Kusema usichokitenda ni katika
hatari iliyo kubwa mbele ya Allah Taala anaposema: Enyi mlio amini! Kwa nini mnasema msiyo yatenda? (61:2).
Licha ya kuwa ni dini iliyosheheni desturi
zinazokubaliana na akili na kumpa mtu uongofu unaoupa nuru moyo, Uislamu pia ni dini
inayobeba maendeleo yanayofaa kwa hali,
mahala na zama zote na kwamba sheria yake
(sharia) inakidhi hali na mahitaji yote ya jamii
katika nyanja zote za maisha lakini haya yote
yamekosa mashiko kuokana na wengi wetu
kuwa wazungumzaji bila kuonesha matendo
ya kile tunachokizungumza.
Ukweli ni kwamba, maadili yetu na sheria
vimepoteza chanzo pekee cha nguvu yake,
yaani dini. Hii imetokana na jamii ya Kiislamu kuthamini na kutukuza tamaduni za nchi
za kimagharibi jambo linalopelekea watu wa
baadhi ya jamii ya Kiislamu hususan vijana
wa kike na kiume kuathirika zaidi na wimbi
hili la umagharibi.
Nimalizie kwa kusema Waislamu makini
wanafahamu kuwa propaganda dhidi ya
sharia za Kiislamu kama mauaji yanayotekelezwa na makundi ya kigaidi kama IS na
Boko Haraam si chochote bali ni udanganyifu wa nchi za Magharibi. Hivyo, katika kuuthibitisha ulimwengu kuwa Uislamu ni dini
ya maadili na tabia njema hatuna budi kuiga
mazuri yaliyofundishwa na Uislamu na si
vinginevyo.
Kwa mtazamo wa watu wenye busara kuzidisha vitendo vinavyoashiria tabia njema za
Uislamu ni bora zaidi kuliko hata mazungumzo ya muda mrefu yahusuyo dini kwani
ukiangalia riwaya mbalimbali utagundua
kuwa Mtume (Rehma na amani ya Allah
ziwe juu yake) alitenda wema kwa ubaya hata
kwa wasio Waislamu walipomkosea jambo
lililopekea wengi wao kuukubali Uislamu.
Jambo la muhimu ni kushikamana na
matendo mema yaliyoamrishwa na dini
kwani tukifanya hivyo hata wale wanaopandikiza mbegu za chuki juu ya Uislamu
watakosa hila na mbinu chafu katika kuupiga
vita Uislamu na Waislamu hivyo kudidimiza
azma yao.
makala
www.islamicftz.org
IDDI jengo
atika muendelezo
wa makala zetu, leo
tunaanza kuutafiti
Uislamu katika sura
yake halisi na namna wenyewe
unavyojieleza. Kwanza, ninukuu maneno ya msomi wa kimagharibi ambaye sasa ni Muislamu safi, bwana Hofman
Murad aliyejaribu kuuelezea
Uislamu.
Murad alisema: Nilianza
kuuona Uislamu kupitia macho yake yenyewe (Uislamu)
imani iliyokuwa haijapotoshwa, imani nzuri ya kuamini mungu mmoja na
atakaye baki kuwa mmoja,
ambaye Yeye ni wa pekee, ambaye ndiye Mkusudiwa, ambaye hakuzaa wala hakuzaliwa, wala hana anayefanana
naye hata mmoja ukilinganisha na miungu ya kikabila,
kimila na utatu.
Murad anaendelea: Quran
imenionesha mwono ambao
uliokuwa rahisi kuonekana na
kueleweka. Taarifa za kiasili za
Quran, mafundisho yake
yenye maadili zilinivutia sana
na kuwa ndio kitu kizuri na
bora kama dhahabu. Hivyo
hakukuwa na nafasi ya kunishawishi nisiamini ukweli wa
utume wa Muhammad. Wale
wanaouelewa uasili wa mwanaadamu hawawezi
kushindwa kuamini hekima
isiyo na mwisho aliyopatiwa
b i n a d a m u k u t o k a kw a
Mwenyezi Mungu katika njia
ya Quran.
Huo ni ushuhuda wa Murad, msomi mkubwa na mwanadiplomasia aliyeshika nafasi
nyingi. Kimsingi Uislamu ni
dini sahihi pekee inayostahiki
kuwa chaguo la kila mwanadamu mwenye akili timamu
kwa sababu zilizo wazi.
Kwanza, Uislamu ni dini ya
Mwenyezi Mungu, aliyemuumba mwanadamu kwa lengo
maalumu. Ni muumba pekee
anayejua mahitajio halisi ya
mwanadamu na ni yeye pekee
anayejua njia sahihi ya kumfikisha mwanadamu kwenye
lengo lake la maisha kwa ushahidi wa Quran.
Allah Taala anasema: Bila
ya shaka dini mbele ya
Mwenyezi Mungu ni Uislamu.
Na w a l i o p e w a k i t a b u
hawakukhitalifiana ila baada
ya kuwajia ujuzi, kwa sababu
ya uhasidi ulio kuwa baina
yao. Na anayezikataa Ishara za
Mwenyezi Mungu basi hakika
Mwenyezi Mungu ni Mwepesi
wa kuhisabu. Na pindi
wakikuhoji, basi sema: Mimi
nimeusalimisha uso wangu
kumwelekea Mwenyezi Mungu, na kadhaalika walio nifuata. Na waambie walio pewa
Kitabu na wasio na kisomo:
Je! Mmesilimu? Wakisilimu
basi wameongoka. Na
wakikengeuka basi juu yako ni
kufikisha ujumbe tu. Na
Mwenyezi Mungu ni Mwenye
kuwaona waja wake (3:19-
17
Uislamu
ni dini ya
kusimamia
haki, usawa
na uadilifu
katika jamii.
Miongoni
mwa mambo
yanayo
vuruga
amani
ulimwenguni
ni kuwepo
kwa dhulma
katika jamii
na dhulma
haiondoki
mpaka haki
iwepo katika
jamii
18
www.islamicftz.org
www.islamicftz.org
19
Mwenyekiti wa taasisi ya The Islamic Foundation (TIF) Aref Nahdi (kushoto) akiwa katika kipindi maalum cha kuhamasisha Amani katika Tv Imaan katikati ya wiki,kulia ni
Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo Sheikh Ibrahim Twaha na katikati ni mwendesha kipindi hicho ambaye pia ni Msimamizi Mkuu wa Tv hiyo Sheikh Chembea.
20
Tariqwww.islamicftz.org
bin
Ziyad: Shujaa
wa Kiislamu
aliyeiteka
Uk 14
6 muharram 1437, jumatatu oktoba 19 - 25, 2015
Yusuph Amin
di na matamanio ya nafsi na
uharibifu kwani lengo lake ni kutangaza na kueneza vitu vya
anasa kwa sura ya usasa.
Kwa mfano, vipo vipindi maalum vya televisheni na maudhui
katika mitandao ya intaneti vinavyotangaza mitindo ya mavazi ya
kike na kiume isiyokubalika si tu
kwa mujibu wa dini ya Uislamu
bali hata katika tamaduni zetu za
kiafrika. Bahati mbaya ilioje
kuwa jamii imekuwa inaiga
mitindo hiyo ya mavazi kwa
hutolewa na kuchapishwa na The Islamic Foundation, P.O.Box 6011 Morogoro, Tanzania E-mail: imaanmedia3@gmail.com