Professional Documents
Culture Documents
www.islamicftz.org
Operesheni tokomeza
madrasa yaanza
Sheikh Mussa
Kundecha
Wachache
wajitokeza
hijja 2015
Na Suleiman Magali
Head office, Lumumba Street, Opp: Viwanja vya Mnazi Mmoja, P. O Box 779 Dar es Salaam, Tanzania
Tell: 255 22 2182482/ 255 222184419, Fax: 255 22 2181424, E-mail: info@Binslum.com
habari
Niqab marufuku
Congo Brazaville
Na Mashirika ya
Habari
amlaka nchini
Congo Brazaville
zimepiga marufuku watu kuvaa
mavazi yanayofunika sura zao
yakiwemo ya Kiislamu kama
niqab na burka katika maeneo yenye mikusanyiko ya
watu.
www.islamicftz.org
nyakati za swala
Na. MJI
1 DAR ES SALAAM
2 ZANZIBAR
3 TANGA
4 MOROGORO
5 MTWARA
6 ARUSHA
7 DODOMA
8 MBEYA
9 KIGOMA
10 MWANZA
11 KAGERA
FAJR
5:13
5:12
5:12
5:23
5:18
5:22
5:27
5:40
5:48
5:34
5:39
DHUHUR ASR
12:21
3:42
12:20
3:42
12:21
3:43
12:29
3:51
12:21
3:42
12:33
3:55
12:35
3:56
12:45
4:07
12:57
4:19
12:46
4:07
12:51
4:13
MAGHARIB
6:17
6:17
6:19
6:24
6:12
6:33
6:31
6:39
6:55
6:47
6:52
ISHAA
7:24
7:24
7:26
7:31
7:21
7:41
7:39
7:47
8:02
7:54
8:00
Serikali yaipongeza
The Islamic Foundation
Na Mwandishi wetu
ujumbe wa The Islamic Foundation ulioongozwa na katibu wa taasisi hiyo, Sheikh Ally
Ajirani, huku viongozi wa kiserikali, akiwemo
Sheha, Diwani na kamati nzima ya uongozi wa
kijiji wakishirikiana bega kwa bega na taasisi
hiyo katika ugawaji wa misaada hiyo.
Sheikh Ajirani alisema, The Islamic Foundation ilikusanya fedha hizo kupitia michango
iliyokusanywa kupitia Radio Imaan na Televisheni Imaan na kisha kununua chakula ambacho kiligawiwa moja kwa moja kwa waathirika.
Vyakula vilivyogawiwa ni mchele, sukari,
unga wa ngano, mafuta ya kula, pamoja na
vinywaji baridi na biskuti kwa ajili ya watoto.
Tuliona wengi waliotoa misaada walichangia vifaa vya ujenzi, lakini sisi tuliona watu
waliharibikiwa makazi na mazao yao, na hivyo
tukaamua tusaidie upande huu uliosahauliwa,
alisema Sheikh Ajirani.
Afyais natural
source of sweet
drinking water
from underground stream
which is blended
with essential
minerals to support and aid perfect metabolism.
WATERCOM LIMITED
P.o. Box 20409, Plot N.4005, Kisarawe11 area
Temeke,Daresalaam, Tanzania
www.watercomtz.com, E-mail:info@watercomtz.com
Mwakilishi wa The Islamic Foundation Pemba, Sheikh Ahmed Masoud (kulia) akiwa na
msaada wa vyakula tayari kuvushwa kwenda kisiwa Panza kwa ajili ya waliopatwa na
maafa visiwani humo. (na mpiga picha wetu)
habari habari
www.islamicftz.org
Wanafunzi wa
Madrasa
Rahmatul
Islamiyya,
Vingunguti jijini
Dar es Salaam.
Na Abdulhakim Abdalla
Nsobya.
ya Ukristo.
Katika makala yake hiyo pia, Rais
Museveni, ameandika kuwa hata nchini Somalia kwenyewe yalipo makao
makuu ya wanamgambo wa AlShabaab sio Waislamu wote wanaowaunga mkono Al-Shabaab.
Napenda pia kuwashauri wale
ambao uchambuzi wao si wakina na
uko kinyume na ukweli, wahalifu nchi-
3
usoni kwa kuwa vitendo vya kukamatwa kwa walimu hao hutokea katika
misikiti na madrasa, jambo ambalo ni
kuingilia uhuru wa dini na kuabudu.
Amesema, anachokiona ni hofu ya
serikali kudhani mafundisho wanayoyapata vijana katika dini yana lengo la
kuwaandaa kupambana nao, jambo
ambalo si sahihi. Alisema madrasa hufunza elimu ya dini kwa lengo la kumjua
Allah na jinsi ya kumuabudu.
Ustadhi wa madrasa ya TarbiyatulIslamiyya, amelaani hatua za kamata
kamata za masheikh wakati mwalimu
mkuu wa madrasa hiyo, Sheikh Awadhi Adam, alisema ingawa hajawahi
kupata mtihani kama huo, amekuwa
akisikia vitendo hivyo vikifanyika huko
mikoani.
Sheikh Adamu alisema, vitendo
hivyo vinapaswa kukemewa na
kuongeza kuwa vikiachwa hivihivi vitazalisha matatizo na migogoro kati ya
Serikali na Waislamu.
Kauli ya mwanasheria:
Gazeti la Imaan lilimtafuta Wakili,
Yahya njama, kutaka kujua msimamo
wa sheria juu ya kadhia ya kukamatwa
kwa walimu wa madrasa, ambapo alieleza kuwa kufungiwa kwa madrasa
hizo kunatokana na kutozingatia sheria
za nchi.
Wakili Njama alisema, Tanzania
haina sheria yoyote inayozungumzia
masuala ya madrasa na kwamba mambo hayo ni masuala yanayohusiana na
dini na si vinginevyo.
Hakuna sheria yoyote hapa nchini
inayotoa maelekezo ya jinsi ya kuziendesha madrasa, na kama katiba inavyosema mambo ya dini yatasimamiwa
na wahusika, kwani Serikali haina dini,
alisema wakili Njama.
Wakili Njama pia amesema, kitendo cha jeshi la Polisi kuwakamata watoto wadogo na kuwapeleka mahabusu
ni kosa kisheria, kwani watoto wale hawana makosa yoyote.
Kuwakamata watoto wadogo na
kuwapeleka mahabusu kunakiuka sheria mbali mbali za mtoto zilizopo hapa
nchini, na hata hivyo mtoto yule hana
kosa. Kama kuna kosa basi ni la mzazi
aliyempeleka kwenda kusoma katika
madrasa hizo, aliongeza Wakili Njama.
Njama amesema kuwa, vitendo vya
jeshi la Polisi kuwavizia walimu wa madrasa nyakati za usiku ni kinyume cha
sheria, kwani shughuli za madrasa hizo
zinajulikana na si sawa na kundi la
wauza bangi na wauza pombe.
Kwa mujibu wa Ustaadh Abubakar
wa Kondoa, uvamizi wa polisi haufanyiki tu kwa madrasa na vituo vya kuhifadhisha Quran, bali pia kwenye shule
za Kiislamu za awali na hata sekodnari.
Mwaka jana mimi na viongozi
wenzangu tulikwenda Shinyanga
kutembelea shule moja ya Kiislamu
mkoani hapo ili kujifunza wenzetu wanavyoendesha shule ya
UK 5
sehemu ya magaidi wa Al-Shabaab,
Museveni aliadika.
Uchambuzi huo wa Rais Museveni
unakuja katika kipindi ambacho
kumekuwa na kampeni katika nchi
kadhaa za Afrika Mashariki za kukandamiza Waislamu kwa kisingizio cha
kupambana na ugaidi. Katika harakati
hizo za danganya toto za kupambana
na ugaidi muonekano wa nje ikiwemo
mavazi ya kanzu na kilemba, pamoja
na madrasa zinazotoa elimu ya Kiislamu (Madrasa) vimekuwa kigezo cha
kuwalenga Waislamu na hivyo kukandamiza haki zao za kikatiba.
www.islamicftz.org
kutoka misikitini
Fanyeni uadilifu kuitafuta nusra ya Allah
Na Nassoro Abei,
Morogoro
Waislam nchini wametakiwa kufanya
mambo mema, ikiwemo kuwasaidia viumbe
vya Allah visivyojiweza ili wapate nusra
kutoka kwa Muumba wao.
Hayo yamesemwa na Sheikh Hassan
Ahmad wakati akitoa khutba ya swala
ya Ijumaa katika msikiti wa Haqi uliopo
mtaa wa Karume, mkoani Morogoro.
Moja ya mambo yanayopelekea
Muislamu kupata nusra ya Allah ni kuwasaidia watu dhaifu na wasiojiweza, kwani watu hao wapo karibu na
Allah wakimuomba tahfiifu juu ya
matatizo yanayowasibu, alisema
Sheikh Hassan.
Katika khutba hiyo, Shekhe Hassan
aliongeza kwamba, sababu nyingine
ya Waislamu kupata nusra ya Allah ni
kufanya uadilifu baina yao na wenzi wao
katika maisha yao ya kila siku.
Sheikh Hassan alisema, Waislamu
wamejisahau kufanya uadilifu na kuwaachia wasio Waislamu, na hivyo
kuikosa nusra ya Allah Subhaanahu
Wataallah.
tujikumbushe
Na Mwandishi Wetu
wezi wa Rajab
umesheheni matukio muhimu ya
kiimani na kihistoria ya Kiislamu. Miongoni mwa
matukio muhimu zaidi ya Kiislamu yaliyotokea katika mwezi
wa Rajab ni tukio la Israa na
Miraaj.
Hili inaaminika lilitokea
mwezi wa Rajab mwaka wa 10
tangu Mtume apewe utume,
sawa na 620 Miladia. Ingawa
kuna ikhtilafu baina ya wanawazuoni kuhusu tukio hili kutokea mwezi wa Rajab, ni katika
tukio hili zilifaradhishwa swala
tano kwa Waislamu.
Tukio jingine muhimu kwa
Waislamu ni lile lililosimuliwa
katika Surat Tawba la msafara
wa kivita wa Mtume kwenda
Tabuk katika mwaka wa tisa
tangu Mtume ahamie Madina.
Mtume (Rehma na amani ziwe
juu yake) alitoka na jeshi la watu
30,000 kulikabili jeshi la Warumi ambao hatimaye waliogopa
na kukimbia. Huu ulikuwa
mwanzo wa Uislamu kuenea
duniani kote.
Tukio jingine katika historia
ya mapambano kati ya haki na
batili ni kutekwa mji wa Jerusalem na ardhi iliyokuwa chini ya
watu wa vita vya msalaba (crusaders) mwaka 583 Hijriyyah
sawa na 1187 Miladia.
Ukombozi huu wa ardhi
takatifu ya Baitul Muqaddas ulifanyika chini ya kiongozi na
jemedari wa mfano katika Uislamu, Jemedari Salah ad-Din
Yusuf bin Ayyub maarufu katika vitabu vya historia vya kimagharibi kama Saladin. Wengi
watakumbuka kitabu cha visa
vya Alfu Lela Ulela (Alfu Layla
wa layla yaani mausiku elfu
na Mosul (Iraq).
Ingawa angeweza kuishi katika majumba ya kifahari kama
walivyokuwa wakiishi maamiri
wengine wa utawala wa waturuki, yeye alichagua kuishi maisha rahisi akijichanganya na
wanajeshi wake.
Alikuwa mchaMungu kiasi
kwamba mwanahistoria
maarufu Ibn Athir alimsifu akisema: Alikuwa zawadi waliyopewa Waislamu na Allah.
Haikuwa ajabu basi yeye kuwa
kinara wa mapambano dhidi ya
makafiri waliokalia ardhi takatifu ya Baitul Muqaddas.
Akiambatana na wapiganaji
wake waliokuwa na ari na nidhamu ya hali ya juu, huku
wakimtegemea Allah pekee,
Imadu d-Din (nguzo ya dini)
Zink alianza kuzikomboa ardhi
za Waislamu akianzia na Edessa mwaka 1144.
Edessa ulikuwa mji ambao
wapiganaji wa msalaba wakiutumia kama ngome (base) yao
nchini Syria katika uvamizi wao
wa kwanza wa Baitul Muqaddas. Baada ya kutekwa na Zink,
sasa ukawa ngome ya kupanga
mashambulizi ya kuikomboa
ardhi takatifu.
Wakati Zink akijiandaa kuukomboa mji wa Jerusalem
(Baitul Muqaddas), mwaka
www.islamicftz.org
inatoka uk 1
Akitoa
mfano,
Dk. Twaha
ameliambia
gazeti la
Imaan kuwa
mwaka jana
Tanzania
bara
pamoja na
visiwani,
ilipeleka
jumla ya
mahujaji
2,500 tu;
huku nafasi
500 zikikosa
watu.
kubwa kwa kundi hilo, ikiwemo kuongeza imani, uadilifu na kuimarika kwa
maadili mema katika maisha yao yote,
alisema Dokta Twaha.
Faida za Hijja:
Operesheni tokomeza
kiislamu.
Tukiwa hotelini tulikofikia tukapewa habari kwamba Mkuu
wa shule hiyo na walimu kadhaa
walivamiwa usiku wa manane na
polisi wenye bunduki na kukamatwa kisha kupelekwa kituo
cha polisi.
Polisi walidai wana shaka
kuwa shuleni pale panatolewa
mafunzo ya ugaidi. Walimu wale
hawakuachiwa mpaka siku tatu
zilipopita, wakatakiwa kuendelea
kuripoti kila siku kwa muda wa
wiki mbili na hakuna mashitaka
yaliyofunguliwa dhidi yao.
Taarifa tulizozipata kutoka
Kondoa ni kwamba, polisi walifika madrasa moja ya kuhifadhisha
Quran na kuwahoji walimu na
wanafunzi kisha wakaenda shule
ya Kiislamu mjini hapo na kufanya hivyo hivyo.
Alipoulizwa anadhani lengo la
kamatakamata na polisi kuvamia
vituo vya Kiislamu ni nini? Ustadh Abubakar alijibu nadhani
lengo ni kuwatisha wazazi wanaopeleka wanafunzi katika shule
za Kiislamu ili shule hizo zikose
wanafunzi na hatimaye zife.
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kwamba hivi sasa Waislamu
katika maeneo tofauti tofauti
nchini wakionekana wamevaa
kanzu na wamefuga ndevu au
wamevaa hijab, wamekuwa wakifwatiliwa na kubughudhiwa na
polisi.
Ziko habari za Ustadh mmoja
aliyekuwa njiani kupeleka posa
inatoka uk 3
Hijja ya 2015:
hutolewa na kuchapishwa
The Islamic Foundation,P.O.Box 6011 Morogoro, Tanzania,E-mail: imaanmedia3@gmail.com
mhariri mtendaji: 0715 559 944, Mhariri: 0786 779 669, afisa masoko: 0785 500 502
TOVUTI: www.islamicftz.org
tahariri / uchambuzi
Madrasa ambazo zimekuwapo kwa miaka mingi, leo zinaonekana kuwa zimeanzishwa
kinyume na sheria! Pia kuna
madai kuwa mitaala ya hizi madrasa haieleweki na kwamba
watoto wenye umri wa kwenda
shule waliopo madrasa hawaendi shule. Hizi ndio baadhi ya hoja
zinazotumika kuhalalisha kampeni hii.
Kwanza, tunauliza, je kuna
sheria inayoongoza uanzishwaji
wa madrasa hapa Tanzania?
Kama sheria hiyo ipo, ni wazi
kuwa watu wengi hawaijui na
ndio maana madrasa zimekuwapo miaka nenda rudi bila
taratibu za usajili.
Lakini, hata kama sheria hiyo
nasaha za wiki
Yusufu Ahmadi
www.islamicftz.org
Dr. Maurice
Bucaille:
Ulinganishi
kamilifu wa
Quran na
elimu ya sasa
unatupelekea
kutambua
uwiano kati ya
viwili hivi
kama
ilivyowahi
kuonyeshwa
mara kwa
mara.
KUFUATANA
NA SHERIA
NCHINI
SAUDIA,
TAREHE YA MWISHO
YA MPYA
KUJISAJILI
NA KUTUMA
TAREHEYA
YAMAHUJAJI
MWISHO KWA
YA KUJISAJILI
NA KUTUMA
MAJINA
NJIA YA MTANDAO
KWA
MAJINA
YA MAHUJAJI
KWA NJIA
YA MTANDAO
KWA
MWAKA
HUU NI TAREHE
8 JUNI2015
SAWA NA
MWAKA HUU
NI
TAREHE
8
JUNI2015
SAWA
NA
TAREHE 20 SHAABAN 1437
TAREHE 20 SHAABAN 1437
MAHUJAJI
WOTE
MNAOMBWAKUJISAJILI
KUJISAJILIMAPEMA
MAPEMA
MAHUJAJI WOTE MNAOMBWA
ILIKUWA
KUWANA
NAUHAKIKA
UHAKIKAWA
WASAFARI
SAFARIYA
YAHIJJA
HIJJA
ILI
makala maalum
www.islamicftz.org
Historia ya Msumbiji
NA ABUU MAYSARA
Mwaka 1971
tofauti za
kifiqh kati
ya Sheikh
Abubacar
Ismael
aliyehitimu
Chuo Kikuu
Madina na
masheikh
wa twariqa
kuhusu
jinsi ya
kusindikiza
jeneza kimya
au kwa sauti
ilitoa fursa
iliyosubiriwa
kwa hamu
na Wareno
kuwadhibiti
Waislamu.
Waislamu walivyotumika - 3
Kutokuelewana Waislamu mwanya kwa watawala
Muumini
wa dini
ya
Kiislamu
akiwa
msikitini
mjini
Maputo,
Msumbiji
www.islamicftz.org
Msafara
wa Israa
na Miiraji
Na Sheikh Shabani Mussa
Aya zinazozungumzia safari ya Miiraj katika Quran zinapatikana katika Suurat Annajm (53:1-18). Allah anasema: Naapa kwa
nyota zinapoanguka. Kwamba mtu wenu
(huyu Nabii Muhammad) hakupotea (kwa
ujinga) wala hakukosa, (hali ya kuwa anajua), Wala hasemi kwa matamanio (ya nafsi
yake), hayakuwa haya (anayosema)
isipokuwa ni wahyi uliyofunuliwa (kwake),
Amemfundisha (Malaika) Mwenye nguvu
(sana) Mwenye uweza (53:1 - 4).
Allah anaendelea: Na yeye (huyu) Jibril
akalingana sawa sawa. Na yeye yu katika
upeo wa kuona (katika mbingu kwa juu kabisa). Kisha akakaribia (kwa Mtume) na
akateremka. Ukawa (ukaribu wao) baina ya
upinde au karibu zaidi. Na akamfunulia
huyo Mtumwa wake (Allah) hayo aliyoyafunua, Moyo haukusema uwongo uliyoyaona. (Moyo wake ulisadikisha haya
yaliyotokea)(53:5 - 11).
Allah anaendelea: Je ! mnabishana naye
juu ya yale anayoyaona (daima)?Na
(Mtume) akamuona(jibril) mara nyingine
(kwa sura ile yake ya Kimalaika katika usiku
wa Miiraji). Kwenye Mkunazi wa kumalizikia mambo yote). karibu yake ndiyo kuna
hiyo Bustani, (pepo) itakayokaliwa (maisha
na watu wema), Kilipoufunika Mkunazi
huo kilichoufunika (katika mambo ya kiajabu ya mbinguni), Jicho halikupepesa wala
halikuruka mpaka (uliowekewa), Kwa yakini aliona (Mtume Muhammad) mambo
makubwa katika alama, (Qudra) za Mola
wake)(53:5 - 19).
Quran na vitabu vyote vilivyokusanya hadith za Mtume (Rehema na amani ziwe juu
yake) na vile vya Sira kwa pamoja vinathibitisha kufanyika kwa safari hii ya Israa na Miiraji, lakini tofauti kubwa iliyopo mbele ya
wanazuoni wa kale na sasa ni katika siku,
mwezi na mwaka iliyotokea safari hii
adhimu.
Imamu Ibnu Kathir(Allah amrehemu)
katika kitabu chake Al-bidayatu Wannihayatu 3/135 ananukuu kutoka kwa: Ibnu
Asakir kwa kuzitaja hadith nyingi zinazoihusu safari hii ya Israa na Miiraji kuwa,
Ilitokea awali ya kuteuliwa kwa Mtume
Muhammad (Rehema na amani juu yake).
Amma Ibnu Is-haq yeye alieleza kufanyika
kwa safari hii ilikuwa ..Kiasi cha Miaka
kumi baada ya kuteuliwa kwa Mtume Muhammad (Rehema na amani juu yake).
Na mapokezi ya Imamu Bayhaqiy kutoka
kwa Mussa bin Uqbah kutoka kwa Zuhriyakisema: Mtume alifanya safari ya Israa
Mwaka mmoja kabla ya kuelekea Madina.
Na kauli kama hiyo imetolewa pia na: Ibnu
Lahiyahkutoka kwa Abi As-wad naye kutoka kwaUr-wah.
Kisha Imam Hakimakapokea kutoka
kwa Al-As swammi naye kutoka kwa Ahmad bin Abdil-Jabbar naye kutoka kwa Yunus bin Bukayr naye kutoka kwa Asbaat bin
Nasri naye kutoka kwa Ismail Suddiy.
kuwa:Mtume alifaradhishiwa swala tano
Beytul Maqdis kwenye usiku aliopelekwa Israa miezi kumi na sita kabla ya kuhama.
Na kwa kauli ya Assuddiy safari ya Israa
ilifanyika katika mwezi wa Dhul-qaadah
wakati kwa kauli ya Zuhriy na Urwah safari
ya Israa ilifanyika Mwezi wa Rabiul-awwal.
Na amesema Abubakarbin Abi Shaybah:
Alitusimulia Athumani naye kutoka kwa
Saidbin Miynaa naye kutoka kwa Jabir na
Ibnu Abbas kwa pamoja walisema: Mtume
alizaliwa katika siku ya Jumatatu ya tarehe
kumi na mbili Mwezi wa Rabiul-awwal katika mwaka wa Ndovu,ndicho kipindi alichopewa Utume, alichopelekwa Miiraji
mbinguni, na ndani ya mwezi kama huo alihama na kufa. Lakini katika riwaya hii kuna
mkatiko. Na kauli hii ndio iliyochaguliwa na
kutumiwa na Al-hafidhu Abdul-ghaniybin
10
www.islamicftz.org
Je hutenguka udhu wa
mwanamke aliyemkosha najisi mwanawe?
Je huchanguka udhu
wa mtu aliyeosha
najisi ya watoto
wake?
Swali: Iliulizwa kamati
ya kudumu ya fat-waa:
Mimi nina wana wadogo,
na nilishatawadha, na nikaosha najisi za wanangu, je
Je kugusa utupu
wa
mtoto
mdogo ku-
natengua udhu?
natengua udhu?
Jawabu: Hili halitengui udhu,
kwani upepo huo haukutoka mahali
pa najisi, kama utokavyo ushuzi
kwenye njia ya haja kubwa. (Fataawa
na Rasailu za Sheikh Uthaimin
4/197).
Swali: Iliulizwa kamati ya kudumu ya fat-waa: Mwanamke anaposwali, na kwenda rukuu na sujudu,
na mara nyingi (hali hii hutokea) anaposujudu na anapoketi baina ya sijida mbili, na anapoketi kwa ajili ya kutoa shahada, hutokwa na upepo
kwenye utupu wake, kiasi cha kusikiwa na walio pembezoni mwake, je kitendo hicho kinabatilisha swala ya
mwanamke? Na wakati mwingine
hutokwa upepo kidogo mno kiasi cha
Je kumgusa mwanamke
kunatengua udhu?
afya yako
Pazi Mwinyimvua
kupoteza maisha pale iwapo kinyesi kitaganda sana katika utumbo na operesheni
ikachelewa kufanywa kwa mgonjwa.
Mtu akikosa vyakula vya protini mwili
utanyongea na atapata matatizo ya moyo
na viungo vingine kushindwa kufanya kazi.
Vyakula vinavyotokana na wanyama ni
chanzo kizuri cha protini kutokana na
kuwa na virutubisho vyote muhimu vya
amino acids.
Karanga, maharage na soya pia vina vitamini kwa wingi. Samaki ni chanzo kizuri
cha protini na mafuta mazuri kiafya, na
yana Omega 3 inayosaidia kumwepusha
mtu kupata magonjwa ya moyo. Hata
hivyo, ulaji wa nyama nyekundu kama vile
ngombe, mbuzi, kondoo na ngamia ziliwe
isizidi nusu kilo kwa wiki.
Miaka milioni mbili iliyopita binadamu alikuwa anakula vyakula vya asili kama
nyama, samaki, matunda, mbogamboga,
jamii ya karanga, mbegu na baadhi ya
vyakula vya mizizi. Zaidi ya hayo, watu walikuwa wanatembea sana kwa miguu, wanafanya kazi za kutoka jasho, hawakai chini muda mrefu na walikuwa wanaishi kijamii na kusaidiana.
Siku hizi katika miji, watu wengi wanatumia vyakula vilivyosindikwa viwandani
ambavyo mara nyingi vina sukari, mafuta
na chumvi nyingi. Vitu hivyo ni hatari sana
kwa afya. Pia, vyakula vilivyosindikwa viwandani vina kemikali zinazovifanya
vyakula hivyo visiharibike haraka. Kemikali hizo zinaweza kudhoofisha afya ya
mlaji.
Zaidi ya hayo, watu wengi siku hizi katika miji wanakaa sana ofisini, wanakaa
sana kutazama televisheni na kutumia
simu, kuingia katika intaneti, au kucheza
michezo kwa kutumia kompyuta au simu.
Vilevile, watu wengi hawalali vya kutosha, licha ya kuwepo ushahidi wa kisayansi
unaomtaka kila mtu mzima kulala kwa saa
7-10 kwa siku ili mwili ufanye kazi vizuri.
Matokeo ya kutolala vya kutosha watu
wengi wana msongo wa mawazo wa kudumu.
Salama ya mwanadamu wa sasa ni kurudi katika asili, kama mwili wake ulivyoumbwa. Mwanadamu anatakiwa ale vyakula vya asili vilivyo sawa na mpango wa vinasaba na baolojia. Pia, kula kwa kiasi, kupunguza chumvi, mafuta, sukari na kemikali katika vyakula. Kurudi katika asili pia
ni pamoja na kutembea kwa miguu baadhi
ya nyakati, kuishi pamoja na kusaidiana,
na kuushughulisha mwili kwa kufanya
mazoezi au kazi za kutoka jasho.
0754 654 900
11
www.islamicftz.org
uchumi na biashara
JAMAL ISSA
Hayo ni kwa
kuwa wamesema: Biashara
ni kama riba
(Quran 2:275)
Sifa njema na shukran
anastahiki yule ambaye
ametukamilishia dini
yetu na akairidhia kuwa
utaratibu kamili wa maisha yetu. Rehma na amani zimfikie kipenzi chetu
mtume Muhammad (Rehma na amani ziwe juu
yake) pamoja na wanaofuata muongozo mpaka
siku ya mwisho.
Ndugu mpezi msomaji
karibu tena katika mfululizo wa makala zetu juu
ya biashara na uchumi
katika Uislamu.
Katika makala ya leo
tutadurusu juu ya riba.
Somo hili kwa kweli ni
pana na halijulikani na
wengi, kwani riba ipo katika namna nyingi sana.
Uchumi wa Kiislamu
umejengwa juu ya msingi
madhubuti usiojikita katika riba. Allah ameharamisha riba na akahalalisha biashara kama anavyotufahamisha katika
Qurani tukufu: Lakini
Mwenyezi Mungu ameihalalisha biashara na
ameiharimisha riba
(2:275).
Kwa uzito wa uharamu wa riba, Mtume (Rehma na amani ziwe juu
yake) akaichagua kuwemo katika mambo ya
msingi ya kutuonya katika khutba yake ya
mwisho.
Baada ya kumshukuru
Allah alianza khutba kwa
kusema: Enyi watu!
Nisikilizeni maneno yangu vizuri, kwani sidhani
kama baada ya mwaka
huu nitakuwa pamoja
nanyi. Hivyo sikilizeni
kwa makini nitakayoyasema na (maneno haya)
mfikishieni kila asiekuwepo hapa leo.
Baada ya kusema
Moja ya taasisi
ya fedha ya
Kiiskamu
ambayo hutoa
mikopo bila
riba.
Mwenyezi
Mungu
huiondolea
baraka
riba, na
huzibariki
sadaka. Na
Mwenyezi
Mungu
hampendi
kila mwenye
kukana na
afanyae
dhambi
(2:276)
Allah alivyohusianisha riba na biashara. Kwanini hapa tena anahusianisha riba na sadaka?
Kwa kweli mtoaji sadaka hutoa
bila ya kutaraji kunufaika na chochote kama ziada, isipokuwa
kumridhisha Allah kwa kuwasaidia viumbe wake na kuwatizama kwa jicho la rahma, lakini riba
12
www.islamicftz.org
ncha ya kalamu
Sheikh Muhammad Issa
i mara nyingi
tumesikia
Msichanganye
dini na siasa
huku sababu kubwa inayotolewa ni kwamba dini haina nafasi katika maisha ya
kijamii ya nchi ya kisekula,
bali ni jambo linalomhusu
mtu binafsi.
Katika nchi za kidemokrasia ya kweli siyo tu dini na
wana dini hujihusisha na siasa, bali kuna vyama vya kisiasa vya kidini vinavyoshiriki
katika uchaguzi na hata kutawala na hakuna jambo linaloharibika. Nchi hizo zina
maendeleo makubwa tu kiuchumi, kijamii na kiteknolojia.
Baadhi ya nchi hizo barani
Ulaya na majina katika vyama
husika katika mabano ni Albania (Christian Democratic
Party), Ubelgiji (Christian Social Party), Ujerumani (Christian Democratic Union (CDU)
ambacho kinasemwa kuwa ni
mshirika wa karibu wa Chadema.
Barani Asia, nchi zenye vyama vya kisiasa vya kidini ni Indonesia, nchi yenye idadi kubwa
ya Waislamu duniani (Christian
Democratic Party) na Samoa (Samoan Democratic United Party).
Kwa Afrika, nchi zenye vyama
vya kidini ni Rwanda Christian
Democratic Party, Afrika ya Kusini
vyama saba vya kidini- African
Christian Democratic Party, United Christian Democratic Party,
Christian Democratic Alliance, Al
13
www.islamicftz.org
Mahusiano ya kibinadamu
USTAADH HABIB HAMIM
Maana ya ulemavu
na nje ya nchi hususan Sudan ambako niliishi na kusoma kwa muda mrefu.
Ulemavu kwa ujumla unatafsiriwa
kuwa ni kukosa au kushindwa kuwa
na fursa ya kushiriki katika maisha ya
kawaida ya kijamii kwa kiwango sawa
na wengine kwa sababu za kimaumbile, kiakili au sababu za kijamii. Ulemavu unaweza kuwa katika maeneo
yafuatayo: kuona, kusikia, akili, viungo kama mkono au mguu, kuongea,
tabia au ulemavu mchanganyiko.
Kwa hiyo basi, ulemavu unaweza kupelekea ugumu wa kutembea, uzito
wa kujifunza, utamkaji wa shida, na
kujitenga katika eneo fulani la tabia.
Ulemavu mwingine huhitaji uangalizi maalum.
Kwa upande mwingine, mtu
mwenye ulemavu ni mtu mwenye udhaifu au upungufu wa viungo, fahamu au akili kwa muundo wa kudumu,
na ambaye uwezo wake wa utendaji
kazi umepungua kutokana na vikwazo vya kimtazamo na kimazingira.
Mtu mwenye ulemavu anaweza kuwa
ameathirika kimwili, katika kuona,
kiakili, kisaikolojia, kielimu au kimawasiliano na atakuwa amepungukiwa
na uwezo wa kujisimamia mambo
yake ya kawaida katika mazingira ya
kijamii. Mfano wa ulemavu ni kukosa
uwezo wa kuona. Hii ndio maana ya
ulemavu, wiki ijayo Mola Muumba
akipenda, tutazungumzia aina
mbalimbali za ulemavu.
habibmitwe@yahoo.co.uk
0718 561 149
mapitio ya vitabu
Kitabu: Al Fusuul Fii Mustwalahi
Hadiithi r-Rasuuli
Mwandishi: Haafidh Thanaau-llwaahi Zaahidy
Mfasiri: Sheikh Muhammad Issa
hazina yetu
14
www.islamicftz.org
Na Yusuph Amin
Je wanazuoni wanamzungumziaje?
Abas Kilima (kulia) akiwa na Sheikh Abubakar Mwilima katika moja ya hafla za Kiislamu.
Abas Kilima
Historia yake:
watoto / matangazo
www.islamicftz.org
Kona ya watoto
ZAHRA EBRAHIM
Asiya, Maryam, Khadija na Fatima ni wanawake wanne walio bora zaidi katika Uislamu.
Ubora wao unatokana na matendo yao makuu
katika kupigania dini ya Mwenyezi Mungu
Subhaanahu wa Taala na kutafuta radhi zake.
Hebu tuone nini kinawafanya wanawake
hawa wawe maalum kiasi cha kubashiriwa kuingia katika pepo ya Allah yenye kila aina ya
starehe, makazi ya kifakhari, bustani tulivu,
mavazi, vyakula, mito ya vinywaji na neema nyingi ambazo dunia haijapata kuzishuhudia.
15
USAJILI
S.2401
KWA WASICHANA TU
MASOMO
USAJILI
S.4384
Mwanza
Arusha
Kigoma
Tabora
Moro
Dsm
Masafa ya Imaan FM
1
2
3
4
5
6
Daresalaam
Morogoro
Arusha
Mwanza
Kigoma
Tabora
104.5 Mhz
96.3 Mhz
90.8 Mhz
105.6 Mhz
92.5 Mhz
101.6 Mhz
7
8
9
10
11
12
Mbeya
Dodoma
Ruvuma
Mtwara
Zanzibar
Pemba
90.3 Mhz
102 Mhz
94.2 Mhz
90.9 Mhz
104.5 Mhz
104.5 Mhz
Mbeya
Ruvuma
Mtwara
Ukweli
kuhusu
riba
Uk 11
15 Rajab 1436, jumatatu May 4 - 10, 2015
ardhi, lengo likiwa kushughulikia
mahitaji ya kijamii kwa wanawake.
Baada ya kupata ardhi baraza huwataka akina mama hao kuorodhesha mahitaji yao ili kupata urahisi
wa kuyashughulikia.
Mayasa alisema ardhi inaweza
k u t u m i k a k u a n z i s h a m i ra d i
mbalimbali kwa manufaa ya wanawake na Uislamu, ikiwemo zahanati, vituo vya wanawake, shule,
miradi ya kilimo na kumbi za mikutano.
Katika kuhakikisha kazi za baraza zinasonga mbele, Mayasa amesema baraza limeweka mikakati
mbalimbali kwa siku za baadae kwa
kuhakikisha wanawake wa Kiislamu wanainuka kiuchumi, ikiwemo
kuanzisha Benki ya Kiislamu ya
Wanawake.
Lakwamua
maelfu ya wanawake kiuchumi
Lajipanga
kuanzisha benki
ya Kiislamu
Baraza la Wanawake
wa Kiislamu Tanzania
Na Yufuph amin
Changamoto:
Akizungumzia changamoto zinazolikabili baraza, Mayasa amesema, kutokana na wingi wa taasisi
wapo wanaodhani kuanzishwa
baraza kuu la wanawake kumevunja shughuli zao. Lakini alitaka taasisi nyingine zisiwe na wasiwasi
kwani baraza halimzuii mtu kutoka
taasisi moja kujiunga na nyingine
kwa wakati mmoja.
Aidha amezitaja changamoto
nyingine kuwa ni baadhi ya mitazamo ya watu wa dini kuhusu mwanamke imekuwa kikwazo katika kufikia malengo. Wajumbe hukosa
ruhusa kwa waume zao kwa kuona
ni watu wa kukaa nyumbani na hawaruhusiwi kufanya shughuli za
dini.
Changamoto nyingine ni nguvu
ndogo ya uchumi, hivyo baraza
linakaribisha sadaka na zaka kutoka kwa waumini mbalimbali.
Pia amewataka wanawake kuondosha dhana kuwa hakuna
umuhimu wa kutafuta elimu, na
kuongeza kuwa, matokeo ya
kukiukwa kanuni za kitabibu kwa
magonjwa ya wanawake kutibiwa
na madaktari wanaume yametokana na dhana hii potofu.
Mayasa amesema, wao kama
baraza wamekuwa wakifanya semina katika vyuo vya kitabibu vya
IMTU na Kairuki ili kuwashawishi
wanafunzi wa kike wasome kwa
juhudi na watumie elimu yao kuisaidia jamii.
Licha ya kuwepo changamoto
hizo, baraza limepata mafanikio
katika uungwaji mkono kwa kiasi
kikubwa, si tu kwa wanawake, bali
hata kwa taasisi za wanaume.
Akifafanua hilo Mayasa amesema, wanapata ushirikiano kutoka
kwa Chama cha Wanataaluma wa
Kiislamu (TAMPRO) katika masuala ya kitaaluma. Pia taasisi ya The
Islamic Foundation, hususan kupitia vyombo vyake vya habari, ambapo vimekuwa vikisaidia kutoa
matangazo ya makongamano
pasipo gharama yeyote.
Katika suala la ujenzi wa misikiti, taasisi ya Islamic Relief Organization ya nchini Kuwait imekuwa
ikisaidia ujenzi wa misikiti pindi
wanapohitajia.
Mayasa amewataka wanawake
wa Kiislamu watambue kuwa Baraza Kuu la Wanawake ni chombo
chao na si cha mtu fulani, hivyo
wakiunge mkono kikamilifu, kwa
mali na nafsi zao katika kuipigania
dini ya Allah.
hutolewa na kuchapishwa na The Islamic Foundation, P.O.Box 6011 Morogoro, Tanzania E-mail: imaanmedia3@gmail.com