MGOMBEA jimbo la Monduli kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Namelok Sokoine, ameahidi kuendeleza yote aliyoasisi, kusimamia na kutekeleza aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Edward Lowassa.
MGOMBEA jimbo la Monduli kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Namelok Sokoine, ameahidi kuendeleza yote aliyoasisi, kusimamia na kutekeleza aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Edward Lowassa.
MGOMBEA jimbo la Monduli kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Namelok Sokoine, ameahidi kuendeleza yote aliyoasisi, kusimamia na kutekeleza aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Edward Lowassa.
MGOMBEA jimbo la Monduli kupitia Chama Cha Mapinduzi
(CCM), Namelok Sokoine, ameahidi kuendeleza yote aliyoasisi, kusimamia na kutekeleza aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Edward Lowassa. Namelok, amemtaja Edward Lowassa, kuwa ni miongoni mwa viongozi walioitendea mengi jimbo hilo katika kipindi chake cha uongozi. Nitajidanganya nikibeza kazi kubwa na nzuri iliyofanywa na Lowassa hapa Monduli kwa kuboresha huduma za elimu, afya, miundombinu na nyingine nyingi. Lowassa, baba yangu Edward Moringe Sokoine na Lepilal Moloimet ni alama muhimu kwa wana Monduli kwa mchango wao kwa jamii yetu, alisema Namelok, mtoto wa waziri mkuu wa zamani, Edward Moringe Sokoine Akizungumzia uamuzi wake wa kuwania ubunge, Namelok alisema Lowassa ndiye alinitambulisha kwa wazee wa mila na wana Monduli kuwa ninafaa kurithi kiti chake cha ubunge. Sitaiangusha imani hiyo kwa kuwatumika wana Monduli kwa kuendeleza yote aliyoanzisha, kusimamia na kutekeleza, Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni za ubunge jimbo la Monduli jana, alimtaja Lowassa kuwa ndiye mwalimu wake kisiasa na kuahidi kumheshimu, kushirikiana naye kwa faida na maslahi ya wana Monduli huku akibainisha kuwa mahusiano yao hayawezi kutetereshwa na harakati au tofauti za kiitikadi kisiasa. Uhusiano kati ya familia ya Lowassa na hayati Edward Moringe Sokoine umejengwa katika misingi imara isiyoweza
kutetereshwa na masuala ya kisiasa au wanaojipitisha kuomba
uongozi kwa kutumia jina la Lowassa, alisisitiza Namelok Akitaja vipaumbele vyake iwapo atachaguliwa kuwa mbunge wa Monduli, Namelok alisema ataboresha huduma za kijamii ikwemo elimu, afya, mawasiliano, miundombinu akianzia pale alipofikia Lowassa. Nitatumia uwezo, nguvu na ushawishi wangu wote kushughulikia na kumaliza kero ya migogoro ya ardhi kati ya wafugaji, wakulima wakubwa, hifadhi za taifa na jeshi la wananchi (JWTZ), ambao kwa mapenzi ya taifa baba yangu aliwapa eneo la mafunzo ya kijeshi kwa sharti kuwa litatumiwa pia kwa ajili ya malisho lakini hivi karibuni wafugaji wanazuiwa, alisema Namelok. Kwa upande wake, mgeni rasmi katika uzinduzi huo, Dk Asha Rose Migiro aliwaomba wakazi wa Monduli kuwachagua wagombea wa CCM kuanzia ngazi ya udiwani na ubunge, lakini akisita kutaja nafasi ya urais na jina la mgombea wa CCM, John Magufuli kutokana na hisia za wananchi waliohudhuria mkutano huo kuonekana kumuunga mkono mgombea wa Chadema, Edward Lowassa. Chagueni madiwani na mbunge wa CCM, Namelok Sokoine pamoja na viongozi wengine wa CCM, alisema Dk Migiro bila kutaja nafasi ya Urais wala jina la Magufuli Akizungumzia kitendo cha wananchi waliohudhuria mkutano huo kuonyesha kumuunga mkono Lowassa katika nafasi ya urais kilimlazimisha mwenyekiti wa kamati ya kampeni za CCM jimbo la Monduli, Paul Kiteleki kuwataka viongozi na makada wa
chama hicho kuepuka suala la kura za urais na kutaja jina la
Magufuli ili kuepuka kuchafua hali ya hewa inayoweza kukinyima chama hicho hata zile za udiwani na ubunge. Kwa wana Monduli, Lowassa ni nguzo muhimu. Wanampenda na kumheshimu kwa kuwatendea mema mengi wakati wa uongozi wake kama mbunge. Tunalazimika kufanya kampeni kwa tahadhari na kupima upepo linapofikia suala la kuomba kura za urais Monduli, alisema Kiteleki alipoulizwa alichowaeleza wananchi kwa lugha ya Kimaasai. Kiteleki alilazimika kuingilia kati kutuliza hali ya hewa iliyokaribia kuchafuka baada ya makada wa CCM Amina Mollel na Victor Njau kuomba kura za urais na kumtaja Magufuli katika mkutano huo na kupokewa na kelele za Lowassa Lowassa.na ishara ya vidole viwili inayotumiwa na Chadema Kuhusu hali ya kisiasa Monduli, Katibu wa umoja wa vijana wa ccm (UVCCM), mkoa wa Manyara, Ezekiel Mollel ambaye ni mzaliwa wa Monduli alisema ingawa chama hicho tawala kina wasiwasi wa kura za urais kutokana na imani ya wananchi kwa Lowassa, lakini kina kinauhakika wa kushinda viti vya udiwani katika kata 16 kati ya ishirini za jimbo la Monduli kutokana na wananchi wengi kuendelea kukiamini CCM na wagombea wake wa ubunge na udiwani.