You are on page 1of 16

www.annuurpapers.co.

tz

Sauti ya Waislamu

(22) AHLU SUNNA WAL JAMAA


Inawatangazia Waislamu wote kuwa imeanza maandalizi yake kwa ajili ya HIJJA 2013 kwa lengo la KUONGEZA UFANISI KATIKA IBADA ZA MAHUJAJI WETU kwa gharama za Dola 4300. Lengo letu ni kukamilisha mipango yetu kabla ya kumaliza mwezi mtukufu wa Ramadhani.Tafadhali wasiliana nasi ifuatavyo: Tanzania Bara: 0717224437; 0777462022;Unguja: 0777458075;Pemba: 0776357117.

Ponda awatembelea Farid gerezani


Kiza kinapozidi kuwa kinene, alfajiri inaingia

ISSN 0856 - 3861 Na. 1081 RAMADHAN 1434, IJUMAA , JULAI 26- AGOSTI 1, 2013 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=

Waislamu wanatambua msimamo wenu wa kupigania haki, pia wanaamini kukamatwa kwenu ni ukweli wa methali isemayo kiza kinapozidi kuwa kinene, ndivyo kupambazuka kunavyo karibia.

RAIS wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein (katikati) akiteta na Makamu wake, Maalim Seif Sharif Hamad. Kulia ni Sheikh Farid Hadd.

Walimu tatizo sugu hijab mashuleni Kisa cha Veer Pratap Singh Waraka wa Serikali wazidi kupuuzwa na Masheikh wa Uamsho
Wazazi watakiwa kusimama kidete
akizungumzia kadhia mbalimbali za uvaaji wa Hijjab kwa wanafunzi wa kike katika shule za msingi. Alisema walimu wengi wamekuwa wakitoa maelekezo kwa wanafunzi wa Kiislamu, wakitaka wavae Hjab wanazotaka wao ambazo zipo nje ya sheria na mafundisho ya Kiislamu. Ust. Ngalongela, alisema amekuwa akifutilia suala la uvaaji wa vazi hilo kwa wa f u n z i wa K i i s l a m u katika shule zilizopo Kata ya Kawe, na kukutana na vikwazo kutoka kwa walimu wa shule hizo. Awali Ust. huyo alika Inaendelea Uk. 2

SHEIKH Azzan Khalid

Na Bakari Mwakangwale I M E E L E Z WA k u w a wenye ufahamu wa kutafsiri Hijjab ni Waislamu na si walimu, ambao wamekuwa wakiwabughudhi wanafunzi wanaovaa vazi hilo kwa mujibu maelekezo ya dini yao wanapokuwa shuleni. Hayo yamebainishwa na mratibu wa Islamic Education Pannel, wilaya ya Kinondoni, Jijini Dar es Salaam Ust. Rajabu Ally Ngalongela, wakati

Ya Malala, Taliban na Uamsho ..


Zanzibar ya leo ni yenye kuhuzunisha Inatatanisha, hujikanganya yenyewe

Hii ndiyo nchi yangu: Ukweli, Haki itawale Waliodaiwa si mapapai hayataoza, wajitizame Wanafanya nini kuleta Haki Sawa kwa Wote

Zanzibar ya leo ni nchi yenye kuhuzunisha; haisikitishi tu, bali inahuzunisha. Ni nchi yenye kutatanisha, wakati mwingine hujikanganya yenyewe. Na viongozi wake? Naona hata haina haja ya kuwaeleza walivyo. Uk. 7

2
www.annuurpapers.co.tz

Tahariri/Makala
Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM. E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk Osi zetu zipo: Manzese Tip Top Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam

RAMADHAN 1434, IJUMAA JULAI 26 - AGOSTI 1, 2013


kujuta kufanya maasi, kuazimia kuwa hatorudia tena maasi hayo. Lakini inavyoonekana mlevi ni kama anamcheza shere Allah (sw) aliyetukuka kwa kuacha mwezi wa Ramadhan peke yake, akidhani kwamba Allah ni wa Ramadhan pekee. Kwa ajili hiyo, hajatimiza masharti ya kukubaliwa toba, hivyo kuingia katika kughadhibikiwa na Allah aliyetukuka. Hivi sasa baa hazijachangamka, ikiisha Ramadhani zifurika! Wa n a o f u r a n i w a l e wa s i o k u wa Wa i s l a m u lakini wakasita kwa kuhishimu ibada ya Waislamu, au ni wale wale wanaotubu katika Ramadhani na wakarejea kuasi kwa waliyotubia baada ya Ramadhani? Waislamu tujitathmini. Ramadhani ni chuo cha mafunzo ya ucha Mungu. Heri yetu kukiyatenda kwa vitendo yale tuliojifunza ndani tya Ramadhani hata baada ya kwisha Ramadhani ili tufuzu katika ucha Mungu uliokusudiwa. Tunawatakia Ramadhani Mubarak. JIBU: Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho. Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu unywaji wa pombe kwa Muislamu anayefunga wakati wa Ramadhaan.

AN-NUUR

AN-NUUR S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786


MAONI YETU

Waislamu wajitathmini katika Ramadhani na baada yake


K AT I K A U i s l a m u , tumeamriwa kufunga mwezi Mtukufu wa Ramadhani, kutekeleza nguzo ya nne ya Uislamu. Kuitekeleza nguzo hiyo ni wajibu kwa Waislamu kwa kuwa lengo lake kubwa ni kuwafanya kuwa wacha Mungu katika maisha yao. Funga ni semina ya kumwezesha Muislamu kupata mafunzo ya kutenda mema na kuacha mabaya, ili kumfanya mja awe katika kufuata amri za Allah katika kipindi kingine chote cha miezi mingine. Ni kwa msingi huo, ndio maana tunashuhudia kwa kiasi kikubwa biashara za kupeleka watu katika maaswi zimepoa. Baa hazifuriki, kumbi za rumba zimelala, misikiti inafurika, stara inaonekana kwa sehemu kubwa ya akina mama. Haya ni baadhi tu ya mabadiliko tunayoyaona kwa kiwango fulani katika kipindi hiki cha mfungo wa Ramadhani. Hali hii imezua maswali na dhana kwa Waislamu na Wasiokuwa Waislamu. Wapo wanaodhani kuwa kudorora kwa biashara za vileo na burudani za dansi, ni kipimo tosha kwamba Waislamu ndio wahusika wakubwa wa starehe hizo. Wa p o w a n a o d h a n i kwamba mwezi mtukufu wa Ramadhani, huwa unaheshimiwa hata na wasiokuwa Waislamu. Ndio maana nao wanasita kuendelea na maasi haya ya ulevi na rumba ikiwa ni ishara ya kuheshimu ibada hiyo ya funga kwa Waislamu, japo wao si Waislamu. Na matokeo yake ndio tunaona kipindi hiki baa na kumbi za sterehe zimedorora tofauti na wakati mwingine. Hakika hapa ndipo ambapo jamii ya Waislamu tunatakiwa kujitathmini na kutafakari. Je, ni kweli kwamba wao ndio mabingwa wa maasi haya au uamuzi wa baadhi ya wasiokuwa Waislamu kusimamisha matendo hayo nao wanachangia kupoa kwa maasi haya wa k a t i wa f u n g a ya Ramadhani? Tunachukua fursa hii k u wa k u m b u s h a wa l e a m b a o n i Wa i s l a m u , ambao walikuwa walevi, wazinzi, wacheza rumba klabu za usiku, ambao wamesitisha matendo hayo kipindi hiki, kuleta toba ya kweli na kuzingatia semina hii Ramadhani, ili wasije rejea tena katika kuzichangamsha baa na starehe nyingine za kuasi na kumcheza shere Allah (sw). Hebu tutizame, mtu anayekunywa sana pombe, halafu ukifika mwezi mtukufu, Ramadhani anasimama kunywa pombe kwa sababu ya kufunga mwezi mtukufu, mwezi ukiisha anarudia pombe, nini hatima yake? Kwanza pamoja na kwamba ni kuasi, unywaji wa pombe una madhara makubwa hapa duniani na kesho Akhera. Allah aliyetukuka anasema: Enyi mlioamini! Bila ya shaka ulevi, na kamari, na kuabudu masanamu, na kupiga ramli, ni uchafu katika kazi ya Shetwani. Basi jiepusheni navyo ili mpate kufanikiwa. Hakika shetwani anataka kuweka kati yenu uadui na chuki kwa ulevi na kamari, na akuzuieni kumkumbuka Allah na kuswali. Basi je, mtaacha? (Al-Maaidah 5: 90 91). Ulevi umeelezwa hapa kama uchafu, uchafu unaofanana na kamari, kuabudu masanamu na kupiga ramli. Ulevi unatia uadui baina ya watu, chuki na unamzuia mtu kutekeleza Ibaadah ya kumdhukuru Allaah na kuswali kwa ajili yake. Mlevi mara nyingi huwa haswali na hupuuza mengi pamoja na kujiingiza

Walimu tatizo sugu hijab mashuleni


Inatoka Uk. 1 katika shule ya Kawe B, ambapo kupitia kipindi cha dini aliwahoji mabinti kwa nini hawavai hijab kama mwanafunzi mwenzao aliyetajwa kwa jina la Naima Abdulshakur. Wanafunzi hao walibu kuwa habu zao wanazo nyumbani lakini wakivaa shuleni hukatazwa na walimu. Alielezwa kuwa Naima, anavaa hivyo kwa kuwa baba yake alika shuleni hapo kumuombea ndipo aliporuhusiwa. Pamoja na ruhusa hiyo alisema, baada ya shule kufunguliwa mwezi huu wa Julai, mwanafunzi huyo alipigwa na mwalimu aliyetajwa kwa jina moja la Lymo, kwa kosa la kuvaa hab ya aina hiyo. Ust. Ngalongela, alisema walipozipata taarifa hizo, aliongozana na Ust. Rashid Nassor, ambaye ni Imam wa Masjid Ihsan, Tangi Bovu kwenda kuonana na mkuu wa shule hiyo. Alisema baada ya kumueleza tukio hilo, Mkuu wa shule alipinga madai ya kuadhibiwa mwafunzi huyo kwa sababu ya kuvaa hab. Tulimwacha, katika kipindi cha dini niliwaeleza wanafunzi wote wenye hijab kama za Naima wa va e n a wa l i p o f i k a siku ya Jumanne, (wiki iliyopita) waliovaa wote walifukuzwa. Alisema Ust. Ngalongela. Alisema baada ya kufukuzwa, alipigiwa simu ambapo yeye pamoja n a v i o n g o z i we n z a k e walikutana Masjidi Waqswa na kuamua kuwapa taarifa Waislamu kwa njia ya simu, wakiwataka wake katika shule ya Kawe B kuna kadhia ya hab. Aliongeza kuwa viongozi wa Waislamu wakiwa na wanafunzi waliofukuzwa wa l i i n g i a o f i s i n i k wa mwalimu mkuu na kuhoji tatizo lililosababisha wanafunzi hao kufukuzwa kama ni uvaaji wa hab au ni kosa jingine. Ust. Ngalongela, alisema wakiwa katika mazungumzo ofizini, nje baadhi ya walimu walipiga simu Polisi na kueleza kuwa Waislamu wamevamia shule na kuzuia walimu kufundisha. Alisema baada ya muda waliona Polisi wamefika shuleni hapo wakiwa katika gari, hata hivyo walikuta hali tulivu tofauti na walivyokishiwa taarifa. Maafande wale wa l i v yo f i k a wa l i k u t a Waislamu nje wametulia wanasubiri tutoke tuwape taarifa, ndipo walipoingia osini na kusema tumesikia hakuna amani hapa walimu wamefungiwa milango. Mkuu wa shule alisema, tunaendelea na kikao na wao wakasema basi sisi tunaondoka endeleeni. Alisema Ust. Ngalongela, akinukuu maongezi hayo. Alieleza kuwa majibu ya swali walilouliza yalikuwa kwamba wanafunzi hao walirudishwa kwa kuwa wapo nje ya sare za shule,

katika madhara makubwa sana. Ama kuhusu hilo, Mtume wa Allaah (Saw) amesema: Mwenye kunywa pombe duniani, kisha hakuleta toba, atanywima Akhera (al-Bukhaariy na Muslim). Hadithi hii inamaanisha kuwa mlevi anayaendelea na ulevi wake, na akakosa kuomba maghra kabla ya kufa kwake, hatokuwa ni mwenye kuipata Akhera. Hii inatuleta katika mashariti ya toba. Ni hakika kuwa ili toba kukubaliwa ni lazima Muislamu atekeleze masharti kadhaa. Ikiwa kosa lake linaingiliana na haki ya Allah aliyetukuka, b a s i m we n ye k u t u b i a anatakiwa atimize mashariti matatu ambayo ni kuacha maasi kabisa,

kwa kuwa sare walizokuwa wamezivaa ni tofauti na wenzao shuleni hapo. Alisema Wajumbe wa Waislamu walitoa maelezo kuhusu usahihi wa vazi hilo la hab na kubainisha kuwa, zile zinazovaliwa na wanafunzi wengi si h i j a b k wa m u j i b u wa Uislamu, bali wanafunzi wanalazimika kuvaa hivyo kutokana na walimu kuzikataa hab stahiki. Ust. Ngalongela, alisema waliwaeleza walimu shuleni hapo kuwa suala la hijab, Waislamu wana waraka wa serikali wa kuwaruhusu baada ya kudai vazi hilo kuvaliwa kwa wanafunzi wa kike wa Kiislamu mashuleni na vyuoni. Serikali iliruhusu vazi hilo livaliwe mashuleni na vyuoni, lakini kwa kuwa yenyewe haina dini, haikutoa maelekezo ya muundo wa hijab, bali tunaojua ni sisi Waislamu, walimu mnapaswa kujua hijab inavaliwaje kutoka kwa Waislamu. Alisema Ust. Ngalongela. Akibu hoja ya walimu kuwa wengi wanavaa hijab na hawafukuzwi, alisema hao wasiofukuzwa wapo nje ya vazi la hab na hao wanaowafukuza ndio haswa wanaovaa hab sahihi katika Uislamu. Ust. Ngalongela pia alipinga hoja ya walimu waliodai kuwa wanafunzi hao wapo nje ya sare na wanachafua utaratibu wa shule, akisema haiwezekani Inaendelea Uk. 4 wafukuzwe kwa hoja hiyo

Na Bakari Mwakangwale

Ponda awatembelea Farid gerezani


VIONGOZI wa Jumuiya ya UAMSHO Zanzibar, wamesema kwamba pamoja na kuzuiwa kwao Gerezani, hawana shaka kuwa ipo siku haki itasimama na hatimaye kupatikana Taifa Uhuru la Zanzibari. Kauli hiyo wameitoa mbele ya Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda, muda mfupi baada ya kukutana na viongozi hao Ijumaa ya wiki iliyopita katika Gereza la Kiinuamiguu, lililopo Mtaa wa Kilimani Zanzibar. Sheikh Ponda, alifika gerezani hapo akiwa katika muendelezo wa ziara zake anazofanya nchini na kuongea na Waislamu, baada ya kumalizika kwa kesi yake na kuhukumiwa kifungo cha mwaka mmoja nje. Akiongea na Mwandishi wa habari hizi katika osi za Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu (T), Kinondoni, Jini Dar es Salaam, mapema wiki hii alisema alifanikiwa kuonana na viongozi wa UAMSHO na kuongea nao kwa muda wa dakika 45. Alisema, Masheikh hao waliopo gerezani kwa muda wa miezi tisa sasa, wapo imara kiimani ambao walitumia fursa hiyo kumpa salamu kwa Wazanzibari huku naye akiwapa salamu kutoka kwa Waislamu wa Bara. Hawana hofu pamoja na kushikiliwa na Dola kwa muda wote huo, kwani wanachoamini wao kuwa wapo katika haki, na uimara wao unakuja kutokana na kuijua vizuri historia ya kupigania haki kuwa hata Mitume wa Mwenyezi Mungu, walipotangaza haki, walipata misukosuko na kupigwa vita na watawala. Alisema Shkh. Ponda, akielezea hali za Viongozi hao wa UAMSHO. Ponda, alisema kuwa Masheikh hao, Mselem Ali, Azan Khalid, Musa Juma pamoja nae Amir F a r i d H a d , k wa k wa u j u m l a a k i ya t a f a k a r i maongezi yao anaona ni wazi kuwa msimamo wao ni kutorudi nyuma katika kupigania haki na zaidi alidai walimuambia hawana shaka kuwa ipo siku haki itasimama na batili itaondoka Visiwani humo. Alisema, Masheikh hao, walimtaka awafikishie ujumbe Wazanzibar katika m i k u t a n o ya k e k u wa wasiache kuzungumzia haki zao za msingi wanazodai kwani kwa k u f a n ya h i v yo n d i yo kuitendea haki Zanzibar. Katika fursa hii mliyoipata ya kuwahutubia Wazanzibar na hatimae Watanganyika, waambieni msimamo wetu bado ni ule ule wa kutetea Taifa Uhuru la Zanzibari na bila shaka pia huo utakuwa ni Uhuru kwa Watanganyika pia, alisema Sheikh Ponda, akimnukuu Amir Farid Had. Sheikh Ponda alisema viongozi hao walimuagiza kutumia vema fursa ya mikutano yake Visiwani humo na hatimae Bara kwa kuinua hamasa za Waislamu huku wakimtaka kuwaelekeza kutumia vema mafunzo na misimamo waliyoitoa juu ya Taifa huru la Zanzibar. Darsa zetu bila shaka zimejenga imani na akida, vilevile zinatosha kuwa semina za kujitambua. Lakini pia tulenga hamasa kubwa na u t a ya r i wa kutetea haki hadharani. K a m a Wa i s l a m u hawatakiwi kurudi nyuma wasinyamaze hata kidogo, alisema Sheikh Ponda, akidai kuwa huo ni ujumbe kutoka kwa Sheikh Mselem Ali. Awali Sheikh Ponda, kwa upande wake aliwapa viongozi hao salamu na hisia za Waislamu wa Bara kufuatia ziara zake katika mikoa kadhaa ya Tanzania Bara zilizoandaliwa na Jumuiya na Taasisi za Kiislamu mara baada ya kutoka Gerezani. Waislamu wa Bara wanatambua msimamo wenu wa kupigania haki, pia wanaamini kukamatwa kwenu ni ukweli wa methali isemayo kiza kinapozidi k u wa k i n e n e n d i v y o kupambazuka kunavyo karibia hivyo wako pamoja nanyi. Alisema Sheikh Ponda, akirejea kauli yake mbele ya viongozi wa UAMSHO Gerezani. Katika ziara yake hiyo Visiwani humo, Sheikh Ponda, pia alipata fursa ya kuwahutubia maelfu ya Wazanzibar katika mihadhara sita iliyoandaliwa na Jumuiya ya UAMSHO katika maeneo mbalimbali ya Unguja. Akiwahutubia maelfu ya waumini walio hudhuria katika muhadhara uliofanyika Mkoa wa Mjini Maghribi Masjid Sahaba Daraja Bovu, Sheikh Ponda, aliwataka Waislamu wa Zanzibar kuchukua hadhari ya njama zinazopikwa kuvunja udugu wao kwa lengo la kuwagawa. Kwa mujibu wa Sheikh Ponda, alisema maelfu ya Waislamu waliokutana katika Msikiti wa harakati m a a r u f u k wa j i n a l a M s i k i t i wa M b u y u n i , walisema wanatafakari hatma ya viongozi wao wanaoshikiliwa na Dola kwa zaidi ya miezi tisa sasa. Msimamo kama huo u l i t o l e wa t e n a k a t i k a m k u s a n y i k o m k u b wa uliofanyika siku iliyofuata (Ijumaa iliyopita) mara tu baada swala ya Ijumaa katika Msikiti wa kwa Mpendae kwa Kicho. Kuonesha hisia zenu kama hivi bila shaka mnajenga nguvu kubwa ya p a m o j a n a wa k a t i utakapofika watawatoa tu viongozi wenu. Alisema Sheikh Ponda,

Habari

RAMADHAN 1434, IJUMAA JULAI 26 - AGOSTI 1, 2013

AN-NUUR

Walimu tatizo sugu hijab mashuleni


Inatoka Uk. 2 (juba) iliyofunika kifua cha mwanamke, nguo yenye mikono mirefu mpaka katika viganja na kushuka chini ya nyonga (Nusu kanzu). Alisema awali wazazi wengi walikuwa waoga katika kuwashonea watoto wao vazi hilo, wakihofia kubughudhiwa na walimu wa o a m a k u f u k u z wa shule. Hata hivyo baada ya muda wazazi wengi walimuelewa kutokana na kuwafahamisha kuwa Serikali ilisharuhusu uvaaji wa habu shuleni na vyuoni, hivyo ni jukumu la Waislamu kutekeleza uvaaji wa vazi hilo kwa mujibu wa sharia. A l i s e m a m wa n z o n i mwa mwaka huu watoto katika Shule ya Kawe A walianza kuvaa vazi h i l o . M wa n a f u n z i wa awali aliyeanza kuvaa kwa mujibu wa Uislamu alifukuzwa na mwalimu aliyetajwa kwa jina moja la Tugawane. Akifafanua zaidi, alisema baada ya kufukuzwa binti huyo, alipigiwa simu na wazazi wa binti huyo k u f u a t i a wa z a z i h a o kushindwa kuelewana na walimu. Naye alifika shuleni hapo kuonana na mwalimu mkuu wa shule kuzungumzia suala hilo. Baada ya kuongea naye kwa kina, Mkuu wa Shule alielewa maana halisi ya hijabu na kusema kama

akiwahutubia waumini wa Nungwi. A i d h a S h k h Po n d a , aliwataka waumini wa Nungwi kujiimarisha kwa miradi ya maendeleo kwa kutumia vizuri hazina kubwa ya ardhi waliyonayo ambayo imekuwa ikivamiwa kwa kasi kubwa na wawekezaji wa mahoteli ya kitalii, ambao kwa asilimia tisini wanaharibu utamaduni wa Mzanzibar. Sheikh Ponda, alisema Jumuiya ya UAMSHO, inatarajia kufanya muhadhara mkubwa siku ya Ijumaa (leo) katika M s i k i t i wa M b u y u n i , lengo likiwa ni kufanya majumuisho ya mihadhara iliyofanyika akiwa huko wiki iliyopita.

wakati walimu wenyewe hajui hab ni nini. Alisema baada ya mjadala wa muda mrefu na kuonekana kama somo limeelewaka, mkuu wa shule alitaka wanafunzi hao waliofukuzwa kuendelea kuvaa hivyo, lakini akitaka wasiongezeke wanafunzi wengine. Mkuu wa shule alisema, kuwaruhusu wengine sasa hivi itakuwa kuwachafua wanafunzi kwa kutofautiana katika sare, hivyo alidai tusubiri mpaka mwakani watakapoweka sheria ya hab tuliyoitaka. Alisema Ust. Ngalongela akirejea hoja za mwalimu. Hata hivyo hoja hiyo ilipingwa na Waislamu na mkuu wa shule kulazimika kukubaliana na Waislamu kuwa, ndani ya miezi miwili wanafunzi wote wa Kiislamu wawe wanavaa hab za aina moja. Kufutia matukio hayo, Ust. Ngalongela, aliwataka Waislamu kuelewa kuwa kuvaa Hjab ni Sharia ya dini yao na kwa upande wa mamlaka (Serikali) sheria ya nchi yao imeruhusu, hivyo ni jukum lao kusimamia amri hizo katika Dini na ile ya Serikali. Kwa miaka zaidi ya m i t a t u s a s a , U s t . N g a l o n g e l a a m e k u wa akitoa maelekezo sahihi ya habu kwa mujibu wa Uislamu kuwa ni nguo

ni hivyo, basi ameafiki. Alisema Ust. Ngalongela. Mkuu wa Shule hiyo ambaye alikuwa ni Mkristo, alitaka kujua nembo ya shule itakaa eneo lipi la vazi hilo, ambapo walikubalina ikae ama juu ya juba au chini kabisa mwa shati (nusu kanzu). Baada ya kuruhusiwa mwanafunzi huyo, wa l i j i t o k e z a we n g i n e waliovaa kama mwenzao, hata hivyo wanafunzi hao nao walifukuzwa na mkuu wa shule msaidizi. Ust. Ngalongela, alisema alionana na mwalimu huyo kisha kumweleza kuwa tatizo hilo walishalimaliza na Mwalimu Mkuu, lakini mwalimu huyo hakuliaki, akidai kuwa hizo sio habu zinazotakiwa shuleni. Ust. Ngalongela alieleza k u wa a l i p o s i k i M k u u wa Shule hiyo karudi kutoka safari ya msibani, alirudi na kuonana naye n a k u m u e l e z a j u u ya kufukuzwa wanafunzi wengine kwa kuvaa hab sahihi. Alisema baada ya kuongea na Mkuu wa Shule, alionyesha kushangaa na kuhoji kwa nini jambo hilo linakuwa linajirudia shuleni kwake. Ust. Ngalongela, alimweleza kuwa tatizo ni yeye mkuu wa shule, kwani baada ya kulimaliza tatizo la hab kwa mwanafunzi wa awali, hakuchukua jukumu Inaendelea Uk. 4

Umoja Nchi za Visiwa Bahari Hindi watua Zanzibar


Ni kwa ajili ya mikakati ya pamoja ya mazingira
umoja huo, uliopangwa kufanyika mwakani huko Samoa. Katika mazungumzo yao, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, aliuhakikishia ujumbe huo kuwa Zanzibar inaunga mkono hatua za kupanua umoja huo, pamoja na mipango yake ya kuhifadhi mazingira. Maalim Seif, alisema kuwa mipango ya kulinda mazingira na maliasili za visiwa vidogo, haina budi kufanywa kwa Na Mwandishi Wetu mashirikiano miongoni mwa nchi husika, kwani mipango hiyo haiwezi kufanikiwa iwapo kila nchi itakuwa na mipango yake peke yake. Alisema kwa upande wa k e Z a n z i b a r k a m a nchi ya visiwa, inatoa umuhimu wa kipekee katika kulinda mazingira ya baharini na nchi kavu, ili maliasili chache zilizopo ziendelee kulindwa na kuwanufaisha wananchi wake kikamilifu. N a y e , B w. R o n a l d Jumeau, ambaye ndiye k i o n g o z i wa u j u m b e huo ambaye ni balozi wa S e y c h e l l e s n c h i n i Marekani, alisema azma ya umoja huo hivi sasa ni kuzidisha mashirikiano na nchi nyengine za visiwa vidogo, vikiwemo hata vilivyo nje ya Bahari ya Hindi kama vile katika bahari ya Pacic. Amesema hatua hiyo itaufanya umoja huo kuwa wenye mafanikio zaidi, ambapo pia nchi hizo zitaweza kupata uzoefu mkubwa wa kulinda na kuhifadhi mazingira, na kuwawezesha wakaazi wake kuzitumia maliasili zao kikamilifu na

HABARI/Matangazo

RAMADHAN 1434, IJUMAA JULAI 26 - AGOSTI 1, 2013

AN-NUUR

Ujumbe wa Umoja wa Nchi za Visiwa vidogo katika Bahari ya Hindi umezuru Zanzibar kwa ajili ya kuifahamisha serikali ya Zanzibar juu ya mikakati ya kusimamia mazingira ya nchi za visiwa. Ujumbe huo ulioongozwa na Ronald Jumeau wa Sychelees, ulika osi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Migombani, kwa ajili ya kumuelezea mipango ya mkutano mkuu wa

Walimu tatizo sugu hijab mashuleni


Inatoka Uk. 3 binti na binti mwenyewe, wakielekea shuleni hapo, nyuma walikuwa wakifuatwa na kundi kubwa la Waislamu. Ust. Ngalongela, alieleza wakiwa ofisini kwa mkuu wa shule, m wa l i m u a l i ye m p i g a mwanafunzi huyo alitetea kuwa hakumpiga kwa sababu ya hab, bali alikuwa akimuadhibu k wa k o s a j i n g i n e n a katika kumuadhibu, ndipo alimtaka asivae kama alivyokuwa amevaa. Katika kikao hicho suala hilo lilimalizwa na msaidizi wa Mratibu Elimu Kata ya Kawe, baada ya kusikiliza k a d h i a h i yo a m b a p o Waislamu walitoa waraka wa serikali ulioruhusu uvaaji wa habu shuleni na vyuoni. Kutokana na waraka w a l i o u t o a Wa i s l a m u ni wazi vazi hili vazi l i m e r u h u s i wa , h i v yo watoto waruhusiwe kuvaliwa bila bughudha mpaka hapo patakapo kuwa na amri nyingine ya serikali kuzia vazi hilo. Alisema Ust. Ngalongela akirejea amri ya Mratibu Elimu Kata. B a a d a ya m u a f a k a huo, Mratibu wa Dini ya Kiislamu Wilaya ya Temeke aliyetajwa kwa jina la Ust. Abubakar, alitoa maelekezo ni hab ya aina gani inayotakiwa kuvaliwa na mabinti wa Kiislamu. Ust. Ngalongela, alisema baada ya kuwekana sawa na walimu wa shule hiyo ya Kawe A, wiki moja baadae kadhia nyingine ilitokea katika shule ya Msingi Tumaini Kawe, kwa mwanafunzi kufukuzwa kwa kuvaa hab sahihi. Alisema iliwalazimu kwenda shuleni hapo na walikutana pia na Mratibu Elimu Kata, ambaye walianza kuongea naye baada ya kuwauliza tatizo ni nini. Ust. Ngalongela, alipomweleza kadhia hiyo na kumfafanulia kuwa Waislamu hawalazimishi sheria za Kiislamu shuleni hapo kama inavyodaiwa, bali wanachohitaji ni haki yao ya msingi kwa vana wao hususani katika vazi la hab ambalo hata serikali imeliruhusu. Kwa mujibu wa Ust. Ngalongela, Mratibu Elimu huyo aliwataka Waislamu kuondoka kwa ahadi kuwa atawaeleza walimu wakuu wote kwa kuwa siku hiyo

la kuwafahamisha walimu wake juu ya usahihi wa vazi hilo kwa wanafunzi wa kike wa Kiislamu. Katika tukio lingine shuleni hapo, mwanafunzi mmoja alipigwa na mwalimu kisha kutakiwa kuvua hijabu yake. Kesi ya kupigwa mwanafunzi huyo ilikishwa Msikitini. Tukio lile liliwagusa Waislamu wa Kawe, baada ya kuona linajirudia mara kwa mara katika shule hiyo hiyo, taarifa zilisambazwa na waliamua kwenda shule hapo kuhoji kwa nini binti huyo apigwe kwa ajili ya hijab. Alisema Ust. Ngalongela. Alisema siku hiyo akiwa ameongozana na mzazi wa

Kongamano Masjid DAWAEL Ilala Sokoni


Baraza Kuu la Wanawake wa Kiislamu Tanzania linawaalika wanawake wote wa Kiislamu katika Kongamano litakalo fanyika Inshaallah Masjid DAWAEL Ilala Sokoni Jumamosi Tarehe 2707/2013 Saa 2:30 hadi saa 7:00 Mchana,Mada swaumu na Mmomonyoko wa Maadili. Tuzingatie Muda. Ukipata Taarifa hii Mwaambie na mwenzio. Amira Mkoa DSM

alikuwa na kikao nao, ili suala hilo lisirudie katika shule zao. Hata hivyo, baada ya kufuatiliwa katika kikao baina yake na wakuu wa shule, Mratibu huyo hakulizungumzia suala hilo kama alivyowaahidi Waislamu. Kadhia ya hab haikuishi hapo, kwani katika Shule ya Msingi Ukwamani Kawe, mwanafunzi mwingine alifukuzwa. Lakini baada ya Ust. Ngalongela kuzungumza na mkuu wa shule na kupewa waraka wa serikali unaoruhusu vazi hilo la Hjab, Mkuu huyo wa shule alimwita mwanafunzi aliyefukuzwa, kisha alimruhusu kuvaa hab hiyo lakini akimtaka akimtaka kutowaeleza wenzake.

k u z i w e z e s h a k u wa endelevu. Licha ya kuwa Zanzibar inaingia katika umoja huo kupitia Ta n z a n i a , i m e k u wa ikinufaika na miradi mbalimbali ya uhifadhi wa mazingira. Ujumbe huo pia umekutana na Waziri wa Nchi Osi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Fatma Abdulhabib Ferej, ambaye ameelezea matumaini yake juu ya Zanzibar inavyoweza kunufaika na umoja huo. Alisema Zanzibar itaendelea kutoa kila aina ya ushirikiano kuhakikisha kuwa nchi za visiwa zinafanya kazi pamoja na kujifunza mafanikio yaliyokiwa na nchi nyengine, ili kufikia malengo ya kuwa na maendeleo endelevu. Amefahamisha kuwa nchi za visiwa ikiwemo Zanzibar zimekuwa zikikumbwa na changamoto kadhaa za kimazingira, ambapo hivi sasa baadhi ya maeneo ya kilimo Zanzibar hayafanyi kazi kutokana na kuvamiwa na maji ya chumvi na kuwafanya wakulima wa maeneo hayo kutokuwa na cha kufanya. Hata hivyo serikali imekuwa ikichukua juhudi kuona kuwa changamoto hizo zinapungua.

BISMILLAHIR RAHMANIR RAHIIM

KUNDUCHI GIRLS ISLAMIC HIGH SCHOOL


DAR ES SALAAM

NAFASI ZA MASOMO KIDATO CHA TANO 2013-2014 MICHEPUO YOTE YA SAYANSI ,SANAA NA BIASHARA IPO
PCB,PCM,CBG,PGM,HGL,HGK,HKL,EGM,HE,ECA,KLA
SHULE NI YA BWENI NA KIPEKEE KWA MABINTI WA KIISLAMU KIMAADILI, KIMALEZI BORA YA KIISLAM TUNENDELEA KUPOKEA WANAFUNZI KWA KIDATO CHA TANO NA WAHAMIAJI KIDATO CHA KWANZA NA TATU 0713465437, 713515054 AU 0756082772

KWA MAWASILIANO ZAIDI:

NAFASI BADO ZIPO KWA KUSOMEA UALIMU KWA SIFA ZIFUATAO:


AWE AMAMALIZA KIDATO CHA S ITA NA KUPATA KUANZIA PRINCIPLA (E) 1 NA S UBS IDIARY (S )-1

CHUO CHA UALIMU UNUNIO

STASHAHADA (DIPLOMA)

CHETI (GRADE III A)


AWE AMAMALIZA KIDATO CHA NNE NA AMEPATA ALAMA ZIS IZOZIDI DIV IV-27 ALIYERUD IA (RES ITING) AWE NA C-4

CHUO NI CHA BWENI KWA WASICHANA NA WAVULANA ADA NI NAFUU SANA NA INALIPWA KWA AWAMU WAHI SASA NAFASI NI CHACHE NA WANANDOA WANAKUBALIWA

WAHITIMU WOTE WANAAJIRIWA SERIKALINI


KUJIUNGA NA CHUO PIGA SIMU MOJA KWA MOJA CHUONI
FOMU ZINPATIKANA KWA WARATIB U WETU NA OFISI ZOTE ZA

MKUU WA CHUO

0713 673495

KUTAYBA SACCOS MIKOANI

MSAJILI 0715 822332 0756 822332 0784 822332

RAMADHAN KAREEM

Habari za Kimataifa/Tangazo

RAMADHAN 1434, IJUMAA JULAI 26 - AGOSTI 1, 2013

AN-NUUR

Morsi agoma kula kizuizini


yenye misingi ya Kiislamu. Lakini sasa baada ya mapinduzi ya Jeshi, upinzani ambao sasa uko madarakani umekuwa ukitaka katiba ya kisekula isiyozingatia Uislamu. Katika hatua nyingine imeripotiwa kwamba maasa wa usalama wa Misri wamezivamia osi za televisheni ya Al Alam ya Iran, inayorusha matangazo yake kwa lugha ya Kiarabu jini Cairo. Mkuu wa ofisi hiyo

Rais wa mpito kufanya marekebisho ya Katiba

CAIRO Muhammad Morsi, Rais aliyengolewa madarakani na jeshi na kuendelea kushikiliwa katika mahabusu za jeshi hilo nchini Misri, ameanza mgomo wa kula. Televisheni ya Russia Today, imemnukuu kiongozi mmoja wa kundi la Ikhwanul Muslimin, Muhammad al Baltaji, akisema katika mahojiano yaliyofanywa na televisheni hiyo kuwa, Morsi ameanza mgomo wa kula mwishoni mwa wiki. Wakati huo huo Waziri Mkuu wa serikali ya mpito ya Misri Hazem al Beblawi, ametaka kukiwa mapatano ya kitaifa ili kuhitimisha migawanyiko miongoni mwa raia wa nchi hiyo. Wa m i s r i k a d h a a wameuliwa katika ghasia zilizoiubuka kati ya wapinzani na wafuasi wa Muhammad Morsi. Akizungumza na t e l e v i s h e n i ya s e r i k a l i mapema wiki hii, al Beblawi alisema kuwa wakati umeka sasa wa kufikiwa suluhu ya kitaifa kwa kuwa Misri imegawanyika. Beblawi amesema, Misri imekuwa uwanja wa mapigano na m i k wa r u z a n o k u f u a t i a k u p i n d u l i wa M o r s i n a kuongeza kuwa, kufikiwa suluhu ya kitaifa ni njia pekee inayoweza kuiondoa Misri katika hali ya sasa. Rais wa muda wa Misri, Adly Mahmoud Mansour, ameunda Kamati ya Wataalamu wa Sheria, ambao watapandekeza mabadiliko katika katiba ya sasa, ambayo inasema taifa hilo linapaswa kutawaliwa kwa misingi ya sheria za Kiislamu. Rais Mansour, Jumamosi iliyopita aliteua kamati ya wataalamu kumi, ambao watapendekeza marekebisho katika katiba ya sasa iliyoidhinishwa wakati wa utawala wa Mohammad Morsi, aliyepinduliwa na jeshi mwanzoni mwa mwezi huu. Katiba ya mpya ya Misri iliidhinishwa rasmi Desemba 2012 kufuatia wananchi kuipitisha kwa kura kwa asilimia 64. M i e z i s i t a b a a d a ya kuidhinishwa katiba hiyo, jeshi la Misri lilimuondoa madarakani Rais Morsi na kuwatia mbaroni wananchama waandamizi wa harakati ya Ikhwanul Mislimin pamoja na kumshikilia Morsi mwenyewe.

Wananchi wa Misri baada ya kuuangusha utawala wa ki Imla wa Hosni Mubarak, walikuwa wakisisitiza kuwepo katiba mpya

FAMILIA ya Rais aliyeondolewa madarakani nchini Misri Mohamed Morsi, imetangaza uamuzi wa kuchukua hatua za kisheria dhidi ya Mkuu wa Majeshi, Jenerali Abdel Faah Al Sisi, kwa kuendelea kumshikilia mateka kiongozi huyo wa Chama cha Muslim Brotherhood. Mtoto wa kike wa Morsi aliyefahamika kwa jina la Shaimaa Mohamed Morsi, ndiye aliyetangaza mpango huo wa kuchukua hatua za kisheria dhidi Jenerali Al Sisi, ambaye ndiye aliyetangaza kwamba Morsi anashikiliwa na Jeshi. Shaimaa ameweka wazi kwamba watachukua hatua hizo za kisheria kwa kuangalia sheria za ndani ya nchi hiyo na hata zile za kimataifa, huku akimtaja mara kadhaa Jenerali Al Sisi kuwa ndiye aliyeongoza mapinduzi ya kijeshi ya kumwaga damu na kumuondoa baba yake madarakani. Binti huyo wa alisema kile kinachofanywa na Jeshi ni utekeji nyara, hivyo wao watachukua sheria dhidi ya hatua hiyo. S h a i m a a a m e wa e l e z a waandishi wa habari Jijini Cairo kuwa, wamelitaka Jeshi kumuachia Morsi, lakini limeendelea kumshikilia kwa madai ya sababu za usalama na kiafya, jambo ambalo limeendelea kuwaacha bila majibu. Familia ya Dk. Morsi imeshasema kuwa haifahamu sehemu alipo baba yao kwa sababu jeshi halawapa taarifa zozote na kwamba, ndiyo maana wameona ni wakati muafaka sasa wa kuchukua hatua za kisheria.

Binti wa Morsi kumchukulia hatua za kisheria Mkuu wa Majeshi Misri


Mataifa kadhaa ya Magharibi hususan Ujerumani pamoja na Umoja wa Ulaya EU, yalishatoa wito wa kuachiwa kwa Morsi, lakini jeshi limeendelea kumshikilia, huku likipambana na maelfu ya waandamanaji wanamuunga mkono kiongozi huyo. Mawaziri wa Mambo ya Kigeni wa Umoja wa Ulaya wametoa wito wa kuachiliwa

ya Al Alam Ahmad al Siou, ametiwa mbaroni. Hata hivyo Maasa hao wa usalama hawakutoa sababu za kitendo chao hicho. Tangu Dkt. Morsi apinduliwe na jeshi, maasa usalama nchini humo wamezifunga stesheni kadhaa za televisheni ikidaiwa kuwa ni katika kile kinachoonekana kuwa ni kuzima juhudi na sauti za wapinzani wa mapinduzi hayo nchini humo.

DKT. Mohamed Morsi


Dk. Morsi anashikiliwa na Jeshi nchini Misri tangu kufanyika kwa mapinduzi yaliyomuondoa madarakani Julai 3 mwaka huu, ambapo nafasi yake ilichukuliwa na Kiongozi wa Mpito Bw. Adly Mahmud Mansour. Jeshi nchini Misri lilishatangaza hapo awali kuwa, haliwezi kumuachia Dk. Morsi kwa sasa kwa madai ya kuwepo sababu za kiusalama na kiafya. Wa f u a s i wa k e wameendelea kufanya maandamano nchi nzima kushinikiza kuachiwa huru na kurejeshwa m a d a r a k a n i k wa k u wa alichaguliwa na wananchi kidemokrasia.(www.irib.ir)

huru wafungwa wote wa kisiasa, akiwemo Muhammad Morsi, Rais aliyeenguliwa madarakani nchini Misri. Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Ujerumani Guido Westerwelle, amesema kuwa vyama na makundi yote ya kisiasa ikiwemo Harakati ya Ikhwaanul Muslimiin, yanapaswa kuwa na nafasi kwenye serikali ijayo ya Misri.

Ahlul Daawa Hajj And Travel Agency


INAPENDA KUWA TAARlFU MAHUJAJI WAKE WOTE NA WAISLAMU KWA JUMLA KUA:IDADI YA MAHUJAJI WAO WA MWAKA HUU 2013 IMEPUNGUZWA KUTOKA MIA TATU MPAKA MIA MOJA NA SABINI TU. KWA HIVYO;(a) WALE WOTE W ALIOJIANDIKISHA W A WAHl KUMALIZA KULIPIA GHARAMA ZAO. (b) W ALIOJIANDIKISHA TU NA HAW AJALIPIA W AJE KULIPIA AU TUT A WAONDOSHA KWENYE ORODHA NA KUW APA NAFASI W ALIOKUW A TAYARI. (c) KUWASILISHA PASSPORT AU KOPI ZA PASSPORT KWA MUDA HUU. (d) PICHA MBILI PASSPORT SIZE KW A AJILI Y A VISA. 2. (a) BEl YETU NI US DOLA 3480 punguzo ni 2% (b) UKIWAHI KULIPIA SA SA NA KUMALIZA TARATlBU ZOTE PUNGUZO NI ASILIMIA SITA KWA HIVYO UT ALIPIA US DOLA 3337 TU NA KABLA Y A TAREHE 25 JULAY 2013. 3. KWA MAWASILIANO ZAIDI FIKA OFISINI KWAO;(a) DAR ES SALAAM MTAA W A DOSI NA MKADINI NYUMBA NAMBA 26 MKABALA NA SHOW ROOM Y A MAGARI TEL 0713 730444 AU 0785 930444 AU 0773 930444. (b) ZANZIBAR MTAA WA RAHA LEO TEL 0777484982 AU 0777413987 AU WASILIANA NA. ( c) MAALIM SElF HUMOUD KIJICHI ZANZIBAR TEL 0777417736. (d) ABDALLA SALEH MAZRUI (HOKO) TEL 0715724444 AU 0773 724444 AU 0784 724444 (e) SHEIKH DAUDI KHAMIS SHEHA PEMBA 0777 679 692 (f) SHEIKH ABUBAKARI MAULANA MARKAZ KIWALANI 0784 453 838 NA BEl NAFUU KULIKO WOTE NA HUDUMA BORA KULIKO WENGI USISAHAU AHLUL DAAWA HAJJ AND TRAVEL AGENCY

6
Na Omar Msangi

VEER Zaara ni sinema ya Kihindi ya mwaka 2004 iliyotolewa na kampuni ya lamu Yash Raj Films. Nadhani ilipewa jina hili kwa sababu ya majina ya washiriki wake wakuu ambao ni Veer Pratap Singh na Zaara Hayat Khan. Katika sinema hii kinaelezwa kisa cha mtu mmoja Mhindi kutoka India aliyekamatwa na kufungwa jela Pakistan kwa miaka 22 akidaiwa kuwa ni jasusi. Sinema inapofunguka anaonekana mfungwa mmoja yupo katika sero ya pekee kajawa na huzuni tele upweke ukimuelemea. Inavyoonekana ilikuwa majira ya baridi kwa sababu anatetemeka kwa baridi na kanyikunyata na blanketi. Taratibu ananyanyuka na kukiendea kiriba cha maji kilichokuwa kimewekwa kwa mbali karibu na lango la chuma. Anapokichukua na kutaka kunywa maji anasita anaposikia sauti ya Athana. Allahu Akbar, Allahu Akbaru (Mungu mkubwa Mungu mkubwa). Hii inakua kama ishara k wa k e k u wa k a t i k a t i ya tabu ile, bado yupo Mungu wa kumlilia na kumtegemea. Kilichofuatia ni kuonekana wakili kana binti ambaye anajipa moyo na kujiambia kwamba lazima amsimamie Veer Pratap Singh mpaka apate haki yake. Hata hivyo, hii ikiwa kesi yake ya mwanzo toka kumaliza kosi yake ya sheria, Wakili wa Serikali, mkongwe, Zakir Ahmed ambaye h a j a wa h i k u s h i n d wa hata katika kesi moja, anambeza akimwambia hataambulia chochote watakapopambana mahakamani. Ve e r P r a t a p S i n g h ndio jina lake halisi, lakini katika kesi ushahidi uliowasilishwa mahakamani ulidai kuwa yeye ni Rajesh Rathore. Rajesh Rathore ambaye alidaiwa kuwa ni kachero wa I n d i a n a a l i i n g i a Pakistan kwa ajili ya kufanya ujasusi. Upande wa mashitaka ukawasilisha vielelezo na ushahidi, kimoja wapo kikiwa ni hati ya kiapo aliyosaini Rajesh Rathore ikidaiwa kuwa anakiri kuwa hilo ndio jina lake na kweli yeye ni jasusi kutoka India. Kwa ushahidi huo Veer Pratap Singh (Rajesh Rathore) akahukumiwa kifungo cha maisha. Baada ya kukaa jela kwa

Kisa cha Veer Pratap Singh na Masheikh wa Uamsho


Hii ndiyo nchi yangu: Ukweli, Haki itawale Waliodaiwa si mapapai hayataoza, wajitizame Wanafanya nini kuleta Haki Sawa kwa Wote

Makala

RAMADHAN 1434, IJUMAA JULAI 26 - AGOSTI 1, 2013


moshi, anatokea kijana mtanashati ambaye baada ya salamu, Zaara anamwambia Veer kuwa yule ni mchumba wake na anamtaka radhi kwa kutomwambia na mapema k u wa a n a m c h u m b a . Huyu ni Raza Shirazi kijana ambaye familia yake ina nafasi kubwa katika serikali ya Pakistan. Katumwa kumfuatilia Zaara kuhakikisha kuwa anarejea salama baada ya zoezi alilotumwa na nyanya yake. Baada ya salamu na kubadilishana maneno mawili matatu, Zaara na mchumba wake wanaondoka na kumwacha Veer kasimama asijue la kufanya. Mengi yalipita hapo kati lakini mwishowe, inaonyeshwa kuwa Veer aliamua kumfuata Zaara Lahore na hali hiyo i k a m c h a n g a n ya s a n a Zaara maana alikuwa hajui aolewe na Raza au atoroke na Veer. Ila mwishowe Veer aliamua kukubali ukweli. Najua wewe ni wa mwingine, lakini hata utakapokuwa kwa mumeo, jua ya kwamba yupo mtu India ambaye yupo tayari kutoa maisha yake kwa ajili yako. Nakupenda sana nitatoa uhai wangu kukulinda na kwa ajili ya furaha yako. Veer alitoa maneno hayo katika kuagana na Zaara, lakini akayasema pia mbele ya Razi jambo lililomfanya Razi kukasirika na kuamua kumkomoa. Hili ni tusi au unanisia, Razi alisema akimkabili Veer Pratap Singh na kujiapiza moyoni kwamba ataona. K wa k u t u m i a n a f a s i yake serikalini, aliamua k u m k o m o a Ve e r k wa kumbambikizia kesi mbaya. Wakati Veer yupo ndani ya basi anarejea kwao India, alistukia wanaingia askari wawili wakamkamata na kumsusha. Inapofunguka Veer yupo rumande yule mchumba wa Zaara, Razi Shirazi, amesimama na makaratasi akimlazimisha Veer ayasaini. Naweza kufanya maisha ya Zaara kuwa Pepo au Jahannam, lakini yote utaamua wewe. Ama unasaini kukubali kila kilichoandikwa hapa, Zaara asalimike au kataa jahannam imkabili Zaara hapa hapa duniani. Uchaguzi ni wako. Alisema Razi akaicha karatasi na kalamu juu

AN-NUUR

BAADHI ya viongozi wa UAMSHO wakiwa katika picha ya pamoja.


miaka 22 alitokea binti mmoja akiitwa Saamiya Mansoor Ali Siddique akataka kuifufua kesi yake. Katika utaratibu wa kisheria ikabidi kuwasiliana na mfungwa jela kutaka amweleze kisa na mkasa. Toka alivyokamatwa na jinsi kesi ilivyoendeshwa mpaka akafungwa. Hata hivyo ilikuwa kazi sana kumshawishi Veer kuzungumza. Kwa miaka yote 22 aliyokaa ndani aligoma kabisa kuzungumza au kueleza lolote kuhusu kesi hiyo. Saamiya Siddique alifanya kazi kubwa sana kumfanya mfungwa yule aliyekaa jela kwa miaka 22 akubali kuzungumza. Na hapo ndio mwanzo wa utamu wa lamu. Veer Pratap Singh, anatamka jina hili wakili Saamiya baada ya kutoa ngonjera ndefu kujieleza ye ye n i n a n i n a k wa nini yupo pale. Taratibu Veer ananyanyua uso wake kutoka katika hali ya k u j i k u n ya t a k a m a anashtuka ni nani huyu anataja jina lake kwa sababu kwa miaka 22 aliyokaa jela, hakuna mtu aliyewahi kulitaja. Kila aliyekuja alimtaja kwa jina la Rajesh Rathore lakini na yeye mwenyewe akajipa jina la mfungwa namba 786 namba ambayo katika baadhi ya madhhebi zinafahamika kuwa zinawakilisha jina la Mungu. Kwa muda wa miaka 22 umekaa kimya. Mwenyezi Mungu kanituma kukuokoa. Anasema Saamiya Siddique na kutamka tena jina la Veer Pratap Singh. Hapo Veer kama anayezinduka kutoka usingizini anaanza kutiririka na visa kwa mtindo wa ash back. Ve e r P r a t a p S i n g h alikuwa mwanajeshi na rubani wa jeshi la anga la India na alikuwa kamanda kiongozi katika kikosi cha uokozi wakati wa majanga. Katika tukio moja basi lilipata ajali likaporomoka katika mlima. Ndani ya gari hiyo alikuwepo Zaara Hayat Khan, msichana mrembo sana kutoka Pakistan. Zaara alikuwa ametumwa na bibi yake kwenda kutupa majivu fulani katika mto mmoja India unaosadikiwa kuwa na Baraka. Wakiwa na helkopta, Veer alikuwa akishuka na kamba maalum na kuwanasua majeruhi waliokwama katika mlima na kuwapandisha katika helk op t a k uwapelek a h o s p i t a l i . M m o j a wa watu hao alikuwa Zaara Hayat Khan. Zaara alikuwa hakuumia na wakati akimpandisha katika helkopta wakawa wanatizamana na kuleta hisia za mapenzi. Baadae anaonyeshwa Ve e r P r a t a p S i n g h akimsindikiza Zaara kwenda kumwanga m a j i v u a l i yo p e wa n a bibi yake katika mto wa Baraka. Baada ya zoezi hilo, kutokana na jinsi walivyopendana, Veer anaamua kumsindikiza Zaara mpaka kwao Lahore, Pakistan. Wakiwa katika kituo cha gari

Inaendelea Uk. 7

7
Inatoka Uk. 6
ya kimeza na kumwacha Veer kuamua anayoa au anasuka. Ni makaratasi hayo, ambapo inadaiwa kuwa Veer Pratap Singh ni Rajesh Rathore na kwamba yeye ni kachero aliyeingia Pakistan kufanya ujasusi. Sinema inamwonyesha Veer akikumbuka ahadi yake mbele ya Zaara (ash back) kwamba hata kama ataolewa na mtu mwingine, ikitokea ikalazimu yeye kutoa uhai wake kwa ajili yake, atafanya hivyo. Veer akaona kuwa ni lazima atimize ahadi yake. Akasaini kiapo kile cha mahakama na ukawa ndio ushahidi uliomtia hatiani. L a k i n i wa k a t i Ve e r akishushwa katika gari na kupelekwa polisi, gari lile alilokuwa akisafiria mbeleni linapata ajali mbaya na abiria wote kufariki. Kwa hiyo kule India, wakajua kuwa Veer kafa. Huku nyuma Zaara naye akajuwa kuwa Veer kafa. Sinema ni ndefu, lakini baada ya Saamiya kufanikiwa kumshawishi Ve e r k u z u n g u m z a , inaonekana wapo mahakamani. Mwisho wa yote anapatikana Zaara na kuja mahakamani kutoa ushahidi kuwa yule si Rajesh Rathore, bali Veer Pratap Singh na inabainika wazi kuwa hat i zilizowasilishwa mahakamani ilikuwa za kughushi. Lakini hata kabla ya Zaara kufika mahakamani, askari mmoja aliyekuwepo wakati kesi hiyo inabuniwa, alishikwa na imani na kusema kweli kuwa Baniani wa watu hakuwa na hatia na kwamba hilo jina la Rajesh Rathore, sio lake. Kwa uchungu mkubwa na uso wa huruma, jaji aliyekuwa akisikiliza kesi ile alimtaka radhi Veer kwa niaba ya Serikali na watu wa Pakistan. Lakini hiyo inakuja baada ya Veer Pratap Singh kukaa jela kwa miaka 22. Aliyekuwa wakili wa Serikali ya Pakistan katika kesi hii, Zakir Ahmed, ambaye anasifika kwa k u t o k u s h i n d wa h a t a kesi moja (hii ilikuwa ya kwanza), baada ya kumalizika kesi alikwenda na kumshika mkono Saamiya na kumpongeza. Alieleza mengi, lakini makubwa mawili: Moja ni jinsi wanasiasa na watu wenye madaraka Serikalini wanavyoweza kusababisha

Kisa cha Veer Pratap Singh na Masheikh wa Uamsho

Habari/Tangazo

RAMADHAN 1434, IJUMAA JULAI 26 - AGOSTI 1, 2013


sana Saamiya kwa kunifundisha thamani ya ukweli na haki. Akavua gwanda lake na tai yake ya kiuwakili na kusema huo ulikuwa ndio mwisho wake wa kufanya kazi ya uwakili. Wa k i l i Z a k i r A h m e d anasema kuwa, alijua sheria ndio kila kitu na k wa m b a u m a d h u b u t i wa nchi unapimwa kwa mfumo wake wa sheria (Judiciary System). Lakini watu watizame na upande mwingine: Ubinadamu. Haki na Ukweli. Leo ni mwezi 17 R a m a d h a n i i k i wa n i takribani miezi 10, mwaka kasoro miezi miwili, tangu Sheikh Farid na Masheikh we n z a k e wa U a m s h o wakamatwe, kufunguliwa kesi na kuzuiliwa dhamana zao. Wapo ndani utadhani wanatumikia kifungo. Afadhali Baniani yule Veer Pratap Singh alishahukumiwa japo kwa dhulma! Ya w e z e k a n a i p o s h e r i a i n a y o wa f a n ya wenye mamlaka wawe na hoja ya kisheria kuwa Masheikh hao wanastahiki kisheria kuendelea kukaa ndani. Lakini pamoja na kuwepo sheria hiyo, swali ni je, hizo tuhuma au kosa linalodaiwa kuwa halistahiki mtu kupewa dhamana limethibiti? Lilipotokea shambulio la bomu katika Kanisa Katoliki lililouwa watu wa t a t u k u l e A r u s h a , Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Kayanza Pinda

AN-NUUR

SHEIKH Farid Hadd


matatizo makubwa kwa watu wasio na hatia kwa lengo la kutosheleza matashi yao binafsi huku wakisingizia kuwa ni kwa masilahi ya taifa. Akatoa mfano wa vita vilivyowahi kutokea huko nyuma baina ya India na Pakistan, 1947, 1965 na 1999 lakini ukitizama hakuna sababu yoyote ya msingi. Tatizo labda ni ubaguzi tu wa kuwatizama watu kwa Uislamu wao (Pakistan) na Uhindi wao (India), ukubwa na udogo wao; vyeo serikalini na ulofa wao wa mitaani. Mwisho kabisa Wakili Zakir Ahmed alimwambia Saamiya Siddique maneno yafuatayo: Saamiya, Thank you for teaching me the value of truth and justice. Akimaanisha, ahsante

JULAI 12 dunia ilishuhudia jinsi Malala Yusufzai, msichana kutoka Pakistan mwenye umri wa miaka 16, alivyotolewa ukumbi na kupokelewa New York na Ban Ki Moon, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa. Isitoshe, tarehe hiyo ambayo ndiyo siku yake ya kuzaliwa ilitangazwa rasmi na Ban Ki Moon kuwa sasa itakuwa ikijulikana kuwa ni Siku ya Malala. Lengo ni kuwapatia elimu watoto wote duniani. Malala Yusufzai Siku hiyo msichana huyo alipewa fursa adhimu ya kuhutubu kwenye mkutano wa kwanza wa Baraza la Vana la Umoja wa Mataifa kwenye makao makuu ya Umoja huo, New York. Alitoa hotuba ya kusisimua katika mazingira yaliyo

Ya Malala, Taliban na Uamsho ..


na tofauti kubwa na yale ya kwao nyumbani mjini Mingora kwenye eneo la Bonde la Swat. Huko kwao Malala alikuwa akiishi pamoja na wazazi wake, nduguze wawili wakiume na kuku wawili aliokuwa akiwafuga. Malala alipata umaarufu kwa sababu moja: alipigwa risasi Oktoba 9 mwaka jana na Mataliban wa Pakistan waliodhamiria kumuua. Kilichomchongea ni ukakamavu wake wa kushikilia kwenda skuli. Jengine lililomchongea ni harakati zake za kuwashajiisha wasichana we n z a k e we n d e s k u l i huko kwao katika tarafa ya Swat. Yote hayo yanahitaji ujasiri mkubwa kwa sababu wasichana kwenda skuli katika eneo la Bonde la Swat si jambo la mchezo. Vuguvugu la Taliban lenye kushamiri katika eneo hilo halitaki msichana yoyote ende skuli. Vuguvugu hilo linaitwa Tehrik-i-Taliban Pakistan na linaongozwa na Jamshed Mehsud ambaye pia anaitwa Hakimullah Mehsud. Kwa mujibu wa fasiri yao ya Uislamu Mataliban wa Pakistan wanaamini kwamba wasichana wa Kiislamu kwenda skuli ni kufuru. Shambulio la kutaka kumuua Malala ni la kinyama na lazima tulilaani. Liliwashtua wengi duniani hata pakafanywa jitihada mahsusi za kumkimbiza Malala Uingereza kwa matibabu na hatimaye

Inaendelea Uk. 8

k u m p a n d i s h a k we n ye jukwaa la Umoja wa Mataifa. Simlaumu Malala kwa utukufu alioupata. Lakini ninaulaumu ulimwengu kwa kimya chake pale watoto wengine wanapouliwa takriban kila siku kama si Afghanistan basi Iraq; kama si Iraq basi Syria au Pakistan au Somalia. Nchini Afghanistan na Pakistan mara kwa mara watoto huuliwa ama na wanajeshi wa Kimarekani au wa NATO au huuliwa na vile vyombo vya Kimarekani virukavyo angani bila ya rubani. Mara zote hizo huambiwa kwamba watoto hao waliuliwa kwa makosa. Huko Syria, Iraq, Somalia na Pakistan wakati mwingine

Inaendelea Uk. 8

8
Inatoka Uk. 7 watoto huuliwa na makundi ya watu wenye itikadi za kidini zilizo sawa na zile za Mataliban wa Pakistan. Kwa hakika miongoni mwa wenye kufanya unyama Syria ni Mataliban wa Pakistan wale wale waliotaka kumuua Malala. Juzi tu walitangaza kuwa mamia ya wapiganaji wao wamekwishapiga kambi Syria na wanashirikiana na kundi la Jabhat al-Nusra dhidi ya serikali ya Bashar. Makundi hayo mawili pamoja na lile la al-Qaeda katika Iraq na mingineo yenye itikadi kama zao yako chini ya mwavuli wa Syrian Islamic Front (SIF). Huko Syria Mataliban na wenzao wamekuwa wakiwaua watoto, wanawake pamoja na wazee. Lakini wakuu wa dunia hii wamekaa kimya kwa vile wauaji hao wanampinga Bashar. Kuna kimya kingine kinachonishangaza. Nacho ni cha wanaharakati wa K i z a n z i b a r i wa l i o z i b a midomo yao kuhusu madhila yanayowakuta wale waliokuwa wakiwaita Mashekhe wetu wa Uamsho. Tangu mashekhe hao 10 waanze kukamatwa Oktoba 16, 2012 mpaka leo kesi yao haijatajwa mahakamani. Hadi sasa wamesomewa tu mashitaka dhidi yao, mashitaka ambayo yanahusika na vurugu zilizotokea Zanzibar Mei mwaka jana. Wa s h i t a k i w a h a o wa l i f i k i s h wa m a r a ya mwisho mahakamani Julai 3 mwaka huu na walitarajiwa kupandishwa tena mahakamani Julai 18. Washitakiwa wenyewe ni Farid Hadi Ahmed, Msellem Ali Msellem, Mussa Juma Issa, Azan Khalid Hamdani, Suleiman Juma Suleiman, Khamis Ali Suleiman, Hassan Bakari Suleiman, Ghalib Ahmada Omar, Abdalla Said Ali na Fikirini Majaliwa Fikirini. M a s h i t a k a yanayowakabili ni kuchochea vurugu, kuharibu mali za umma na za watu binafsi zenye thamani ya shilingi milioni 5 0 0 , k u f a n ya v u r u g u katika eneo la Magogoni na kuhatarisha usalama wa taifa la Zanzibar. Wa n a s h i t a k i w a p i a kuhusu kadhia ya Farid Hadi Ahmed aliyetoweka Oktoba 16, 2012. Shekhe huyo aliibuka siku nne baadaye akidai kwamba alitekwa nyara na watu waliovaa barkoa

Makala

RAMADHAN 1434, IJUMAA JULAI 26 - AGOSTI 1, 2013


wanawafikiria wananchi wenzao walio gerezani. Nualo ni kwamba ingawa uamuzi ni wa mahakama, wengi wenye kuifuatilia kesi hii wanaamini washitakiwa hao wanaendelea kuwekwa ndani kwa sababu hivyo ndivyo watakavyo viongozi wa juu wa serikali ya Zanzibar. Mara mbili tatu hivi Rais Ali Mohamed Shein mwenyewe amesema hadharani kuwa atawashughulikia wanaochochea fujo. Wakati mwingine huwataja Uamsho. Zanzibar ya leo ni nchi yenye kuhuzunisha; haisikitishi tu, bali inahuzunisha. Ni nchi yenye kutatanisha, wakati mwingine hujikanganya yenyewe. Na viongozi wake? Naona hata haina haja ya kuwaeleza walivyo... (Makala imetolewa kwa hisani ya Ahmed Rajab/ Mtandao wa KijamiiMzalendo net)

AN-NUUR

Ya Malala, Taliban na Uamsho ..


waliojitambulisha kuwa ni polisi. Serikali imelikanusha dai hilo. Mashekhe hao wa m e f u n g i wa k we n ye gereza la Kiinua Miguu wakiwa chini ya ulinzi mkali. Kama wiki mbili za mwanzo baada ya kutiwa nguvuni wakidhalilishwa kwa kunyimwa hata nafasi ya kubadili nguo au ya kuonana na familia zao. Tena kila mtuhumiwa alikuwa akiwekwa katika chumba cha peke yake. Tunavyosikia ni kwamba siku hizi wameondoshewa m a d h i l a h a yo i n g a wa bado mazingira yao si ya kuridhisha. Cha kushangaza ni kwamba hatusikii sauti zozote zenye kuwatetea. Labda kwa sababu wao ni mashekhe na si wanasiasa. Labda wangekuwa wanasiasa tungewaona wanaharakati, kwa mfano, wakiwasiliana na jumuiya za kimataifa za haki za binadamu na kuzizindua kuhusu janga lililowafika mashekhe hao. Labda madevu ya hao mashekhe yanawatia hofu wanaharakati, wanachelea wasije wakashutumiwa kuwa wanawatetea magaidi maana siku hizi kwa wakubwa wa dunia hii madevu, Uislamu na utetezi wa haki ni mchanganyiko wa hatari. Na si kwa hao wakubwa tu, bali hata kwa baadhi ya taasisi, magazeti, na wanasiasa wa Tanzania Bara ambao bila ya ushahidi wowote wameihusisha Uamsho na vitendo vya kigaidi. Juu ya yote hayo, kuna sababu halali za kuwatetea. Sababu kubwa ni kazi walioifanya ya kuwaamsha Wa z a n z i b a r i w e n z a o wautambue utaifa wao na waachane na chuki na uhasama uliokuwepo baina yao kwa muda mrefu. Jengine jema walilolifanya ni kuwahimiza vijana wa Kizanzibari warudi kwenye maadili ya Kiislamu badala ya kujihusisha na vitendo vinavyoleta madhara katika jamii kama vile vya kubugia mihadarati na uasherati. Pengine kuna wanaharakati wenye kujuta, wenye kuona kwamba walipoteza nguvu zao walipokuwa wakiwaunga mkono hao mashekhe. Wale waliokuwa na majazba waliokuwa wakiota kwamba siku moja nchi yao itaamka ghafla ionekane na sura nyingine, sasa itawabidi waote ndoto nyingine. Sina dhamira ya kuingilia kesi inayowakabili washitakiwa hao. Hiyo ni kazi ya mahakama na ya mawakili. Dhamiri yangu ni kukizungumzia hiki kimya kilichotanda kama wingu juu ya kesi hii. Na zaidi nataka kugusia haki wanayonyimwa washitakiwa ya kuachiwa kwa dhamana huku kesi ikiwa inaendelea. Kucheleweshwa kusikilizwa kwa kesi hiyo ni adha kubwa kwa washitakiwa. Inavyoonyesha ni kama serikali imeamua kuwatia adabu ingawa hawakupatikana na hatia. Ikiwa dhana hiyo ni sahihi, basi serikali itakuwa imeamua hivyo kwa sababu

za kisiasa. Serikali inazidi kujifaragua ikiamini kwamba kuwatia adabu viongozi wenye muelekeo wa Kiislamu hakutowakera wakubwa wa dunia hii. Labda serikali inaamini kwamba balozi za Marekani na Uingereza zitayafumbia macho wanayotendewa mashekhe hao kwa sababu z i m e k w i sh a t i wa s u mu ya Uamsho kusingiziwa ugaidi. Ndio maana kesi hiyo ikawa inaakhirishwa na kuakhirishwa kwa lengo la kuwaweka ndani tu mashekhe hao. Mara ya mwisho Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar alisema wanasubiri waletewe daari la kesi kutoka Mahakama ya Rufaa, Dar es Salaam. S i j u i Wa z a n z i b a r i wenzangu wanapofuturu na aila zao katika mwezi huu mtukufu kama

Kisa cha Veer Pratap Singh na Masheikh wa Uamsho


Inatoka Uk. 7 alitangaza Bungeni k u wa wa m e k a m a t wa Waarabu wanne. Alitoa kauli hiyo kwa tahadhari sana akiisherehesha kwa kusema kuwa Waarabu hao walikamatwa katika utaratibu tu wa kawaida k wa m b a l i n a p o t o k e a tukio kama lile ni lazima mipaka ifungwe. Kwa hiyo wageni wanaovuka mpaka watakamatwa ili kuhojiwa kujiridhisha kuwa hawahusiki. Baada ya kauli hiyo ya Serikali, An nuur iliandika ikihoji: Je, Namanga walipita Waarabu pekee? Hoja yenyewe ni kuwa kama ulikuwa utaratibu wa kawaida tu wa kufunga mpaka na kukamatwa kila mgeni anayepita, basi wangekamatwa pia Wa g a n d a , Wa z a m b i a , Waingereza, Wamarekani na tunajua mji wa Arusha na mpaka wa Namanga ulivyo na harakati nyingi za wageni wanaosari kati ya Nairobi na Arusha. Mwandishi yeye katika fikira zake ameandika kutahadharisha kuwa hii ya kukamata Waarabu pekee inaweza kujenga dhana kuwa hawa wamelengwa kwa sababu ya Uarabu (Uislamu) wao. Na wasiwasi huo unapata nguvu ukizingatia kuwa toka mwanzo wa tukio zilishaanza propaganda katika vyombo vya habari kwamba muhusika alikuwa kavaa kanzu. Lakini kwa upande mwingine, wenye mamlaka nao wanaweza wakaja juu. Wakaleta madai kuwa huo ni uchochezi. Gazeti linalenga kutahadharisha kwamba habari italeta utata na dhana mbaya, wenye mamlaka wakaishikia bango kuwa ni habari ya uchochezi na wakatumia sheria zilizopo kuchukua hatua. Swali ni je, habari ilikuwa ikichochea au ikitoa tahadhari? Bila ya kuingilia uhuru wa mahakama, ndio hapa nasema, pamoja na kuwepo sheria inayowaweka rumande Masheikh hao na kuzuilia dhamana zao, kuna haja ya kutizama upande wa pili: Truth and Justice. Ukweli na Haki. Wapo watu waliwahi kukaa ndani miezi kadhaa au miaka kwa mashitaka ya kisiasa kule Zanzibar. Inasemekana kuwa watu waliokuwa karibu na Rais wakati ule Dkt. Komandoo Salmin Amur walimwendea na k u m wo m b a a wa a c h i e watu wale. Wacha wakae, kwani n i m a p a p a i k wa m b a yataoza, inasemekana hayo ndiyo yalikuwa majibu ya komandoo.

Mazungumzo yakaisha. Watu wale wakati ule waliodaiwa sio mapapai na wakiona kuwa walikuwa wakidhulumiwa, kwamba sheria ilitumika vibaya dhidi yao, hivi sasa wapo madarakani katika nafasi m b a l i m b a l i . S wa l i n i je, kuna juhudi yoyote wanayofanya kuhakikisha kuwa haki kwa wote, ukweli na uadilifu unakuwepo? Kutokana na ushahidi uliowasilishwa mahakamani, Veer Pratap Singh alikaa jela miaka 22 ndio inakuja kujulikana kuwa ushahidi ulikuwa wa uwongo. Nani atalipa dhulma hii? Japo Jaji aliomba radhi kwa niaba ya Serikali ya Pakistan kwa sababu ilikuwa Jamhuri ndiyo iliyomshitaki Veer, samahani hii italipa mateso ya miaka 22 jela? Miaka 22 mke amekosa mapenzi ya mume, watoto wamekosa malezi na huduma ya baba, huenda wamekuwa chokoraa, mitaani, samahani itasaidia nini? Ni kwa kuzingatia yote hayo, Wakili Zakir Ahmed alimshukuru Saamiya Siddique akimwambia, ahsante sana kwa kunionyesha upande wa pili: Ubinadamu, Ukweli na Haki.

9
Na Said Rajab. T U A N G A L I E mfano mwingine wa kimapinduzi kutoka kwenye Sunna ya Mtume wa Mwenyezi Mungu. Watawala wa Qurayshi walimuomba baba yake mdogo Mtume amuombe Muhammad (saw) kwa niaba yao, aachane kabisa na harakati zake. Baba yake mdogo alimkabili Mtume kwa mapendekezo haya: Kama unataka wadhifa a u h a d h i , wa k u u wa Maqurayshi wako tayari kukupa wadhifa wowote unaotaka; Kama unataka kuwa mkuu wa Makka yote hii, wakuu wa Maqurayshi wa k o t a ya r i k u k u p a ukubwa huo; Kama umeshikwa na mapepo wabaya, basi wakuu wa Maqurayshi wa k o t a ya r i k u k u p a mganga bora kabisa aliyekuwepo. Mapendekezo mawili ya kwanza yanaonekana kuwa mazuri. Baadhi ya Waislamu wa leo, wanaokwenda na wakati, wangekimbilia mapendekezo hayo, wakidhani ni fursa ya kusimamisha Uislamu kwa kutumia njia iliyowekwa na makari. Kwanini Mtume wa Mwenyezi Mungu alikataa mapendekezo yote hayo? Katika hali na mazingira hayo, nini lilikuwa jibu la Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa Waislamu wa zama zote? Kwa haki ya Mwenyezi Mungu, Ewe baba yangu mdogo, hata kama wangeliweka jua kwenye mkono wangu wa kulia na mwezi kwenye mkono wangu wa kushoto, ili niache harakati hizi, sitoacha mpaka Mwenyezi Mungu anipe ushindi au nife nikifanya kazi hii. Kauli hii ya kitume ndiyo iliyopaswa kuwa maelezo mafupi ya kinga ya kimapinduzi ya Waislamu, dhidi ya mbinu zote chafu za makafiri, kuwaingiza Wa i s l a m u k w e n y e mfumo wao, ili kuwatoa kwenye malengo mapana ya Kiislamu. Msimamo h u o wa k i m a p i n d u z i wa Mtume, ndiyo uliowakomboa Waislamu wa awali kutoka kwenye aina zote za woga: Wala hawakuwa wenye kumdhuru yoyote kwa hayo ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu Qur (2:102) Na kama Mwenyezi Mungu akipenda

kunidhuru, uombezi wako hautanifaa kitu, wa l a h a wa t a n i o k o a ! Qur(36:23) Sema: Halitatusibu ila alilotuandikia Mwenyezi Mungu Qur (9:51) Aya nyingi ndani ya Qur an zinazungumzia jinsi ya kuwakomboa Waislamu kutokana na utumwa wa kifikra na kuwategemea viumbe b a d a l a ya M we n ye z i Mungu: ..bila shaka wale m n a o w a a b u d u mkamuacha Mwenyezi M u n g u , w a o hawakumilikiini riziki, takeni riziki kwa Mwenyezi Mungu, na Muabuduni na Mshukuruni. Kwake mtarudishwa Qur(29:17) Sema: Ni nani anayekuruzukuni kutoka mbinguni na ardhini? Waambie: Mwenyezi Mungu Qur(34:24) Hakika hiyo ndiyo riziki yetu (tutakayowapa), isiyomalizika (isiyotindika) Qur(38:54) Na mwisho, msukumo wa kimapinduzi wa Quran unakabiliana pia na kifo. Muislamu haogopi kufa. Lakini hiyo haina maana kwamba Waislamu wa n a p e n d a k u u a a u kuuliwa. Muislamu anakabiliana na kifo iwapo kifo hicho kitakuwa ni kitendo cha ibada au uchamungu. Baadhi ya Waislamu wanaotumiwa na Taghut wanaogopa sana kifo. Wanaziogopa hata Aya za Quran kuhusu changamoto ya kifo: Bila shaka sisi tunahuisha na kufisha, na marejeo ni kwetu Qur(50:43) Na sisi ndiyo tunaohuisha na tunaosha; na sisi ndiyo warithi (wa yote hayo wakati ambao hapana kitakachokuwa kihai) Qur(15:23) N a ye n d i ye aliyekuhuisheni kisha atakufisheni, kisha atakufufueniQur (22:66) Na kwamba Yeye ndiye anayeleta ya kufurahisha na kuhuzunisha. Na kwamba Yeye ndiye Afishaye na kuhuisha Qur(53:43:44). Sisi tumekuwekeeni mauti, basi hatutashindwa (kukufueni wala) Qur(56:60) Ni mtazamo wa kimapinduzi tu uliyo ndani ya kitabu cha Mwenyezi Mungu, ndiyo unaoweza kuondoa vipengele vyote

Uislamu na Mapinduzi - 2
v ya wo g a wa k i j i n g a kwa Waislamu. Baada ya Waislamu kujawa na hamasa hii ya kimapinduzi, n d i p o wa t a k a p o we z a kukabiliana vilivyo na Taghut. Waislamu wa awali walipokuwa tayari wameshajengwa kwenye msingi huo wa kimapinduzi, Aya zifuatazo za Quran zilishuka: Basi waandalieni nguvu mziwezazo (silaha) na mafarasi waliofungwa tayari tayari, ili kwazo muogopeshe maadui wa Mwenyezi Mungu na maadui zenu.. Qur (8:60). Kwa yakini Mwenyezi Mungu anawapenda wale wanaopigana katika njia yake safu safu, kama kwamba wao ni jengo moja lililokamatana barabara Qur(61:4). Na nyote piganeni na makari kama wao wote wanavyopigana nanyi.. Qur(9:36) Na piganeni katika njia ya Mwenyezi Mungu na wale wanaokupigeni wala msipindukie mipaka (mkawapiga wa s i o k u p i g e n i ) Q u r (2:190). Na piganeni nao mpaka kusiwe na mateso (wao kuwatesa waislamu bure), na dini iwe kwa ajili ya Mwenyezi Mungu tu Qur(2:193). Ewe Mtume (wa Mwenyezi Mungu)

Makala

RAMADHAN 1434, IJUMAA JULAI 26 - AGOSTI 1, 2013


Kaaba. Miongoni mwao, alikuwa Abdulla bin Saad, Abdulla bin Khattal na waimbaji wake wawili wa kike, ambao mara nyingi waliimba nyimbo za kumkashifu Mtume: Wa m a l i z e n i h a t a mkiwaona wamejificha k w e n y e K a a b a N i agizo la kimapinduzi kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, ambalo limebaki mpaka leo kama mafundisho kwa Waislamu wote duniani. Sera zote hizo na vitendo vya kimapinduzi vilivyofanywa na kipenzi chetu, Mtume Muhammad (saw),ndiyo leo hii vinapingwa na jumuiya ya kimataifa, zikiwemo t a a s i s i z i n a z o i t wa z a kupigania haki za binadamu. Hata mawazo ya baadhi ya Waislamu, yanaweza kuhoji taswira ya kimapinduzi ya Mtume wa Mwenyezi Mungu, kama ilivyo ndani ya Quran: Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Na walio pamoja naye ni wenye nyoyo thabiti mbele ya makafiri na wenye kuhurumiana wao kwa wao Qur(48:29). Kwa kifupi suala ndiyo hilo. Haiba ya kimapinduzi ya Mtume wa Mwenyezi Mungu imetoweka. Ujasiri wake kimapambano haupo kwenye akili na nyoyo za mamilioni ya wale wanaodai kumfuata. Hapa kuna kazi kubwa sana ya kukarabati haiba ya kimapinduzi ya kiongozi wetu mkuu na mwalimu.

AN-NUUR

wahimize walioamini waende vitani Qur(8:65). Enyi mlioamini! Mkutanapo vitani na wale waliokufuru msiwageuzie migongo (mkakimbia) Qur(8:15). Aya hizo na nyingine nyingi ndani ya Qur an zinatosha kuondoa taswira potofu ya Mtume Muhammad (saw), ambayo Waislamu poa (moderates) wa leo wanataka kuenga. Mtume wa Mwenyezi Mungu alikuwa ni mwanamapinduzi hasa wa Kiislamu. Amekamilika idara zote. Mtume ambaye ndiye kiigizo cha Waislamu wote, alishiriki vita 27 ikiwemo misafara. Aliagiza kuangamizwa kwa watu 400 wa kabila la Bani Quraida, waliotaka kuwahujumu Waislamu baada ya makubaliano, akiwemo kafiri mmoja aliyeitwa Ubay bin Khalaf. Agizo la Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa makamanda wake, wakati wa ukombozi wa Makka (Fathu Makka), lilikuwa wasimuue mtu yeyote, isipokuwa kama mtu huyo alikuwa na nia ya kuwaua Waislamu. Lakini pamoja na hayo, kuna baadhi ya watu Mtume aliagiza wauawe, hata kama wangekutwa wamejisalimisha ndani ya

RAMADHAN KARIM
Funga na Hukmu zake, Watu 10 Walioruhusiwa kula Mchana wa Ramadhani, Mambo 10 yasiyoharibu funga Maswali na majibu

SWAUMU YA RAMADHAN

FUNGA NA HUKMU ZAKE

VINAPATIKANA MSIKITI WA MTORO KATIKA DUKA LA SAIMU GWAO NA IBN HAZM MEDIA CENTRE Mawasiliano: 0713 471090

SHEIKH NURDIN KISHKI

Jipatie vitabu vyenye mafunzo ya Funga ya Ramadhani, vilivyoandaliwa na Sheikh Nurdin Kishki kama vile:- Hadithi 30 kuhusu Funga ya Ramadhan. Hukumu za Funga ya Ramadhan. Ipi Idadi sahihi ya Swala ya Tarawehe. Vingine ni Ndoa Talaka na Eda. Pamoja na Uislamu si Dini ya Ugaidi. Kwa mahitaji ya jumla na reja reja, ka dukani kwa Saimu Gwao, Msikiti wa Mtoro au Ibn Hazim MediaCentre. Simu:-0713 471 090, 0715 825 672, 0773 194 646.

10
Nabtadi kuangaza, Sunnah hii kwa kaumu, Si sawia kuibeza, kwani ni Sunnah adhimu, Si nyingine nadokeza, Tarawehe ya msimu, Sunnah hii ya msimu, kwanini twaipuuza.

Mashairi/Habari

RAMADHAN 1434, IJUMAA JULAI 26 - AGOSTI 1, 2013

AN-NUUR

Tarawehe, si sunnah tu !

Si sunnah twajisemeza, kupunguza umuhimu, Kathiri twaipuuza, kwa ghururi ya rajimu, Ya kwake twayatukuza, japo ya kyendawazimu, Sunnah hii ya msimu, kwanini twaipuuza. Nini tutamueleza, Hakimu wa mahakimu , Hilo ka tuuliza, siku ile ya hukumu, Yu nani wa kumjuza, amama atakadamu, Sunnah hii ya msimu, kwanini twaipuuza. Twadunisha yenye izza, twaadhimisha ya ghamu, Yatotunyima mwangaza, kwa la kaburi dhwalamu, Akhera nako ni kiza, na mzomzo nadamu, Sunnah hii ya msimu, kwanini twaipuuza. Yalo laghwu twatukuza, ya kheri hatuna hamu, Karata kutwa twacheza, pasipo kukosa hamu, Na nikahi twachombeza, bayana kwa maharimu, Sunnah hii ya msimu, kwanini twaipuuza. Kwa pool twajitokeza, lilosheheni haramu, Kamari linoikuza, kwa kulisi kaumu, Allah alotukataza, twapokezana kwa zamu, Sunnah hii ya msimu, kwanini twaipuuza. Kucheza bao twaweza, mchana kutwa twadumu Wasaa twaupoteza, kwenye dhumna kukumu, Na runinga zatumeza, kama joka la mdimu, Sunnah hii ya msimu, kwanini twaipuuza. Thamaniya metimiza, risala yangu metimu, Kwa Mola kujisogeza, si kwa faradhi kutimu, Bali kujinyenyekeza, kwa sunnah kujilazimu, Sunnah hii ya msimu, si vyema kuipuuza. ABUU NYAMKOMOGI MWANZA.

Mkenya ashinda kuhifadhi Quran Dar


Na Shaban Rajab
MOHAMMED Al Ahdal kutoka nchini Kenya, ameibuka mshinda wa kwanza katika fainali ya shindano la kusoma na kuhifadhi Quran lililofanyika Masjid Idrissa, Kariakoo jijini Dar es Salaam Jumamosi iliyopita. Kufuatia ushindi huo, mgeni rasmi katika m a s h a n d a n o h a yo , Mbunge wa jimbo la Ilala Bw. Mussa Azzan (Zungu), alimkabidhi mshindi zawadi yake ambayo ni fedha taslim shilingi milioni moja. B w. A l A h d a l alishindia kiasi hicho cha fedha ambazo ndizo zilizokuwa zawadi ya mshindi wa kwanza, baada ya k u wa z i d i we n z a k e wanne alioingia nao hatua ya fainali. M s h i n d i wa p i l i katika mashindano hayo alikuwa ni Zubeir Bakar kutoka Dar, ambaye aliweka kibindoni kitita cha shilingi laki saba huku nafasi ya tatu ikichukuliwa na Abdallah Mohammed S a l e h wa D a r p i a , ambaye alipata zawadi ya shilingi laki tano na nafasi ya nne ilichukuliwa na Hussen Yahya kutoka Kondoa mkoani Dodoma, aliyezawadiwa kitita cha shilingi laki tatu. Nafasi ya tano ilikwenda kwa Yahya Hussen wa Dar ambaye alipata laki tatu pia. Katika hatua ya awali ya mashindano hayo,

MSIKITI uliojengwa na Taasisi ya Africa Islamic Relief of Kuwait katika Shule ya Sekondari ya Kiislamu ya Aljebra Kigamboni Dar es Salaam, umekabidhiwa shuleni hapo na Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Sami Mohamed hivi karibuni.

Swaumu na ndimi zetu


Ulimi tunu adhimu, ya Manani kwa insani, Ulimi tangu kadimu, kwa uneni namba wani, Ulimi mwema mwalimu, na muovu kwa waneni, Ndimi zetu tuchungeni, wafungaji Ramadhani. Ulimi johari njema, tukufu yenye thamani, Ulimi kwa watu wema, u lulu na Marani, Ulimi kwa taadhima, kwa kweli wakuthamini, Ndimi zetu tuchungeni, wafungaji Ramadhani. Ulimi wainajisi, waovu yako thamani, Ulimi wanakutusi, kwa kukupa sui nduni, Ulimi u ibilisi, eti mkubwa shetani, Ndimi zetu tuchungeni, wafungaji Ramadhani. Ulimi u sura mbili, kwa ya insafu mizani, Ulimi anokujali, kwa kheri wamuauni, Ulimi asokujali, kwa shari haumukhini, Ndimi zetu tuchungeni, wafungaji Ramadhani. Ulimi sasa kwanini, tuutie lawamani, Ulimi mimi sioni, ulaumiwe kwanini, Ulimi kosale nini, nuzeni ikhiwani, Ndimi zetu tuchungeni, wafungaji Ramadhani. Ulimi wa Ramadhani, wafungaji uchungeni, Ulimi kwa Qur-ani, kusoma utumieni, Ulimi za Adinani, kwao hadithi someni, Ndimi zetu tuchungeni, wafungaji Ramadhani. Ulimi utumieni, kumdhukuru Manani, Ulimi uzuieni, kuwasengenya insani, Ulimi ukalifuni, mema unene jamani, Ndimi zetu tuchungeni, wafungaji Ramadhani. Ulimi nanezo beti, zimeka ukingoni, Ulimi kwa khairati, nifanye mwenzo mwandani, Ulimi kwa shururati, uwe adui mubini, Ndimi zetu tuchungeni, wafungaji Ramadhani. ABUU NYAMKOMOGI MWANZA.

Maalim Seif afuturu na Masheikh Zbar


Azuru wagonjwa, wawa
Na Mwandishi Wetu

mahafidhi 39 kutoka mikoa mbalimbali wa s h i r i k i , a m b a p o walichujwa na kuibakia watano, ambao ndio

walioingia hatua ya fainali Jumamosi na Bw. Mohammed Al Ahdal kuibuka mshindi.

Mashindano hayo yameandaliwa na taasisi ya Khidmatul Quran Islamic Foundation ya jini Dar es Salaam.

*MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, amewahimiza W a i s l a m u kushirikiana na kusaidiana kwa dhati ili kudumisha umoja miongoni mwao. Alifafanua kwamba umoja na mshikamano ndio nguzo ya kuzidisha mapenzi miongoni mwa Waislamu, hivyo kutaka utamaduni huo uendelezwe kwa maslahi wananchi na taifa kwa ujumla. Maalim Seif alitoa kauli hiyo alipokuwa akitoa shukrani kwa Masheikh na wananchi waliojumuika naye katika futari a l i yo i a n d a a n y u m b a n i k wa k e Mbweni kwa ajili ya viongozi hao wa dini. Aliwashukuru Masheikh kwa kujitokeza kwa wingi

katika futari hiyo na k wa m b a , k i t e n d o hicho ni ishara ya mapenzi waliyonayo v i o n g o z i wa d i n i kwa viongozi wao wa kitaifa. Wa k a t i h u o huo, Maalim Seif amehitimisha ziara yake ya kutembelea wagonjwa na wawa kwa upande wa Unguja, baada ya kufanya ziara katika mkoa wa Mjini Magharibi. Aw a l i a l i f a n y a ziara katika wilaya za Kusini na Kati Unguja, yakiwemo maeneo ya Kizimkazi Mkunguni, Kijini Makunduchi, Jambiani na Ndani. Makamu huyo wa Rais pia alitembelea maeneo ya wilaya za Mjini na Magharibi na kuonana na wa g o n j wa k a t i k a maeneo ya Mbweni, Tomondo, Magogoni na Mji Mkongwe. Akiongozana na viongozi mbalimbali wakiwemo Waziri wa

Nchi, Osi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, Fatma Abdulhabib Ferej na Naibu Waziri wa Elimu Zahra Ali Hamad, Maalim Seif alianza ziara yake mapema asubuhi katika mitaa wa Mbweni matrekta, Kiembe samaki na Mwanakwerekwe, kabla ya kusitisha ziara hiyo kwa ajili ya kuhudhuria mazishi ya wanajeshi wawili wa Zanzibar wa l i o f a r i k i h u k o Darfur nchini Sudan. Hata hivyo alihitimisha ziara hiyo kwa kutembelea Jimbo la Mji Mkongwe, ambako alikwenda kuwajuilia hali na kuwafari mzee Salim Mzee wa Darajani na mzee Ali Yussuf wa Mkunazini. Maalim Seif pia anatarajiwa kufanya ziara akma hiyo katika mikoa ya Pemba hivi karibuni, ndani ya mwezi huu mtukufu wa Ramadhani.

11
Na: Mujahid Mwinyimvua

Makala/Habari
kutumika kama futari. Kundi la pili la vyakula ni vyakula vinavyokaa tumboni kwa muda mrefu (kiasi cha saa 6 mapa 8 au zaidi). Vyakula hivyo ni kama vile nafaka na mbegu ngano, shahiri, mtama, mahindi, mchele na maharage. Inashauriwa na wataalamu wa vyakula wa kiislamu kuwa vyakula kama hivi viliwe kama daku au usiku sana kwa wale wanaoshindwa kuamka na kula daku. Vyakula hivi vitawapa nguvu ya kuhimili mikiki mikiki ya saumu mchana na pia wataweza kumudu majukumu mengine ya kazi za mchana. Kwa hiyo, vyakula hivi ndio vizuri zaidi kuliwa kama daku. Katika funga nia kubwa ya Mwenyezi Mungu ni kupima utii wetu kwake, sio kutukomoa. Ndio maana funga ya Kiislamu inahimiza kula daku karibu na alfajiri na kutufuru mara tu jua linapo zama. Maana yake hizo ni takriban saa 14 (kati ya saa 24 za siku nzima) (pale ambapo mchana so mrefu) zinatosha kupima utii wetu kwa Mola. Hii maana yake ni kuwa Uislamu unazingatia namna Allah a l i v yo u u m b a m w i l i . Swaumu ya muda fulani ni tiba katika mwili, lakini ukizidisha muda sana bila mwili kuupa chakula, utakidhuru kiwiliwili hasa ubongo. Madai ya baadhi ya watu Baadhi ya wasiokuwa waislamu wanabeza na kudai kuwa sisi tunakula a l f a j i r, h a l a f u n d i o tunafunga. Wajaribu na wao kufunga japo kwa saa 12 tu wataona ugumu wa swaumu, hasa kwa a s i e f u n g a k wa i m a n i ya kumkubali Mola Muumba. Tunakumbuka Mwalimu Julius K. Nyerere alivyofunga na waislamu enzi za kudai uhuru, kabla ya jua kuzama alisema kichwa kinamuuma na apewe asproo. Masheikh wakamhamasisha asubiri mpaka muda wa kufuturu ulipoka. Hii ndio swaumu haina mchezo kwa mtu anaependa dunia tu. Kwa hakika kula na kufanya jimai ndio furaha kubwa katika maisha ya kidunia, na wengi wanamuasi Mola kwa hayo mawili, yaani tumbo na utupu. Makundi ya vyakula Wa t u w a n a o f u n g a wanatakiwa kuchagua na kula vyakula kutoka katika makundi mbalimbali kwa

RAMADHAN 1434, IJUMAA JULAI 26 - AGOSTI 1, 2013


mchicha, bamia, karoti, maboga, nyanya pamoja na mboga nyingine za asili kama mlenda, mchunga, figiri na mnavu. Mboga mboga zote ni chanzo kizuri cha vitamini na madini. Zaidi ya hayo, mboga mboga hasa za majani ni chanzo kizuri sana cha nyuzi nyuzi za lishe. Ingawa Quran imebainisha kuwa Mwenyezi Mungu katuumbia mboga mboga kwa manufaa yetu, lakini Waislamu wengi hawana habari kabisa na ulaji wa vyakula hivyo hasa wakati wanapo kula futari. Mafuta na sukari Mafuta ni pamoja na samli, siagi, mafuta ya nazi, majarini, mafuta ya alizeti, ufuta, mahindi, na mawese. Inashauriwa kuwa watu watumie zaidi mafuta yanayotokana n a m i m e a b a d a l a ya wanyama. Sukari ni pamoja na asali na ile inayotokana na miwa. Vyote hivyo vina kiwango kikubwa na nishati iliyomakinika (concentrated). Maji ya kunywa Wakat mwng wa usku wa Ramadhani ni muhimu sana mfungaj kunywa maji ili kupunguza hatari ya mwili kukaa muda mrefu bila maji ya kutosha mchana wa mfungo. Maji na juisi huondoa sumu kutoka katika mwili. Kwa mtu mzima anatakiwa anywe glasi nane za maji (kama lita moja na nusu). Wakati wa mfungo tujitahidi ili angalau tusiwe chini ya glasi nne kwa usiku wote. Pia, wafungaji wakumbke tulivyosema huko nyuma kuwa sio vizuri mtu kunywa kwa wingi chai au kahawa au soda ya coca cola/pepsi wakati wa kula mlo wa daku. Hii ni kwa sababu chai au kahawa au soda (ya coka cola na pepsi cola) hutengeneza mkojo mwingi, hivyo maji na madini yatapotea kwa njia ya mkojo kunapo kucha. Vilivile, milo yote wakati wa Ramadhani isiwe na chumvi nyingi au sukari nyingi kwa sababu mchana utakuwa na kiu sana na utapoteza maji kwa njia ya mkojo. Ni visuri kunywa tangawizi au mchai chai au maji ya moto kama mtu hawezi kula daku bila chai au kahawa nyingi. Kahawa au chai au soda (kina coka) ukinywa kabla ya usiku wa manane hakuna shida sana.

AN-NUUR

Daku ni chakula kinacholiwa usiku wa manane kwa ajili ya kujiandaa kufunga siku inayofuata. Kula daku ni jambo lililokokotezwa sana na Uislamu kama tunavyojifunza katika Quraa na Hadithi za Mtume Muhammad (rehma na aman zmfke): .....Na kuleni na kunyweni mpaka ubainike kwenu weupe wa Alfajir katika weusi wa usiku..... (Quran: 2:187). Mtume Muhamad (rehma na aman zmfke) amesisitiza sana kula daku. Tuone hadithi moja ifuatayo: Kuleni daku, kwani ipo baraka katika kula daku. Na tofauti ya fadhila ya funga zetu sisi na Ahlul Kitabu (Wayahudi na Wakristo) ni huko kula daku. Mlo bora wa daku Vy a k u l a v i n a w e z a kugawanywa katika makundi makuu mawili kwa kigezo cha muda wake wa kukaa tumboni. K u n d i l a k wa n z a n i vyakula vinavyo chukua muda mfupi, saa 2 mpaka 4 kusagwa. Mfano wa vyakula hivyo ni vile laini kama ndizi, viazi na matunda. Kama tuliona katika makala zilizopita, vyakula laini ni vizuri

UMUHIMU WA MLO WA DAKU

kila mlo wa futari na daku. Makundi hayo ya vyakula ni: Nafaka, vyakula aina ya mizizi na ndizi za kupika Kundi hili la vyakula linajumuisha nafaka kama mahindi, mchele, mtama, ulezi na ngano; ndizi za kupika na vile vya aina ya mizizi kama magimbi, mihogo na viazi. Vyakula hivi huupa mwili nishati (nguvu) vile vile vitamini, madini na protini kiasi kidogo. Vy a k u l a j a m i i y a mikunde, vile vya kokwa na vyenye asili ya wanyama Vy a k u l a v i l i v y o k o katika kundi hili ni pamoja na maharage, mbaazi, karanga, korosho, nyama, samaki, mayai na maziwa ambavyo vyote ni chanzo kikubwa cha protini. Pia, vyakula hivyo ni chanzo cha vitamini na madini. Matunda Matunda ni chanzo kizuri cha vitamini C, vitamini za aina nyingine na baadhi ya madini. Kundi hili linajumuisha matunda kama matikiti, zabibu, mapapai, maembe, machungwa, limau, ndimu, machenza, nanasi, pamoja na matunda pori kama ubuyu, mabungo na ukwaju. Mboga mboga Kundi hili linajumuisha matembele, kisamvu, majani ya maboga,

AL-MADRASATIL FADHAKIL iliyopo Kata ya KIBAMBA kwa kushirikiana na uongozi wa Madrasa pamoja na USTADH WA MADRASA wameandaa mashindano ya kuhifadhi QUR'AN JUZUU Tatu (3) na HADITHI ZA MTUME (S.A.W.). Kwa wanafunzi wa Madrasa Kata ya Mbezi na Kibamba. Ynayotarajiwa kufanyika Ramadhani ya (11) mpaka Ramadhani ya (14). Kwa ajili ya kuitukuza na kupata fadhira zaidi za Qur'an na sifa zaidi za Mtume Muhammad (S.A.W.) wanaomba Waislamu wote Watanzania wenye uwezo. Na wale wote waliojaaliwa na Allah (s.w.) wawasaidie ili kufanikisha kupata zawadi za kuwapa motisha vijana wote watakaoshiriki ambao ni zaidi ya (80) na wanawaomba kuhudhuria kwa watakaojaaliwa na Allah (s.w.). Kwa mawasiliano: 0757 375993 MWENYEKITI 0171 649313 USTADH

Msaada unahitajika

Inawaomba Waislamu kuchangia kamati ili iweze kusaidia Familia za Waislamu 52 walioko Jela. Tuma Mchango wako kwa Amiri Buiya S. Buiya 0763 241270 M.pesa na 0655 241270 Tigo pesa Katibu Ally Mbaruku 0777 816040 Ezy Pesa au 0784 816040 Airtel Money Kwa mawasiliano zaidi pia unaweza ukapiga simu kwa Namba hizo hapo juu. Unapotoa katika kheri, hakika umejiwekea akiba isiyoharibika.

Kamati ya Maafa ya Shura ya Maimamu Tanzania

12

AN-NUUR
MAKALA

Bismillah Rahmanir Rahim UMOJA WA WANAFUNZI WA KIISLAM WALIOSOMA NCHINI SUDANI (INTERNATIONAL UNIVERSITY OF AFRICA)

UWAWASU
INA WAALIKA WASOMI WOTE WALIOSOMA NCHINI SUDAN KUHUDHURIA MKUTANO MUHIMU MAALUMU NA FUTARI YA PAMOJA MKUTANO UTAFANYIKA KATIKA
UKUMBI WA ITIQAMA- MSIKITI WA ILALA

KARIBU NA MACHINGA COMPLEX

12

RAMADHAN 1434, IJUMAA JULAI 26 - AGOSTI 1, 2013

TAREHE 2-8-2013 sawa na mwezi 24 Ramadhani baada ya swala ya ijumaa. Sote tuwasili hapo Tafadhari mjulishe na mwingine asikose

Waliohifadhi Quran wapewe elimu ya juu


Na Bakari Mwakangwale
WAISLAMU wametakiwa kuwaendeleza kitaaluma vijana wanaohifadhi Qur an, ili waje kuwa viongozi bora katika jamii. Hayo yamesemwa na Ust. Hussein Ismail, akiwahutubia Waislamu na wazazi katika mashindano ya kusoma na kuhifadhi Qur an, yaliyofanyika katika viwanja vya Masjid Islamic Yombo, Jini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki iliyopita. Ust. Ismail, alisema hivi sasa kumekuwa na muamko mkubwa kwa Waislamu na wazazi kwa kuhifadhisha watoto kuisoma na kuihifadhi Qur an, ukilinganisha na kipindi cha nyuma. Alisema, jambo hilo ni la kheri kwa Waislamu na Taifa kwa ujumla kwani jamii inapokuwa na wasomi wengi wanayoua Qur an na wakaitafsri kwa matendo, husadia kujenga jamii iliyo na maadili. Lakini hayo hayawezi kufikiwa ikiwa vipaji vya watoto hawa vikaachwa hivi hivi, hawa Mahafidhi tunawatazama vipi? Ni jukumu la Waislamu na wa z a z i k u wa e n d e l e z a kielimu kwani kiongozi bora ni yule anaye mjua na kumuogopa Mungu wake. Alisema Ust. Ismail. Ust. Ismaili, alisema hivi sasa kila kituo cha Madrasa kuna juhudi zinafanyika za kuhifadhisha watoto Qur an, hivyo ni vyema kusoma vipaji vya watoto hao ili waweze kuendelezwa kitaaluma zaidi. Ust. Ismail, aliwaasa wazazi wa watoto hao na Waislamu kwa ujumla kutobweteka na kuridhika kwa kiwango walichofikia watoto wao katika kuhifadhi tu, bali wajue kuwa bado wanadhima pia katika kuwapa elimu zote kwani alidai katika Uislamu hakuna elimu ya Dini na elimu Dunia. Mtoto asizame katika Qur an pekee, zote ni elimu za Mwenyezi Mungu hakuna elimu ya dunia na elimu akhera yote hayo yanaenda sambamba ni makosa kutenganisha elimu. Alisema ust. Ismail. Alisema, hivi sasa kunachangamoto nyingi zinawak ab ili Wai slam u kutona na kushindwa kuwaanda vijana ambao katika utendaji wao wakawa

0713508555, 0769 757676, 0715455137

Vijana Zanzibar wataka Benki, Polisi Katiba Mpya


Na Haji Mtumwa, Zanzibar
TUME ya Mabadiliko ya Katiba imeshauriwa kuzipa uwezo wa kumiliki Bank Kuu nchi washirika wa Muungano wa Tanzania ili kuzifanya kuwa na uhuru wa matumizi ya kibenki ambayo yatawawezesha kukua kwa uchumi wao kwa haraka. Ushauri huo umetolewa na baadhi ya wajumbe wa B a r a z a l a K a t i b a lililoandaliwa na Jumuiya ya Vana Elimu na Maadili Z a n z i b a r ( Z AY E M ) wakati wakadili rasimu iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba Tanzania. Walisema kuwa ni vyema Tume ikaona kuwapo kwa umuhimu mkubwa wa kuziachia nchi washirika kwa Muungano, ziweze kuwa na Bank Kuu badala ya jukumu hilo kupewa Serikali ya Muungano pekee yake. Mwalimu Aleiy ambaye ni mjumbe wa baraza hilo alisema kuwa tume kuipa u m i l i k i wa B a n k K u u Serikali ya Muungano si jambo la busara, kwani alifahamisha kuwa kufanya hivyo ni sawa na kuzinyima uhuru nchi washirika katika masuala ya kifedha. Alisema kuwa uamuzi huo wa tume kwa kiasi fulani unaweza kuleta ucheleweshaji wa uchumi kwa nchi washirika kutokana na kubanwa na Serikali ya Muungano katika masuala yao ya kiuchumi ambayo yanategemea fedha. Aidha Wajumbe hao wakichangia rasimu hiyo walipendekeza kwa tume ya mabadiliko ya k a t i b a k u z i p a u we z o

FARIDA Jumaa (8), akisoma Qur an katika mashindano ya kuhifadhi Qur an, yaliyofanyika Yombo, Jini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita. wanazingatia maadili ya dini yao. Kwa upande wake, mgeni rasmi katika hafla hiyo ambaye ni Mkurugenzi msaidizi wa Chuo Cha M a r k a z i C h a n g o m b e , Doktour Swalahuden Maftaha, alisema mbora miongoni mwa watu ni yule aliyeisoma Qur an kisha akaifundisha. Aliwataka walimu wanaofundisha na kuhifadhisha Qur an, kutoa mafunzo pia kwa watoto hao kuisoma, kuihifadhi kisha kuizingatia ili waweze kukia lengo. Kila anayeifundisha Qur an atilie mkazo pia kwa kuzingatiwa ile maana yake, maana yale ni maamrisho k u t o k a k wa M we n ye z i Mungu kisha yafanyiwe kazi, ikiwa hilo litazingatiwa tunaweza kufika mbali. Alisema Doktour Maaha. Aidha, Mkurugenzi huyo wa Markazi Changmbe, aliwataka walimu wa Madrasa, kufundisha na kuhimiza ibada ya swala kwa vijana wanaowasomesha Qur an, kwani alidai haifai kwa anayeisoma Qur an, (hadhi) kisha asiwe mwenye kusimamisha swala. Jumla ya Madrasa nane zilishiriki katika mashindano hayo yaliyoandaliwa n a u m o j a wa M a d r a s a zinazohifadhisha Qur an, Yombo. Umoja huo ulianzishwa mwaka 2011, umesema m p a k a s a s a wa m e p a t a mafanikio kadhaa ikiwa ni kupata ongezeko kubwa la vana wanaohifadhi Qur an katika Madrasa hizo. Mafanikio mengine yametajwa kuwa ni umoja huo kutoa wanafunzi (Mahadhi) wanao kwenda kushiriki mashindano mbalimbali yakiwemo ya Afrika Mashariki. Umoja huo umesema, mbali ya mafanikio hayo lakini pia wamekutana na changamoto mbalimbali i k i we m o u p u n g u f u wa Misahafu, Juzuu na vitabu mbalimbali. Pia tuna uhaba wa maeneo ya kufundishia ikiwemo tatizo sugu la mishahara kwa walimu wanaohifadhisha na kufundisha Qur an. Tu n a o m b a wa d a u mbalimbali kutuunga mkono katika kuondoa changamoto hizo kwa lengo la kustawisha Uislamu na vana wetu kwa ujumla. Ulisema uongozi huo.

nchi washirika kila mmoja atumie fedha yake katika nchi yao ili kuondosha msongano wa maingiliaona ya kifedha. Walisema kuwa hatua hiyo itaziwezesha nchi washirika wa Muungano kujitegemea katika kukuza uchumi wao kwa kuwa na fedha yake badala ya kuwapo kwa fedha ya pamoja kwa nchi zote. Tunaamini wazi kuwa kila nchi mshirika wa Muungano wa Tanzania akatumia fedha yake katika nchi yake kwa kiasi fulani itasaidia sana katika kutafautisha nchi na nchi badala ya kuwapo kwa fedha ya pamoja, walisema wajumbe hao. Masoud Saleh a k i wa s i l i s h a k a z i z a vikundi alisema kuwa ni vyema kwa Tume ya mabadiliko ya katika ikaliondoa suala la Polisi kuwa la Muungano na badala yake suala hilo kuwa la nchi washirika. Alisema kuwa kazi kubwa ya Jeshi la Polisi ni kulinda raia na mali zao, hivyo ni vyema tume ikaona kuwa ili nchi washirika kuwa nguvu katika utawala wao hakuna budi suala hilo wakapewa wao badala ya kuwapo kwa Serikali ya Muungano. Kwa kuwa Jeshi l a Po l i s i l i n a k we n d a sambamba na mahitaji ya wananchi hivyo tunashauri kwa tume suala hilo wakaachiwa n c h i wa s h i r i k a h a s a ukaangali kila mmoja atakuwa na katiba ya nchi yake, alisema Masoud. Alifahamisha kuwa pindi suala hilo likaachiwa Serikali ya Muungano, i n a we z e k a n a l i k a t o a huduma kinyume na malengo yao, kutokana na kila nchi watakuwa na

Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Limited, S.L.P. 78495 Dar es Salaam.

Taasisi ya Khidmat Islamiya inawatanganzia Waislamu wote Safari ya Hijja kwa Gharama ya Dola 4450 tu. unaweza kulipa kwa awamu (Kuhijiwa) ni Dola 1450 tu. Kuondoka ni 5/10/2013 kurudi 27/10/ 2013 Piga Simu 0784 786680, 0713 986 671, 0774 786 680 E-Mail) hajjkhidmat@gmail.com , Tovuti (Website) www.khidmatislamiya.com

Safari ya Hijja Dola 4450 tu. 1434/2013

Markazi Ummu Suhail ni kituo cha kuhifadhisha Qur aan kwa Mabinti wa Kiislamu. Kituo ni cha bweni kipo mkoani Kilimanjaro wilaya ya hai. Umri: kuanzia miaka 13 na kuendelea. Kituo kitafunguliwa 9/08/2013 Inshaalah. Fomu za kujiunga zinapatikana msikiti wa Riadha, wahi nafasi ni chache Kwa mawasiliano zaidi tupigie simu namba 0754 029 518 Mlete mwanao apate elimu yenye manufaa.

14

RAMADHAN 1434, IJUMAA JULAI 26 - AGOSTI 1, 2013

AN-NUUR

15

RAMADHAN 1434, IJUMAA JULAI 26 - AGOSTI 1, 2013

AN-NUUR

16

RAMADHAN 1434, IJUMAA JULAI 26 - AGOSTI 1, 2013

AN-NUUR

You might also like