Professional Documents
Culture Documents
tz
Sauti ya Waislamu
Ni Diamond Jumapili
ISSN 0856 - 3861 Na. 1073 RAJAB 1434, IJUMAA MEI 31-JUNI 5, 2013 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=
Ya NECTA, propaganda kujadiliwa Bakwata, Jumuiya waikabili Serikali Wahoji USIRI, kuita Wakristo pekee Hali ya Sheikh Ilunga, India kuelezwa
CHUO Cha Kiislamu Cha Al-jazeera, cha Jini Mwanza, kimelikisha Mahakamani Gazeti la Mtanzania, kikidai dia ya Shilingi Bilioni Mbili, kufuatia kuripoti habari kuwa Chuo hicho kinaendesha mafunzo ya Ugaidi. Gazeti hilo litokalo kila siku, limefunguliwa mashitaka na Chuo hicho na kwa mara ya kwanza limefikishwa
Mahakamani April, 30, 2013, katika Mahakama Kuu ya Jijini Mwanza, kujibu mashitaka yanayolikabili, na kuahirishwa hadi Julai 16, 2013. Hata hivyo kesi hiyo imedaiwa kushindwa kusikilizwa na kulazimika Jaji anayesikiliza kesi hiyo Mh. Mwangesi, kuiarisha kufuatia mwakilishi wa gazeti hilo Jini Mwanza, kudai kuwa hakuwa na
Inaendelea Uk. 2
SHEIKH Ilunga Hassan Kapungu akiwa hospitalini nchini India. Picha ndogo juu kushoto ni mke wake akiimuuguza nchini humo.
2
S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786 Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM. www.annuurpapers.co.tz E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk Osi zetu zipo: Manzese Tip Top Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam
Tahariri/Habari
AN-NUUR
AN-NUUR
MAONI YETU
INATARAJIWA kuwa Waislamu watafanya kongamano kubwa katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam Jumapili ijayo. Katika kongamano hilo inatarajiwa kuwa pamoja na mambo mengine, kutazungumziwa uamuzi wa Serikali kujitoa kutahini somo la dini katika mitihani ya kitaifa. Habari za awali zinafahamisha kuwa, katika kufikia uamuzi huo, Serikali ilikutana na wadau wa elimu kutoka taasisi za Kikriso pekee bila kuwashirikisha Wa i s l a m u . H a t a B A K W A T A inayojulikana kama kipenzi cha Serikali na inayotambuliwa na Serikali kama msemaji na mwakilishi wa Waislamu, haikualikwa katika kikao hicho cha majadiliano. BAKWATA walipewa tu taarifa baada ya Serikali kukubaliana n a Wa k r i s t o , t e n a ikaambiwa kuwa taarifa hiyo iwe siri (wasiambiwe Waislamu?). Kama ilivyoelezwa katika habari yetu i n a y o o n g o z a , B A K W A T A wameshaiandikia Serikali kupinga uamuzi huo na kusajili malalamiko yao kwamba inakuwaje Serikali kukaa na upande mmoja tu wa jamii kupitisha maamuzi makubwa yenye athari kwa watu wote bila ya kuwashirikisha Waislamu. Kwa upande mwingine, taarifa za uhakika ni kuwa japo suala la mitihani ya kidato cha nne na sita ni la muungano, hata Serikali ya Zanzibar haikuarifiwa wala
kushirikishwa katika kupitisha uamuzi huu. Na mpaka BAKWATA na Islamic Education Panel wanawasilisha malalamiko yao Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, bado Serikali ya Zanzibar ilikuwa haapewa taarifa rasmi. Sisi tunajaribu kukiri: Kama Zanzibar ingekuwa kama ilivyo Rombo au Kibosho, kwa maana ya kuwa na idadi kubwa ya Wakristo kiasi cha asilimia 90 ya Wazanzibari wote, je, bado Serikali ingekaa bila ya kuishirikisha Zanzibar katika kujadili na kupitisha maamuzi makubwa kama hayo yanayohitaji ridhaa ya pande zote mbili za muungano? Hali kama hizi na utendaji kama huu, ndio aliowahi kusema Dkt. John Sivalon kwamba inakuwa tabu mtu kujua kwamba je, hili ni la Serikali au ni la Kanisa. Kwa upande mwingine, utendaji kama huu ndani ya Serikali, ndio unapelekea Waislamu k u s e m a k u wa k u n a mfumokristo usio rasmi kikatiba na kisheria unaoendesha mambo. Na ndio wanaoupiga vita kwa sababu unawabagua na kuwadhulumu Waislamu. Sisi tunasema kuwa kuwashutumu, kuwakemea na kutishia kuwachukulia hatua wanaodai kuwa kuna mfumokristo, sio ufumbuzi na wala hakuwezi kuondoa malalamiko na madai y a Wa i s l a m u . N a kama inadaiwa kuwa madai haya yatavuruga amani, basi kuwakemea hakutaleta amani. Amani ya kweli na ya kudumu italetwa kwa kuyatambua na kuyashughulikia madai ya wanaolalamika.
hati ya mashitaka. Wa k i o n g e a n a Mwandishi wa habari hizi, kwa njia ya simu kutoka Jijini Mwanza, viongozi wa Chuo hicho wamesema tayari wameshalifungulia mashitaka gazeti hilo, baada ya kukaidi kukanusha tuhuma dhidi ya Chuo chao. Mjumbe wa Bodi ya Chuo cha Al-Jazeera, Sheikh Jabir Katura alisema kwamba wameshalikisha gazeti hilo katika Mahakama Kuu ya Jini Mwanza, na kukutana na mwakalishi wao, aliyedai hakuwa amejiandaa. Sheikh Jabir Katura, alisema kuwa mwakilishi huyo aliye h a p o J i j i n i M wa n z a aliieleza Mahakama kuwa walikuwa hawana taarifa rasmi, hivyo shauri hilo lililazimika kuahirishwa. Mwenyekiti wa Chuo hicho, Alhaj Ramadhani Mazige, akizungumzia kilichojiri katika kesi h i yo , a l i s e m a a wa l i waliliandikia gazeti hilo, wakiwataka wathibitishe yale waliyoandika kuhusu Chuo chao kupitia Gazeti lao la Mtanzania katika matoleo matatu, lakini hawakufanya hivyo. Tu l i w a p a m u d a wa wiki mbili ili wathibitishe habari zile, wakashindwa kufanya hivyo, na kuwaeleza nia yetu ya kuwakisha M a h a k a m a n i wa s i p o f a n ya h i v yo , lakini hawakuonyesha ushirikiano wowote. Mpaka muda huo ukaisha. Alisema Alhaji Mazige. Alhaj Mazige, alisema kesi hiyo iliyo chini ya Jaji Mwangesi, imekaa katika sura mbili kwanza, Al-Jazeera inadai fidia ya kuchafuliwa na kudhalilishwa hivyo ilipwe kiasi cha Shilingi Bilioni Moja. Ama alisema, madai
ya pili ni ya Ramadhani Maziga, ambaye ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Al-Jazeera, na ni Diwani wa Kata ya Nasio, aliyetajwa k wa k u d h a l i l i s h w a kwa kutajwa kwa jina akidaiwa anawapiga majini viongozi wakubwa hivyo kushindwa kwenda kushughulikia kadhia ya chuo chake ikiwa ndiye anawakaribisha Al Shabab na magaidi wengine. Kwa kuwa alitajwa kwa jina katika gazeti hilo, na yeye naye ametaka kuthibitishiwa hayo madai yaliyoandikwa na gazeti hilo la Mtanzania, naye alipwe fidia ya Bilioni moja, hivyo jumla gazeti hilo linatakiwa litoe fidia ya Shilingi Bilioni mbili kwa misingi hiyo. Alisema Alhaj Mazige. Awali Alhaj Mazige, alilieleza gazeti hili kuwa , April 30, 2013, walika Mahakamani, ambapo alijitokeza mwakilishi wao, aliyemkumbuka kwa jina moja la Fred, ambaye mbele ya Mahakama, alidai kuwa ni mwakilishi wa Mkoa wa Mwanza wa gazeti hilo. Alisema, mwakilishi huyo, alidai Mahakamani hapo kuwa alipigiwa simu na Makao Makuu ya Gazeti hilo Dar es Salaam, kwamba leo (April 30, 2013) ni kesi yao hivyo ahudhurie Mahakamani. Akiwa Mahakamani hapo, Alhaji Mazige, alidai mwakilishi huyo aliieleza Mahakama kuwa hajapata maelezo ya mashitaka yanayowakabili, zaidi ya kutakiwa na wakuu wake ake hapo tu. Alhaj Mazige, alisema wakili wao aliyemtaja kwa jina la Shekh Waziri, alithibitisha kuituma hati hiyo ya mashitaka Dar es Salaam, hata hivyo alidai Jaji anayesikiliza kesi hiyo, aliamuru waondoke wakakamilishe zoezi hilo, na mwakilishi wao
apatiwe pia. Hakimu alitupa siku 21, turekebishe utata huo kisha tumpelekee majibu ya pande zote mbili, huku akitupangia tarehe ya kusikilizwa tena kesi hiyo ambayo itakuwa Julai 16, 2013. Alisema Alhaji Mazige. Alhaji Mazige, alisema siku hiyo hiyo ya April 30, walishughuliki suala hilo, na kumkabidhi mwakilishi wa gazeti hilo (Fred) akasaini na kupeleka kopi Mahakamani kama alivyo amuru Jaji, na sasa alidai wanasubiri majibu kutoka kwa gazeti la Mtanzania. Mpaka hivi naongea na wewe, ( Jumatano wiki hii) hatujayapata majibu yao toka April 30, 2013, na tulipewa siku 21, sisi tuandike na wao wajibu, hatujui watatoa lini majibu yao, sisi tuna subiri tarehe ya kwenda Mahakamani, ifike. Alisema Alhaji Mazige. Alhaji Mazige, alisema kwa mara ya kwanza zilipotoka habari hizo walivuta subira, lakini katika toleo lingine lilofuata waliendelea na habari hizo, ambazo aliziita ni za uzushi zenye lengo la kuupaka matope Uislamu na Waislamu nchini, jambo ambalo liliwapa mshtuko mkubwa. Alisema, iliwalazimu wawaandikie barua ya k u wa t a k a wa s i t i s h e habari zao kwa kuwa hazina ukweli na ni za uchochezi, huku wakiwatahadharisha kuwa endapo w a t a e n d e l e a watawachukulia hatua za kisheria. H a t a h i v yo a l i d a i walipuuza, nakutoa tena kwa mara ya tatu habari hizo zikiwa na uzushi uleule. Alhaji Mazige, alisema gazeti hilo liliandika habari hizo katika matoleo yake tofauti tofauti kwa kupamba vichwa vya habari vikisema, Hofu ya Alqaida nchini, Njia fupi ya Mwanza hadi AlJazeera.
Habari
AN-NUUR
WAISLAMU Jijini Dar es Salaama wanatarajia kufanya Kongamano ambalo pamoja na mambo mengine, watajadili dhamira ya Serikali ya kufuta Masomo ya Dini mashuleni. M e n g i n e yatakayozungumziwa ni juu ya propaganda inayoendelea nchini a m b a p o Wa i s l a m u w a m e k u w a wakibambikiziwa shutuma mbalimbali kwa lengo tu la kuwapaka matope. Kwa mujibu wa waandaaji wa Kongamano hilo, Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Kongamano hilo litafanyika siku ya Jumapili ya Juni 2, 2013, katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Upanga, Jijini Dar es Salaam. Taarifa hiyo ilisema kuwa Kongamano hilo linatarajia kuanza majira ya saa tatu asubuhi na kuhitimishwa saa nane mchana, na kuwataka Waislamu kuka kwa wingi. Kongamano hilo linafuatia kikao cha pamoja cha Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini wakiwepo Baraza Kuu la Waislamu nchini, BAKWATA ambapo walihoji hatua ya Serikali kukutana kisiri na taasisi za Kikristo na kukia hatua ya kufuta mitihani ya Somo la dini katika mitihani ya taifa. Katika kikao hicho kilichofanyika katika o f i s i z a TA M P R O
mapema Jumatatu wiki hii, mjumbe kutoka Bakwata alisema kuwa wao washaiandikia Serikali kupinga uamuzi huo na kuhoji ni kwa nini jambo hilo limefanywa SIRI bila ya kuwashirikisha Waislamu. Kwa upande mwingine, Islamic Education Panel walitoa taarifa wakisema kuwa nao washaiandikia Serikali kupinga jambo hilo na kusema kuwa limefunikwa na utata mwingi na hasa ilivyokuwa Serikali ilikaa na Wakristo pekee na kuchukua maamuzi ambayo yatakuja kuathiri Waislamu hasa ikizingatiwa kuwa kila mwaka Vyuo Vikuu vya MUM, Chukwani, Tunguu na Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar, vinachukua wanafunzi waliofaulu somo la Islamic Knowledge kwa ajili ya kozi za Sheria na Shariah, I slamic Banking/Marketing pamoja na kozi za
Ualimu na Islamic Studies. Taarifa za kiuchunguzi zinaonyesha kuwa pamoja na kuwa suala la mitihani ya kidato cha nne na sita ni la Muungano, l a k i n i Wi z a r a y a Elimu na Mafunzo ya Amali, Zanzibar, haikushirikishwa katika suala hili na hadi Waislamu Bara wanakutana kujadili suala hili, bado Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilikuwa haijaariwa. Kwa mujibu wa taarifa za waandaaji wa kongamano hilo, lengo kubwa ni kuwapa taarifa Waislamu na kuwaunganisha katika kukabiliana na changamoto kama hizi. Pia yatazungumziwa matukio yanayoibuka mara kwa mara hapa nchini na kuhusishwa Waislamu moja kwa moja hata kabla ya kufanyiwa uchunguzi, jambo ambalo ni
malengo ya mapinduzi
Na Mwandishi Wetu
Inaendelea Uk. 7
WAZANZIBARI wanapodai kuwa na mamlaka kamili ya nchi na dola ya Zanzibar, wanatetea haki na maslahi ya nchi yao, na kwamba hakuna sababu ya kubezwa wala kupuuzwa. Hayo yamesemwa na Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, katika ukumbi wa Salama hoteli ya Bwawani, wakati akifungua kongamano la pili la kitaifa linalohusu Maridhiano ya Wazanzibari. Maalim Seif amesema, dhamira ya msingi ya ukombozi wa Zanzibar kupitia Mapinduzi ya Januari 12, 1964, ni Zanzibar kuweza kujitawala yenyewe na kuwa na mamlaka kamili. Hata hivyo akasema kuwa dhamira ya Mapinduzi ilianza kukiukwa baada ya kutiwa saini kwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambao uliipunguzia Zanzibar mamlaka yake. Kwa hiyo akawataka wanakongamano hao kuwaongoza wajumbe wa mabaraza ya katiba katika kutetea maoni na maslahi ya Zanzibar. Maalim Seif amefahamisha kuwa akiwa ni kiongozi wa Zanzibar, atasimamia na kutetea mawazo ya Wazanzibari walio wengi katika kupata haki zao za msingi ndani na nje ya Zanzibar.
SHEIKH Ilunga Hassan Kapungu akiwa hospitalini nchini India hivi karibuni.
Akifafanua zaidi kuhusu msimamo wake amesema hiyo haina maana kuwa Wa z a n z i b a r i h a w a t a k i Muungano, bali wanataka kuwepo kwa Tanzanyika na Zanzibar zenye mamlaka kamili, halafu kuwepo na muungano wa mkataba, ili kila nchi iweze kuendesha mambo yake kwa uhuru. Kuwa na mamlaka kamili sio kwa maslahi ya watu wachache bali kwa watu wote, ni kama mvua, yaani inaponyesha mimea yote inanawirika, alifafanua Maalim Seif na kuongeza, Tu n a t a k a k u r e j e s h a heshima ya nchi yetu, tuwe na sera na Wizara yetu ya Mambo ya Nje, bendera yetu ipepee nchi za kigeni, Umoja wa Mataifa na Jumuiya nyengine za Kimataifa zikiwemo Jumuiya ya Madola, Umoja wa Afrika na Jumuiya ya Afrika Mashariki. Akizungumzia kuhusu mafanikio ya maridhiano amesema yamerejesha umoja wa Wazanzibari na kuondosha uhasama na chuki miongoni kwa wananchi. Ameipongeza kamati ya maridhiano chini ya Mwenyekiti wake Mzee Hassan Nassor Moyo kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kuyaendeleza maridhiano hayo na umoja wa Wazanzibari. Nae Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano ambaye ni mwanasiasa mkongwe wa Zanzibar Mzee Hassan Nassor Moyo amesema maridhiano hayo yaliyoasisiwa na Rais Mstaafu wa Zanzibar Dkt. Amani Abeid Karume na Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad, yameondoa fitna na chuki zilizodumu kwa muda mrefu miongoni mwa wananchi. Amesema kamati yake inaisubiri kwa hamu kubwa rasimu ya Katiba mpya itakayotolewa, ili waweze kuichambua kuona kama imezingatia maoni ya wananchi na maslahi ya Zanzibar. Akiwasilisha mapendekezo ya kamati hiyo Mzee Moyo amesema kila nchi katika Muungano inapaswa kuwa na uraia wake, sera yake ya mambo ya nje na Muungano uwe na JINA la Muungano wa Jamhuri za Tanzania au United Republics of Tanzania.
MATUKIO/MAKALA
AN-NUUR
Kujisajili: Shilingi 50,000/= kwa mtu mmoja. (Kwa ajili ya cheti cha ushiriki, Kitabu cha muongozo, na chakula kwa siku zote tatu) Muhimu: Washiriki watapatiwa vyeti na kitabu cha muongozo wa ufugaji kuku kilichoandikwa kwa lugha ya Kiswahili ili kukidhi haja. Pia watapata fursa ya kutembelea na kusoma kwa vitendo (eld) Kujisajili: Ili kujisajili tuma SMS kwenye namba 0714 151532, 0767151532, 0716574266 au ka TAMPRO Makao Makuu, Magomeni Usalama, jirani na Halmshauri ya Manispaa ya Kinondoni. Wahi kuijiandikisha kwani nafasi ni chache. Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kupitia 0714 151532, 0767151532, 0716574266 au info@tampro.org
Masjid Aswabirina
Kitunda kibeberu Dar es salaam. Uongozi wa Masjid Aswabirina Tunapenda kutoa shukran zetu za Dhati kwa Waislamu wote waliofanikisha Msikiti huu kukia hapa ulipo. Hivyo basi tunatarajia kufanya ufunguzi wa msikiti huo tarehe 28 Shaaban ili uanze kutumika Rasmi katika mwezi mtukufu wa Ramadhani. Ili kufanya ufunguzi huo tunaomba msaada wenu wa kujengewa choo, Kisima cha maji pamoja na ununuzi wa Uwanja uliopo mbele ya Msikiti gharama ya uwanja huo ni Milioni Tisa ( 9) kwa ajili ya upanuzi wa ujenzi wa shule ya awali na chuo. Pia Tunaendelea kuwaomba wahisani waendele kutusaidia ili kufanikisha kukamilika kwa ujenzi huu. Tuma Mchango wako Account Na: K.C.B 3300386233 jina la A/c Aswabirina au kwa Tigo Pesa 0714 565619 au Mpesa 0753 673820 Amir Khatibu Yunus
Masjid Mtambani inawatangazia Waislamu wote kuwa itafanya mhadhara mkubwa Inshaalah siku ya Ijumaa (Leo) Tarehe 31/05/2013. Muda: Baada ya Swala ya Ijumaa. Mahala: Masjid Mtambani Wahadhiri: Ust. Filambi na Ust. Siraj Kutoka Morogoro Wabillah Tauq
Muhadhara Mtambani
5
Na Mwandishi Maalum KAULI ya Umoja wa Afrika kukosa imani na Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC), inaonekana kuwiana na mtizamo wa wasomi mbalimbali mashuhuri ambao wanaituhumu ICC kupoteza dira na uhalali wake. Mmoja wa wasomi hao mashuhuri ni Profesa Noam C h o m s k y, r a i a m s o m i bingwa wa Marekani ambaye anamwona Rais Obama kama muhalifu ambaye inabidi akishwe ICC. Katika kikao chao kilichofanyika jijini Addis Ababa hivi karibuni, viongozi hao wameishutumu ICC kama chombo kisicho na uadilifu, chenye ubalakala (double standard) kinachoandama zaidi viongozi wa Afrika. Akitoa shutuma hizo, Waziri Mkuu wa Ethiopia ambaye ni Mwenyekiti mpya wa Umoja wa Afrika, Hailemariam Desalegn, anasema kuwa, Mahakama ya Uhalifu ya KimataifaInternational Criminal Court (ICC) ilianzishwa ili kuzuiya watu kutesa na kuuwa wengine bila ya kuchukuliwa hatua. Hata hivyo akasema kuwa hivi sasa mahakama hiyo imepoteza wasifu wake na kuwa kama chombo cha kuwasaka Waafrika. The intention was to avoid any kind of impunity but now the process has degenerated into some kind of race hunting. Alisema Hailemariam Desalegn huku akihimiza kuwa watakisha
Habari za Kimataifa/Tangazo
AN-NUUR
AU wamesema kweli
ICC imepoteza dira na uhalali wake Raia tu wa USA hawezi kusimama ICC ICC Ikithubutu Uholanzi inavamiwa Chomsky aeleza ugaidi wa Bush, Blair
6
Na Omar Msangi
WASWAHILi wana msemao, mgeni njoo mwenyeji apone. Hivi sasa zimepamba harakati za ujio wa Rais wa Marekani Barack Obama anayetarajiwa kuingia nchini Julai 1, 2013 akiandamana na jumla ya watu wasiopungua 1,000. Kwa mujibu wa taarifa za baadhi ya vyombo vya habari wiki hii, kuna wasiwasi mkubwa kwamba huenda hoteli zenye hadhi ya kimataifa zilizopo jijini Dar es Salaam, hazitatosheleza malazi ya wageni. Iwapo taarifa hizo kama zilivyoripotiwa katika baadhi ya magazeti ni kweli, hatujui Serikali yetu itafanya utaratibu gani kuhakikisha kuwa nchi haingii aibu kwa kushindwa kuwapatia wageni wetu mahali pa kulala. Kwa upande mwingine, Serikali kupitia Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mheshimiwa Bernad Membe, imesema kuwa inaandaa taratibu za mapokezi ikiwa ni pamoja na kuchapisha sare maalum zitakazovaliwa na vikundi vya burudani. Vitu vingine ni fulana na kofia maalum kwa mapokezi hayo. Lakini pia Serikali imetoa taarifa ya awali ikionyesha jinsi Watanzania watakavyonufaika na ujio huo. Kubwa linalosemwa hivi sasa ni kuwa tumeaminika k w a Wa m a r e k a n i m p a k a tumeongezewa donge la fedha za fuko la Millennium Challenge Corporation ( MCC), na kwa hiyo mengi yanatarajiwa kuletwa zikiwemo fursa za kibaishara. Pamoja na ukweli na uzuri wa yote hayo, nadhani yapo mengine mawili ambayo kama tukijipanga vizuri, tunaweza kuyapata kutokana na ujio wa Rais Obama. Na kwa hakika
MAKALA
AN-NUUR
Inatoka Uk. 5 (kwamba Rais wa Marekani naye asakwe kupelekwa ICC kama anavyosakwa Omar Hassan El Bashir na Uhuru Kenyatta!). Alisema Chomsky akijibu s w a l i k u t o k a RT k u w a iwapo anadhani kuwa kuna uwezekano wa kuona wahalifu wa vita Weupe kutoka mataifa yenye himaya kusimama kizimbani jinsi Rios Montt alivyosimama? Efrain Rios Montt alikuwa Rais wa Guatemala ambaye anashutumiwa kwa kufanya mauwaji ya kutisha kwa watu wake ambapo inakisiwa kuwa alikaribia kuhilikisha kabisa kabila la watu wa ki-Maya. Chomsky anasema kuwa haki haiwezi kutendeka kama Marekani nayo haitasimama kizimbani kwani ilihusika sana katika mauwaji hayo wakati ikiendesha siasa za kibeberu Guatemala na Latin Amerika kwa ujumla. Marekani ilihusika na
AU wamesema kweli
jambo hilo katika hatua zake zote, Mwishowe kulikuwa na makala asubuhi hii ikisema kuna kitu kinakosekana katika mashitaka hayo, nafasi ya Marekani. Nilifurahi kuona makala hiyo. Akijenga hoja yake kuhusu uhalifu wa Bush na Blair, Prof. Chomsky anasema kuwa hakuna uhalifu mbaya unaozidi ule wa kuvamia nchi ya watu, kufanya mauwaji ya raia wasio na hatia na kuharibu miji na vijiji. Akasema kuwa kuna kanuni zinazorudi nyuma miaka 800 wakati wa Magna Carta inayosema kuwa watu hawawezi kuuawa na dola bila kuhukumiwa na raia wenzao. Akasema, visingizio vyovyote vitakavyotolewa juu ya uvamizi wa Marekani, haviwezi kutengua kanuni hii ambayo ina umri wa miaka 800. Nilizungumzia Magna Carta, ambayo ina umri wa miaka 800, lakini kuna kitu kingine ambacho kina umri wa miaka 70 takriban. Kinaitwa jopo la Nuremberg, ambayo ni sehemu ya msingi wa sheria ya sasa ya kimataifa. Inaelezea uvamizi kama jinai kubwa zaidi, inayotofautiana na makosa mengine ya kivita, na inajumuisha uovu mwingine unaofuata. Uvamizi wa Marekani na Uingereza ilikuwa ni mfano bora zaidi wa uvamizi (wa nchi huru), hilo halina maswali. Ambayo ina maana kuwa walikuwa wawajibika kwa maovu yote yaliyofuata kama mabomu (ya kujitoa mhanga, kutegwa,
Inaendelea Uk.10
n.k.) Mizozo mikali ilianza, ikaenea kote katika ukanda huo. Ni kweli kuwa ukanda huo unachanwachanwa na mzozo huu. Hii ni sehemu ya uovu uliofuata. Alisema Prof. Chomsky akionyesha jinsi uvamizi wa Marekani katika nchi ya Iraq ulivyoleta balaa kubwa. Akasema kuwa sio tu kwamba inakuwa vigumu kumkisha Mahakamani Rais wa Marekani au Waziri Mkuu wa Uingereza, lakini ICC haiwezi kumgusa raia tu wa kawaida wa Marekani. Akifafanua akasema kuwa kuna sheria ya Marekani ambayo barani Ulaya inaitwa Sheria ya kuvamia Uholanzi. Hiyo ni Sheria ya Bunge la Marekani iliyosainiwa na Rais, ambayo inamruhusu Rais kutumia nguvu
kumwokoa raia wa Marekani aliyepelekwa The Hague (ICC) kujibu mashitaka. Akizungumzia kwa upande wa Rais Obama anasema kuwa, huyu ni Rais ambaye anatumia mbinu ya kuuwa kama namna ya kuboresha sera za Rais aliyemtangulia George W Bush ya kukamata na kutesa. Mbinu za Bush zilikuwa kuwakamata watu na kuwatesa, Obama ameboresha - anawaua tu na yeyote mwingine atakayekuwa karibu. Alisema Chomsky akinukuu makala katika gazeti la Wall Street Journal akisisitiza kuwa anachofanya Rais Obama katika mauwaji ya droni ni ugaidi wa kutisha kwa sababu anauwa watuhumiwa na walio jirani na mtuhumiwa. Shambulio la droni ni silaha ya kigaidi; Inaendelea Uk. 10
Makala
AN-NUUR
Ni Diamond Jumapili
Inatoka Uk. 3
SHEIKH Ilunga Hassan Kapungu akiwa hospitalini nchini India. Kushoto ni mkewe.
hatari. Ilisema taarifa hiyo. Aidha, imefafanua taarifa hiyo kwamba, Waislamu watatanabahishawa hatari ya mwenendo huo na baada ya mkutano huo utakao hutubiwa na Masheikh mbalimbali kutoka Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar, yatatolewa maazimio ya pamoja. Kongamano hilo litahudhuriwa na wajumbe kutoka
mikoani, na baada ya hapo yatatolewa maazimio ya pamoja k a m a Wa i s l a m u Kitaifa, kwa lengo la kuchukua tahadhari baada ya kutahadharishwa na Masheikh wao. Ilisema taarifa hiyo. Mmoja wa viongozi wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu (T), alipohojiwa uwepo wa Kongamano hilo na maudhui yake alithibisha hilo na kudai maandalizi yanaendelea huku
akisistiza Waislamu kuhudhuria kwa wingi. Alisema, miongoni mwa mambo ambayo yatapewa nafasi kubwa kujadiliwa katika Kongamano hilo la Waislamu ni kuhusu Serikali kuamua kufuta mitihani ya somo la dini jambo ambalo limestua Waislamu wengi nchini. Aidha alisema kwamba Waislamu watajadili upepo wa matukio makubwa yaliyotokea nchini
na kuhusishwa kwa namna moja ama nyinge na Waislamu nchini. Kiongozi huyo alisema, wamekuwa wakipokea simu nyingi kutoka kwa Waislamu ndani na nje ya Jiji, wakitaka kujua kwa kina hatua za Serikali kufuta mitihani ya kitaifa ya somo hilo. Tokea taarifa za kufutwa mtihani wa kitaifa wa somo la Maarifa ya Uislamu unaosimamiwa na Serikali kuwafikia W a i s l a m u ,
wamekuwa wakipiga simu kutaka kujua mustabali wa somo hilo, hivyo tumeona ni vyema tufanye Kongamano kujadali suala hili kwa pamoja. Alisema Kiongozi huyo. Habari zilizotukia wakati tukienda m i t a m b o n i zilifahamisha pia kuwa fursa hiyo itatumika kutoa taarifa fupi juu ya hali ya Sheikh Ilunga Hassan Kapungu na maendeleo ya matibabu yake.
Makala
AN-NUUR
Na Khalid S Mtwangi
THERE is little doubt that tension between Christians and Muslims has lately taken a turn for the worse as never before in the history of this country. It is amazing and a credit to the people that streets and households in cosmopolitan melting pots such as Dar es Salaam look serene. Before now it would NOT have been correct to suggest that this unfortunate situation as well applied to relation between religions. Dr Magoti Evarist has alluded to such a state of affairs in his missive in the CITIZEN ON SUNDAY of May 5, 20. But as was manifestly demonstrated during the MwembeChai fracas here Muslims vented their anger at the Government leaving the string of churches and other Christian establishments in the vicinity, and there are quite a number, untouched. During this catastrophic manifestation of naked power in their possession some Government ofcials simply decided to stamp their power and authority on Muslims to teach them a lesson they would never forget. The sad fact about this matter is that Christian brethren, including those one would have given credit with having a broader outlook on the affairs of the world, have decided to live in a cocoon in so far Muslim affairs are concerned. There is every reason to arrest this obviously perilous situation that could be pregnant with a manifestation that could be predictably detrimental to peace and harmony of the people of this country. However there must be a
variation of suggestions that have been put forward by Dr Magoti Evarist. My suggestion, or indeed, recommendation would be to appeal to the Church hierarchy to preach to their ock fair play in everyday life. It amazes many Muslims that Christians, especially among the intelligentsia and the academia, are wholly oblivious, indeed immune, to the many complaints that are aired by Muslims about what has been termed as dhulma that happens to be the Muslims lot. It would appear that to them that is simply a lot of hot air? Take a load of this. A team of ofcials from the Ministry of Education proceeds to Morogoro to hide themselves to complete an urgent peace of assignment. Eid el Udh-ha happens to fall when these ofcials are ensconced out there building the nation. The man in charge simply does not recognise Eid el Udh-ha so he insists the ofcers keep on working and need not attend prayers on that very important Holy Day to remember Nabii Ibrahim SA who is accepted by all as the Father of all Monotheism that ostensibly would include what is known today as Christianity. But come Sunday the whole team was given the day off to attend prayers. Needles to point out that the man in charge professed Christianity!!! Again at Morogoro. The Municipal Education Officer writes officially to all primary school head teachers to submit to him a list each of all Roman Catholic pupils in their schools. What for? Complaints were directed at the Ministry by Muslim organizations, but as a rule and Muslims are used to it , the bureaucracy in the Government would not respond; they never do. A teacher in one Tanga goes into a tirade against Rasu-ul-Llah Muhammad SAW and Islam generally. To their credit Muslims do not breath fire regarding what is really kashfa with
Here you have a good example of representatives of Christianity who simply have no time for Islam and Muslims. What about the attitude of Muslims in this country towards their Christian cousins? First, being a tiny minority in the establishment Muslims have no opportunity to ex their weak muscles. Those that are waungwana would not want to be lumped with the uneducated kanzu clad lot, and they know which side of their thick slice of boo is smeared with all the goodies. Muslims do not seek any privileged position; but they seek only haki. Finally, Dr Magoti Evarist needs to be congratulated for the courage he has shown in his missive. It is rare for some one of his stature to accept though grudgingly that there are faults elsewhere as well and not just among Muslims. Archbishop Eliezar Sendoro is one Christian clergy who has taken pains
NAFASI ZA KAZI Inawatangazia nafasi ya kazi upande wa wauzaji (Salesman) Sifa za muombaji Awe kijana wa kitanzania Awe na umri kati ya miaka 25-45 Awe tayari kuweka dhamana ya mali isiyohamishika Awe na wadhamini watatu ( 3) wenye ajira zinazotambulika kiserikali Awe na elimu siyochini ya kidato cha nne Awe na uzoefu wa kazi usiopungua miaka mitatu katika fani hiyo. MAWASILIANO Zaidi: Piga Simu: 0789 272 737 Maombi yote yatumwe katika mtandano. Email: fairlandcom@yahoo.com Au kwa Barua S.L.P 4804- DSM MAOMBI YAAMBATANISHWE NA PASSPORT SIZE.
Makala
AN-NUUR
Shule hizi ni za Kiislamu zenye lengo la kuwapa wanafunzi taaluma ya hali ya juu na malezi bora ya Kiislamu kwa gharama nafuu. Shule hizi ni za mchanganyiko wa wavulana na wasichana na zinapokea wanafunzi wa bweni tu. Masomo yanayofundishwa ni Islamic knowledge, Combinations za SAYANSI, ARTS, BIASHARA pamoja na COMPYUTA. Muombaji awe na Crediti 3 au zaidi na angalau D ya Elimu ya Dini ya Kiislamu katika matokeo ya kidato cha nne. Ikiwa ana F au hakufanya Elimu ya Dini ya Kiislamu, basi awe tayari kusoma programu maalum ya Maarifa ya Uislamu atakapokuwa kidato cha tano. Kwa wale ambao walisharudisha fomu wanatakiwa wawasilishe result slips za matokeo mapya mapema kwenye osi waliporejesha fomu hizo ili yaunganishwe na fomu zao. Waombaji wapya wenye sifa wanashauriwa kuendelea kuchukua fomu.Tarehe ya mwisho ya kurejesha fomu itatangazwa baadaye. Fomu za Maombi zinapatikana kwa gharama ya shilingi 10,000/= katika vituo vilivyoorodheshwa hapa chini.
Arusha Kilimanjaro Osi ya Islamic Education Panel Jambo Plastic Ghorofa ya 2 mkabala na msikiti Mkuu Bondeni - 0763 282 371/ 0784 406 610 Moshi: Msikiti wa Riadha 0654 723 418 Same: Kirinjiko Islamic Secondry School: 0784 296424/0655 697 075 Uongofu Bookshop: - 0784 982525/ Mandia Shop - Lushoto: 0782257533 Nyasaka Islamic Secondary School 0717 417685/0786 417685 Osi ya Islamic Education Panel - Mwanza - Mtaa wa Ruji mkabala na Msikiti Al-Amin 0785 086 770 Duka la Kansolele -Stendi ya zamani sokoni - 0714587193 Bukoba: Alhuda Caf Kwa mzee Kinobe karibu na osi za TRA. - 0688 479 667 Msiikiti wa Majengo-0718866869 Kahama osi ya AN NUUR Karibu na msikiti wa Ibadhi: 0753 993930 Ubungo Islamic High School 0754 260 241/0712033556 Osi ya Islamic Ed. Panel Temeke -Msikiti wa Nurul Yakin 0655144474 Wasiliana na Ramadhani Chale :0715704380 Hijra Islamic Primary School : 0716 544757/0712 325086 Osis ya Islamic Ed. Panel karibu Nuru snack Hotel 0714285465 Babati: Shule ya Msingi Hangoni: 0784 667575 Msikiti wa mwanga Kigoma: 0753 355224 Kibondo Islamic Nursery School: 0784 442860 Kasulu: Murubona Isl.SS. 0714710802 Wapemba Store: 0784 974041/0786 959663 Amana Islamic S.S 0786 729 973 Kwa Kawanga Karibu na Msikiti wa NURU 0715 681701/0716791113 Mkuzo Islamic High School. 0716 791113 Duka la vifaa vya Kiislamu nje ya Msikiti wa Uyole 0713 200209 Rexona Video mkabala na Mbeya RETICO: 0713 200209 Sumbawanga: Masjid TAQWA 0717082 073 Kituo cha Kiislamu Isevya: 0784 944566 Madrastun Najah: 0714 522 122 Wete: Wete Islamic Education Center: 0777 432331 Madrasatul Fallah: 0777125074Osi ya ust. Yusufu Ally jirani na msikiti mkuu 0653705627
Tanga Mwanza Musoma Kagera Shinyanga Dar es SalaamMorogoro Dodoma Singida Manyara Kigoma Lindi Mtwara Songea Mbeya Rukwa Tabora Iringa Pemba Unguja Maa -
6. Pia Fomu zinapatikana kwenye Tovuti: www.ipctz.org. Ikumbukwe kuwa watakaopata fomu kupitia tovuti (download) watatakiwa kuzilipia wakati wa kuzirejesha.
10
alishitakiwa kwa mauwaji ya polisi watatu waliolipuliwa kwa bomu lililokuwa limetegwa katika gari mwaka 1972. Ni katika kesi hiyo ambapo siri ya kuwepo harakati za kigaidi za Gladio zilifichuka. (Tanzama CIA Organized Secret Army in Western Europe-Washington Post, Novemba 14, 1990). Ufupi wa maneno Vincenzo Vinciguerra anasema kuwa watu wasio na hatia, raia, wanawake na watoto, walishambuliwa na kuuliwa (kufanyiwa ugaidi), ili kusimika kitisho na kuwafanya raia kutaka ulinzi zaidi kutoka kwa Serikali. Hapana shaka wakati huo wa siasa za vita baridi, waliosingiziwa kufanya ugaidi huo ni Wakomunisti, vyama vya siasa na makundi katika jamii yenye mrengo wa kikomunisti. Kwa mujibu wa taarifa zilizofichuliwa na aliyewahi kuwa kachero wa FBI Sibel Edmonds, kinachoitwa vita dhidi ya ugaidi hivi sasa na wanaoitwa magaidi hivi leo, ni watu walioandaliwa, wakapewa mafunzo, fedha na kuwezeshwa na mataifa hayo hayo ya NATO katika operesheni mpya inayojulikana kama Gladio B. Chini ya operesheni hiyo inaelezwa kuwa, mwaka 1997 NATO walimwomba Rais Hosni Mubarak awaachie huru Waislamu waliotuhumiwa kumuuwa Anwar Sadat na ambao wana uhusiano na Ayman al-Zawahiri (Al Qaida) na wafungwa hawa wakasarishwa kwa ndege hadi Uturuki chini ya uangalizi wa Marekani ambapo waliunganishwa na wanaodaiwa kuwa ni magaidi hivi sasa. Zaidi Edmonds anasema kuwa akiwa mkalimani wa FBI (Kiarabu na Kifursi) alishuhudia al-Zawahiri na Mujahideena wengine wanaoitwa hivi leo magaidi, wakikutana na maosa waandamizi wa Serikali ya Marekani katika Ubalozi wa Marekani, Baku katika nchi ya Azerbaijan. Wakati uhalisia wa uwepo wa Gladio barani Ulaya ni suala la nyaraka za historia. Edmonds amesema kuwa mkakati huo huo
Inatoka Uk. 6
Makala
AN-NUUR
Inatoka Uk. 6 hatulizungumzii hivyo. Ni kwamba, kiria, unatembea mtaani na hujui kuwa dakika tano zijazo kutakuwa na mlipuko mtaa wa pili kutoka angani, ambako huwezi kuona. Kuna mtu fulani atauawa, na yeyote atakayekuwa karibu atauawa, na huenda ukajeruhiwa kama uko hapo. Hii ni silaha ya kuwatisha watu. Inavitisha vijiji, mikoa, maeneo makubwa. Kusema kweli ndiyo kampeni kubwa zaidi ya vitisho vya kigaidi iliyowahi kuwepo, tena kwa mbali. Pamoja na uhalifu wote huo anasema Prof. Noam Chomsky kuwa si jambo la kukirika kuwa itaka siku
Rais wa Marekani asimame katika ICC. Wa k a t i h u o h u o mwandishi mashuhuri John Pilger naye amezungumzia suala hilo akisema maafa yanayotokea Iraq hivi sasa ni msiba unaowakumbusha walimwengu kuwa wahalifu ambao hawajafikishwa mahakamani. Katika makala yake From Iraq, a tragic reminder to prosecute the war criminals, John Pilger ametaja mambo mawili ukiacha mauwaji yaliyofanyika wakati wa uvamizi.
AU wamesema kweli
Anasema, kutokana na tati mbalimbali, hivi sasa kuna ongezeko kubwa sana la ugonjwa wa saratani na watoto wanaozaliwa wakiwa na ulemavu na maumbile yasiyo ya kawaida (congenital malformations). Na kwamba ongezeko la matatizo hayo ya kutisha ni kutokana na uraniua iliyokuwepo katika mabomu (depleted uranium shells UD) yaliyolipuliwa Iraq. Anasema, taarifa zinaonyesha kuwa kabla ya uvamizi wa Marekani, kulikuwa na wastani wa watu wawili mpaka watatu wa ugonjwa, lakini sasa kunatokea wagonjwa 35 kila mwezi. Tafiti zaidi zinasema kuwa kiasi miaka mitano ijayo, wagonjwa wa saratani watakuwa kati ya asilimia 40 mnpaka 48 ya wagonjwa wote na kwamba hata mimea imeathirika na matumizi ya mabumu hayo yenye uranium kiasi cha kutokulika. John Pilger anasema msiba unaowakumba wananchi wa Iraq hauna tofauti na ule wa Hiroshima na Nagasaki. Kwa upande mwingine Pilger anasema kuwa uvamizi wa Bush na Blair huko Iraq
kuchuma na kuzuiya washindani wengine miongoni mwa mataifa makubwa kuingia katika nchi hizo. Lakini jingine ni kuwa nchi ikiwa na fujo, haiwezi kuwa imara na kupata muda wa kutafakari kuweka sera nzuri na msimamo imara wa kulinda rasilimali zake. Kongo, DRC, ni mfano tosha. Sasa pengine kwa ujio huu adhimu kwetu, ingekuwa vyema kama katika mazungumzo yetu na mgeni wetu Rais Barack Obama, tutaingiza na agenda hii. Kwamba katika ushirikiano wetu huu, ukiwemo huu wa kuwepo kwa FBI kutusaidia kuchunguza bomu la Arusha, je, haitatuingiza katika harakati za Operation Gladio B? Vi n c e n z o Vi n c i g u e r r a anasema kuwa kitendawili cha Peteano bombing na Bologna massacre ambapo waliuliwa watu 85, kinateguliwa kwa kufichuka harakati za Operation Gladio. Sasa itakuwa ni vyema na sisi kujihakikishia kuwa hatuwi na akina Valerio Fioravanti na Francesca Mambro miongoni mwetu wa kutuletea maafa kama lile la Kanisani Arusha. Katika kikao cha mashirika ya mafuta katika nchi za Afrika Mashariki (East Africa Petrolium Conferenece) mwaka 2008 kilichofanyika katika Hoteli ya Ngurudoto, Arusha, na kufunguliwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete, alikuwepo mjumbe mualikwa kutoka Angola akiwakilisha Shirika la Petroli la Chevron. Katika hotuba yake mjumbe huyo akitumia vielelezo vya picha, alieleza jinsi kampuni ya Chevron kutoka Marekani inavyotoa misaada, huduma na asante kwa wananchi wa Angola, hasa wanaozunguka migodi. Alisema, msaada wao kwa wananchi ni Dola milioni moja kwa mwaka ikijumuisha ujenzi wa visima vya maji na madarasa ya shule za msingi.
umeacha msiba wa mauwaji ya wenyewe kwa wenyewe ambapo kila uchao kuna mtu/ watu wanauliwa au kutiwa vilema. Akimnukuu Von Sponeck, anasema kuwa taarifa ya Serikali ya Iraq inaonyesha kuwa kiasi watoto milioni 4. 5 wamekuwa yatima kwa baba na mama kutokana na vita. Hiyo ni sawa na kusema kuwa asilimia 14 ya watoto wa Iraq ni yatima huku mamilioni wakiwa hawana makazi. Anamalizia Pilger akisema kuwa uhalifu na uovu huo waliofanyiwa watu wa Iraq, unaita ukisema kuwa kuna mhalifu kajificha mahali anatakiwa kukamatwa na kukishwa mahakamani.
11
Makala
AN-NUUR
HIVI karibuni tumesoma makala mengi yaliyoandikwa na Watanzania Bara na machache yaliyoandikwa na Wazanzibari kukhusu muungano. Makala zilizoandikwa na Watanzania Bara takriban zote zilikuwa zikiusifu na kuutukuza muungano, lakini makala na barua nyingi zilizoandikwa na Wa z a n z i b a r i , k h a s a katika mitandao, zilikuwa zinaonesha wazi kutokuridhika kwao na muungano na wengine kutaka muungano uvunjike leo kabla ya kesho. Katika maelezo ya Wazanzibari wengi unaona wazi kuwa muungano umewabana vibaya sana kiuchumi na katika mambo mengi mengineyo yanayoendesha nchi, na tumesoma vile wanavyoona uchungu kuiona nchi yao ilivyotawaliwa kwa m a b a v u n a Ta n z a n i a Bara. Lakini Tanzania Bara wengi hawahisi hivyo; wanaona utawala wao ni bora kuliko tawala zote zilizotangulia. Lakini ukitizama utaona kuwa aina ya muugano uliopo unaweza kulinganishwa na muundo wa ukoloni wa Kifaransa ambao ni tafauti na wa Kiingereza. Waingereza walitawala makoloni yao na waliotawaliwa walijua moja kwamoja kuwa wametawaliwa. Lakini, Mfaransa alizifanya koloni zake kuwa ni sehemu ya Ufaransa na mtawaliwa alikuwa na haki ya kuwa Mfaransa na hata kuhamia Ufaransa bila ya matatizo na kuweza kushiriki katika maisha na siasa za huko Ufaransa. Huu ndio muundo wa ukoloni wa Tanganyika juu ya Zanzibar. Wafaransa wengi sio kuwa walistaajabu tu kwanini katika hali kama hiyo ya watawaliwa kuwa wana haki Ufaransa kudai uhuru wao, bali Wafaransa wengi waliudhika sana kuona nchi zilizotawaliwa kudai uhuru wao. Sasa nenda ukawaulize waliotawaliwa na Wafaransa, kama vile Algeria, Ngazija na kwingi kwingineko, kwanini basi wakadai uhuru wao usikilize jawabu zao. Tanzania Bara pia, kama Wafaransa, wanastaajabu sana wanapowasikia Wazanzibari wengi wakidai uhuru wao watokane na utawala wa mabavu wa Bara, lakini Wazanzibari wengi wanaoathirika na muungano hawana taabu ya kukuelezea yanayowaathiri wao na nchi yao. Hivi karibuni tumeshuhudia pia gwaride la majeshi ambalo
12
AN-NUUR
MAKALA
Taasisi ya Khidmat Islamiya inawatanganzia Waislamu wote Safari ya Hijja kwa Gharama ya Dola 4450 tu. unaweza kulipa kwa awamu (Kuhijiwa) ni Dola 1450 tu. Kuondoka ni 5/10/2013 kurudi 27/10/ 2013 Piga Simu 0784 786680, 0713 986 671, 0774 786 680 E-Mail) hajjkhidmat@gmail.com , Tovuti (Website) www.khidmatislamiya.com
12
Na Bakari Mwakangwale
nafasi propaganda iwe ndio mwongozo wao ili isiwe ni chanzo cha Taifa letu kutumbukia katika vurugu za kidini. Alisema Ustadh Kiago. Kiago alitaadharisha kwamba mauaji makubwa yaliyotokea nchini Rwanda, yalianza katika sura kama hiyo ambapo jamii moja ilikuwa ikisingiziwa maovu. Alisema, wakati jamii hiyo ikilalamika kuhusiana na propaganda hizo, vyombo vya dola na wanasiasa wake walipuuza na kuegemea upande mmoja wa jamii ya Wanyarwanda bila ya kufanya juhudi za kufuatilia uhakika wa Propaganda
na dhuluma zilizokuwa zikilalamikiwa. Aliitanabahisha Serikali, viongozi wa Madhebu yote pamoja na wanasiasa na jamii kwa ujumla kwamba, Kimsingi katika nchi hii hakuna mgogoro kati ya Waislamu na Wakristo. Alisema makundi hayo mawili huko mitaani yanaishi pamoja kwa kushirikiana katika mambo mbalimbali ya kijamii. Hivyo alisema, Serikali itambue kuwa kuna watu wachache ambao wanataka kulitumbukiza Taifa katika machafuko, na kwamba ikiwa makini (Serikali) ina uwezo wa kuzima vuguvugu hili linaloashiria hali mbaya nchini.
SERIKALI na Chama tawala Cha CCM, vimetajwa kuwa ndiyo chanzo cha vurugu Mkoani Mtwara, kwa kuicha nyuma kimaendeleo mikoa ya Kusini. Madai hayo yametolewa na Ustadhi Salum Machano, akiwahutubia Waislamu Ijumaa ya wiki iliyopita Masjidi Haqa, Buguruni Jijini Dar es salaam. Ust. Machano, alikuwa akizungumzia vurugu zilizoibuka mapema wiki iliyopita Mkoani Mtwara, wananchi wakigomea mpango wa Serikali kuisafirisha Gesi kwenda Jijini Dar es Salaam, kutoka Mkoani humo. Akitoa taarifa Bungeni, kufuatia ghasia zilizoibuka Mkoani Mtwara, wiki iliyopita Waziri wa Mambo ya ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi, alisema, Serikali itahakikisha inawasaka vinara wa vurugu hizo ndani na nje ya nchi na kuhakikisha inawatia mbaroni. Ust. Machano, alisema Serikali isitafute mchawi kufuatia kuibuka kwa vurugu zinatokana na sakata la gesi bali wachawi ni wao wenyewe. Akifafanua, Ust. Machano, alisema sababu
hayawezi kufuta msimamo walionao zaidi ya kulipoza na kuibuka mara kwa mara. Ust. Machano, alisema katika nchi hii kuna wananchi wapo katika shida kwa muda mrefu, wakiwemo watu wa Mikoa ya Kusini. Matumizi sahihi ya akili ni kuhoji unapoletewa maelezo au taarifa, lazima mwenywe akili timamu ahoji ili apate ufafanuzi, na ndio maana Mitume wote walipata changamoto kutoka kwa watu wao na wao (Mitume) walikuwa wakijibu hoja, na si vitisho. Alisema Ust. Machano. Alisema, katika Quran suratul Bakara, Allah (sw), amemzungumzia Nabii Ibrahim, baba wa Imani kwamba ametumia akili yake vizuri katika kuhoji. Nabii huyu alihoji kwa Allah akitaka kujua ni vipi atamfufua mwanaadamu siku ya kiama, ili moyo wake upate yakini zaidi. Alisema Ust. Machano. Ust. Machano, alidai kwamba ni kawaida ya viongozi ambao wameishiwa majibu kwa watu wanaowaongoza, kutokana na kutokuwa na ahadi za kweli, na kinyume chake badala ya kujibu hoja huwashambulia.
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Limited, S.L.P. 78495 Dar es Salaam.