Professional Documents
Culture Documents
tz
Sauti ya Waislamu
ISSN 0856 - 3861 Na. 1062 JAMADUL AWWAL 1434, IJUMAA MACHI 15-21, 2013 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=
kujiuzulu katika wadhifa wake kutokana na kushindwa kusimamia Wizara yake katika wa majukumu KATIBU mkuu wa Chama cha utekelezaji Wananchi CUF Mh. Maalim yake. Akizungumza katika mkutano Seif Sharif Hamad amemtaka Waziri wa Mambo ya Ndani ya Inaendelea Uk. 6 Nchi Dkt. Emmanuel Nchimbi
2
AN-NUUR
Tahariri/Habari/Tangazo
AN-NUUR
S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786 Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM. www.annuurpapers.co.tz E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk Osi zetu zipo: Manzese Tip Top Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam
MAONI YETU
ajenda imetayarishwa kutaka kulazimisha chuki za kidini Zanzibar, kwa sababu huko Tanzania Bara kumetokea matukio mabaya zaidi, lakini hayajahusishwa na ugaidi. Alitoa mfano matukio ya kuuawa kwa Kamanda wa Polisi Mkoa, na kuchinjwa kwa Padri huko Geita, kuwa ni mabaya kabisa, lakini hakuna hata chombo cha habari kimoja kilichohusisha matukio hayo na Ugaidi. Nasema Zanzibar hakuna Ugaidi, hakuna ugomvi wa kidini. Yanayotokea yametusikitisha sana, ni matokeo ya uhalifu wa kupindukia, linaloweza kufanywa lifanywe kuwanasa wahalifu hawa, na kuwafikisha mbele ya vyombo vya sharia, alisema Makamu wa Kwanza wa Rais. Aliwataka wananchi wote wa Zanzibar kwa wakati huu kuwa watulivu na wasitawaliwe na jazba na wala wasichokozane, pia wasikubali kuchokozeka. Sisi tungependa kutilia mkazo kwa kusema kuwa kwa hakika wanaopalilia agenda ya ugaidi ndio magaidi kwa sababu wanachofanya ni kujenga mazingira ya kuteswa na kuuliwa watu wasio na hatia. Uzoefu unaonyesha kuwa mahali popote duniani ambapo wachafuzi, mafatani na wasaliti walifanikiwa kupandikiza kitisho cha ugaidi, basi kilichofuatia ni mateso na mauwaji kwa wananchi wasio na hatia. Ni kutokana na uzoefu huo kama unavyodhihiri katika nchi za Afghanistan, Pakistan, Yemen, Kenya, Somali na huko Amerika ya Kusini katika miaka ya nyuma, tunadhani kuwa itakuwa jambo la busara kusisitiza nasaha hizi za Maalim Seif na kuwataka Watanzania wote kuwazomea na kuwakomesha wale wote wanaotaka kupandikiza chuki za kidini na kitisho cha ugaidi miongoni mwetu. Tukifanya hivyo itakuwa salama kwetu sote, lakini tukiwafumbia macho na kuwachekea, tujue itakuwa msiba kwetu sote pia.
Uongozi wa Masjid Tungi, Temeke jijini Dar es Salaam unawaarifu Waislamu wote kuwa, kutakuwa na Ibada maalum ya Itqaf msikitini hapo. Siku: Jumamosi ijayo tarehe 23/03/2013 msikitini hapo baada ya swala ya Isha.
WOTE MNAKARIBISHWA WABILLAH TAWFIIQ
Habari
kama hiyo kutolewa na Waziri Mkuu hadharani, lau angetokea jasusi yeyote akailipua hospitali hiyo na kuuwa raia wengi wasio na hatia, hivi nani ambaye asingeamini kuwa uovu huo umefanywa na Waislamu? Linasema na kuhoji tamko la Waislamu kwamba kwa nini serikali ipandikize chuki ya aina hiyo kwa raia wake? Na inafanya hivyo kwa masilahi ya nani? Mfano wa pili unaotolewa kuonyesha jinsi serikali inavyopandikiza chuki na kupalilia fitna na uhasama kati ya Waislamu n a Wa k r i s t o , n i p a l e ilipodai kuwa Waislamu
AN-NUUR
JUMUIYA na Taasisi za Kiislamu nchini, zimetoa tamko kuelezea na kutoa tahadhari juu ya kampeni zinazoendelea za kulitumbukiza Taifa katika machafuko ya kidini. Katika tamko hilo ambalo limewasilishwa rasmi kwa Waziri Mkuu, Serikali ya Jamhuri ya Tanzania imetuhumiwa kuhusika kuchochea chuki na kupandikiza farka na fitna miongoni mwa Waislamu na Wakristo jambo lililoelezwa kuwa ni la hatari. Jambo la hatari sana ambalo sasa linatudhuru, ni kampeni za serikali za kuwasingizia Waislamu mambo mazito ya kuhatarisha amani na utulivu nchini ili kuhalalisha dhana kuwa Waislamu ni watu hatari. Imesema sehemu ya tamko hilo na kutoa mfano wa uzushi uliowahi kutangazwa na aliyekuwa Waziri Mkuu Mheshimiwa Frederick Sumaye. Ikaelezwa kuwa katika uzushi huo Sumaye alidai kuwa kuna magaidi wa Kiislamu waliokuwa wamefuzu mafunzo nje ya nchi na walikuwa wamerejea nchini na kwamba shabaha yao ya kwanza ilikuwa kulipua hospitali ya Muhimbili. Na kweli baada ya kauli hiyo ya Sumaye, Waislamu watatu wafanyakazi wa Muhimbili akiwemo Profesa Jahazi, bingwa wa Bio-Chemistry, wakatiwa mbaroni kwa tuhumza za kupanga kuilipua hospitali. Ta m k o h i l o l a Waislamu linasema kuwa japo watuhumiwa wote waliachiwa baada ya siku chache, lakini tayari sumu ya propaganda chafu ilikuwa imekwishapenyezwa. Kwa Waziri Mkuu kutangaza uzushi kama huo, ni dhahiri kuwa lengo lilikuwa ni kuwafanya wananchi wengine wawachukie Waislamu kwa kukusudia kufanya uovu wa kulipua hospitali. (Na) la kuzingatia hapa ni kwamba baada ya kauli
wakitumiwa na watu wa nje walikuwa wamepanga kulipua makanisa siku ya Jumapili tarehe 2 Septemba 2001. Hiyo ilikuwa ni baada ya maandamano ya Waislamu ya tarehe 24 Agosti 2001 Wa i s l a m u w a k i p i n g a kufungwa Hamisi Dibagula kwa kusema kuwa Yesu si Mungu. Ta m k o l i n a s e m a kuwa baada ya kauli hiyo ya serikali kuwa Waislamu wana mpango wa kulipua makanisa, askari walitawanywa makanisani kuwalinda Wakristo dhidi ya Waislamu wanaotaka kuwadhuru kwa mabomu.
Je, baada ya kauli hizo, akitokea jasusi yeyote akatega bomu na kuuwa watu kanisani, ni nani atakayeshutumiwa kwa mauwaji hayo kama si Waislamu? Tamko linahoji. Pamoja na shutuma hizo kwa serikali, vinashutumiwa pia baadhi ya vyombo vya habari ambavyo vimekuwa vikizua urongo dhidi ya Waislamu na hakuna hatua zozote zinazochukuliwa. Umetajwa mfano wa yale madai kuwa Waislamu walikuwa wameandaa jeshi na silaha za kuulia Wakristo na kwamba alipokuwa Rais, Alhaj Ally Hassan Mwinyi alikuwa amewagawia
WA K O L O N I w a Kijerumani na wa Kiingereza waliamini kuwa Waislamu ni watu hatari sana, kidini na kisiasa. Hivyo waliweka mikakati kadhaa ya kuwadhibiti. Imani hiyo ya wakoloni ilitokana na msimamo madhubuti wa Waislamu wa kuwa tayari kwa udi na ambari kupambana na wakoloni hao ili nchi yetu iwe huru. Vema, mmetuhukumu tunyongwe nasi tumekubali. Tumekubali kwa sababu ni sisi wenyewe tulioendea maji ya dawa Ngarambe kwa hiari yetu; kwa sababu hatukuona haki ya kutawaliwa na nyinyi wahuni. Na kwa sasa kwa kuwa mmenipata, basi ninyongeni haraka kusudi jina langu libaki likikumbukwa kwamba nilikuwa mmoja niliyepigania nchi yangu (Selemani Mamba, Maji Maji hero). Kauli ya shujaa Suleiman Mamba aliyowaambia wakoloni wa kijerumani wakati wa kunyongwa kwake tuliyoinukuu hapo juu inaonesha msimamo huo ambao ni wa hatari kwa maslahi ya wakoloni. Ili kulinda maslahi yao, wakoloni wakaona njia rahisi ni kutugawa ili watutawale. Kwa kuwa waliosimama kidete
Waislamu majambia ya kuwachinjia Wakristo wote nchini. Ukiacha matukio hayo ya miaka ya nyuma, tamko linagusia pia jinsi matukio ya hivi karibuni ya sakata la kuchinja Wakristo na lile la kuuliwa Padri Zanzibar, yanavyovishwa gamba la ugaidi na watuhumiwa wakiwa ni Waislamu. Na katika jitihada hizo za kuwachafua Waislamu, inatajwa kuwa ndio sababu serikali imekimbilia kuwaita FBI bila kujali kuwa kufanya hivyo ni kujidhalilisha. Tamko linasema kuwa mabeberu wenye kiu na rasilimali zetu, wanatumia mwanya huo kujipenyeza kikachero na kijeshi huku sisi tukidhani na kufurahia kuwa tunashirikiana na taifa kubwa kumbe tumejitia wenyewe kitanzi cha ukibaraka. Hakuwezi kuwa na ushirikiano wa kweli baina ya nchi yenye nguvu na nchi dhaifu. Katika ushirikiano wa nchi kama hizo ukweli ni kwamba nchi dhaifu inakuwa ni kibaraka tu wa nchi yenye nguvu. Tamko la Waislamu lilisema hayo likinukuu sehemu ya hotuba mashuhuri sana ya kuwaaga wananchi wa Marekani iliyotolewa na Rais George Washington 19 Septemba, 1796. Ta m k o l i k a s i s i t i z a kuwa kwa waliosoma na kulielewa Azimio la Arusha, yote aliyosema G e o r g e Wa s h i n g t o n , aliyasema Mwalimu Nyerere katika jitihada zake za kulinusuru taifa letu. (Lakini) leo kwa papara yetu ya kujipendekeza kwa Wamarekani imekia hadi kuwakaribisha ndani ya kambi zetu za jeshi kana kwamba na wao ni Watanzani wenzetu! Ni kutokana na ukweli huo alioeleza aliyekuwa Rais wa Marekani G e o r g e Wa s h i n g t o n , tamko limeonyesha jinsi hao washirika wetu wanavyotumia udhaifu wetu mpaka kukamata vijana wetu na kuwapachika ugaidi huku serikali yetu ikishindwa kuwatetea. Baada ya serikali yetu Inaendelea Uk. 4
Habari
AN-NUUR
msimamo huo wa Sheikh Selemani Mamba, tamko la Waislamu likasema kuwa Waislamu wataendelea kupinga mpango huu wa makusudi wa kuwagawa Watanzania kwa msingi ya kidini. Na kwamba kwa kufanya hivyo watakuwa wametoa mchango wao katika kudumisha amani, utulivu na mshikamano katika nchi hii. watu wa nchi nyingine kuja kulitatua! Tumesikitishwa sana na mfano mbaya unaooneshwa na serikali yetu ya kuwakimbilia watu wasio na uchungu wowote na nchi yetu kuja kutusaidia kutatua mambo yetu. Na tunashangazwa na tabia ya wananchi wenzetu wanaodhani kuwa matatizo yetu makubwa au madogo ya kiutawala yanaweza kumalizwa kwa kuyapeleka kwenye Baraza la Wawakilishi wa Marekani. Haya ni matatizo yetu na ni lazima tufanye kila njia kuyatatua sisi wenyewe. Waislamu tunajua kuwa kila anayepingana na mabeberu anakuwa gaidi na sasa nchi zetu zimeanza kupewa drone za kuulia raia wao. Sisi tunaapa hatutakwenda kuwalalamikia Marekani au watu wengine matatizo na misukosuko inayotukumba kama raia. Tutafanya kila tunaloweza upatikane ufumbuzi unaotokana na sisi wenyewe kama raia wa nchi hii. Kwa uzoefu wetu wa miaka hamsini wa namna serikali yetu inavyowatazama Waislamu, tunatarajia kuwa mwaka huu utakuwa wa mateso makubwa kwa Waislamu na hasa kwa viongozi wetu kwa kubambikiziwa kesi zisizokuwa na kichwa wala miguu, kudhalilishwa na kunyimwa dhamana kama mbo ya kuwaadhibu watu hatari kidini na kisiasa. Hilo likitokea tutalazimika kutafakari hatima yetu baada ya miaka hamsini ya kuvumilia. (Sehemu ya Tamko la Waislamu lililowasilishwa kwa Waziri Mkuu kuhusu Kampeni Zinazoendelea za Kulitumbukiza Taifa Katika Machafuko ya Kidini.)
na baadhi ya vyombo vya habari bila ya kuchukuliwa hatua yoyote. Kwa mfano jarida maarufu la Family Mirror toleo la pili la Mei 1993, lilitangaza kwa maandishi ya kukoza kuwa vijana 500 wa Kiislamu wamejiandikisha katika Jeshi la Kiislamu ili kuwauwa Wakristo, na kwamba serikali imekamata bandarini makontena ya silaha za Jeshi la Waislamu. Waziri wa Mambo ya Ndani wa wakati huo alikiri kuwa alikuwa nazo taarifa hizo. Katika toleo lililotangulia ilidaiwa kuwa Waislamu walikuwa wamepanga kuuchoma moto ubalozi wa Vatican nchini na kumwua Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Katoliki la Dar es Salaam, Muadhama Kadinali Polycarp Pengo. Jarida jingine la Tanzania Analysis la 22 Julai, 1995 lilidai kuwa Rais Mwinyi amewagawia Waislamu majambia ya kuwachinjia Wakristo wote nchini, kwa sababu Waislamu hawataki Mkristo awe Rais. Baada ya serikali yetu kufungua mlango wa kuwasingizia Waislamu mambo yanayohatarisha amani na usalama wa nchi, Wamarekani wameutumia udhaifu wetu huo kutuparaganya zaidi na kwa kiasi kikubwa kwa kushirikiana na serikali yetu wenyewe. Serikali ya Marekani nayo ikautumia mwanya huo kudau kuwa mtoto Ghailani kuwa ndiye aliyeulipua Ubalozi wa Marekani mwaka 1998 na ikamkamata na kumpeleka Guantanamo kwa ridhaa ya serikali yetu. Prof. Haroub Othman, (Mwenyezi Mungu amrehemu) alifanya kila aliloweza kumtetea mtoto huyu lakini hakufanikiwa. Allah atamlipa kwa jitihada zake na amjaalie kijana huyu
aliyetolewa kafara subira na hatima njema. Hatujui kama viongozi wetu wamewahi kuwaomba viongozi wa Marekani kumwachia kijana huyo, kama walivyoomba Waingereza na kufanikiwa kuwanusuru raia wao. Lakini tunajua kuwa viongozi wa Uingereza waliwaombea askari wao wawili, Brett Richard na Nigel David ambao 10 Novemba 2004 walimbaka kwa zamu binti wa Kitanzania Konjesta Mwikaye katika fukwe za Hoteli ya Silversands na kisha kumwua. Waislamu tulipigania uhuru wa nchi yetu ili sisi wananchi wa nchi hii tuwe na haki na uhuru wa kujiamulia mambo yetu sisi wenyewe. Hatukupigania uhuru ili tuwe vibaraka wa watu wengine. Tulipigania uhuru kwa kushirikiana na Watanzania wenzetu wa makabila na dini mbalimbali ili tuishi kwa amani na udugu kama raia huru na sawa katika nchi yetu. Hatukupigania uhuru ili baada ya uhuru utaratibu ule ule wa kuwagawa raia kwa misingi ya dini au ukabila uendelee. Kama tulivyosimama kidete kuupinga ubaguzi miongoni mwetu wakati wa kupigania uhuru na tukafanikiwa, tutaendelea kuupinga mpango huu wa makusudi wa kutugawa ili kuwe na machafuko nchini kwa manufaa ya wakoloni mamboleo, na Insha-Allah tutafaulu. Waislamu tulipigania uhuru kwa kujua kuwa maana ya kujitawala ni pamoja na kuwa na uwezo wa kuyakabili na kuyatatua matatizo yetu sisi wenyewe. Hatukupigania uhuru ili kukitokea tatizo lolote miongoni mwetu tuwaombe
5
TEHRAN RAIS Mahmoud Ahmadinejad wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na mwenzake wa Pakistan Asif Ali Zardari, Jumatatu ya wiki hii wamezindua rasmi awamu ya kwanza ya ujenzi wa bomba la kusarisha gesi utakaogharimu mabilioni ya dola. Marais hao wawili wamehudhuria hafla ya uzinduzi huo iliyofanyika mpakani mwa nchi hizo mbili na kuhudhuriwa pia na Waziri wa Mafuta wa Iran Rostam Qasemi na Waziri wa Mambo ya Nje Ali Akbar Salehi. Bomba hilo litasafirisha gesi asilia kutoka Iran kuelekea nchini Pakistan na viongozi wa nchi hizi mbili, wamesema kuwa mradi huo utaimarisha amani, usalama na maendeleo ya Iran, Pakistan pamoja na mataifa mengine ya eneo hilo. Bomba hilo la gesi litakalokuwa na urefu wa kilometa 1,600, litapunguza uhaba wa nishati nchini Pakistan kwa kusafirisha kila siku cubic meters za gesi asilia milioni 21.5 (8.7 billion cubic meters kwa mwaka) kutoka Iran hadi Pakistan. Hata hivyo baada ya kuzinduliwa rasmi awamu ya kwanza ya ujenzi wa bomba hilo la kusarisha gesi kutoka Jamhuri ya Kiislamu ya Iran hadi Pakistan, serikali ya Marekani imeingilia kati mradi huo na kutoa vitisho vya kuiwekea vikwazo Pakistan kwa vile imeshirikiana na Iran kwenye mradi huo. Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Marekani Victoria Nuland, amesema kuwa Washington imeingiwa na wasiwasi juu ya ujenzi wa bomba hilo la kusarisha gesi kutoka Iran hadi Pakistan. Licha kuwepo vikwazo kadhaa, mradi wa bomba la gesi kutoka Iran hadi Pakistan utatekelezwa ipasavyo, amebainisha Waziri wa Habari na Utangazaji wa Pakistan, Firdous Ashiq Awan, katika mkutano wa hadhara ulioitishwa katika wilaya ya Marla mjini Lahore mwishoni mwa wiki. Wa s h i n g t o n b a a d a ya kusikia mpango huo imekuwa ikifanya jitihada za kuishinikiza Pakistani kufuta mradi huo licha ya kwamba Pakistan imekuwa ikihangaika kukidhi mahitaji yake ya nishati, ambayo yameongezeka kwa kasi siku
Habari za Kimataifa
AN-NUUR
RAIS Mahmoud Ahmednejad wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (kulia) na Rais wa Pakistan Asif Ali Zardari, wakisaini mkataba wa ujenzi wa bomba la gesi kutoka Iran kwenda Pakistan mwanzoni mwa wiki hii.
wa Rais na Bunge nchini Misri. Taarifa hiyo imeongeza kuwa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, nayo tayari imeshatia saini makubaliano hayo na nchi ya Sudan Kusini pia imetangaza kuwa itayasaini hivi karibuni. Nchi 11 zinazochangia maji ya Mto Nile ni Uganda, Kenya, Tanzania, Rwanda, Misri, Sudan, Sudan Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Eritrea na Burundi.
yanatoa huduma kwa Marekani hasa kwa kutilia maanani kwamba, Taliban na Washington wamekuwa wakifanya mazungumzo bila ya serikali ya Kabul kuwa na taarifa ya mazungumzo hayo. Ta y a r i s e r i k a l i y a Marekani imetoa taarifa na kukanusha vikali tuhuma za kuweko uhusiano kati yao na kundi la Taliban. Wakati huo huo Rais Karzai amevipiga marufuku vikosi vya kigeni vinavyoongozwa na Marekani kuingia katika maeneo ya Vyuo Vikuu vya nchi hiyo na kuwatia mbaroni wanachuo. Amesisitiza kuwa, hatua hizo zinakinzana na mamlaka ya kujitawala Afghanistan.
Habari/Matangazo
AN-NUUR
MAHAKAMA ya Hakimu Mfawidhi Wilaya ya Nyamagana, imesema itapitia hoja zilizowasilishwa Mahakamani hapo na Wakili wa upande wa utetezi, kupinga zuio la dhamana lililowekwa
wa hadhara wa Chama hicho uliofanyika katika viwanja vya Mbagala Zakhiem Maalim Seif ambae pia ni Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar amesema Dkt. Nchimbi analazimika kujiuzulu kutokana na wizara yake kushindwa kusimamia ulinzi wa Wananchi na mali zao. Amesema, jukumu la ulinzi wa raia na mali zao ni jukumu la serikali hivyo kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi ambayo ndio yenye jukumu la kusimamia ulinzi imeshindwa kutekeleza wajibu huo. Amesema matukio ya kihalifu yanayo endelea kujitokeza nchini iwemo kushambuliwa pamoja na kuuwawa kwa viongozi na raia wasio na hatia kunatokana na serikali kushindwa kuimarisha ulinzi kwa raia wake. Kumekuwa na matukio mbalimbali ya kihalifu yanayotokea hapa nchini ambayo Waziri Nchimbi na wizara yake wameshindwa kuyatafutia ufumbuzi hadi leo, hivyo hana budi kujiuzulu kwani ameshindwa kutekeleza wajibu wake kama waziri anaehusika usalama wa raia na mali zao, alisema Maalim Seif. Akizungumzia matukio ya kushambuliwa kwa viongozi wa dini yaliotokea Zanzibar hivi karibuni kuwa hayapaswi kuhusishwa na itikadi za kidini kutokana na utamaduni wa muda mrefu wa kuvumiliana kidini uliojengeka kwa Wananchi wa Zanzibar. Aidha Maalim seif amechukizwa na kauli ya Dkt. Nchimbi kulihusisha tukio la kuuwawa kwa Padre Evarist Mushi na matukio ya kigaidi na kusema tukio hilo si la kigaidi kwani Zanzibar hakuna ugaidi. Huyu ana lengo gani na Zanzibar hata kutangaza ugaidi kwa Zanzibar kwani Zanzibar hakuna ugaidi na wala hautatokea kamwe. Alisema
Maalim Seif. Akizungumzia mwenendo wa Serikali ya Umoja wa kitaifa ya Zanzibar amesema Serikali kwa kiasi kikubwa imefanikiwa kuleta maendeleo kwa Wananchi wake ikiwa ni pamoja na kuinua juhudi za wakulima katika ukuzaji wa kilimo chenye tija kwa wakulima na taifa kwa ujumla. Amesema kuwa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imefanikiwa kuinua zao la karafuu kwa kupandisha bei ya karafuu kutoka shilingi elfu tatu kwa kilo hadi elfu kumi bei ambayo inampa mkulima asilimia thamanini ya bei ya soko la dunia. Pia imefanikiwa kukuza kilimo cha mpunga kwa kuwapatia wakulima wa kilimo hicho kwa kuwapatia wataalamu wa kutosha pamoja na kushusha gharama za pembejeo za kilimo ikiwemo mbolea na dawa za kuulia wadudu ili kuwawezesha wakulima kulima kilimo chenye tija na kuondokana na utegemezi wa chakula kutoka nje. Aidha amesema kuwa serikali imefanikiwa kuongeza kiwango cha mishahara ya wafanyakazi hadi asilimia ishirini na tano kwa wafanyakazi wa kima cha chini ili kuweza kujikimu kimaisha. Nae Naibu katibu mkuu wa CUF Tanzania Bara Mh. Julius Mtatiro amewataka wanachama hicho kujitokeza katika kuwania nafasi za ujumbe wa mabaraza ya katiba ili kuweza kupata katiba bora itakayo endana na mahitaji ya Wananchi. Amesema kuwa kutokushiriki katika mabaraza ya katiba ya wilaya kutawapa nafasi watu wasiotaka maslahi mazuri kwa wananchi kuingia katika mabaraza hayo jambo litakalo sababisha kukosekana kwa katiba bora.
Sheikh Jabir Katura (kulia) akisisitiza jambo katika moja ya mikutano yake hivi karibuni.
Hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Bw. Mwambapa, alisema Mahakani hapo Jumatano wiki hii kwamba, ufafanuzi juu ya madai ya Wakili wa upande wa utetezi yaliyowasilishwa Mahakani hapo ya kutaka kuondolewa zuio la dhamana kwa mshtakiwa, utatolewa Machi 27, 2013, kesi hiyo itakapotajwa tena. Sheikh Jabir Katura, mmoja wa viongozi wa Kiislamu wanaofuatilia kesi hiyo, alisema Waislamu wengi wa Kanda ya Ziwa wanaona kama kesi aliyofunguliwa Imam Hamza, imelenga kumshikisha adabu kutokana na na kutoa msimamo ambao ulimkera Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuhusu sakata la kuchinja Mkoani Geita. Alisema kuwa wakati wa sakata la kuchinja kule Geita, Imam Hamza alikuwa kiongozi wa upande wa Waislamu katika hatua za kutafuta suluhu juu ya mzozo huo. Alisema katika mazungumzo ya kupata suluhu yaliyohusisha pande mbili kati ya Waislamu na Wakristo chini ya Waziri Mkuu Pinda, upande wa Waislamu wakiongozwa na Imam Hamza, ulitaka kwanza watuhumiwa Waislamu ambao wameswekwa ndani kufuatia kadhia iliyotokea, nao kuachiwa kama ambavyo wenzao Wakristo walivyoachiwa, ili mazungumzo hayo yawe ya suluhu ya haki na ya kweli. Sheikh Katura, alisema pengine msimamo huo wa Imam Hamza na Waislamu ulimkera Waziri Mkuu na sasa inaonekana kuwa kuna haja ya kumshikisha adabu. Alisema pamoja na kwamba moja ya sababu za kumkamata na kumfungulia kesi Imam Hamza, ni madai ya kusikika akifanya uchochezi kupitia mahubiri yake katika CD, lakini alisema katika CD hizo, hakuna ambapo Imam Hamza, kachochea zaidi ya kueleza hali ya yale yaliyojiri kule Geita na kufafanua jinsi Waislamu wanavyopuuzwa kila wanapojitetea. Ndege wote watalia lakini akilia Bundi ni uchuro, ni mojo ya CD inayotajwa kusikika Imam Hamza akihubiri, ambayo inadaiwa kuwa kuna uchochezi ndani yake.
SHAMBA LINAUZWA
SHAMBA LA EKARI 14 LINAUZWA KWA HARAKA LIPO CHAMAZI-DOVYA DAR ES SALAAM BEI NI MAELEWANO KWA MAWASILIANO: PIGA SIMU: 0759 450425 0784 463207 0754 479783 WAHI MAPEMA BAHATI NI YAKO
Inawatangazia Waislamu wote Kuwa Imeandaa Safari ya Hijja Mwaka 2013 Sawa na Mwaka 1434 Hijria kwa Dola US$ 3550 tu. Umra kwa Mwezi wa Ramadhani itakuwa ni Dola US$ 1995 Fomu zinapatikana katika osi zifuatazo:1. Osi ya Ahlul Daawa Dar es salaam Mtaa wa Dosi na Mkadini Nyumba Namba 26 Mkabala na Showroom ya Magari Tel 0713 730 444, au 0773 804101 au 0785 930444 na 0773 930444. 2. Osi ya Ahlul Daawa Zanzibar Rahaleo Tel 0777 484982 au 0777 413 987. 3. Abubakar Maulana wa Markaz Kiwalani Dar es salaam 0784 453838 4. Abdallah Salehe Mazrui ( HOKO) Dar es salaam 0715 724 444 5. Salim Is-haq Dar es salaam 0754 286010 au 0774 786101 6. Dukani kwa Abdala Hadh Mazrui wete pemba 0777 482 665 7. Dukani kwa Mohamed Hadh Mazrui Mkoani Pemba 0777 456911 8. Sheikh Daudi khamis sheha 0777 679692 9. Maalim Seif Humoud Hamed Kijichi Zanzibar 0777 417736 Wahi kulipia. Osi ya Ahlul Daawa Dar es salaam 0713 730 444 au 0773 804101 au 0785 930444. Osi ya Ahlul Daawa Zanzibar Rahaleo 0777 484982 au 0777 413 987. Maalim Seif Humoud Hamed Kijichi Zanzibar 0777 417736 Sheikh Salim Mohamed Salim 0774 412974 au Kupitia ACCOUNT NAMBA 048101000030 NBC Tanbih: Atakae maliza Taratibu zote kuanzia sasa Mpaka 15 July 2013 atapata Punguzo la asilimia 16% atalipia $ Dola 2982 tu. Atakae maliza Taratibu zote kuanzia Tarehe 16-july Hadi Tarehe 15 Augost 2013 atapata Punguzo la Asilimia sita 6% atalipia Dola $3337 tu. Kutakuwa na umra ya utangulizi kabla ya Umra ya Hijja kwa atakae maliza kufanya hivyo. Atakae maliza taratibu zote mwanzo ndie atakae shughulikiwa mwanzo. Ukilipia kwa njia ya Account kwanza piga simu 0774 412975. Kumbuka Kikundi cha Ahlul Daawa Kwa Bei nafuu kuliko wote na Huduma bora Kuliko wengi. Nyote mnakaribishwa
7
Na Bakari Mwakangwale WAISLAMU wametakiwa kukataa propaganda zinazopandikizwa na watu wasioitakia mema nchi hii, kuwa kuna uhasama baina ya Waislamu na Wakristo. Wi t o h u o u m e t o l e w a na Amir wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu (T), Sheikh Mussa Yusuph Kundecha akiongea na viongozi wa Jumuiya na Taasisi mbalimbali za Kiislamu katika semina maalum iliyofanyika katika Hoteli ya Lamada, Ilala Jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki iliyopita. Amir Kundecha amesema Waislamu siku zote kilio chao kipo kwa Serikali na si Wakristo na msingi mkubwa wa malalamiko yao ni kutotendewa haki kama watu wengine katika jamii. Amir Kundecha aliwataka viongozi hao kufikisha ujumbe huo kwa Waislamu ili kuepuka na kukataa propaganda zinazolazimishwa kuwa kuna uhasama baina ya Waislamu na wasiokuwa Waislamu katika jamii. Ningelikuombeni mkaondoe dhana hiyo katika jamii kwa maana maalumu na maana mahususi, kataeni kuonyesha kuna mvutano na wasiokuwa Waislamu, sisi tuna tatizo na Serikali yetu kupuuza madai yetu. Alisema Amir Kundecha. Alisema, kimsingi katika nchi hii hakuna mgogoro kati ya Waislamu na Wakristo kwani wanaishi pamoja kwa kushirikiana katika mambo mbalimbali ya kijamii. Amir Kundecha alionyesha wasiwasi wake kwa Serikali kwamba inaweza kuwa chanzo cha kuvunjika kwa amani kutokana na kupuuza na kutoshughulikia madai ya msingi ya Waislamu. Alianisha madai hayo kuwa ni pamoja na tatizo la Baraza la Mitihani, kuwepo kwa Mahakama ya Kadhi, suala la Tanzania kujiunga na OIC na kuwepo kwa MoU kati ya Serikali na Makanisa. Akifafanua hayo alisema, umma wa Kiislamu nchini una tatizo dhidi ya Serikali yao kwa kuzuiwa kuwa na mahusiano ya kitaasisi na Taasisi ya Kimataifa ya Kiislamu ya OIC. Ukitazama hoja zinazotolewa kuzuiwa Waislamu kuwa na mahusiano na Taasisi hiyo pamoja na Serikali kujiridhisha kuwa hakuna Tatizo Tanzania kujiunga utakuta ni hoja zisizo na msingi kabisa.
Habari/Matangazo
AN-NUUR
Amir wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu (T), Sheikh Mussa Yusuph Kundecha akiongea na viongozi wa Jumuiya na Taasisi mbalimbali za Kiislamu katika semina maalum iliyofanyika katika Hoteli ya Lamada, Ilala Jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki iliyopita.
Alisema, akiwa katika moja ya mkutano wa viongiozi wa dini, alipata kusimama kiongozi mmoja akidai kuwa OIC, ni taasisi ya kidini na ni hatari kabisa kwa umoja wa kitaifa na amani ya nchi. Alisema, baada ya kutolewa kwa hoja hiyo, alimtaka mtoa hoja aonyeshe kipengele cha Katiba ya OIC, ambacho ana wasiwasi nacho huku akihoji uhalali wa kuwepo nchini Ubalozi wa Makao Makuu ya Kanisa Katoliki Vatcan, ili hali hiyo si nchi. Akifafanua hali ya mvutano kama huo, Amir Kundecha, alisema kinachotaka kujengwa miongoni mwa wanajamii ni kuonesha kuwa upo mvutano na tatizo baina ya Waislamu na wasiokuwa Waislamu nchini. Alisema, mfano wa hivi sasa ni kuwa Waislamu wameilalamikia Serikali kuhusu Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), lakini wanapuuzwa. Nyinyi kwa umri wenu, mmepata hata siku moja kusikia Waislamu wakilalamika juu ya jambo hilo? Nasema tunapuuzwa kwa sababu Serikali imekataa kwa makusudi kuona uzito wa tunacho kilalamikia na siku zote imepuuza jambo hilo. Alisema Amir Kundecha.
Alisema, kadhia hiyo n a N E C TA , Wa i s l a m u waliipeleka kama tatizo mahala husika, lakini alidai kwa kuwa kuna dhana ya kupuuza jambo likisemwa na Waislamu, hata kama lina ukweli, badala yake walipewa majibu yasiyofaa. Amir Kundecha, alisema CHADEMA, walipeleka hoja yao binafsi katika kikao cha Bunge lililopita kuhusu N E C TA , n a u k i a n g a l i a yale yaliyolalamikiwa ni sawa na yale malalamiko ya Waislamu yaliyopuuzwa, kilichobadilika ni mahali palipoandikwa Waislamu pameandikwa CHADEMA. Amir Kundecha, alidai kwamba tatizo lingine la Waislamu na Serikali yao ni kugawanywa (na Serikali) kwa nguvu miongoni mwa Waislamu. Akitolea mfano juu ya madai hayo, Amir Kundecha alisema, wakati Waislamu wanahangaika na masuala ya Mahakama ya Kadhi, Waislamu walikubaliana kuunda timu ya pamoja, kutoka Jumuiya na Taasisi mbalimbali za Kiislamu. Alisema, timu hiyo iliundwa ikiwa na washiriki 25, kwa bahati mbaya alidai katika kikao kilichoitishwa na Serikali na kufanyika Mkoani
Dodoma, mgeni rasmi akiwa ni Makamu wa Rais, Dk. Ghalib Bilali, Serikali iliamua kuwagawa Waislamu. Serikali kwa makusudi ikaamua kutugawa Waislamu, ikijua kabisa wanachokifanya kitaleta mtafaruku mkubwa huku nje. Timu ina uwakilishi wa Taasisi 25, lakini Serikali ikaiita Taasisi ya Bakwata tu, na kuwapa fulsa ya kuchagua Makadhi nchi nzima. Aliainisha Amir Kundecha. Alisema, ipo mifano mingi juu ya Serikali kuwapindishia
TANGAZO
AN-NUUR
9
Na Ahmed Omar Khamis
Makala
AN-NUUR
SIKU ya tarehe 3 Machi 1996, enzi zile Wazanzibari walipogawanywa na kutiwa chuki baina yao, ilidaiwa na serikali kuwa masa watatu wa usalama waliokuwa kwenye doria huko katika kijiji cha Shengejuu, kisiwani Pemba, walipigwa na kuporwa silaha na wanakijiji. Kwa sura ya kawaida ya uaskari, ni vigumu kuaminika kwamba askari watatu wakiwa na silaha mikononi waporwe silaha zao wote watatu na wapigwe bila ya wao hata kujeruhi mtu yeyote au kujeruhiwa wao wenyewe. Muda sio mrefu, siku ya pili yake tu, kijiji hicho kilivamiwa na kiasi cha askari wapatao 300 wa kikosi cha FFU na jeshi la wananchi (JWTZ) waliokuwa wako kamili kivita. Unyama, mateso na vitendo vya kihuni walifanyiwa wananchi wa kijiji cha Shengejuu waliokuwa hawana hatia yoyote. Baadhi ya wanakijiji walipigwa hadi kuzirai, wengine waliibiwa mali zao kama vile kuku na mbuzi, maduka yaliporwa, wanawake walibakwa na watu wapatao 80 waliwekwa ndani. Kati ya watu hao 80, watu 30 waliachiliwa huru na waliobaki waliendelea kusota ndani kwa kipindi kirefu sana. Kiongozi mmoja mkuu wa SMZ wakati ule, aliwahi kufanya mkutano na waandishi wa habari kuelezea hali ya mtafaruku inayoendelea katika kijiji hicho cha Shengejuu, na hapa namnukuu moja ya kauli zake aliyoitoa kupitia kikao hichoSasa tunataka kuwafanya watu wajue kama serikali ipo. Katika enzi hizo wafuasi wa CUF walikuwa wakisingiziwa kuhusika na hujuma mbalimbali kama vile kuchomwa moto madarasa ya skuli, kupaka vinyesi kwenye kuta za skuli, kutia vinyesi kwenye visima n.k. Hizi bila shaka zilikuwa ni mwendelezo wa propaganda chafu za kisiasa zilizokuwa na lengo la kujenga picha ya uongo na kuhalalisha hujuma dhidi ya watu wasio na hatia. Waliokuwa wakifanya haya ni watu waliofundishwa vyema propaganda na siasa chafu za uchochezi. Wa k i t e k e l e z a v i t e n d o hivyo huku wakilindwa na
10
Makala/Tangazo
AN-NUUR
husumbuliwa na kudhalilishwa na maofisa wa magereza. Wanalazimishwa kusubiri kwa muda mrefu, hadi saa nne, kabla ya wafungwa kuletwa kwao. Matokeo yake ni kuwa mawakili hao hushindwa kukutana na wafungwa wote waliokusudia kuwaona kwa sababu muda wao humalizika kwa haraka. Kwa mfano, Februari 4, 2003, wakili wa Addameer, Bw. Mahmoud Hassan, alilazimika kusubiri kwa saa tatu katika jela ya Neveh Terzah kabla ya mfungwa kuletwa. Hakuna sababu yoyote iliyotolewa kwa wakili huyo kuwekwa ndani ya gereza akisubiri kwa muda wote huo. H i v i n d i v y o wanavyodhalilishwa wafungwa wa kike katika magereza ya Israel. Katika muda wa miaka 43 iliyopita inakisiwa kuwa wanawake wa Kipalestina takriban 10,000 wamekamatwa na kufungwa chini ya amri ya wavamizi wa Kiisraeli. Wafungwa wa kike kwa kawaida huwa wanafungwa katika jela za Hasharon na Damon. Jela hizi ziko nje ya maeneo ya Palestina yaliyovamiwa mwaka 1967. Huu ni uhalifu wa kifungu cha 76 cha Makubaliano ya Geneva, ambacho kinasema dola inayovamia nchi nyingine hairuhusiwi kuwafunga raia wa nchi hiyo nje ya nchi yao. Imeandaliwa na Kituo c ha Habari cha Palestina (Tanzania) P.O Box 20307, 612 UN Road Upanga West, Dar es Salaam Tel: 2152813, 2150643 Fax: 2153257 Email: pict@pal-tz.org Website: www. pal-tz.org
VIWANJA VILIVYOPIMWA KONGOWE KIBAHA TOWNSHIP REGISTERED PLAN No. 70995 BLOCK H
PLOT HATUA ENEO MRABA GHARAMA TSH
H1 H2 H3 H4 H5 H6 H7 H8 H9 H10 H11
50 x 29 32 x 32 50 x 30 37 x 30 50 X 45 33 x 37 60 x 45 50 x 40 67 x 50 70 x 45 90 x 50
1341 Sqm 1136 Sqm 1470 Sqm 1115 Sqm 2259 Sqm 1566 Sqm 2423 Sqm 1984 Sqm 3564 Sqm 2842 Sqm 3780 Sqm
4,023,000/= 3408000/= 4410000/= 3345000/= 6750000/= 4695000/= 7269000/= 5952000/= 10692000/= 8526000/= 11340000/=
Vipo Barabara ya Kongowe-Soga Kilomita moja toka barabara ya Morogoro. Simu No.0755 090 754/0715 090 754.
11
Na Dr. Noordin Jella
ZANZIBAR kwa miaka mingi kimekuwa ni kisiwa cha amani ya kweli hata ukaangusha kiroba cha mamilioni ya pesa atakayeziokota atazipeleka Zanzibar TV kwa mtangazaji au msikitini kwa Imamu ili akatangazie umma mwenye mzigo wake aje achukue. Lakini baada ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi hapa nchini mwaka 1992 kisiwa hiki cha amani kimejikuta mara kwa mara kikitwishwa lawama za kigaidi zinazotolewa na wanasiasa uchwara waliochoka kukiri kwa kigezo maalumu cha kuibaka demokrasia na ustaarabu visiwani humo. Ta t i z o l a k u b a k w a k w a demokrasia visiwani Zanzibar ni tatizo sugu na la muda mrefu lakini kabla sijathibitisha hilo hapo baadae, ningeomba tuangalie kwa makini na upana maana ya ugaidi. Kwanza kabisa kabla hatujaanza kuliangalia suala lenyewe kwa kirefu, ni vizuri tuyajibu maswali machache muhimu yafuatayo: Ugaidi maana yake nini? Nani anaweza kuwa gaidi? Je, kuna aina ngapi za ugaidi? Je, Nchimbi ana uzoefu au uhusiano gani na ugaidi au magaidi? Je, gaidi anaweza kuwa mtu binafsi au hata serikali inaweza kuwa ya kigaidi? Haya ni maswala muhimu sana ambayo kila mmoja wetu anatakiwa atafute majibu yake ili tuweze kuhalalisha msemo wa Nchimbi au kuukanusha: Gaidi ni neno la kigeni ambalo limefanywa kutafasiriwa kwenye lugha ya Kiswahili lakini neno lenyewe linatokana na neno la Kiingereza la Terrorist. Sasa kulingana na tafasiri ya neno hili kutoka kwenye kamusi ya Kiingereza ya Oxford ni kwamba gaidi ni mtu ambaye anatumia vitendo vya vurugu na huku vikiambatana na vitisho vyenye madhumuni ya kushinda au kudhibiti aidha serikali au jamii. Kulingana na tafasiri hii, mtu au serikali inaweza kuwa gaidi. Aina za ugadi zinaweza kuwa nyingi inategemea na mtu au serikali imeamua kutumia mbinu zipi? Kulingana na tafasiri ya ugaidi nilivyoielezea hapo juu, Waziri Nchimbi kama mwanasisa (Mbunge) inawezekana kabisa tena mara nyingi tu katika harakati zake za kuwa mbunge aidha alishawahi kuwa gaidi au alishawahi kuwasadia magaidi hasa ukizingatia kwamba uchaguzi wa viongozi wa umma hapa nchini si huru na wala si wa haki! Tumeshaona kwamba mtu au kikundi cha watu kinaweza kuwa cha kigaidi, pia serikali inaweza kuwa ya kigaidi au taasisi za serikali na vyombo vya umma kama vile kitengo cha usalama wa taifa, jeshi la polisi, tume ya uchaguzi, takukuru nakadhalika. Pamoja na tafasiri ya neno ugaidi kama lilivyoelezewa kwenye kamusi ya Oxford, lakini uelewa wa neno hili kwa
Makala
AN-NUUR
matukio kama hayo yakitokea huku Bara wanasiasa wanatumia maneno mengine kuyatafasiri, isipokuwa yakitokea kule kisiwani Zanzibar basi tayari lazima matukio hayo yahusishwe na ugaidi kwa vile neno Ugaidi lina mashiko mazuri na matamu sana kwa serikali ya CCM. Serikali ya CCM wameweza kufaidi matunda ya Zanzibar kwa kutumia neno rahisi sana kulitamka la Ugaidi kwa zaidi ya miaka 20 sasa! Hivyo kwa mtu mchambuzi mzuri wa mambo ya siasa hapa nchini hasa siasa za kule Zanzibar hatashangaa hata kibaka akihusishwa na vitendo vya ugaidi kwa vile neno hilo linaleta kula! Wazanzibar na Watanganyika wote kwa ujumla wapo katika kipindi muhimu sana cha kutafuta katiba mpya itakayoweza kuyaongoza mataifa haya mawili kwa miaka mingine mingi ijayo. Wananchi wa Zanzibar wamekuwa wawazi kwa kueleza bayana kwamba hawaridhiki na mfumo wa muungano uliopo hivi sasa na kwa maana hiyo walikuwa wanataka mfumo huo ubadilishwe; pia kwa upande wa Tanganyika nao wanataka serikali yao iliyouwawa tangu mwaka 1964 ifufuliwe na kuwe na muungano wa kweli unaozijumuisha nchi hizi mbili kiukweki na kikamilifu. Kwa vile tunajua kwamba siasa ni mchezo mchafu; nina wasiwasi neno ugaidi lisije kutumiwa kama kigezo cha kubaka democrasia ya kupitisha katiba inayoandaliwa hivi sasa, hasa ukizingatia kwamba wananchi wa Zanzibar walio wengi hawautaki muungano kama ulivyo hivi sasa! Kuuwawa kwa padri kumeifanya serikali ihusishe vyombo vya nje vya ulinzi vya Marekani kama vile FBI. Kwa Wamarekani neno Ugaidi wao ni biashara kubwa sana ambayo inawaingizia mabilioni ya dola kila mwaka (terrorism is a big business), hivyo nchi yoyote duniani bila ya kujali kwamba ipo kona gani ya dunia, madhali imesema kuna ugaidi basi Wamarekani wapo tayari wakati wowote wapeleke askari wao wakafe huko potelea mbali, lakini wahakikishe kwamba wanafanya biashara kubwa kutokana na neno hilo la ugaidi! Sisi tunapolitumia neno ugaidi, hatufikirii suala la biashara, hapana, bali sisi tunasema hivyo ili kuibaka demokrasia tuendelee kuwepo madarakani na huku tukiwa tumeshawawezesha wale wakosoaji wakubwa duniani wa ubakwaji wa demokrasia kufanya biashara inayotokana na neno ugaidi ambalo tayari tumewatonya nalo! Mwisho kabisa napenda nimshauri Dr. Nchimbi kama mwanasiasa mchanga anayetaka kujivunia ujana wake wa siasa hapo baadae atakapokuwa mzee, kwamba aachane na siasa za kizazi cha wazee wa CCM ambazo zimepitwa na wakati; siasa za wazee hao hazina mvuto tena Tanzania.
12
Sheikh huyu Sheikh gani
Simtaki Sheikh huyu, sifa zake siyo njema, Yafaa kumuepuka, Sheikh huyu sio mwema, Yazidi yake jeuri, wala hana sifa njema, Sheikh huyu Sheikh gani, aso faida na umma. Yu pamoja na kar, hajui cheo neema, Hugawa Waislamu, kwa zao dhamira njema, Ghururi za ulimwengu, Sheikh zimemwandama, Sheikh huyu Sheikh gani, aso faida na umma. Kitabu chakojolewa, mbio mbio kulalama, Kakojolea mtoto, asitupiwe lawama, Hivi unakithamini, kitabu chake Rabana, Sheikh huyu Sheikh gani, aso faida na umma. Majumba hata magari, sio vitu vya maana, Ipo siku siku moja, vyote vitakusakama, Muogope Mola wako, adhabu zake ni pana, Sheikh huyu Sheikh gani, aso faida na umma. Bora wangu ufukara, kesho nipate salama, Kuliko maisha bora, dhulma kukutawala, Huwezi pata salama, tubu utaangamia, Sheikh huyu Sheikh gani, aso faida na umma. Mwisho ninakuusia, ewe Sheikh ulo Dar, Wengi waloangamia, fedha ziliwahadaa, Waliuza utu wao, dini wakaikataa, Sheikh huyu Sheikh gani, aso faida na umma. Abaa Abdul-azizi (Ngamia wa Jangwani) Dar.
Mashairi/Barua/Makala
AN-NUUR
Kama ningeliwezaga, nami pia kuandika, Kalamu ningeshikaga, maswali ningewatwika, Wote wanaovuruga, amani yetu hakika, Kama ningeliwezaga, hofu kando kuiweka. Kama ningeliwezaga, kusema na kutamka, Kipaza ningeshikaga, yote ningeyatapika, Yanayo tuumizaga, kote yangeli sikika, Kama ningeliwezaga, hofu kando kuiweka. Kama ningeliwezaga, kutunga zikatungika, Habari za kuwazuga, wananchi potosheka, Mapema tungekaga, nchi yetu kuchafuka, Kama ningeliwezaga, hofu kando kuiweka. Kama ningeliwezaga, ukweli kuutamka, Ningelivalia njuga, bahari nikaivuka, Visiwani tiananga, wauaji kuwasaka, Kama ningeliwezaga, hofu kando kuiweka. Kama ningeliwezaga, kuongopa pasi shaka, Ningeliwachafuaga, nyote mkawa mwanuka, Kwangu ningesashaga, uchafu ukaondoka, Kama ningeliwezaga, hofu kando kuiweka. Kama ningeliwezaga, kuamuru Amrika, Wote ningeliwaswaga, barazani vibaraka, Ummatumewachokaga,nanyingizenu dhihaka, Kama ningeliwezaga, hofu kando kuiweka. Kama ningeliwezaga, kufuta likafutika, Baraza ngelifutaga, kabisa likafutika, Moyo wa niumizaga, kushoto wakijiweka, Kama ningeliwezaga, hofu kando kuiweka. Kama ningeliwezaga, kutangaza Tanganyika. Visiwani hawanaga, sheria imeshindika, Raia kumilikaga, silaha mekatazika, Kama ningeliwezaga, hofu kando kuiweka. Kama ningeliwezaga, uliza likajibika, Nani aliyempaga, silaha ikatumika? Mauaji kafanyaga, au nje ametoka? Kama ningeliwezaga, hofu kando kuiweka. Kama ningeliwezaga, kaditama nimeka, Hili ningelisemaga, uongo siyo kichaka, Timamu kujichaga, majinuni sina shaka, Kama ningeliwezaga, hofu kando kuiweka. Isihaka Hemed Mzuzuri Morogoro
Kama!
Hapa ndipo inapozuka shaka kubwa miongoni mwetu kuamini au kutoamini mfumo mzima wa utoaji haki, utendaji haki. Sisi siku zote tunaingia ndani ya tukio, kama alivyofanya Waziri wa Mambo ya Ndani Mheshimiwa Dr. Emmanuel Nchimbi. Lakini tujue kuwa polisi kama taasisi, sidhani kama wananchi wengi wanaiamini vya kutosha. Mnakumbuka lile tukio la kuibiwa mfanya biashara Dar es Salaam juzi juzi tu; na pesa zilizopatikana waligawana jamaa! Hiyo ripoti ya Afande Suleiman Kova iko wapi? Kama polisi imefikia kufanya haya na mengine mengi itakuaje? Tumuamini nani? Mwananchi Zanzibar
Aombe deni lake au haki yake kwa upendo na sio kwa ubabe na iwe kwa ulaini bila kutumia nguvu na achunge hali ya mdeni wake, na akiwa hana kitu amsubirie au amsamehe hilo deni lake. Amesema Mwenyezi Mungu mtukufu, Na anapokuwa mdaiwa hana kitu, na asubiriwe hadi atakapopata na mtakapotoa sadaka ni kheri kwenu ikiwa mnajua . Barakat 28. Msamaha katika ulipaji deni:Arudishe haki kwa mwenyewe kwa wakati waliokubaliana na wala asimlazimishe kwa nguvu, kisha akafuatia kutekeleza haki kwa mwenyewe na wingi wa asante na dua au kumkimbia ikiwa anaweza. Na mfano hai na bora kabisa ni ule ambao mtu mmoja alikuwa anamdai Mtume, akaja kuliomba deni hilo kabla ya muda, akakusudia Sayidina Omar kutaka kumuua, Mtume akasema; Nilitarajia kuwa utaniamrisha kuwa nimlipe, tena kwa vizuri zaidi, akaamrisha alipwe deni lake na ziada, akasema hii ziada ni malipo ya kule kumtisha kwako ewe Omar. Vile vile miongoni mwa msamaha wa Kiislamu ni kuongea maneno mazuri na kauli nzuri. Amesema Mwenyezi Mungu mtukufu, Nasema waambie waja wangu waseme yaliyo mazuri zaidi. Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu, Neno zuri ni sadaka. Hii ni baadhi ya mifano hai ya kuonyesha msamaha wa Uislamu, ambao laiti tunge yazungumzia kwa upana, basi pasingalitosha. Lakini tunatosheka na maneno haya mafupi ambayo yatampa msomaji picha ya uhakika juu ya msamaha wa Kiislam na utukufu wa sheria zake. Basi Mwenyezi Mungu ndiyo mumwezeshaji.
13
MAKALA
AN-NUUR
Inaendelea Uk. 14
14
Makala
AN-NUUR
Inatoka Uk. 13
kigaidi-State Terrorism. Dola linapokua gaidi hua hatari kuliko chui mla watu, mwenye njaa kali. Wakati Fulani Mfalme mmoja huko katika China ya kale, alikitembelea kijiji kimoja katika mahmia yake. Alipoka kwenye kijiji hicho alimkuta mama mmoja analia kwa uchungu mkubwa na huku anaomboleza. Mfalme akaingiwa na huzuni na akasimamisha msafara wake, kisha akamuuliza yule mama, nini kilichomsibu. Mama yule akamueleza Mfalme kwamba mwanawe ameliwa na chui asubuhi ya siku ile. Mfalme akambembeleza sana na akamtia moyo kwa kumwambia kua asikate tamaa Mwenyezi Mungu atampa mtoto mwengine. Yule mama akapiga mayowe na kuangua kilio kuliko cha mwanzo. Mama yule akamwambia mfalme, chui huyu kaua mume wangu kwanza na kisha kaua watoto wangu watano na huyu wa leo ni wa sita, sina tena mtu mimi. Mfalme akahuzunishwa sana na masahibu yaliomkuta mama yule. Baadae mfalme
yule akamshauri yule mama aondoke kwenye kijiji kile. Mama yule akamwambia mfalme kwamba siwezi kuhama hapa, kwani katika kijiji chetu kuna utawala mzuri unaoheshimu haki za watu. Mfalme akasema, kumbe watawala wabaya ni hatari kuliko chui mla watu. Vivyo hivyo, kumbe dola linapokua gaidi ni hatari kuliko chui mla watu. Dola linapokua gaidi maisha ya raia hua kitu kisicho na thamani na utu wa mtu hua hauna maana. Lakini baya zaidi ni kua dola inapokua gaidi hua si rahisi kujibadili na hata ikicha kucha zake basi meno yake yataonekana pale inapocheka. Zanzibar hivi sasa ni tulivu na shwari kutokana na damu nyingi iliyomwagika huko nyuma ambayo hatimae ilipelekea kupatikana hiki kifaa kinachoitwa Mwafaka. Lakini madhara na simanzi za enzi ya dola ya kigaidi bado zipo na ni vigumu kusahaulika kwa sababu bado serikai zilizopo madarakani hazitaki kukubali kwamba mambo yaliofanyika huko nyuma yalikua ni makosa makubwa
ya kisiasa na kijamii. Sasa hivi katika ulimwengu wetu huu kumezuka utamaduni wa kisiasa ambao unaleta mwelekeo mwema wa kuleta umoja wa kitaifa, utengemano na uzalendo. Utamaduni huu ni ule wa kutafuta maridhiano kwa nia ya kusahau yaliopita na kuanza ukurasa mpya katika Taifa. Ili kuondoa sura mbaya ya ugaidi wa dola uliofanyika huko nyuma dhidi ya raia basi haitakua jambo la aibu serikali kukiri kua waliotangulia walitenda kosa. Kinyume cha hivyo, serikali zetu zinapoendelea kukaa kimya na kujifanya viziwi basi huenda jambo hili huko mbele likachukua sura nyengine. Viongozi wetu wasijifanye vipofu na viziwi, wasikilize na watazame nini kinatokea ulimwenguni hii leo kuhusu masuala kama haya. Kumnyima mwananchi haki yake ya kiraia kuihoji Serikali na pia kuwakataza watu wasiyaseme maovu yaliofanywa na Serikali dhidi ya raia zake ni bado kuendeleza ugaidi wa dola. Hivi sasa Kadinali Pengo ametoa matamko mazito anasema:
Hili si tukio la dharura, kiasi kwamba watu wetu wa usalama wa Taifa washindwe kuzuia, hili lilijulikana na lingeweza kuzuilika. Kwa maneno hayo ya Kardinali panahitajika uchunguzi wa hali ya juu. Vile vile tusikimbilie ugaidi tu, hata kauli ya Rais Kikwete alioitoa miezi ya nyuma ya kuwaonya baadhi ya Viongozi wa dini ambao wanajishirikisha na uuzaji wa madawa ya kulevya ni vizuri kutupiwa macho. Siku zote tunasikia kwamba Zanzibar ni njia kuu za madawa ya kulevya. Jambo hilo lisidharauliwe hata kidogo, lifanyiwe kazi. Pia tusisahau kuwa Wajerumani walichoma moto jengo la Bunge la Wajerumani ili wapate kuwasingizia wapinzani wa serikali na kuwakamata na mwishowe kuwauwa. Ni jambo zuri kushirikiana na maraki zetu ili kuwatafuta wauwaji hawa. Lakini wananchi wote wa Tanzania wanangojea ripoti ya uchunguzi itolewe kwa vile pesa nyingi za walipa kodi zitatumika kwa shughuli hiyo.
15
TANGAZO
AN-NUUR
1.
KIRINJIKO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL NYASAKA ISLAMIC SECONDARY SCHOOL UBUNGO ISLAMIC HIGH SCHOO L
Shule hizi ni za Kiislamu zenye lengo la kuwapa wanafunzi taaluma ya hali ya juu na malezi bora ya Kiislamu kwa gharama nafuu. Shule hizi ni za mchanganyiko wa wavulana na wasichana na zinapokea wanafunzi wa bweni tu. 2. Masomo yanayofundishwa ni Islamic knowledge, Combinations za SAYANSI, ARTS, BIASHARA pamoja na COMPYUTA. 3. Muombaji awe na Crediti 3 au zaidi na angalau D ya Elimu ya Dini ya Kiislamu katika matokeo ya kidato cha nne. Ikiwa ana F au hakufanya Elimu ya Dini ya Kiislamu, basi awe tayari kusoma programu maalum ya Maarifa ya Uislamu atakapokuwa kidato cha tano. 4. Mwisho wa kuchukua na kurudisha fomu ni tarehe 18 /05 /2013 5. Fomu za Maombi zinapatikana kwa gharama ya shilingi 10,000/= katika vituo vilivyoorodheshwa hapa chini. 6. Arusha Kilimanjaro Tanga Mwanza Musoma Kagera Shinyanga Osi ya Islamic Education Panel Jambo Plastic Ghorofa ya 2 mkabala na msikiti Mkuu Bondeni - 0763 282 371/ 0784 406 610 Moshi: Msikiti wa Riadha 0654 723 418 Same: Kirinjiko Islamic Secondry School: 0784 296424/0655 697 075 Uongofu Bookshop: - 0784 982525/ Mandia Shop - Lushoto: 0782257533 Nyasaka Islamic Secondary School 0717 417685/0786 417685 Osi ya Islamic Education Panel - Mwanza - Mtaa wa Ruji mkabala na Msikiti Al-Amin 0785 086 770 Duka la Kansolele -Stendi ya zamani sokoni - 0714587193 Bukoba: Alhuda Caf Kwa mzee Kinobe karibu na osi za TRA. - 0688 479 667 Msiikiti wa Majengo-0718866869 Kahama osi ya AN NUUR Karibu na msikiti wa Ibadhi: 0753 993930 Ubungo Islamic High School 0754 260 241/0712033556 Osi ya Islamic Ed. Panel Temeke -Msikiti wa Nurul Yakin 0655144474 Wasiliana na Ramadhani Chale :0715704380 Hijra Islamic Primary School : 0716 544757/0712 325086 Osis ya Islamic Ed. Panel karibu Nuru snack Hotel 0714285465 Babati: Shule ya Msingi Hangoni: 0784 667575 Msikiti wa mwanga Kigoma: 0753 355224 Kibondo Islamic Nursery School: 0784 442860 Kasulu: Murubona Isl.SS. 0714710802 Wapemba Store: 0784 974041/0786 959663 Amana Islamic S.S 0786 729 973 Kwa Kawanga Karibu na Msikiti wa NURU 0715 681701/0716791113 Mkuzo Islamic High School. 0716 791113 Duka la vifaa vya Kiislamu nje ya Msikiti wa Uyole 0713 200209 Rexona Video mkabala na Mbeya RETICO: 0713 200209 Sumbawanga: Masjid TAQWA 0717082 073 Kituo cha Kiislamu Isevya: 0784 944566 Madrastun Najah: 0714 522 122 Wete: Wete Islamic Education Center: 0777 432331 Madrasatul Fallah: 0777125074Osi ya ust. Yusufu Ally jirani na msikiti mkuu 0653705627
Dar es Salaam Morogoro Dodoma Singida Manyara Kigoma Lindi Mtwara Songea Mbeya Rukwa Tabora Iringa Pemba Unguja Maa -
Pia Fomu zinapatikana kwenye Tovuti: www.ipctz.org. Ikumbukwe kuwa watakaopata fomu kupitia tovuti (download) watatakiwa kuzilipia wakati wa kuzirejesha. USIKOSE NAFASI HII ADHIMU WAHI KUCHUKUA FOMU SASA! Wabillah Tawiq MKURUGENZI
16
AN-NUUR
16
AN-NUUR
Na Bakari Mwakangwale SERIKALI imetakiwa kuacha kupiga propaganda chafu dhidi ya Waislamu. Wito huo umetolewa na Jumuiya na Taasisi za Kiislamu, katika ukumbi wa Hoteli ya Lamada, Jijini Dar es Salaam, Jumamosi ya wiki iliyopita. Akisoma tamko la Waislamu kupitia Jumuiya na Taasisi mbele ya waandishi wa habari, Maalim Yassin Kachechele, alisema Serikali inapaswa kuwa makini katika kushughulikia kadhia za kidini zinazojitokeza hivi sasa nchini kabla ya kuelekeza shutuma na madai kwa Waislamu kwani ni hatari. Serikali iwe makini isiyachukulie mambo haya upande mmoja tu kuwa hayo ni mambo ya ugaidi na ugaidi huo ukaelekezwa k w a Wa i s l a m u , n i hatari. Alisema Maalim Kachechele. Maalim Kachechele, alisema hivi sasa kumekuwa na kamatakamata kwa vijana wa Kiislamu na kutiwa ndani na hata kufunguliwa mashata kwa tuhuma za uchochezi wa kidini. Hivyo, kupitia tamko hilo Maalim Kachechele, alisema vyombo vya dola vinapaswa kufanya shughuli zake kwa umakini katika kuyafuatilia kwa ukaribu
BAADHI ya viongozi wa taasisi za Kiislamu wakiwa katika semina iliyoandaliwa na Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini na kufanyika katika Hoteli ya Lamada, Ilala Jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
matukio hayo ili isiwe chanzo cha kulitumbukiza Taifa katika vurugu za kidini. Tamko hilo lilisema, kuuwawa na kujeruhiwa kwa
viongozi au waumini wa dini zote nchini hakukuanza sasa, kwani ishatokea pia Masheikh na Waislamu kuuwawa na hata kujeruhiwa lakini Serikali
haikusema kuwa matukio hayo ni mipango ya kigaidi, dhidi ya dini yoyote. Maalim Kachechele, alisema imekuwa ni desturi
hivi sasa kila inapotekea kwa Waislamu kuelekeza madai yao kwa Serikali yao, huibuliwa uvumi na tuhuma kwao kuwa wana mipango ya kuvamia na kuchoma Makanisa, vituo vya Polisi au osi za Chama fulani cha siasa. Hivi Waislamu wajihisi vipi kwa tuhuma kama hizo zisizo na ushahidi? Ni wazi mwenendo huu unawatia wasiwasi Waislamu kuwa kuna agenda ya siri dhidi yao na pia hujenga chuki na wenzao Wakristo. Alisema Maalim Kachechele. Tamko hilo lilifafanua k u w a , Wa i s l a m u k a m a wanaadamu wengine wanapenda kuishi kwa amani na utulivu, na kwamba hakuna binaadamu anayependa kusemwa vibaya, kuishi kwa hofu na ukosefu wa amani. Alisema, mwenendo wa kuwalaumu Waislamu kuwa wanavunja amani si jambo la kuvumilia kwani linajenga mfarakano miongoni mwa Waislamu na Wakristo. Kulikuwa na sababu gani kwa Serikali kukimbilia kusema ni tukio la kigaidi wakati haijafanya uchunguzi? Huku si kutoa muelekeo wa majibu ya uchunguzi? Kwani kila mauaji yanayofanyika nchini ni ugaidi? Inaonekana lengo ni kuwapaka tope Waislamu pamoja na dini yao. Limesema na kuhoji tamko hilo.
CHAMA cha wananchi CUF kupitia Katibu Mkuu wake ambae pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, kimemuhakikishia Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Tanzania, Jaji Joseph Wa r i o b a , k w a m b a Wazanzibari kwa umoja wao hawatokubali chochote kile ambacho kitasababisha kukosekana kwa Zanzibar yenye mamlaka kamili kitaifa na kimataifa itakayofuatiwa na mfumo mpya wa ushirikiano na Tanganyika kupitia
Muungano. Maalim Seif aliyasema hayo huko Makunduchi mkoa wa kusini Unguja hivi karibuni alipokuwa akizungumza na wananchi mbali mbali kwenye mkutano wa hadhara. Katika mazungumzo yake Maalim Seif amesema kuwa maoni ya Wazanzibar walio wengi wanataka mamlaka kamili ya nchi yao, kwa hiyo ni lazima jambo hilo litimie. Kufuatia mkutano huo Maalim Seif amesema kuwa kwa sasa Zanzibar haiwezi tena kukubali kukosa mamlaka yake ya kuwa na udhibiti wa mambo ya nje na mahusiano ya kimataifa kwani imechoka na
udhalilishaji inaofanyiwa kupitia Serikali ya Muungano. Maalim ametolea mifano mbali mbali ukiwemo ule wa Serikali ya Muungano kuilazimisha Zanzibar kujitoa katika Umoja wa Nchi za Kiislamu (OIC) mwaka 1993. Alifahamisha wazi kuwa kwa sasa Zanzibar inataka kuwa na Wizara na Waziri wake wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na haitokubali chochote chini ya hapo. Amesema kuwa udhibiti wa mambo ya nje ndiyo kigezo cha nchi kukubalika na kutambulika kimataifa na Zanzibar inataka kurejesha mamlaka hayo na kurejesha kiti chake kwenye Umoja wa Mataifa.
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Limited, S.L.P. 78495 Dar es Salaam.