Professional Documents
Culture Documents
tz
Sauti ya Waislamu
ISSN 0856 - 3861 Na. 1061 RABBIUL THAN 1434, IJUMAA MACHI 8 - 14, 2013 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=
Hakuna kitu kinachowaliza wenye akili zaidi kuliko wasiwasi wa kuokoka na Moto na kupata Pepo! Hijja peke yake ndiyo inayoweza kumsasha muislamu na madhambi yote, akarudi kama siku aliyozaliwa na mama yake, na akapata Pepo katika muda wa siku tano. Hivyo hakuna matumizi bora ya fedha kuliko kwenda Hijja. Wewe ndugu yetu ushakwenda mara ngapi?KaribuAhlu Sunna wal Jamaa. Gharama zote ni Dola 4,300 tu. Tafadhaliwasiliana nasi ifuatavyo: Tanzania Bara: 0717224437; 0777462022;Unguja: 0777458075;Pemba: 0776357117.
Hamad, amesema Zanzibar imepoteza fursa nyingi kwa kutokuwa mwanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kiislamu Duniani (OIC). Na Mwandishi Maalum, Maalim Seif Sharif Zbar KIKOSI Maalum cha kutuliza ghasia (FFU) kikiwa katika eneo la Markaz Chang'ombe Hamad, ambaye ni Makamo Jijini Dar es Salaam Oktoba 17, 2012. KATIBU Mkuu wa Chama wa Kwanza wa Rais wa c h a Wa n a n c h i , C U F Inaendelea Uk. 3 Maalim Seif Sharif
Mwenyekiti wa Jumuiya wa Jumuiya ya Al-Yousuf Sheikh Al-Youseif (kushoto) akiwa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, Osini kwake Migombani.
Waislamu kukutana kutawakal kwa Allah (s.w) Masheikh kujadili kulegalega mahusiano ya kidini
2
www.annuurpapers.co.tz
Tahariri/Tangazo
Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM. E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk Osi zetu zipo: Manzese Tip Top Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam
AN-NUUR
au wao kufanya watakavyo? Tusisahau kuwa hawa ndio wale waliosema kwa kujiamini na jeuri kuwa Iraq kuna silaha za maangamizi. Lakini baada ya walilokusudia kufanikiwa kwa maana kuwa baada ya kuvamia nchi ya watu na kuuwa mamilioni ya watu na kufanya uharibifu na ufusadi wa kutisha, wenyewe hao hao bila ya aibu wakasema kuwa waliongopa, Saddam hakuwa na silaha za maangamizi. Kama alivyosema Rais wetu Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete na kama alivyosema Waziri wa Mambo ya Ndani Mheshimiwa Emmanuel Nchimbi na pia baadhi ya makamanda wetu wa Polisi, inavyoonekana tunawaamini sana washirika wetu hawa. Lakini swali ni je, kama watatuambia Uamsho wana kiwanda cha silaha za maangamizi kama walivyodai kuwa zipo kule Iraq tutaamini maadhali wamesema wao? Tuna ubavu wa kupinga watakayosema kama tutakuwa na wasiwasi kuwa wanaongopa au sio sahihi? Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na Jumuiya ya Kimataifa kwa ujumla ilisema Iraq hakuna silaha za maangamizi na ikapinga nchi hiyo
kuvamiwa, lakini Marekani ikavamia ikafanya ufisadi iliokusudia kufanya. Je, na sisi tupo tayari kubeba gharama ya matokeo ya ukachero wao kama itakuja katika sura ileile ya madai ya silaha za maangamizi Iraq? Akizungumza katika mahojiano maalumu na baadhi ya vyombo vya habari wiki iliyopita, Kamishna wa Polisi Zanzibar, Musa Ali Musa alithibitisha kwamba jeshi lake limekuwa likishirikiana na FBI katika upelelezi huo na kwamba idadi ya waliokamatwa imeongezeka. Ni kweli tumekuwa tukishirikiana na FBI katika upelelezi ili kuhakikisha kuwa, wahusika wa tukio la kuuawa kwa Padri Mushi wanakamatwa. Hii itasaidia kupunguza vitendo vinavyohusishwa na matukio ya kigaidi yakiwamo mauaji,alisema Kamishna Musa. Labda tuulize, ujuzi gani na ufahamu gani wa kuwajua Wazanzibari na Watanzania waliokuja nao FBI kiasi cha kuwezesha kufika tu wanakamatwa watu? Au wamekuja na orodha yao na polisi wetu wanafanya kutumwa tukamatie yule na yule na yule? Yamewahi kufanyika mauwaji mengi sana nchini hapa, yakiwemo ya Kamanda wa Polisi Mwanza, lakini yote yalichukuliwa kama matukio ya kihalifu na vyombo vyetu vya usalama na sheria vikayashughulikia kwa umakini mkubwa. Kitu
gani kinawafanya polisi wetu wakimbilie kuleta msamiati wa ugaidi katika tukio hili? Je, huu ni wao wenyewe au wameletewa na washirika wao FBI? Sisi tunadhani kuwa kabla ya polisi wetu kukimbilia kuwa na imani na ujuzi na ufanyaji kazi wa FBI, wangefanya kwanza semina nao wawaombe wawafahamishe uzuri na kwa kituo kile kizungumkuti cha Anthrax Terror Attack kimeishia wapi? T u n a s e m a kizungumkuti kwa sababu awali wataalamu hao tuliowaagiza kutoka Washington na wenzao katika ukachero nchini mwao walisema kuwa kimeta kile kilitoka kwa Al Qaida waliotumwa na Saddam Hussein. Walimwengu wakaonyeshwa na bahasha zilizoandikwa Allahu Akbar ili kukazia kuwa waliohusika ni Waislamu, Al Qaida. Hata hivyo baadae wakawa wanaparurana
wenyewe kwa wenyewe baada ya taarifa kuvuja kuwa kimeta kile kilitokea katika maabara zao wenyewe, tena za kijeshi. Katika kitisho kile cha kimeta ilielezwa kuwa watu saba walikufa. Je, sisi tumejiandaa kulipa gharama kiasi gani (katika sura ya kuuliwa au kuteswa Watanzania wasio na hatia) kama mambo tutakayofanyiwa ni sawa na haya ya Anthrax Terror Attacks na yale ya silaha za maangamizi Iraq? Kwa hakika kwa mtu yeyote mwenye akili yake timamu na hasa akiwa na japo chembe ya uzalendo na mwenye kujali ubinadamu na utu wake, akitafakari juu ya ujio huu wa FBI, hatakosa kuona kuwa tumekwa na msiba. Kama tuliambiwa kuwa giza limetanda alipokufa Mwalimu Nyerere, zile zilikuwa nyimbo na ngonjera tu za kuomboleza msiba, sasa ndio giza limetanda kweli.
P.O. Box 55105, Tel: 2450069, 0712 974428 Fax: 2450822 D Salaam E-mail: ipcubungoislamic@gmail.com
Mlete mwanao apate Elimu bora itakayomwezesha kujiunga na Kidato cha Tano.
Kwa mawasiliano zaidi piga namba: 0714 888557/0659 204013 Wabillah Tawiq MKUU WA SHULE
Habari
AN-NUUR
manne, isipokuwa mshtakiwa namba moja (Sheikh Ponda) na mshtakiwa namba tano (Ust. Mukadam), ambao wanakabiliwa na mashtaka matano. Hakim Nongwa alisema pamoja na Mawakili wa upande wa utetezi kutoa maelezeo ya kina katika utetezi wao juu ya shauri hilo, Mahakama imeona ni vyema iwape nafasi washitakiwa waweze kupanda kizimbani kutoa utetezi wao. Mahakama inaona washtakiwa wote waliokamatwa katika kiwanja kile, ni vyema wapande kizimbani ili watoe utetezi wao, waseme sababu zilizofanya waingie pale. Alisema Hakimu Nongwa. Kwa mujibu wa Wakili wa upande wa utetezi Bw. Juma Nassoro, ameileza mahakama hiyo kuwa jumla ya mashahidi sitini wataka mahakani hapo kutoa ushahidi wao upande kwa upande wa utetezi.
Serika l i y a Z a n z i b a r, aliongeza kuwa iwapo Zanzibar ingepata fursa ya kuwa mwanachama wa OIC, ingekuwa mbali kiuchumi kwa vile Jumuiya hiyo imekuwa ikichangia sana maendeleo ya kiuchumi kwa nchi wanachama. Maalim Seif alieleza hayo katika viwanja vya Jamhuri Jimbo la Makunduchi, wakati akihutubia mkutano wa hadhara uliotishwa na Chama hicho hivi karibuni. Kielezea kusikitishwa kwake na kitendo cha Zanzibar kukoseshwa Uanachama wa Jumuiya hiyo, alisema kitendo cha Zanzibar kuzuiwa kujiunga na jumuia hiyo huenda ni mpango maalum ulioandaliwa wa kuipotezea Zanzibar umaarufu duniani. Zanzibar ndio dola kongwe zaidi katika ukanda huu wa Kusini mwa Afrika, lakini tumepoteza umaarufu wetu, alieleza kwa masikitiko. Alielezea kusikitishwa kwake na vitendo vya baadhi ya viongozi wa upande wa pili wa Muungano, kwa kutoithamini Zanzibar
na kuipotezea haki zake ambazo ingepaswa kuzipata. Maalim Seif alitoa mfano wa ujio wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman, ambaye alizuru nchini siku za hivi karibuni na alipowasili nchini Rais Mwai Kibaki wa Kenya. Alisema wageni wote hao hakuna aliyepelekwa Zanzibar na kuelezea kasoro hiyo kuwa ni miongoni kwa vitendo vinavyoinyima Zanzibar fursa. Pamoja na yote hayo, lakini Wawakilishi wa Zanzibar walitakiwa waende wakatoe maoni y a o m b e l e y a Wa z i r i huyo wa Oman, lakini kwa masikitiko makubwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania aliyapuuza maoni na mapendekezo ya Wazanzibari. Sijui inakuwaje Waziri wa upande mmoja anaweza kuiamulia nchi yenye Rais, alieleza na kuhoji. Maalim Seif alifahamisha kuwa mambo yote hayo yanatokana na Zanzibar kutokuwa na mamlaka kamili na kwamba, wakati umeka sasa kwa Wazanzibari kuungana
Inaendelea Uk. 4
Habari
AN-NUUR
WAISLAMU kutoka sehemu mbalimbali nchini, wanatarajiwa kufanya ibada maalum ya Itiqafu kesho, katika Msikiti wa Kichangani T.I.C Magomeni, Jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kutawakali kwa Mwenyezi Mungu na kuomba dua maalum kutokana na matatizo ya kiimani yanayoendelea nchini. Kwa mujibu wa taarifa
kutoka kwa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu (T), imeeleza kwamba Itiqafu hiyo itaanza msikitini hapo majira ya saa tatu, usiku wa Jumamosi (Kesho) kuamkia siku ya Jumapili. Itiqafu hii imeandaliwa na Jumuiya na Taasisi za Kiislamu itaanza majira ya saa tatu usiku wa Machi 9, mpaka Machi 10, Alfajiri. Viongozi na wajumbe kutoka mikoani watahudhuria Itiqafu hiyo. Imesema taarifa hiyo. Mmoja wa viongozi
wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu (T), aliyejitambulisha kwa jina moja la Abdallah, alisema itiqafu hiyo itatanguliwa na Semina na mkutano wa viongozi wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini utakaofanyika katika Hoteli ya Lamada Ilala Boma jijini. Semina hiyo itafanyika siku ya Jumamosi kesho Machi 9, 2013, kuanzia majira ya saa tatu asubuhi mpaka saa nane mchana. Taarifa hiyo ya Jumuia na
Taasisi za Kiislam nchini, ilieleza kuwa hivi sasa inafahamika kwamba nchi yetu inapita katika kipindi kigumu cha mahusiano ya kidini. Ta a r i f a i m e e l e z a kuwa kutokana na hali ilivyo, viongozi wa Dini ya Kiislam, wameona kuwa wana wajibu wa kukutana ili kuelimishana na kujadili hali hiyo, na hatimae kuishauri serikali na Watanzania namna bora ya kuimarisha mahusiano ya kidini.
Tayari Jukwaa la Waislam Tanzania (Tanzania Muslim Forum), limekamilisha maandilizi kwa ajili ya Semina na Mkutano wa Viongozi hao, lengo likiwa ni kuelimishana na kujadili hali ya kulegalega kwa mahusiano ya kidini nchini, na kutizama ni namna gani hali hiyo itaepukwa. Mkutano huo utahudhuriwa na Masheikh n a Vi o n g o z i k u t o k a Jumuiya mbalimbali za Kiislam kutoka jijini Dar es Salaam na mikoani.
WAZAZI wa Kiislamu wametakiwa kutoa kipaumbele kwa watoto wao kuihifadhi Quran, ili iweze kuwajenga katika maadili mema na kuwaepusha vitendo vibaya. Wito huo umetolewa na Ustadhi Mbwana Urari, wa Taasisi ya Afrika Muslim Agency, wakati akiongea mara baada ya mashindano ya kuhifadhi Quran kwa vijana wa Kiislamu, yaliyofanyika katika Msikiti wa Makukula Buguruni, Jijini Dar es salaam. Ustadhi Mbwana, alisema katika Ulimwengi wa sasa wazazi wanawahimiza kuwapeleka watoto wao katika Madrasa ambazo zinahifadhisha Quran, ili wasije kujiingiza katika mambo yasiyoendana na maadili mema. Alisema hivi sasa maadili na nidhamu katika jamii yamemomonyoka kwa kiasi kubwa, lakini njia pekee ya kujenga na kurudisha maadili hayo ni kuwafundisha watoto dini yao kupitia katika Madrasa zinazo hifadhisha Quran. Alieleza kuwa madhumuni makubwa ya kuandaa mashindano hayo, ni kuwafanya vijana wa Kiislamu kukijua kitabu chao kitukufu cha Quran kupitia njia ya kuzihifadhi aya za Quran katika vifua vyao. Alisema kuhifadhi kitabu cha Mwenyezi
Mungu kifuani katika umri mdogo, ndiyo njia ambayo ikitumiwa na wanazuoni wakubwa. Hii ni njia ambayo imefundishwa na Mtume (s a w), ikafuatwa na Maswahaba wa Mtume. Na sisi vilevile tunaiendeleza njia hiyo ili kuienzi na kuilinda Qur an, mbali na kuifanya jamii kuishi katika misingi ya maadili mema yenye nidhamu ya kumjiua Mwenyezi Mungu Alisema Ust. Mbwana. Aidha aliwasihi vijana wa Kiislamu wanapaswa kutambu kwamba, kuhifadhi na kuisoma Quran ni kwa manufaa yao hapa duniani na kesho akhera. Kutokana na sababu hiyo, aliwataka wanafunzi hao waelewa kwamba, wanapohimizwa kusoma, basi waichukue rai hiyo kwa kwa uzito kwani elimu pekee ndiyo itakayo wajengea maisha mazuri hapa duniani na kesho akhera. Akizungumzia hatua ya Taasisi ya Afrika Muslimu Agency kugawa vitabu bure kwa Waislamu, Ust. Mbwana alisema lengo ni kurahisisha kutoa mafundisho ya Kiislamu, ili jamii iweze kuujua Uislamu wao kwa urahisi. Tu n a g a w a v i t a b u vyenye mafunzo ya Uislamu bure, ikiwa ni katika muendelezo ule ule wa kutaka Waislamu wayajue mafunzo
mbalimbali ya dini yao bure bila ya gharama yoyote ile. Alisisitiza Ust. Mbwana. Katika kilele hicho cha mashindano ya Quran, Waislamu waliweza kupata vitabu mbalimbali vyenye mafundisho ya Uislamu kama vile Mwanamke katika Twahara, stara ya mwanamke (Hijabu), ambavyo viligaiwa na Taasisi hiyo. Mashindano hayo ni mfululizo wa kazi za kila siku za Kiislamu ambazo hufanywa na Taasisi ya Afrika Muslim Agency. Naye Ustadhi Shaaban Hijja wa Masjid Makukula, Buguruni Jijini Dar es salaam, katika hotuba yake ya swala ya Ijumaa Msikitini hapo, alisisitiza suala la Waislamu kuipigania dini yao kwa hali na mali. Alisema Mwenyezi Mungu alishafahamisha kuwa biashara ambayo itawaokoa watu na adhabu yenye kuumiza ni kumuamini Allah (s.w) na Mtume wake, kisha kupigania jihadi dini ya Mungu. Akifafanua zaidi, Ustadhi Hijja alisema jihadi ina mapana yake na kwamba, haina maana tu ya kuitetea dini kwa silaha, bali hata kuhifadhisha watoto Quran na kuwapa elimu kwa ujumla nayo ni jihadi.
jambo dogo, lakini katika Uislamu ni jambo kubwa na lina uzito wake.
ili kuweka mustakbali mwema wa nchi yao. Akielezea kuhusu demokrasia ya vyama vingi, Maalim Seif aliwataka wananchi kuwa huru kuitumia fursa hiyo kwani ni haki yao ya kikatiba.
Amesema kila mtu yuko huru kujiunga na chama chochote cha siasa na kuwa na imani ya dini anayoitaka bila ya kuingiliwa katika maamuzi hayo. Hatua hiyo imekuja baada ya aliyekua kaimu Katibu wa Vijana wa CCM Wilaya ya Kusini Bw. Muaze Haji, kujiengua katika chama hicho na kujiunga na CUF. Akizungumza katika mkutano huo Bw. Muaze alisema hakushawishiwa na mtu kujiunga na CUF bali ameamua baada ya kuona kuwa anachokipigania Maalim Seif kina maslahi kwa Wazanzibari wote. Kabla ya mkutano huo Maalim Seif alitembelea shamba la kisasa la kilimo cha migomba la Bw. Haji Kinazi, ambapo alieleza kuwa kilimo hicho kinaweza kuwakomboa wakulima kwa kuongeza uzalishaji na kukuza kipato chao. Alisema iwapo kilimo hicho kitaendelezwa, kitaweza kuwakomboa
hilo na mikoa mengine ya Zanzibar. Kwa upande wake mkulima wa kilimo hicho bw. Haji Kinazi, amesema tayari ameshaona mafanikio ya kilimo hicho na kwamba anakusudia kukiendeleza zaidi ili aweze kujikomboa kiuchumi. Alisema tatizo kubwa lililokuwa likimkabili ni uhaba wa maji, lakini hivi sasa wanaimarisha miundombinu ya maji na kuendeleza kilimo hicho kwa uhakika. Naye mtaalamu wa kilimo hicho Bw. Omar Mohd alisema, mazao yatokanayo na kilimo hicho cha kisasa ni mazuri na yanaweza kuleta tija kubwa
kwa wakulima. Amesema kupitia utaalamu huo, migomba inaweza kustahamil i maradhi na
ukame na kuwawezesha wakulima kupata mazao mengi yaliyo bora ambayo wanaweza kusarishwa nje ya nchi.
Habari za Kimataifa
AN-NUUR
binafsi. OIC imesema kuwa kufuatia pendekezo lililotolewa na Kuwait la kuasisi mfuko huo wa fedha, Jumuiya hiyo sasa inajiandaa kuunda timu ya ufuatiliaji, kwa ajili ya kuainisha fedha zinazohitajika kuanzisha mfuko huo. Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano cha Jumuiya hiyo, amesema kuwa mfuko huo ambao makao yake makuu yatakuwa nchini Kuwait, ni mfuko wa wakfu na kwamba utakuwa ukitetea na kuilinda dini ya Kiislamu na matukufu yake pamoja na shakhsia wa Kiislamu. (IRIB)
za kutenda jinai za kivita. Aidha Rais huyo amesema kuwa, amefanya mazungumzo na Amir wa Qatar juu ya masuala yanayohusu mahusiano ya pande mbili, na kimataifa. K u n d i l a wanamgambo wa al Shabab linalotuhumiwa kufungamana na mtandao wa al Qaeda, linadhibiti baadhi ya maeneo katikati na kusini mwa Somalia, na mara kadhaa limekuwa likipambana na vikosi vya serikali na vile vya kulinda amani vya Umoja wa Afrika AMISOM.
Makala
AN-NUUR
Na Mwandishi Maalum
K WA w a l e w e n g i waliokuwa washabiki wa sinema miaka ya 1960, sina shaka wanamkumbuka sana muigizaji mmoja wa Kiingereza anaejulikana kwa jina la kisanii kama James Bond, 007. James Bond ni kachero wa kufikirika katika hadithi na maandiko ya awali ya mwandishi Ian Flemming. Kachero huyu amechorwa kuwa ni ngao na nguzo ya ufumbuzi wa siri zenye utata mkubwa na kuhatarisha usalama wa nchi ikiwemo Uingereza. Kwa jinsi alivyo na uwezo mkubwa wa kuitambua kazi yake na kuifanya vilivyo, James Bond, hupambana na makundi ya watu wabaya wenye nia ya kuvuruga amani na usalama wa watu duniani. Kabla sijaporoja sana na kuacha njia niliyokususdia, naomba niwatambulishe kuwa makala hii inakuja kwa kumnasibisha muhusika James Bond, na hali ya hujuma na fitina iliyoelekezwa katika visiwa vya Zanzibar na wananchi wake, hasa mara tu baada ya muamko mkubwa wa wananchi kudai haki zao za kimsingi katika Muungano. Muda mfupi uliopita,
WANANACHI wa Zanzibar wakiwa katika moja ya mikutano yao ya hadhara iliyowahi kufanyika visiwani humo. [Picha kutoka Maktaba yetu] dalili kuwa zamu yetu ya kuhujumiwa imeka. Labda sasa, niwarudishe tena nyuma kidogo kwenye kichwa cha habari. Nilisema tunahitaji James Bond, na hili nisieleweke kwamba nimemsahau Mola, hapana, namtumia James Bond kisanii zaidi ili kutoa ujumbe wangu niliokusudia. Nje ya hapo nabaki na imani kamili kuwa ni Mungu pekee atakaetuokoa na hujuma hizi. Nafikiri kwa hili nimefahamika, kwa wale waumini . Muundo wa fitina na hujuma tuliyopangiwa Zanzibar unafanana na ile hujuma iliyopangwa na kikundi kimoja cha maharamia waliojificha katika Pango la Volcano (Crater) kule Japan, katika filamu ya James Bond ya mwaka 1967, inayoitwa You only live twice, ambapo muhusika mkuu James Bond (Sean Connery) anatumwa kufuatilia kadhia hio. Filamu inaanza kwa satalaiti moja ya Marekani iliyokwenda katika sayari ya Venus, kumezwa na satalaiti nyengine iliyokuwa na nembo ya Urusi (USSR). Tukio hili lilizua mtafaruku mkubwa ambapo Marekani walimshutumu Mrusi kwa hujuma hii. Mrusi alikataa kata kata kuhusika na hujuma hii lakini Marekani ilionya kuwa iwapo tukio kama lile litatokea tena, basi kutazuka vita kuu ya tatu ya dunia. Kadhia hii kwa vile ilikuwa ikipangwa na kikundi cha waasi waliojificha milimani kwenye pango la mlima wa volcano, watu waasi wasioitakia mema dunia, na watu wasio na hatia, lilikuwa jaribio la hujuma gumu kubainika. Kwa hali hii uwezekano wa kutokea vita ulikuwa mkubwa kwani chanzo cha tatizo kilikuwa hakijajulikana hasa. Kwa bahati nzuri, Serikali ya Uingereza ikamnasihi Mmarekani kuwa haioneshei kwamba Urusi walihusika na ikaahidi kufatilia. Kama kawaida, Uingereza ilimtuma James Bond (Sean Connery) kwenda Japan kufuatilia ukweli. Hali ilikwa ngumu lakini kwa ujasiri mkubwa Bond, aliweza kuibaini njama na tina iliyokuwa imepangwa kuwagombanisha Marekani na Urusi na kuipatia ufumbuzi sekunde chache kabla ya satalaiti ya pili kuliwa tena na satalaiti ya adui. James Bond akaoka dunia na maafa makubwa. Sasa kwanini tunamhitaji aje na huku? Naam, kwa muda mrefu sana kuna dalili nyingi na majaribio mengi ya kuiharibia jina Zanzibar kwa kupitia visingizo vya Uislamu wenye msimamo mkali. Kisa na sababu, Wazanzibar wamedai nchi yao. Hichi ndicho kilichowachongea. Tumeona kuanzia kutekwa kwa Ustadh Farid, Mungu akatuokoa na maafa. Akamwagiwa tindikali Soraga, Mungu akasimama nasi. Kapigwa Risasi Padre Mkenda, tukaponea chupu chupu. Haya ni moja ya majaribio machache tu yanayaonasibishwa na Uisilamu ili kuichafua Zanzibar na kuondoa amani iliyopo, inayofanywa na kikundi maalum chenye nia mbaya ya kuhujumu Uislamu na ustawi wa Z a n z i b a r. Tu m e o n a matukio ya maandamano na fujo za kutiwa moto makanisa, maskani, kuuliwa polisi Bububu, zote hizo ni tna na hujuma chini ya mwavuli mmoja ambao ni James Bond tu angeweza kuuchuwa kwa sasa, ukitoa Muumba. Kwa upande mwengine, likuepukalo lina heri nawe na likufikalo lina heri pia, wakati anauwawa padre Mushi, viongozi kadhaa wa Uamsho wako Rumande kwa miezi, na hata harakati zao zimekufa. Sasa kisingizio kitatolewa
Makala
AN-NUUR
la kwanza kuulizwa ni kama ninakunywa pombe au sinywi; wakiwa na maana kama nakunywa nijiunge na timu yao ya kunywa vodka! Na niliposema sinywi nikawa nimewavunja moyo kwa vile wamekosa mchezaji mpya. Na ndiyo maana wanafunzi wengi toka Urusi miaka ya nyuma walikuwa wakirudi nyumbani ni walevi wa kupindukia. Watanzania siyo walevi wa vodka kama vile wenzetu wa kule Urusi hii pia inachangiwa na hali ya hewa. Tanzania ni nchi ya joto kali, na vodka ni pombe ambayo ukiinywa lazima mwili unawaka moto, lakini pamoja na kwamba sisi siyo walevi wa vodka ila sisi tumeingia katika ulevi mwingine wa kushabikia mpira! Ushabiki wa mpira umekuwa kama ugonjwa wa kuambukiza ambao umesambaa kwa kila Mtanzania haijalishi anaishi mjini au kijijini; ushabiki wa mpira umekuwa ugonjwa ambao umesambaa mpaka kwenye damu zetu (football maniac). Kila kona ukipita ni matangazo ya kuonyesha mechi za mpira wa ligi za Ulaya, na serikali imetutengenezea kitu kinachoitwa digitali hivyo watu wote wamesahau kila kitu isipokuwa mpira wa ligi
ya Ulaya ndiyo taswira ya taifa sasa hivi. Watu wa rika tofauti wote kwa pamoja kra zao zote zipo kwenye ligi ya Ulaya. Afadhali hata basi tungelikuwa tunashabikia ligi ya kwetu hapa nyumbani ili tuweze kukuza kiwango cha mpira cha nchi yetu kwa kuchangia na kununua bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na vilabu vyetu hapa nyumbani! Lakini cha kushangaza sisi tunashabikia vipaji vya nchi zingine na watu wengine wamediriki hata kutoa michango yao kwa vilabu vya huko Ulaya wakati timu zetu hapa zinadoda! Kama ambavyo nimesema kwamba tatizo hili la ushabiki wa mpira kwa vilabu vya Ulaya si kwa watu wazima tu basi, hapana, hata watoto wadogo wamepumbazwa sana na ligi ya Ulaya; na kwa kuthibitisha maneno yangu haya nadhani mnakumbuka hata kwenye matokeo ya mtihani ya kidato cha nne wanafunzi wengi wamechora picha za wachezaji wa mpira wa ligi ya Ulaya kama vile Messi na mengineyo! Warusi wao walikuwa wajanja pamoja na kwamba waliwaruhusu watu wote wanywe vodka ili waweze kufanya walivyotaka, lakini walikuwa makini
sana kutokuwaruhusu watu wote wenye akili na vipaji mbali mbali kunywa vodka, walikuwa hawaruhusiwi kabisa labda kama ni kwenye sherehe tu basi na pia siyo kwa kiwango cha kulewa. Walioruhusiwa kunywa
mpaka kujikojolea ni wale watu wa kawaida wasiokuwa na umuhimu sana katika kukiri juu ya hali ya uchumi na maendeleo ya nchi kwa ujumla. Sasa sijui sisi serikali yetu inakiria nini kuhusu ushabiki huu wa mpira wa ligi ya Ulaya ambao sasa umegeuka kuwa siyo starehe tu, bali pia umekuwa ni sehemu ya maisha ya Watanzania na sehemu ya elimu muhimu kwa vijana wetu wanaosoma shule za msingi na sekondari! Watoto wengi wanashinda kwenye vibanda vinavyoonyesha ligi za mpira wa Ulaya hata wakati mwingine wa masomo, na jioni badala ya kujisomea pia wapo mbele ya runinga wanaangalia mpira! Najua serikali inakusudia nini kuhusu hili, lakini imekusudia vibaya kwa vile hata kama imeamua kutudhibiti sisi wazazi ambao ni watetezi wa taifa la leo, lakini ni kwanini isione kwamba si haki kukidhibiti pia kizazi cha kesho! Warusi nao pia walikuwa wakomunist lakini siyo kila mtu aliruhusiwa kunywa vodka, hapana. Sasa sisi mbona wote tumefunguliwa TV tuangalie ligi ya mpira ya Ulaya wakati twiga na dhahabu vinayoyomaa!!!??? Ndiyo maana nasema usipokunywa vodka utaishia kushabikia mpira.
TANGAZO
VITABU VIPYA VYA MIHADHARA, MASWALI NA MAJIBU BAINA YA WAHADHIRI WA KIISLAMU NA WACHUNGAJI, PAMOJA NA MAWAIDHA YA SHEIKH NURDIN KISHKI. VINAPATIKANA MSIKITI WA MTORO (DUKANI KWA SAIMU) KARIAKOO. PIA VINAPATIKA KATIKA MADUKA YOTE YA VITABU VYA DINI JIJINI DAR ES SALAAM, KWA JUMLA NA REJAREJA. PATA NAKALA YAKO SASA. 0713 47 10 90, 0685 47 10 90, 0773 19 46 6.
TANGAZO
AN-NUUR
Makala
AN-NUUR
MUHESHIMIWA Rais Mstaafu, Al Haj Mzee Ali Hassan Mwinyi, amependekeza Masheikh na Maaskofu wakutane wazungumze kuhusu kule kusuguwana kulikojitokeza hivi karbuni. Hakika ndugu Wakristo wamezua makubwa hivi karibuni na lawama zimelengwa kwa Waislam. Mkristo alikojolea Qurani, Waislam walitoa taarifa Polisi kwa kuwa kitendo hicho ni jinai kwa sheria za nchi. Lakini huko Polisi, kwa sababu wanazozifahamu wenyewe, ambazo si kazi kubwa kutanabahi ni zipi, wao walijichelewesha kuchukua hatua za kisheria zinazotakikana. Kwa ujinga wao Waislam wakapoteza subra na kuchukua sheria mikononi mwao na matokeo yake yakawa vurugu tupu, Waislam wakilaumiwa kwa mkasa huo. Kiongozi wa Polisi angetegemewa kusema ukweli wa mambo yalivyokuwa, lakini yeye alitangaza tu, kuwa amechoka na wafanya fujo. Hakuwataja hao wafanya fujo ni kina nani lakini mtu yeyote yule mwenye akili ya kukiri, haingekuwa kazi kubwa kutambua kuwa hao ni Waislam. Imekuwa ni ajabu kubwa sana humu nchini kuzuka rabsha kati ya Waislam na Wakristo kwa sababu ya kuchinja wanyama, ambao nyama zao zinauzwa katika mabucha. Mimi sasa ni mzee na maisha yangu yote nimeyamalizia nchini humu; haikutokea hata siku moja Wakristo wazue ugomvi kwa sababu ya kuchinja. Rafiki yangu Mchaga kanieleza kuwa huko kwao kila siku wamependelea Muislam awachinjie ngombe ama mbuzi wa chakula. Kwa mila zao, wao hawawezi kula
Na Khalid S Mtwangi
nyama iliyochinjwa na mwanamume ambaye hakutahiriwa. Kwa hiyo hata kwa Mchaga mwenzao mwanamume, hawawezi kuwa na uhakika kabisa kuwa huyo bwana katahiriwa. Kwa zaidi ya asilimia tisini na tisa mwanamume mtu mzima Muislam atakuwa katahiriwa. Hivyo wako tayari kula nyama iliyochinjwa na Muislam kwa sababu wana uhakika kuwa imechinjwa kihalali na mtu mwenye tohara. Inatambulika kuwa waliozua balaa la kuchinja ni baadhi ya wafuasi wa madh-hebi hizi za Pentecost wanaofadhiliwa sana na Born Again wa Marekani. Watu hawa ndio mwanzo wa mauwaji makubwa yaliyokuwa yakitekelezwa na viongozi kama vile Bw. George H Bush, aliyekuwa Rais wa Marekani, aliyeapa kueneza Vita Vya Msalaba. Pia itambulike kuwa hawa Born Again (hakika wanaitwa FUNDAMETALISTS) hawataki kabisa kusikia kuwa kuna Uislam n a U k ato li k i d u n i an i kiasi kwamba, Papa wanamtuhumu kuwa anaeneza ushirikina (wanamwita purveyor of superstition). Tazama website za kina Pat Robertson ama marehemu Jerry Falwell. Haya waliyozuwa hawa wanaotaka wawe wanachinja, wamezua sokomoko huko Geita mpaka yakatokea maafa kwa Mchungaji kauawa. Halafu yametokea mauaji ya Fr. Evarist Mushi, huko Zanzibar. Inasikitisha sana kuwa bila kuwepo ushahidi wowote, lawama za mauwaji hayo wametwikwa Waislam kama waumini wa Uislam. Maana yake sio kama aliyetenda kitendo hicho ni muhalifu ambaye ana jina la Kiislam, la. Inaelekea kuwa aliyeuwa ni Muislam na aliyefanya uhalifu huo ameutekeleza kwa sababu ya Uislam wake. Shutuma hizo hazikutoka kwa Wakristo tu bali baadhi ya Masheikh nao walijitosa kwa hoja na aya za Qurani kumlaani huyo Muislam ambaye mpaka sasa hajajulikana. Maaskofu na Wakristo wote kwa ujumla wamefarijika sana! Masheikh wamewafariji
Wakristo na kuwahuzunisha wafuasi wao Waislam. Kufuatana na matokeo haya machache yaliyoorodheshwa, ni rahisi kufikia maamuzi kuwa kweli kumetokea msuguwano kati ya Wakristo na Waislam. Hali kama hiyo hakika inaweza kuwa hatari sana kwa nchi hii. Isipokuwa ikumbukwe kuwa WaTanzania, na hasa WaTanzania Waislam ni wastahmilivu sana na kwa kawaida huheshimu sana sheria na viongozi. Mafunzo yao ya MADRASA yanawafanya wawe na heshima kwa walio viongozi wenye madaraka. Hii ni kweli kabisa ingawa kunaweza kutokea wasomaji wasikubaliane na hoja hiyo. Waislam wamekuwa wakiitwa kuwa ni docile (wanyonge sana). Kweli hali hiyo imeanza kubadilika lakini hayo ni kwa sababu kila kitu kina mwisho wake. Wanaelewa kuwa huko nyuma wametumiwa sana kwa maslahi binafsi na kusimika Ukristo. Wanamkumbuka kwa dhati Al Marhum Sheikh Mzee Takdir, mpiganaji shupavu wa uhuru. Mabadiliko hayo kwanza yamedhihirika katika mihadhara waliyokuwa wakiihubiria katika miaka ya tisini. Hii iliwaudhi sana Wakristo na ajabu ni kwamba, wale wasomi ndio waliokuwa wakiudhika zaidi, kuliko Wakristo wa kawaida ambao walipendelea sana kuendesha mijadala kwa hoja, wakishindana na hawa wahadhiri wa Kiislam. Lakini kukasirika kule
ilidhihirisha kiasi Waislam walivyokuwa wakionewa kila siku kuwa wao ni docile. Lakini ikumbukwe huko nyuma kulikuwa na mihadhara mingi ya wahubiri Wakristo wengi walikuja nchini humu na waliyokuwa wakiita kwa mfano September crusade na kadhalika. Mihadhara hii ya Wakristo nayo wahadhiri wake walikuwa wakijaribu kuuchambua Uislam wakipotosha mafundisho ya dini hiyo ya kweli ya Allah. Waislam hawakulalamika kusema kuwa Uislam ulikuwa ukikashfiwa. Bado hata hivyo wale waliosoma maandishi kama vile kitabu WANA WA IBRAHIM walifahamu kiasi gani si tu, Uislam ulikuwa ukikashwa bali hata Rasulul-Llah Muhammad (SAW) alikuwa akidharauliwa. Na kwa hakika Wakristo wengi hawamkubali wala kumuamini Muhammad (sw). Imeandikwa kuwa Uislam hauwezi kuwa ni dini ya kweli kwa sababu Warabu, akiwemo Mtume Mhammad (SAW) walitokana na kizazi cha Ismail (AS), na huyu Ismail alizaliwa na mtumwa na wala huyo Ismail (AS) hakubarikiwa. Kwa hiyo wanasema Uislam hauwezi kuwa ni dini ya kweli. Soma kitabu hicho WANA WA IBRAHIM ama DINI MBALI MBALI NA UTUME WETU. Vyote hivi vimeandikwa na Kanisa Katoliki. Yote haya yakitoka, Waislam hawakulalamika KASHFA hata siku moja.
Wakristo walipolalamika tu, eti dini yao inakashiwa Serikali nzima ilikuja juu. Sasa hivi kweli Ukristo umesimama kwenye msingi dhaifu ambao hauwezi kabisa kustahimili upekuzi wenye mantiki? Cardinal Manning wa Westminster aliwahi kunukuliwa akisema kuwa Dogma supersedes history (yaani amri inaweza kuwa bora na juu ya matukio ya historia). Huyu Cardinal Manning sio kiongozi wa kawaida tu, yeye alikuwa msaidizi wa karibu sana wa Papa Paul VI, aliyetoa mafundisho kuwa Papa hakosei (Infallibility of the Pope) anapokuwa katika kiti cha enzi. Kweli kutokana na haya yote, uko ule mkwaruzano k a t i y a Wa k r i s t o n a Waislam nchini humu. Hata wale maadui wa kivita vya kuuana, hasa kuna siku lazima wakae chini kuzungumzia uhasama wao. Wamarekani wanazungumza na Taliban. Kuna shida moja lakini ambayo ni lazima ikubalike na upande wa Wakristo. Waislam wana historia ya kuvumiliana sana na wenzao Wakristo; historia ya nchi hii ni wazi kabisa kwa hilo. Ubaya ni kuwa hawa ndugu Wakristo, hasa wale walio na madaraka, makubwa na madogo, hawakubali kabisa kuwa Waislam wanadhulumiwa baadhi ya haki zao. Ushahidi umetolewa kwa mfano, maandiko ya Dr. Sivalon katika kitabu chake KANISA KATOLIKLI NA SIASA YA TANZANIA Inandelea Uk. 12
10
Makala
AN-NUUR
kupigania ukombozi na uhuru wa nchi yao. Pamoja na upinzani huu mkali unaoonyeshwa n a Wa p a l e s t i n a dhidi ya Israel, wao hawazungumzii kuanzishwa kwa Intifada ya tatu. Hata hivyo upinzani wa Wapalestina ni dhidi ya uvamizi wa ardhi yao na Israel pamoja na udhalilishwaji na ukandamizwaji unaofanywa na Israel. Kila Israel inavyozidisha ukandamizaji huo, ndivyo na Wapalestina nao wanavyoongeza upinzani wao dhidi ya wavamizi. Ni kweli upinzani huu wa Wapalestina wanaodai haki yao ya kitaifa, unaweza ukachukua taswira tofauti. Lakini kilicho dhahiri ni k u w a Wa p a l e s t i n a hawatatumia nguvu. Rais Mahmoud Abbas, anasisitiza upinzani bila ya kutumia nguvu, akisema yeye hayuko tayari kuburuzwa katika umwagaji wa damu, jambo ambacho Israel wanataka lifanyike. Kwa upande wa pili, watawala wa Israeli
na vyombo vyao vya habari wanawachochea Wapalestina waelekee kwenye Intifada mpya. Wanaelewa kuwa wao ndio wenye nguvu na silaha za kisasa zinazoweza kuwaua Wapalestina kwa urahisi. Kwa kuwachochea Wapalestina waingie uwanjani, Israel watakuwa na kisingizio cha kutumia silaha zao za maangamizi, pamoja na kufanya majaribio ya silaha zao mpya, kama walivyofanya huko Lebanon na Gaza. Wapalestina wanaotumia nguvu watasingiziwa kuwa ni magaidi na Waisraeli watapata kisingizio cha kuwashambulia kwa madai ya kile wanachopenda kukiita ulinzi wa Israel. Wakati huohuo, Israel inaendesha propaganda zao kwa kudai kuwa hawawezi kufanya mazungumzo ya amani na Wapalestina. Kwa maneno mengine, harakati za ukombozi wa Palestina zitatoa mwanya kwa Israel kuzidisha ukandamizaji wake dhidi ya wananchi wa Palestina,
huku wakidai kuwa Israel imezungukwa na maadui wanaotishia usalama wake. Watazungumzia kile wanachokiita mihimili ya uovu inayoundwa na Iran, Syria, Hezbollah na Hamas. Wa n a c h o h i t a j i Wapalestina kwa kweli si Intifada nyingine dhidi ya udhalimu wa Israel, bali ni ukombozi na Uhuru wa ardhi yao iliyovamiwa na Israel. Kwa bahati mbaya lengo hili haliwezi likakiwa kwa kutupa mawe mbele ya majeshi ya Israel yenye silaha nzito na za mauaji. Intifada mpya ya Wapalestina ni pamoja na maandamano yanayofanyika kila siku na kila wiki, dhidi ya Israel katika maeneo kama Bilin, Nilin na Maasara,Hebron, Kafr Qaddoum na Jenin. Migomo ya njaa inayoendeshwa na mashujaa wa Kipalestina walio katika magereza ya Israel. Jitihada hizi hazitazaa matunda ya haraka ya kuikomboa Palestina. Kitakachofanyika ni
11
Makala
AN-NUUR
wowote kumwambia baba, ilimradi mke mwenza aonekane mbaya na hata kuachika. Tabia hiyo inajengeka kwa mtoto kidogo kidogo. Kuwa muongo na kuharibu mahusiano ya familia linakuwa jambo la kawaida kwake hadi ukubwani. Madhara mengine anayoweza kuyapata mtoto ni kule kuhisi kuwa baba anampendelae mama mwingine. Japokuwa kweli baba anaweza kuwa na udhaifu wa kibinadamu, basi mke asiwe tena kichocheo. Badala ya kukaa na mzazi mwenzake kuzungumzia upungufu huo na kujadili namna ya kuuondoa kwa siri na kuyamaliza, ndio kwanza anauchochea maafa katika Inaendelea Uk. 12
mapenzi na huruma kati ya Waislamu, kwamba Muislamu anapompenda Muislamu mwenzie basi amwambie kuwa ninakupenda kwa ajili ya Mungu. Alikuja mtu mmoja kwa Mtume
Dk. Emad Rabie Ahmad Mohamed Shukurani zote ni za Mwenyezi Mungu na Rehema na Amani zimkie yule aliyeletwa kuwa ni Rehema kwa viumbe wote, Bwana wetu Muhamad na Jamaa zake na sahaba zake wote. Ama baada ya utangulizi huu, kwa hakika huruma na mapenzi ni alama za Uislamu. Kwa hakika umekuja Uislamu ili kupandikiza kanuni za udugu na kusaidiana watu na ili waeneze huruma na mapenzi kwa viumbe vyote. Ametuonyesha Allah (sw) katika Surat Al Imrami, juu ya neema hii inayojulisha utukufu wa jambo hili la kueneza udugu na huruma, mapenzi na kusogeleana na kuwa karibu badala ya kukimbiana na kunyanya paana na kuchukiana. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu, Na shikamaneni katika kamba ya Mwenyezi Mungu nyote na wala msifarikiane, na zikumbukeni neema za
Awe anawapenda Mwenyezi Mungu na Mtume wake k u lik o v itu v in g in e n a ampende mtu isipokuwa kwa ajili ya mwenyezi Mungu hadi mwisho wa hadithi hii tukufu. Kama isipokuwa muumini na awachukue waharibifu na mafisadi na waovu na yote hayo ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Na katika hadithi yenye maana hii, yeyote Mwenye kupenda kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na akachukia kwa
(S.A.W), anasema ewe Mtume (Mimi ninampenda Fulani, Mtume akasemsa nenda ukamwambaie juu ya mapenzi na huruma hiyo iwe ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu Mtukufu. Kwa sahihi ya maneno ya Mtume (S.A.W), amesema mambo matatu atakayekuwa nayo, basi amepata utamu wa imani.
ajili ya Mwenyezi Mungu na akatoa mali kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na akazuia mali kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, kwa hakika amekamilika imani.
12
Kifungo si suluhisho!
Mtimani nina ghamu, kwa kifungo cha Imani, Kunena yanilazimu, kwa uchungu ikhiwani, Kwa idhaatu adhimu, leo kuwa kifungoni, Kuifungia Imani, katu sio suluhisho. Suluhisho muadhamu, la mazonge ya nchini, Ni haki kustakimu, sawa kwa kila insani, Si kwa Imani kudumu, miezi sita kifungoni, Kuifungia Imani, katu sio suluhisho. Haki ni jambo adimu, kwa baadhi ya insani, Si leo tangu kadimu, kwa hapa petu nchini, Tangu enzi za Mwalimu, si za juzi za Imani, Kuifungia imani, katu sio suluhisho. Haki chungu kwa dhalimu, si leo tangu zamani, I tamu kwa madhulumu, bila kujali Imani, Dhuluma ndiyo jarimu, na si Redio Imani, Kuifungia Imani, katu sio suluhisho. Haki daima dawamu, huwa ni yenye kuwini, Tangu enzi za Adamu, baba wa wote insani, Haki ni yenye kukumu, hata pasipo Imani, Kuifungia Imani, katu sio suluhisho. Kalamu ya madhulumu, i karibu ukingoni, Vyovyote itavyokumu, dhuluma haitawini, Tatizo ni udhalimu, na si Redio Imani, Kuifungia Imani, katu sio suluhisho. Allah alimu-hakimu, kwa Kifungo cha Imani, Wamjua muhujumu, wa Redio yetu Imani, Twakwomba umuhukumu, akhera na duniani, Haki ndiyo suluhisho, si kuifunga Imani. ABUU NYAMKOMOGI MWANZA.
Mashairi/Barua
AN-NUUR
Inatoka Uk. 10
BARA 1953 HADI 1985. Haielekei kama kuna viongozi wa Serikali, wanasiasa na watendaji (civil servants) kama
kwa serikali na sio kwa Wakristo ama Makanisa. Wakati wa kadhia ya MwembeChai hakuna hata kanisa moja kati ya yale yaliyo karibu na
wamesoma klijitabu hiki. Halafu aliyeandika kitabu DEVELOPMENT AND FRELIGION IN TANZANIA, kilichoandikwa na Jan P van Bergen, ambaye katoa siri zinazohusu mawazo ya Hayati Mwalimu Nyerere kuhusu Uislam na Waislam, kuwa yeye ni Mkatoliki na ni Rais wa nchi hii mwenye madaraka makubwa sana. Afisa wa Elimu wa Munispaa ya Morogoro anapowaandikia walimu wa shule za msingi kuwa anataka majina ya wanafunzi wa Kikatoliki waliomo darasa la saba, maana yake nini. Hata pale wadau wengine walipolalamikia kitendo hicho kwa maandishi, si Wizara ya Elimu wala Osi ya Waziri Mkuu walioona kwamba hawa waliolalamika wanastahili kupewa heshima ya kupelekewa majibu. Iko mifano mingi ya dharau ya namna hiyo dhidi ya Waislam kutoka Serikalini. Huko nyuma ghadhabu za Waislam kutokana na dharau na dhuluma kama hizo zilikuwa zikielekezwa
Inatoka Uk. 11 familia kwa kuwaeleza wanawe udhaifu huo. Kitendo cha mama kumwambia mwanawe udhaifu huo, fahamu ka kuwa mtoto atapunguza mpenzi kwa baba yake na kwa mama yake mkubwa au mdogo na kwa ndugu zake wanaotokana na mama mwingine na hatimaye kwa familia nzima kwa ujumla. Hata atakapokuwa mtu mzima, hatamjali baba yake wala mama mdogo au mkubwa na wanawe pia, jambo ambalo ni kosa kubwa kwa mtoto kutowatendea wema wazazi wake. Jamii itabakia kumlaumu kuwa hajali mzazi au wazazi wake, kumbe wazazi w enyewe
katika CIVIL SERVICE ni waumini wa Kanisa Katoliki. Hivi Kanisa hilo halifundishi kutoa haki kwa wote bila upendeleo? Hivi wale waliomo katika CATHOLIC OLD BOYS ASSOCIATION (COBA) hawaipendi nchi ya Tanzania kuweza kulegeza kamba angalau kidogo kwa usalama wa Tanzania? Mwisho ikubalike kuwa Waislam hawaukashifu Ukristo. Hili lilipelekwa mpaka Mahakama ya Rufaa na Mahakimu wakahukumu kuwa Waislam wanapohubiri kufuatana na mafundisho ya dini yao, hiyo sio kashfa kwa Ukristo wala Wakristo. Kwanini ukweli huu haukubaliwi?
Amani iko mikononi mwa hawa watendaji wa serekali walio Wakristo; ni wao waache dhulma, dharau na kibri, na watende haki kwa wote. Waislam hawataki upendeleo wowote wanataka haki yao tu. Kumbuka Askofu Mkuu mstaafu Elinaza Sandoro, mara nyingi alikuwa akisema kuwa panapokuwa hakuna haki, hapawezi kuwa na amani. Ni yeye tu aliye kiongozi wa Kikristo anayeyaona hayo? Hakuna wengine wa madh-hebi zingine kama vile Katoliki wanatambua hayo? Kutokana na maelezo ya Muhasham Polycarp Cardinal Pengo, idadi kubwa zaidi ya waliomo
ya tofauti za uzao wa wazazi wa kike. Mtoto akifunzwa tabia njema bila kujenga hisia za utofauti ndani ya familia ya uke wenza, akawa na heshima na kuwatii wazazi wake hata kama sio wa kumzaa, akawaheshimu na kuwatii wake za baba yake, nao wake wenza wakaona kuwa watoto wao wote ni wa familia moja, ya baba mmoja, watafaulu na kuwa familia ya mfano bora wa kuigwa katika jamii. Amesema Mtume (s.a.w), wakirimuni watoto wenu na muwafunze tabia njema. Ni vyema tukaishi na familia zetu kwa furaha, upendo, kuaminiana na masikilizano ili kuleta picha halisi ya maisha mazuri ya Kiislamu. Tuishi na familia zetu huku tukifahamu kuwa kila mmoja wetu ni mchunga na kila
VIWANJA VILIVYOPIMWA KONGOWE KIBAHA TOWNSHIP REGISTERED PLAN No. 70995 BLOCK H
PLOT HATUA ENEO MRABA GHARAMA TSH
H1 H2 H3 H4 H5 H6 H7 H8 H9 H10 H11
50 x 29 32 x 32 50 x 30 37 x 30 50 X 45 33 x 37 60 x 45 50 x 40 67 x 50 70 x 45 90 x 50
1341 Sqm 1136 Sqm 1470 Sqm 1115 Sqm 2259 Sqm 1566 Sqm 2423 Sqm 1984 Sqm 3564 Sqm 2842 Sqm 3780 Sqm
4,023,000/= 3408000/= 4410000/= 3345000/= 6750000/= 4695000/= 7269000/= 5952000/= 10692000/= 8526000/= 11340000/=
Vipo Barabara ya Kongowe-Soga Kilomita moja toka barabara ya Morogoro. Simu No.0755 090 754/0715 090 754.
13
MAKALA
AN-NUUR
Na Suleiman Ramadhani
Naam haki hupewi ila huchukuliwa rights are never given are taken, ni maneno yasiyosahaulika ya mpigania haki za waamerika weusi na Uislamu kwa ujumla Malcom X. Huo ndio ukweli ulio wazi kwa wapigania haki wote duniani. Imepita sasa miaka kumi na tano toka yalipotokea mauaji ya Mwembechai, hakuna anayejali dhulma iliyofanyika ya kukatisha maisha ya Waislamu w ann e kw a maku s ud i na kuwaachia vilema wengine. Hili litabaki historia ya maandishi na huzuni kwa kizazi cha leo na kesho. Kila unapoibana haki na yenyewe hujidhihirisha na hatimaye huonekana pia mwisho wa siku hushinda. Serikali ya awamu ya tatu iliwadhibiti na kuwakandamiza Waislamu. Viongozi wa Kanisa Katoliki waliichochea na kuishinikiza serikali ya Mkapa idhibiti m i h a d h a r a y a Wa i s l a m u iliyokuwa kero yao kwa kipindi chote cha Rais Mwinyi. Kama wafanyavyo sasa hivi. Mwaka mmoja kabla ya mauaji ya Mwembechai, Askofu Elinaza Sendoro, alikaririwa na gazeti la Mtanzania, 21 Februari, 1997 akisema Mihadhara ya dini itazua vita. Pia gazeti la Majira, 10 Aprili, 1997 lilimkariri Askofu Basil Sambano, akilalamikia mihadhara ya kidini na katika tahariri yake ya tarehe 2 April, 1997 Majira liliandika Ushauri wa Askofu Pengo kuhusu mihadhara uzingatiwe. Kauli hiyo aliyoizungumzia mhariri ilitolewa na kufanyiwa kazi mwaka mmoja baadaye katika mauaji ya Mwembechai, kauli hiyo ilisema: Hakuna sababu ya kuhoa kuudhi mtu au kikundi fulani cha watu. Tunasema katika hilo ni vizuri kutumia mbinu za kumwua nyani. Kauli hiyo imebeba msemo wa Kiswahili usemao Ukitaka kumuua nyani usimtazame usoni. Kauli hii ilikuwa ikiiagiza serikali kuwashughulikia Waislamu bila kuwaangalia wao wana hadhi gani katika jamii, au wana haki gani katika jamii. Wa i s l a m u w a l i k u w a wakiendesha mhadhara wa dini kwenye uwanja uliopo msikitini Mwembechai, Dar es Salaam kwa siku kadhaa bila tatizo lolote mwanzoni mwa mwezi Februari, 1998. Mhadhara huo ulihudhuriwa na watu wa dini mbalimbali. Hapakuwa na tukio lolote lile la uvunjifu wa amani, badala yake yalisikika malalamiko ya Padri wa Parokia ya Mburahati, Padri Camillius Lwambano, tena kwa
Inaendelea Uk. 14
14
Makala
AN-NUUR
Inatoka Uk. 13
nne. Walifanya vizuri katika maarifa ya Uislamu na masomo mengine pia. Matokeo hayo ya Zahaki na wenzake yaliwapa moyo wanafunzi wengine wa Kiislamu kujisajili kwa ajili ya somo hilo. Matokeo yao ya mtihani wa mwaka 1990 kidato cha sita, kiasi fulani yalimshitua kila mmoja. Walifaulu vizuri masomo yote lakini somo la Islamic Knowledge walifeli. Mfano Zahaki alifaulu vizuri masomo ya Fizikia, Kemia na Baiyolojia. Wote waliofanya maarifa ya Uislamu katika shule yao mwaka huo walifeli somo hilo. Wanafunzi wa Kiislamu wengi walichukia somo la maarifa ya Kiislamu na kujiondoa katika usajili wa kulifanyia mtihani. Zahaki alikatishwa tamaa na kushangazwa juu ya kufeli kwake somo hilo. Walipofuatilia Baraza la Mitihani Dar es Salaam akiwa na wenzake Ayubu Masenza, Ali Kalisi kujua tatizo, wakaambiwa walifanya mtihani mmoja tu kati ya mitatu ya somo hilo waliyotakiwa kufanya. Zahaki anasema walifanya yote mitatu na si mmoja kama walivyoelezwa lakini vitabu vya kujibia vya mitihani miwili havikuonekana. Haya pia yalithibitishwa na msimamizi wa usahihishaji wa somo hilo kwa mwaka ule Bwana Burhani Mtengwa, kuwa walipewa na kusahihisha vitabu vya majibu ya mtihani mmoja tu (we received and marked only one paper) kutoka shule ya wavulana Tabora. Uchunguzi wa wanafunzi ulionesha kuwa hujuma hii ilifanywa na Mkuu wa shule yao wa wakati huo Bwana Alexander Ndeki, ambaye alikuja kuwa Kamishina wa Elimu, na lengo ilikuwa kuwakatisha tamaa wanafunzi wasisome somo hilo. Anakumbuka Mkuu yule wa shule alitumia kipindi kimoja cha Baraza la Shule la Wanafunzi, kutilia msisitizo umuhimu wa kutotumia majina ambayo hayaelezei wewe ni dini gani. Alisema majina kama Kitanga Wanja au Maziku Masanja yalikuwa yakiwachanganya. Hakikisha una jina linalokutambulisha wazi wewe ni dini gani ili tuweze kukusaidia haraka unapokuwa na shida. Anasema Zahaki wakati ule hakulipa umuhimu jambo lile hadi 1998, alipojua jina lake lilivyomgharimu kwa utambulisho wake wa kidini. Na ilikuwa 1998, bila kutarajia, kufeli kwake kwa Islamic Knowledge kukamrudi katika osi ya Kamanda wa Polisi wa mkoa Alfred Gewe. Akizidi kusimulia mkasa huo anasema; Nilipojiunga na jeshi la Polisi 1992 haikunichukua muda mrefu kugundua kuwa katika mtazamo wa askari wenzangu Wakristo, waliunganisha moja kwa moja kati ya uhalifu na dini linapokuja suala linalomhusu Muislamu. Mkristo akifanya uhalifu, hata liwe kosa kubwa vipi, hatahusishwa na yeyote isipokuwa yeye mwenyewe. Wakati Muislamu akifanya uhalifu hata kama ni dogo kiasi gani itahusishwa na jamii
nzima ya Kiislamu. Askari Wakristo watakuja kwangu na kulalamika,Ustaadh, unaona watu wako wanavyofanya waliniita Ustaadh kwa kuwa nilikuwa nachunga sala na nilijitahidi kuishi Kiislamu. Ni mauaji yaliyofanywa na Polisi Msikiti wa Mwembechai, ndiyo yaliyogeuza maisha yangu. Siku ile nilikuwa zamu ya mchana na kujikuta katika wakati mgumu, nilikuwa nikipokea mawasiliano yote osini juu ya kinachoendelea Mwembechai. Kamanda wa operesheni alikuwa Bwana Kombe. Nilichokisikia kwa maosa wa Polisi Wakristo Mwembe chai kilinitisha, walisema kwa uwazi Hawa Waislamu wamezidi sana, lazima leo tukawakomeshe. Ndiyo bwana! wanatukera sana sisi Wakristo, leo watatukoma. Kila taarifa ya kifo cha Muislamu kilipokelewa kwa shangwe na furaha. Iliniuma sana kuona kuwa hata sheria hazifuatwi ila ni chuki za kidini zilizowekwa mbele. Anaeleza Sajenti Zahaki kuwa; baada ya tukio la Mwembechai nilipokuwa nikikutana na waumini wiki mbili baadaye zilikuwa ni ngumu kwangu, kwani walikuwa wakiniuliza Ndugu zetu mbona mnatuuwa? Tumekukoseeni nini, mbona mnatuua? Tukio lililobadili historia ya maisha yangu, na ambalo lilipelekea kufukuzwa katika jeshi la polisi, lilitokea saa 2.00 asubuhi ya Jumapili tarehe 1, Machi 1998. Nilikuwa na utamaduni wa muda mrefu kuwaruhusu askari Wakristo walio chini yangu, ambao wote walikuwa Wakristo, kwenda Kanisani Jumapili. Walipoondoka siku ile, nilianza kusoma nakala ya gazeti la AnNuur ambalo liliendelea kuripoti habari za Mwembechai. Nilipomaliza kulisoma, niliinua kichwa juu na kutazama kalenda iliyokuwa ukutani ambayo bado ilisomeka mwezi Februari, na siku hyo ilikuwa siku ya kwanza ya mwezi Machi. Niliishusha ile kalenda mezani na kuizungushia duara tarehe 13 ya Februari kwa peni nyekundu. Nikachora mishale mingi kuelekea tarehe ile na kuanza kuandika maoni yangu, niliandika, hii ni siku Waislamu walipouawa Mwembechai; ni siku Waislamu walipoteswa Mwembechai; ni siku Waislamu wanawake walipoharasiwa Mwembechai; ni siku msikiti wa Mwembechai uliponajisiwa, nakadhalika. Nikaandika polisi walivyotakiwa kufanya kwa mujibu wa sheria za polisi, katiba ya nchi na nikamnukuu Abraham Lincon. Polisi walitakiwa wawakamate watuhumiwa na kuwakabidhi mahakamani na si kuwaadhibu. Niliandika kwa hisia za ndani. Niliiacha ile karatasi mezani mwangu, nilirudi nyumbani huku maneno Ndugu zetu mbona mnatuua? likijirudia kichwani mwangu huku nikijiuliza siku ya hukumu nitajibu nini mimi? Msabato, Staff Sergent Richard Ogutu, aliichukua ile kalenda na kuipeleka kwa uongozi. Tarehe 3 Machi, 1998
nikaitwa kwa RPC Alfred Gewe, pamoja naye, alikuwepo Mkuu wa Operesheni ya Mwembechai Mr. Kombe na Asa Usalama wa Mkoa (RSO), Saidi Mwema (IGP kwa sasa), Staff officer, Buka Kibona na SSP Sammari. Nilihojiwa na Alfred Gewe. Mahojiano yetu yalikuwa kama ifuatavyo; A G : We w e n i Z a h a k i Rashid? ZR: Ndiyo AG: Ni mtu wa Kigoma? ZR: Ndiyo AG: Nimeona katika taarifa zako kuwa umesoma Uislamu. Je, unaujua Uislamu vizuri? ZR: Ndiyo, Mie sio mjinga wa dini yangu. Naufahamu Uislamu vizuri. AG: Unaujua Uislamu vizuri wakati ulipata F ya Islamic Knowledge? ZR: Nilibaki kimya. (nikimkumbuka headmaster aliyenisababishia kupata F na inajirudia tena kukumbushwa iliniuma sana) AG: Uko upande gani katika sakata la Mwembechai? ZR: Nijibu kama Ofisa wa Polisi au kama Muislamu? AG: Kwanini unaniuliza swali hilo? ZR: Kwasababu ulianza kunihoji juu ya ufahamu wangu dhidi ya Uislamu. Najua wewe ni RPC na mimi ni Osa wa Polisi. Swali lako linanichanganya. Ndio maana nakuuliza nikujibu kama Osa wa Polisi au kama Muislamu? AG: Je, umeandika chochote kile juu ya tatizo la Mwembechai katika gazeti, karatasi au sehemu yeyote ile? ZR: (Sikutaka kupoteza muda nikajibu wazi). Ndiyo, Tarehe 1 March,1998 niliandika tukio hilo katika karatasi ya kalenda. AG: Kalenda yenyewe ndiyo hii? ZR: Ndiyo yenyewe. AG: Tutachunguza, tukigundua hauko pamoja nasi, tutakuruhusu ukapige magoti kwenye makapeti msikiti wa Mwembechai. Nikafukuzwa kazi rasmi katika jeshi la polisi tarehe 1 Agosti, 1998. Uamuzi ule uliwasilishwa kwangu tarehe 1 Juni 1999 na kamanda wa Polisi wa wilaya kituo cha Oysterbay (OCD), Bwana Magosi, alinisomea kwa niaba ya RPC, Alfred Gewe kama ifuatavyo: 1. Mtuhumiwa ni mfuasi mtiifu wa imani ya Kiislamu. 2. Kwahiyo tunaamini, akiendelea kubaki katika jeshi la polisi, hawezi kutimiza imani yake vizuri. Ni vizuri akawa nje ya jeshi, hivyo aweze kufuata dini yake bila kikwazo. 3. Hatujui ni kwa kiwango gani jeshi la polisi limeathirika na kuwepo kwake katika kitengo cha uzuiaji wa makosa ya jinai kipindi cha utumishi wake. 4. Alichokifanya ni uhaini. 5. Kwa hivyo nimependekeza kwa IGP, kuwa afukuzwe. Anaweza kukata
rufaa kama hatoridhishwa na maamuzi. Hayo ndio maamuzi yaliyochukuliwa na Alfred Gewe kama RPC kumfukuza Asa wa Polisi kwa kuwa tu, anafuata dini yake ya Kiislamu vizuri. Zahaki anaeleza kuwa wakati wa kupambana na uhalifu, askari wa jeshi letu la polisi ambao ni Wakristo wazuri huchukuliwa kama rasilimali na wale Waislamu wanaofuata dini yao vizuri huonekana ni watu hatari. Kuwa Muislamu mzuri ni kigezo kikubwa cha kutokuwa na sifa ndani ya jeshi la polisi. Waislamu kwa kadri watakavyoifuata dini yao vizuri hawatakiwi kuajiriwa na jeshi la Polisi. Ndio maana hadi leo hii askari Waislamu ni waoga na hawataki kujulikana kama wanaufuata Uislamu wao, wengine hata kufanya ibada ni ngumu kwao ili kuwaridhisha wenzao kuwa wako pamoja. Haya ni mambo ya kusikitisha s a n a , w a k a t i Wa k r i s t o wakionekana wa thamani kwa uumini wao mzuri wa Kikristo, Waislamu wamekuwa wakibaguliwa na kuonekana ni watu hatari kwa kufuata Uislamu wao, na hawafai kulitumikia jeshi la polisi. Huyo huenda ni mmoja tu kati ya wengi wanaofukuzwa kazi au kuhamishwa vituo ambao taarifa zao hazijawekwa hadharani. Leo ni miaka kumi na tano (15) sasa toka mauaji ya Mwembe chai yatokee na madhara yake yapo hadi leo. Uimara na ujasiri wa imani kwa Waislamu umeongezeka maradufu. Waislamu hawajaacha kudai haki pale wanapodhulumiwa. Hakuna kiongozi wa serikali anaye wasikiliza wanapodai kuonewa na kudhulumiwa. Wanapoamua kuandamana kuonesha hisia zao huandamwa kwa virungu, mateke na mabomu ya machozi na hatimaye kukamatwa na kujazwa mahabusu bila matatizo au dhulma wanayoilalamikia kuondolewa. Mpaka sasa kuna kesi zaidi ya ishirini dhidi ya Waislamu humu nchini zikihusisha serikali na Waislamu, ikiwemo ile ya Sheikh Ponda Issa Ponda na waumini wengine arobaini na tisa. Ndugu zangu wananchi na viongozi wapenda haki na kupenda kuiona haki inatendeka, sio wakati wakukata tamaa kuipigania haki. Kwani haki inaendana na Mwenyezi mungu na dhulma inaendana na sheitwan. Haki itasimama tu siku moja na wale wote walioipigania haki watakumbukwa daima duniani na kesho akhera watapata malipo mema pamoja na wema waliotangulia. Wanataka kuizima Nuru ya Mwenyezi Mungu kwa vinywa vyao, na Mwenyezi Mungu anakataa ila aitimize Nuru yake ijapo kuwa makari watachukia Quran 9:32.
15
TANGAZO
AN-NUUR
1.
KIRINJIKO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL NYASAKA ISLAMIC SECONDARY SCHOOL UBUNGO ISLAMIC HIGH SCHOO L
Shule hizi ni za Kiislamu zenye lengo la kuwapa wanafunzi taaluma ya hali ya juu na malezi bora ya Kiislamu kwa gharama nafuu. Shule hizi ni za mchanganyiko wa wavulana na wasichana na zinapokea wanafunzi wa bweni tu. 2. Masomo yanayofundishwa ni Islamic knowledge, Combinations za SAYANSI, ARTS, BIASHARA pamoja na COMPYUTA. 3. Muombaji awe na Crediti 3 au zaidi na angalau D ya Elimu ya Dini ya Kiislamu katika matokeo ya kidato cha nne. Ikiwa ana F au hakufanya Elimu ya Dini ya Kiislamu, basi awe tayari kusoma programu maalum ya Maarifa ya Uislamu atakapokuwa kidato cha tano. 4. Mwisho wa kuchukua na kurudisha fomu ni tarehe 18 /05 /2013 5. Fomu za Maombi zinapatikana kwa gharama ya shilingi 10,000/= katika vituo vilivyoorodheshwa hapa chini. 6. Arusha Kilimanjaro Tanga Mwanza Musoma Kagera Shinyanga Osi ya Islamic Education Panel Jambo Plastic Ghorofa ya 2 mkabala na msikiti Mkuu Bondeni - 0763 282 371/ 0784 406 610 Moshi: Msikiti wa Riadha 0654 723 418 Same: Kirinjiko Islamic Secondry School: 0784 296424/0655 697 075 Uongofu Bookshop: - 0784 982525/ Mandia Shop - Lushoto: 0782257533 Nyasaka Islamic Secondary School 0717 417685/0786 417685 Osi ya Islamic Education Panel - Mwanza - Mtaa wa Ruji mkabala na Msikiti Al-Amin 0785 086 770 Duka la Kansolele -Stendi ya zamani sokoni - 0714587193 Bukoba: Alhuda Caf Kwa mzee Kinobe karibu na osi za TRA. - 0688 479 667 Msiikiti wa Majengo-0718866869 Kahama osi ya AN NUUR Karibu na msikiti wa Ibadhi: 0753 993930 Ubungo Islamic High School 0754 260 241/0712033556 Osi ya Islamic Ed. Panel Temeke -Msikiti wa Nurul Yakin 0655144474 Wasiliana na Ramadhani Chale :0715704380 Hijra Islamic Primary School : 0716 544757/0712 325086 Osis ya Islamic Ed. Panel karibu Nuru snack Hotel 0714285465 Babati: Shule ya Msingi Hangoni: 0784 667575 Msikiti wa mwanga Kigoma: 0753 355224 Kibondo Islamic Nursery School: 0784 442860 Kasulu: Murubona Isl.SS. 0714710802 Wapemba Store: 0784 974041/0786 959663 Amana Islamic S.S 0786 729 973 Kwa Kawanga Karibu na Msikiti wa NURU 0715 681701/0716791113 Mkuzo Islamic High School. 0716 791113 Duka la vifaa vya Kiislamu nje ya Msikiti wa Uyole 0713 200209 Rexona Video mkabala na Mbeya RETICO: 0713 200209 Sumbawanga: Masjid TAQWA 0717082 073 Kituo cha Kiislamu Isevya: 0784 944566 Madrastun Najah: 0714 522 122 Wete: Wete Islamic Education Center: 0777 432331 Madrasatul Fallah: 0777125074Osi ya ust. Yusufu Ally jirani na msikiti mkuu 0653705627
Dar es Salaam Morogoro Dodoma Singida Manyara Kigoma Lindi Mtwara Songea Mbeya Rukwa Tabora Iringa Pemba Unguja Maa -
Pia Fomu zinapatikana kwenye Tovuti: www.ipctz.org. Ikumbukwe kuwa watakaopata fomu kupitia tovuti (download) watatakiwa kuzilipia wakati wa kuzirejesha. USIKOSE NAFASI HII ADHIMU WAHI KUCHUKUA FOMU SASA! Wabillah Tawiq MKURUGENZI
16
AN-NUUR
16
Na Mwandishi Maalum, Zanzibar
AN-NUUR
SHEIKH Musa Athumani Kagimbo (kushoto), ambaye alikuwa Sheikh wa Bakwata mkoa wa Kagera, amefariki dunia Jumapili iliyopita ya Machi 03.
wake alikuwa kiongozi wa kusimamia Uislamu akianzia kijiji cha Nshamba na mwaka 1,975 alipata nafasi ya kuwa Shekhe wa wilaya ya Muleba hadi 1,993. Mwijage alisema kuwa mwaka huo wa 1993 alifariki Shekhe wa mkoa, Sheikh Mikidadi Yusufu Katula wa kijiji cha Muhutwe. Alisema kufuatia kutangulia mbele ya haki Sheikh Katula, Baraza la Maulamaa mkoa lilimpendekeza Sheikh Musa Kagimbo kushikilia kiti hicho baada ya kukubalika na waumini. Marehemu wakati wa uhai wake alipenda kusisitiza mshikamano, akipinga mtafaruku wa kutengana na amesimamia miradi mingi ya Kiislamu Muleba na mkoa kwa ujumla. Kilichopo sasa ni kumuombea apumzike na kupata radhi zake Allah (S.W). Alisema Mwijage. Aidha Katibu huyo aliwataka waumini kumuenzi Sheikh Kagimbo kwa yale mema aliyoanzisha na kuyasisitiza wakati wa uhai wake, ikiwa ni pamoja na kuimarisha mahusiano kwa madhehebu yote ya kidini bila kujali tofauti za kiitikadi, za kimadhehebu au mitazamo.
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Limited, S.L.P. 78495 Dar es Salaam.