Professional Documents
Culture Documents
Hivi karibuni kumekuwa na taarifa mbalimbali zisizo rasmi kuhusu hali na mwenendo wa
Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF). Baadhi ya taarifa hizo zimekuwa zikieleza
kwamba mali za Mfuko huo zimetumiwa vibaya na hivyo kuathiri mafao kwa wanachama.
Taarifa hizi zimesababisha hofu na taharuki miongoni mwa wanachama wa NSSF na wadau
wa Sekta ya Hifadhi ya jamii kwa ujumla kwa kuhofia usalama wa wa fedha na mafao yao.
Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) inapenda kuwaondoa
hofu wanachama wote wa Mfuko wa NSSF na Wananchi kwa ujumla na kuwahakikishi
kwamba Mfuko wa NSSF upo katika hali nzuri kifedha na unaendelea kulipa mafao ya
wanachama kama kawaida.
Imetolewa na
Kitengo cha Mawasiliano
Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii
S.L.P 31846
Tovuti: www.ssra.go.tz
Dar es Salaam
1