Professional Documents
Culture Documents
Serikali imevalia njuga swala la deni la Mifuko ya Hifadhi ya Jamii. Hadi kufika mwezi
Machi, 2016 tayari Serikali ilikuwa imeshalipa Jumla ya Bilioni 173.11 kwa Mfuko wa
PSPF. Mfuko huo umeweza kulipa Hundi 49,467 ambapo kati ya hizo hundi 46,000 ni
za pensheni za kila mwezi kwa wastaafu na Hundi 3,467 ni za madai mapya ya
Pensheni. Taarifa zinaonesha kwamba Serikali imedhamiria kulipa deni lote la
michango ifikapo June 2016.
Kuhusu hati Fungani (Non cash Bond) taarifa zinaonyesha kwamba mifuko ambayo
ilikuwa bado kuridhia hati ya Makubaliano (deed of settlement) hivi sasa imeridhia.
Serikali inatarajia kutoa Hati Fungani (non-cash bond) ya Shilingi Trilioni 2.6 yenye
riba ya asilimia 6.5 kwenda PSPF. Hati Fungani hii itaiva kwa muda tofauti ili
kuwezesha mfuko kukidhi mahitaji yake ya malipo ya mafao. Hati fungani hizi zitaiva
kwa vipindi tofauti tofauti. Yaani kuna hati fungani za miaka 3, miaka 5, miaka 7, miaka
10 na kuendelea.
MIRADI YA UWEKEZAJI
Mamlaka kwa kushirikiana na Benki Kuu ya Tanzania kwa mujibu wa Kifungu cha 6(2)
(c) cha Sheria Na.8 ya mwaka 2008 ikisomwa pamoja na kifungu cha 40 na kifungu
cha 48 Mamlaka ilikamilisha kaguzi za Mifuko kwa mwaka 2015. Kaguzi hizi
zimepelekea Mamlaka kwa kushirikiana na Benki Kuu kufanya kaguzi maalumu
(Special Inspection) kwenye majengo na milki za Mifuko yote ya Hifadhi ya Jamii ikiwa
ni pamoja na Mfuko wa NSSF. Kaguzi hizi zimeanza toka mwezi Januari 2016. Huu
ni ukaguzi wa kina sana hivyo unatarajiwa kuchukua kati ya miezi 6 hadi 9 kulingana
na upatikanaji wa taarifa zinazohusika. Hata hivyo wakati kaguzi zikiendelea Mifuko
iliyovuka viwango vya uwekezaji tayari imezuiwa kuendelea kuwekeza katika maeneo
hayo. Taarifa ya ukaguzi maalumu, itakapokamilika itasaidia Serikali kuchukua hatua
1
Deni la pensheni limepungua toka asilimia 58 ya pato la Taifa mwaka 2010 hadi
asilimia 25 mwaka 2015.
Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inalipa mafao ya muda mrefu kama vile;- fao la Pensheni
ya Uzee, Mirathi na Ulemavu. Kwa upande wa mafao ya muda mfupi Mifuko inalipa
mafao ya;- Uzazi, Elimu, Afya, Mazishi na Kuumia kazini pamoja na huduma
zingine kama vile Mikopo ya makazi, elimu na mikopo ya kuanza maisha baada ya
kuajiriwa.
inavyoongezeka ambapo kwa kipindi cha miaka 50 ijayo umri wa kuishi baada ya
kustaafu kwa wanaume itakuwa miaka 22.9 na wanawake miaka 24.9.