Professional Documents
Culture Documents
10.
Sehemu ya taarifa hiyo ya gazeti la MwanaHALISI imeendelea kudai na
kunukuliwa Serikali ililazimika kukopa kwa siri kiasi hicho cha fedha
kutoka Stanbic kwa kuweka dhamana ya hati fungani, ili kufanikisha
upatikanajiwa fedha za kumlipa Singasinga wa IPTL, ameeleza mmoja wa
maofisa wa Stanbic ambaye ametoka katika benki hiyo hivi karibuni. []
Kigogo huyo anasema, kwa vile wakubwa walishapanga kumlipa Sethi,
kabla ya Desemba 2013, ikabidi wakope benki kwa kuweka dhamana hati
fungani zilizoshushwa bei (discounted treasury bills).
Kwa mujibu wa Ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali (iliyotajwa hapo juu) kwenye
ukurasa wake wa 16 inaelezea wazi kabisa kuwa umiliki wa hati fungani
zilizowekezwa na BoT kutokana na fedha zilizokuwa kwenye akaunti ya Escrow ya
Tegeta, ulihamishwa kwenda kwa PAP tarehe 6 Desemba, 2013. Madai ya kuwa
serikali ilikopa kwa kuweka hati fungani zilizoshushwa bei ni uongo na uzushi
usiokuwa na ukweli wowote.
11.
Sehemu ya taarifa hiyo ya gazeti la MwanaHALISI imeendelea kudai na
kunukuliwa Taarifa zinasema, katika kiasi hicho cha dola 180 milioni, dola
takriban 100 milioni, kilitoroshewa nje katika nchi za Falme za Kiarabu,
huko Dubai na Afrika Kusini, kabla ya kuhamishiwa tena nchini Austria.
Nchini Austria, taarifa zinasema, ndiko ambako mtoto wa mmoja wa
waliokuwa viongozi wa juu serikalini, amefungua akaunti. Hizi ni taarifa za
uongo zisizokuwa na chembe ya ukweli na ni tuhuma zisizokuwa na ushahidi
wowote.
12.
Kwa machache haya ya uongo na uzushi tuliyoyanukuu na mengine mengi
ambayo tumeamua kutokuyatolea ufafanuzi kwa nia ya kuiweka taarifa hii kwa
ufupi, tungependa kuomba vyombo husika kuchukua hatua dhidi ya waliohusika na
uenezi wa taarifa hizi za kizushi kwa kuwafikisha mbele ya vyombo vya dola na
kuwahoji ili ukweli wa tuhuma ujulikane. Tunaamini kwamba tabia ya kuikashifu
kampuni yetu na kuwakashifu viongozi wa serikali bila ya kuwa na uthibitisho
isipokomeshwa, basi nchi itajaa waropokaji na heshima ya serikali na vyombo vyake
itaporomoka. Tabia hii isipokomeshwa itaathiri hali ya uwekezaji nchini kwani
itawakatisha tamaa wawekezaji wengine wanaotaka kuwekeza nchini.
13.
Kwa muhtasari, taarifa zilichochapishwa kwenye makala husika ni uzushi
usiokuwa na ukweli wowote. Tungewaomba Watanzania na wote waliosoma au
watakaosoma makala husika wazipuuzie taarifa hizo. Pia tunawataka wahariri na
wachapishaji wa gazeti la MwanaHALISI kuomba radhi kwa taarifa hizo za kizushi
ndani ya siku kumi na nne (14). Kushindwa kufanya hivyo, hatua za kisheria
zitachukuliwa ikiwemo kulifikisha gazeti, wahariri na wachapishaji wake
mahakamani.
14.
IPTL/PAP tuko tayari kutoa ushirikiano kwa mtu yeyote mwenye ushahidi wa
rushwa kufikisha mbele ya vyombo husika na kuhakikisha rushwa inakomeshwa.
3
15.
Tunaomba pia vyombo mbalimbali vinavyohusika na kulinda amani na
utengamano wa nchi yetu ikiwemo jeshi la polisi kuwachukulia hatua mwandishi wa
makala hiyo na wahariri wa gazeti la MwanaHALISI kwa kuvunja sheria za nchi kwa
kuandika habari za uchochezi.
Ahsanteni sana.