UNA Tanzania inaandaa ripoti kivuli juu ya utekelezaji wa mkataba wa CEDAW Tanzania. Taasisi inaongoza mchakato huu na mashirika mengine 25 ya kitanzania.
UNA Tanzania inaandaa ripoti kivuli juu ya utekelezaji wa mkataba wa CEDAW Tanzania. Taasisi inaongoza mchakato huu na mashirika mengine 25 ya kitanzania.
UNA Tanzania inaandaa ripoti kivuli juu ya utekelezaji wa mkataba wa CEDAW Tanzania. Taasisi inaongoza mchakato huu na mashirika mengine 25 ya kitanzania.
United Nations Association of Tanzania | bringing people closer to the UN
Taarifa kwa Vyombo vya Habari; Asasi Zisizo za Serikali
(AZISE) kuandaa ripoti kivuli Juni 13, 2014 - Dar es Salaam, Tanzania Asasi ya Umoja wa Mataifa Tanzania (United Nations Association of Tanzania) inaongoza mchakato wa asasi za kiraia 25 inaingia kuandaa ripoti kivuli ya Asasi za Kiraia kwa ajili ya Mkataba wa Kutokomeza Aina Zote za Unyanyasaji wa Wanawake (Convention on Elimination of All forms of Discrimination Against Women au CEDAW). CEDAW ni mkataba wa kimataifa ambao nchi wanachama wa mkataba wamekubaliana kutokomeza aina zote za unyanyasaji dhidi ya wanawake. Tanzania ilianza utekelezaji wa mkataba mwezi September 1985. Makubaliano haya yanahitaji nchi wanachama kuwasilisha ripoti ya utekelezaji Umoja wa Mataifa kwa vipindi maalumu. Tanzania mara ya mwisho kuwasilisha ripoti ilikuwa mwaka 2008 na mwaka 2014 itawasilisha tena. Tanzania kama nchi mwanachama inatakiwa kuwasilisha ripoti yake ya utekekelezaji wa makubaliano kwa kamati ya CEDAW mwezi September 2014. Ripoti kivuli ya asasi hii pia itawashilishwa Umoja wa Mataifa sambamba na ripoti ya serikali. Ripoti inayosimamiwa na UNA Tanzania itajikita katika maeneo maalumu tisa ambayo ni Afya, Elimu, Ukeketaji, Sheria kandamizi dhidi ya wanawake, Mila kandamizi na shurutishi, Ukatili dhidi ya wanawake, Uelewa wa Mkataba, na Maana ya unyanyasaji wa wanawake katika sheria za nchi. Kwa maelezo zaidi, wasiliana na UNA Tanzania kupitia info@una.or.tz Imetolewa na: Nancy Kaizilege Katibu Mkuu UNA Tanzania