You are on page 1of 10

Ofisi ya Mawasiliano Serikalini inapokea habari za matukio mbalimbali

kwa ajili ya News Bullettin hii na Jarida la Wizara ya Nishati na Madini


Wasiliana nasi Kitengo cha mawasiliano kwa simu Namba +255 22 2110490 Fax 2110389 Mob: +255 732 999263
au Fika Ofsi ya Mawasiliano Ghorofa ya Tano (MEM) Barua pepe: badra77@yahoo.com
Ofisi ya Mawasiliano Serikalini inapokea habari za matukio mbalimbali
kwa ajili ya News Bullettin hii na Jarida la Wizara ya Nishati na Madini
Toleo No.19 Limesambazwa kwa Taasisi na Idara zote MEM Juni 6-12, 2014
Ngonyani Kaimu Mkurugenzi STAMICO uk6
SOMA UK 2
Naibu Waziri wa Nishati na Madini
anayeshughulikia madini Mhe. Stephen
Masele
Atakayeajiri
Watoto
migodini
kukiona
nMasele asisitiza
Watoto
wakijishughulisha
na kazi za madini
Soma uk2
2 | MEM News Bulletin
NISHATI
FIVE
PILLARS
OF
REFORMS
TEL 2110490
FAX 2110389
MOB 0732999263
KWA HABARI PIGA SIMU
KITENGO CHA MAWASILIANO
BODI YA UHARIRI
MHARIRI MKUU
Badra Masoud
MSANIFU
Essy Ogunde
WAANDISHI
Veronica Simba
Asteria Muhozya
Greyson Mwase
Teresia Mhagama
Nuru Mwasampeta
INCREASE EFFICIENCY
QUALITY DELIVERY
OF GOODS/SERVICE
SATISFICATION OF
THE CLIENT
SATISFICATION OF
BUSINESS PARTNERS
SATISFICATION OF
SHAREHOLDERS
Na Greyson Mwase, Tarime
N
aibu Waziri wa
Nishati na Madini
anayeshughulikia ma-
dini Stephen Masele
amekemea vikali tabia ya wami-
liki wa migodi kuajiri watoto
wenye umri wa chini ya miaka
18 kwani inarudisha maende-
leo ya watoto hao na jamii kwa
ujumla.
Waziri Masele ameyasema
hayo kwenye ufunguzi wa se-
mina iliyoshirikisha wachimbaji
wadogo, madiwani, viongozi wa
vijiji, wilaya, madiwani pamoja
na viongozi wa vyama vya
siasa iliyofanyika katika jimbo
la Mwibara wilaya ya Bunda
mkoani Mara.
Masele alisema kuwa kume-
kuwepo na tabia ya wamiliki wa
migodi, ikiwa ni pamoja na wa-
zazi wenye watoto wenye umri
chini ya miaka 18 kuruhusu
watoto hao kufanya kazi kwenye
migodi badala ya kuwahimiza
kwenda shule na kupata elimu
itakayowasaidia kutoka kwenye
giza.
Kutokuwapeleka watoto
shule na kuwahimiza kushiriki
katika shughuli za madini ni
kuwaharibu kisaikolojia kwa ku-
wakosesha elimu kama haki yao
kimsingi, ni kosa kubwa sana.
Alisema Waziri Masele
Masele alieleza kuwa
umefka wakati wa wamiliki
wa migodi pamoja na wazazi
kuwahimiza watoto kuhudhuria
shule ili kuweza kuwa wataalamu
wa kutegemewa baadaye katika
taifa kama marubani, wahandisi,
mawaziri na madaktari.
Aliongeza kuwa mkakati wa
Serikali ni kuhakikisha kuwa kila
sekta inasimamiwa na wata-
alamu ambao ni wazawa kwa
kuhakikisha inalipa kipaumbele
suala la elimu.
Inatakiwa pindi migodi
mikubwa inapoanzishwa wataal-
amu wengi kwenye migodi wawe
ni wazawa badala ya kuishia
kuwa vibarua na nafasi zao ku-
chukuliwa na wataalamu kutoka
nje. Alisisitiza Waziri Masele.
Aliongeza kuwa ili nchi
yeyote iweze kupiga hatua
kimaendeleo inahitaji wataalamu
katika kada mbalimbali na ku-
ongeza kuwa serikali ipo tayari
kutoa msaada katika kuzalisha
wataalamu hususani katika sekta
za nishati na madini.
Akielezea mikakati ya
serikali katika kuimarisha
sekta ya madini Waziri Masele
alieleza kuwa serikali kupitia
Wizara imeanza kufufua vyama
vya uchimbaji madini ikiwa ni
pamoja na kuanza kutoa ruzuku
kwa wachimbaji wadogo kwani
wana mchango mkubwa sana
katika pato la taifa.
Waziri Masele alieleza kuwa
serikali ilianza kutoa ruzuku na
itaendelea kutoa ruzuku kwa
wachimbaji wadogo watakaot-
hibitishwa na chama cha
wachimbaji madini kuwa wa-
najishughulisha na shughuli za
uchimbaji madini lengo likiwa
ni kuboresha maisha yao.
Alitaja mikakati mingine
kuwa ni pamoja na kuende-
lea kutoa elimu ya kanuni za
uchimbaji bora na salama wa
madini kwa kutumia wataalamu
wake sehemu zote zenye madini
nchini.
Akielezea kanuni za uchim-
baji salama wa madini Waziri
Masele aliwataka wachimbaji
wadogo kuachana na matumizi
ya zebaki katika uchenjuaji
madini kwani zina athari kubwa
kiafya na badala yake watumie
cyanide.
Waziri Masele alisema kuwa
matumizi ya zebaki yana athari
kubwa kwa mchimbaji madini
ikiwa ni pamoja na jamii inayom-
zunguka na hata vizazi vijavyo.
Alitaja athari za zebaki ni
pamoja na magonjwa ya kansa,
pamoja na kuwa na kuwa na
vizazi vya watoto wenye ulemavu
wa mtindio wa ubongo.
Unajua athari hizi zinaweza
kuonekana hata baaada ya muda
mrefu, watu wanaweza kuathirika
kwa kula viumbe kama sa-
maki vilivyoathiriwa na zebaki
iliyotokana na maji yaliyooshea
madini hayo kutiririshwa ziwani
au kwenye mito. Alisisitiza
Waziri Masele.
Aliwataka wachimbaji
wadogo kufuata kanuni za umi-
liki leseni ili kuepuka migogoro
inayoweza kujitokeza kati yao na
wamiliki wa migodi.
Waziri Masele aliongeza
kuwa kumiliki ardhi hakutoshi
kumpa uhalali mmiliki wa eneo
husika kuchimba madini kwani
ardhi ni eneo la juu likiwa ni
pamoja na mimea na mito na si
madini yaliyopo chini yake.
Aliwataka wamiliki wa ardhi
yenye madini kuomba leseni ya
uchimbaji madini ili kuweza
kuchimba madini au kuingia ubia
na wenye kuhitaji maeneo yao.
Ni marufuku kuajiri watoto migodini-Masele
Baadhi ya wajumbe
wakifuatilia mada
iliyokuwa ikiwasilishwa
na mwezeshaji kutoka
Wizara ya Nishati
na Madini Mhandisi
Kungulu Kasongi
(hayupo pichani)
MEM News Bulletin | 3
MADINI
Na Teresia Mhagama
S
erikali inafanya kila jitihada ili
kuhakikisha kuwa mapungufu
yaliyojitokeza katika uwekezaji
wa sekta ya madini, hayajirudii
tena katika sekta ndogo ya gesi asilia.
Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu
wa Wizara ya Nishati na Madini Elia-
kim Maswi wakati akiongea na Waziri
wa Nchi katika Jamhuri ya Singapore
anayeshughulikia mahusiano ya ndani
na nje ya nchi, Bw. Masagos Zulkifi
aliyefka Makao Makuu ya Wizara ya
Nishati na Madini jijini Dar es Salaam
ili kuzungumzia fursa za uwekezaji
katika gesi asilia na mafuta hasa katika
kushauri namna bora ya kutekeleza
mradi wa gesi iliyosindikwa (LNG).
Katibu Mkuu alimweleza Waziri
huyo wa Singapore kuwa serikali hivi
sasa inajikita zaidi katika kuhakikisha
kuwa miradi mbalimbali ya uwekezaji
inayofanyika nchini inawanufaisha wa-
nanchi moja kwa moja kuanzia ngazi
ya chini ili nao waone matunda ya
maliasili ambazo serikali inazisimamia
na kuziendeleza.
Ili kuhakikisha wananchi wa-
nashiriki katika utekelezaji wa miradi
mbalimbali na wao wafaidike na miradi
hii, ni lazima kuwe na uwazi ambao
utawafanya washiriki na waelewe nini
kinaendelea na wao kujiona ni sehemu
ya miradi hiyo.Alisema Katibu Mkuu.
Waziri Zulkif ambaye aliambatana
na watendaji mbalimbali kutoka baadhi
ya makampuni ya serikali na binafsi
ameeleza kuwa nchi ya Singapore ina
uzoefu na utaalam katika kutoa ushauri
wa namna ya kuetekeleza miradi ya gesi
iliyosindikwa hasa ujenzi wa nyumba
za bei nafuu kwa wananchi wanaopisha
miradi ya LNG, ujenzi wa vyuo vya
ufundi pamoja na utoaji wa huduma za
ulinzi.
Ameeleza kuwa ziara hii imefanyika
kufuatia ziara ya Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya
Mrisho Kikwete aliyeitembelea Singa-
Ili kuhakikisha wananchi wanashiriki katika
utekelezaji wa miradi mbalimbali na wao
wafaidike na miradi hii, ni lazima kuwe
na uwazi ambao utawafanya washiriki na
waelewe nini kinaendelea na wao kujiona ni
sehemu ya miradi hiyo
<
Wadau
utafutaji,
uzalishaji
mafuta, gesi,
kutoa maoni
Na Asteria Muhozya,
Dar es Salaam
W
adau wa shu-
ghuli za utafut-
aji na uzalishaji
mafuta, gesi na
biashara ya bid-
haa za mafuta wanatarajia kutoa
maoni kuhusu rasimu ya sera ya
Petroli katika warsha itakayowa-
kutanisha yenye lengo la kujadili
na kupata maoni yao kuhusu
sera hiyo, itakayofanyika hivi
karibuni Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza kuhusu mku-
tano huo, Mjiolojia Mwandamizi
Wizara ya Nishati na Madini
Adam Zuberi ameeleza kuwa,
warsha hiyo ni ya pili kufuatia
ya kwanza iliyofanyika mwezi
Machi, 2014 ambayo ilisam-
bazwa kwa wadau muhimu wa
sekta hiyo kutoka katika taasisi
mbalimbali za serikali na kutoa
maoni yaliyowezesha kupatikana
kwa rasimu ya sasa ya Sera ya
Petroli.
Ameongeza kuwa, warsha
ya sasa inalenga kuwakutanisha
wadau muhimu mbalimbali
wanaojishughulisha na shughuli
za utafutaji na uzalishaji mafuta,
gesi na biashara ya bidhaa za
mafuta nchini, ili waweze kupitia
kwa pamoja rasimu ya sera hiyo
kuweza kupata maoni zaidi
yatakayosaidia kuboresha sera
hiyo.
Zuberi ameeleza kuwa, seri-
kali imeona ipo haja ya kuwa na
sera mahsusi kwa ajili ya masuala
ya petroli nchini kutokana na
ugunduzi wa kiasi kikubwa cha
gesi katika kina kirefu cha bahari
kuu ikiwa ni pamoja na ukuaji
wa shughuli za petroli nchini.
Pamoja na hayo ameongeza
kuwa, sera ya petroli inatarajia
kutoa mwelekeo wa namna
ambavyo Tanzania na watan-
zania watakavyonufaika na
sekta ya petroli nchini na namna
itakavyochangia katika ukuaji
wa kijamii na kiuchumi kwa
manufaa ya taifa.
Aidha ameogeza kuwa,
Serikali ina lenga kuhakikisha
kuwa sera hiyo inasaidia kubore-
sha maisha ya watanzania kwa
miongo mingi kupitia sekta hiyo
kwa kuzingatia dira na dhima za
sera hiyo.
Na Greyson Mwase, Bunda.
W
achimbaji wadogo wam-
etakiwa kujenga utamad-
uni wa kupima afya zao
mara kwa mara kama njia
mojawapo ya kupambana na ugonjwa
wa Ukimwi unaoonekana kushambulia
hasa wakazi wanaoishi karibu na maeneo
ya migodi ya madini
Wito huo umetolewa na mhadhiri
kutoka ChuoKikuu cha Dar es salaam
Dkt. Crispian Kinabo kwenye semina
iliyoshirikisha wachimbaji wadogo,
wakuu wa vijiji, wakuu wa vyama na
madiwani iiliyofanyika huko Mwibara
wilayani Bunda, mkoani Mara.
Dkt. Kinabo alieleza kuwa takwimu
zinaonesha kuwa maeneo ya migodi
yanaongoza kwa maambukizi ya virusi
vya ukimwi na kuwataka wachimbaji
hao kulinda afya zao pamoja na jamii
inayowazunguka.
Akizungumia hali ya maambukizi
ya ugonjwa wa Ukimwi nchini Dkt.
Kinabo alisema kuwa takribani wananchi
milioni mbili wanaishi na virusi vya
Ukimwi na wananchi 700,000 wamefkia
katika kiwango cha kuanza kutumia
dawa za kurefusha maisha (ARVs)
Dkt. Kinabo aliongeza kuwa kwa
ujumla asilimia 5.1 ya watanzania wenye
umri kati ya miaka 15 na 49 wanaishi na
virusi vya Ukimwi.
Aliongeza kuwa ili kukabiliana na
ugonjwa wa Ukimwi wachimbaji wadogo
wanatakiwa kuwa mfano bora katika
jamii inayowazunguka kwa kubadili
mienendo yao na kupima afya zao mara
kwa mara.
Inatakiwa ifke mahali muachane
kabisa na michepuko na kubaki njia kuu
kwa kuwa waaminifu kwa wenzi wenu.
Alisisitiza Dkt. Kinabo.
Pimeni afya zenu - Dkt. Kinabo
Hatutaki kurudia makosa-Maswi
pore mwezi Juni 2013, ziara iliyopele-
kea mahusiano mapya ya uendelezaji
wa sekta mbalimbali ikiwemo mipango
miji, mafunzo ya ufundi, uendelezaji
bandari na sekta ya mafuta na gesi
asilia.
Bw. Zulkifi ameishukuru serikali
ya Tanzania kwa ushirikiano alioupata
na kueleza kuwa Singapore inahi-
taji kushirikiana na Tanzania katika
uwekezaji kwa kuwa Tanzania ime-
jaliwa kuwa na rasilimali nyingi na Sin-
gapore imepiga hatua katika masuala
ya kiteknolojia hivyo kwa pamoja nchi
hizi zishirikiane kuendeleza rasilimali
zilizopo.
Naye Katibu Mkuu, Bw. Maswi
aliwakaribisha wawekezaji hao na
kueleza kuwa serikali bado inakaribisha
wawekezaji wa ndani na wa nje ya nchi.
Picha ya Juu; Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Eliakim Maswi (wapili kutoka
kushoto) akiongea na Waziri wa Nchi katika Jamhuri ya Singapore anayeshughulikia
mahusiano ya ndani na nje ya nchi, Bw. Masagos Zulkifli (wapili kutoka kulia picha ya chini)
aliyefika Makao Makuu ya Wizara ya Nishati na Madini jijini Dar es Salaam
4 | MEM News Bulletin
Dodoma
B
aada ya Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kupitisha
makadirio ya Mapato na Matumizi ya
Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka
2014/2015, Waziri wa Nishati na Madini
Profesa Sospeter Muhongo amesema
sasa ni kazi tu, kwa kuwa watanzania
wana matumaini makubwa na Wizara ya
Nishati na Madini.
Waziri Muhongo aliyasema hayo mara
baada ya kukutana na watendaji wa Wizara
na Taasisi zake waliokuwepo mjini Dodoma
kuhudhuria vikao vya Bunge vilivyokuwa
vikijadili makadirio hayo na kuyapitisha.
Waziri Muhongo alitumia fursa hiyo
kuwaasa wafanyakazi wote wa Wizara na
Taasisi zake kuchapa kazi kwa bidii kwa
kuwa Wizara ya Nishati na Madini ni moyo
wa uchumi kwa kuwa inasimamia sekta
muhimu za Nishati na Madini ambazo ni
kichocheo kikubwa cha ukuaji wa uchumi
wa nchi.
Profesa Muhongo pia alishukuru
uhusiano mzuri wa kazi uliopo kati yake
na viongozi wengine wa Wizara pamoja na
wafanyakazi wote. Hata hivyo aliwataka
wafanyakazi wasio wachapakazi
kubadilika na kujituma.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter
Muhongo akinena jambo na Msemaji wa Wizara
Bi. Badra Masoud pamoja na Mkurugenzi Mtendaji
TANESCO Eng. Felchesmi Mramba.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim
Maswi akipongezwa na Wafanyakazi.
Naibu Waziri wa
Nishati na Madini
anayeshughulikia
madini Mhe. Stephen
Masele akishukuru
kwa ushirikiano mzuri
anaopata kutoka kwa
viongozi wa wizara
pamoja na watumishi.
LAZIMA TUFANIKIWE
Na Teresia Mhagama, Dodoma
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akipongezwa na
wafanyakazi wa Wizara/Taasisi mara baada ya kupitishwa kwa Bajeti ya
wizara kwa mwaka 2014/15.
MEM News Bulletin | 5
Dodoma
Waziri Muhongo
ahudhuria kongamano
la Nishati Marekani
Picha za juu zikimwonyesha Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akiwa katika kongamano hilo
W
aziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter
Muhongo ameshiriki kongamano la Umoja wa
Mataifa lijulikanalo kama Nishati Endelevu kwa
Wote lililofanyika nchini Marekani mnamo tarehe 4-6
Juni 2014.
Moja ya mambo yaliyojadiliwa katika kongamano
hilo ni pamoja na upatikanaji wa Nishati ya uhakika na
salama kwa watu wote ifikapo 2030.
Baada ya kongamano hilo Mhe. Waziri pia
atakwenda Washington DC kukutana na ``The US
Enegy Department pamoja na Wafadhili wa Miradi ya
Miradi ya Changamoto za Millenia (MCC) inayoendelea
nchini Tanzania .
Mtalaamu kutoka Kitengo cha Wachimbaji Wadogo,
Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Mhandisi Charles
Mawala akiwasilisha mada wakati wa semina.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia
madini Mhe. Stephen Masele akifungua mafunzo ya
wachimbaji wadogo yaliyofanyika Kibara, mkoani
Mara. Semina hiyo ilishirikisha viongozi wa vijiji, vyama
pamoja na madiwani lengo likiwa ni kuwapa uelewa
wa sheria na kanuni za uchimbaji wa madini. Aliyekaa
katikati ni Mbunge wa Jimbo la Mwibara Mhe. Kangi
Lugora. Kushoto ni Kamishna Msaidizi Uendelezaji wa
Uchimbaji Mdogo Mhandisi Fredy Mahobe.
6 | MEM News Bulletin
Tunalenga
kuboresha utendaji
na kupunguza hali ya
kukosa maelewano
katika utekelezaji
wa sheria ya madini
SHERIA ZA MADINI
Masele
N
aibu Waziri wa
Nishati na Madini
anayeshughulikia ma-
dini, Mhe. Stephen
Masele anatarajiwa
kufungua mkutano baina ya Wiz-
ara, Wakuu wa Mikoa, Wilaya, na
Wakurugenzi wa Halmashauri kwa
ajili ya kujadili na kujenga uelewa
wa pamoja kuhusu utekelezaji wa
sheria ya madini.
Mkutano huo wa siku moja
unafanyika ili kuweka uelewa wa
pamoja kuhusu utekelezaji wa
sheria hiyo kwa lengo la kuboresha
utendaji na kuona namna ya kutatua
matatizo yaliyopo katika sekta hiyo.
Akizungumza kuhusu mku-
tano huo, Kamishna Msaidizi
anayeshughulikia wachimbaji
wadogo Mhandisi John Nayopa,
ameeleza kuwa, serikali inalenga
kuweka mazingira ya pamoja katika
utekelezaji wa sheria ya madini
kutokana na kuwepo malalamiko na
mivutano ya namna ya utekelezaji
kati yake na serikali za mitaa ili
kuwa na sauti moja ambayo
itasaidia kuleta matokeo bora na
manufaa kwa taifa kupitia sekta ya
madini.
Tunalenga kuboresha utendaji
na kupunguza hali ya kukosa maele-
wano katika utekelezaji wa sheria ya
madini. Tunataka kujadili jambo
hilo ili tuwe na uelewa wa pamoja.
Amesisistiza Nayopa.
Akieleza zaidi kuhusu mku-
tano huo, Kamishna Msaidizi wa
Madini, uratibu Mhandisi John
Shija, ameeleza kuwa, mkutano
huo unatarajia kutoa fursa kwa
wizara kuwaelimisha watendaji hao
kuhusu majukumu ya wizara hasa
juu ya namna ya kusimamia sheria
ya madini ikiwa ni pamoja na sekta
ndogo ya wachimbaji wadogo.
Aidha ameongeza kuwa, mku-
tano huo ni muhimu kwa kuwa,
unatarajia kujenga na kuimarisha
mahusiano na maelewano mazuri
baina ya wizara na watendaji hao
atika kusimamia shughuli mbalim-
bali za miradi ya sekta ya madini
jambo ambalo litasaidia kwa kiasi
kikubwa kuunganisha shughuli za
madini na shughuli nyingine za
kiuchumi.
Ameongeza kuwa, mada zitaka-
zowasilishwa katika mkutano huo
zitawasaidia watendaji hao kupata
uelewa zaidi kuhusu sekta ya nishati
na utekelezaji wa sheria ya madini
jambo ambalo litakuwa msaada
mkubwa wa utekelezaji wa sekta ya
madini kutokana na umuhimu wake
kwa maendeleo ya taifa na katika
kuwaendeleza wachimbaji wadogo
na wadau wote wa sekta hiyo.
Wakuu wa Mikoa, Wilaya
kujadili Sheria ya Madini
Na Asteria Muhozya,
Dar es Salaam
Na Issa Mtuwa - Stamico
W
aziri wa Nishati
na Madini, Prof.
Sospeter Muhongo
amemteua Ka-
mishna Msaidizi wa
Madini, Mhandisi Edwin Ngonyani
(pichani) kuwa Kaimu Mkurugenzi
wa Shirika la taifa la Madini (STA-
MICO) kuanzia Juni 2, 2014.
Ngonyani anachukua nafasi ya
Grey Mwakalukwa aliyestaafu kwa
mujibu wa sheria.
Mara baada ya kuanza kazi katika
nafasi hiyo mpya, Ngonyani amehidi
kufanya kazi kwa bidii na ufanisi huku
akiwataka Wafanyakazi wa STA-
MICO kubadilika ili sekta ya madini
iweze kuchangia pato la taifa kwa kiasi
kikubwa.
Hivi sasa tunaingia katika
awamu ya kupeleka fedha hazina na
si kuchukua fedha hazina. Alisisitiza
Ngonyani wakati akizungumza na
Wafanyakazi kwa mara ya kwanza.
Ngonyani ameeleza kuwa, shirika
hilo linatakiwa kuzalisha kwa kiwango
cha kutosha na mapato yake kuwasil-
ishwa Hazina ili kuchangia katika
uchumi wa taifa badala ya kuwa shirika
linalokwenda kupiga hodi hazina
kuomba fedha za kuliendesha. Hivyo,
amewataka kufanya kazi kwa bidii,
kuwa wabunifu na kudumisha umoja.
Aidha, amemshukuru Waziri wa
Nishati na Madini , Profesa Sospeter
Muhongo kwa uteuzi huo katika
shirika hilo ambalo ni muhimu katika
kuchangia uchumi wa taifa na kuhaidi
kutomwangusha.
Akimkaribisha Kaimu Mkurugen-
zi Mtendaji, aliyekuwa Mkurugenzi
wa Shirika hilo Gray Mwakalukwa
ambaye anastaafu, aliwataka watumishi
wa STAMICO kumpa ushirikiano
kiongozi huyo ili kuweza kufkia
malengo ya shirika hilo kuhakikisha
linawavusha watanzania katika hatua
nyingine kiuchumi.
Aidha, Mwakaluka alitumia
fursa hiyo kuwaaga watumishi hao na
kuwashukuru kwa ushirikiano walio
uonesha katika kipindi chote cha
uongozi wake.
Kabla ya uteuzi Ngonyani alikuwa
ni Kamishna Msaidizi Mkaguzi wa
Migodi Wizara ya Nishati na Madini.
Aidha, tangu aprili, 2013 alikuwa
mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa
STAMICO.
Mhandisi Ngonyani ateuliwa Kaimu Mkurugenzi STAMICO
nAmeahidi kuchapa kazi kwa ufanisi nSTAMICO kuchangia pato la taifa
MEM News Bulletin | 7
NISHATI
MUHIMU KUZINGATIA
UJUMBE WA WAZIRI WIKI HII
MARUFUKU MAJADILIANO YA MIKATABA NJE YA NCHI
MIKUTANO, MAJADILIANO YA MIKATABA INAYOHUSU
RASILIMALI ZETU ZA GESI ASILIA NA MAFUTA
NI MARUFUKU KUFANYIKA NJE YA NCHI
Na Veronica Simba
Z
aidi ya Kaya 800 za
Watanzania waishio Viji-
jini zinatarajiwa kuungan-
ishiwa huduma ya umeme
katika kipindi cha mwaka
mmoja, kuanzia Julai, 2014 kupitia
Mradi maalumu wa uunganishaji
umeme wa jua (solar energy).
Mradi huo wa majaribio una-
tokana na jitihada zinazofanywa na
Serikali katika kuhakikisha inawaletea
wananchi wake maendeleo, hususan
walioko vijijini.
Kwa mujibu wa Kamishna
Msaidizi anayeshughulikia masuala
ya Nishati Mbadala, Bw. Edward
Ishengoma, jumla ya makontena 14
ya umeme jua yanatarajiwa kufungwa
katika baadhi ya Vijiji vilivyoko
Kongwa-Dodoma, Igalula-Tabora,
Katavi na Ruvuma.
Kamishna Msaidizi Ishengoma
amesema mradi huo utatekelezwa na
Kampuni ya Elektro-Merl GmbH
kwa gharama ya Euro milioni 5.3
ambazo ni zaidi ya shilingi bilioni 13
za Tanzania, kwa mkopo wa masharti
nafuu kutoka Serikali ya Austria kupi-
tia benki yake ya UNICREDIT.
Akifafanua zaidi, Ishengoma
amesema uwezo wa kila Kontena
moja ni Kv 13.75 na linaweza
kusambaza umeme kwa nyumba/kaya
60. Hata hivyo, amebainisha kwamba
mbali na kuunganisha umeme kwe-
nye makazi ya watu, Mradi unalenga
kuunganisha huduma hiyo kwa waja-
siriamali, mashule na vituo vya afya.
Vituo vya afya, shule na biashara
ndogondogo zinazofanywa na wanan-
chi wajasiriamali ni baadhi ya maeneo
muhimu yanayohitaji huduma ya
umeme; hivyo mbali na kuwapatia
wananchi huduma ya umeme majum-
bani, tutalenga sehemu hizo muhimu
ili kuchangia utekelezaji wa Malengo
ya Maendeleo ya Milenia (Mille-
nium Development Goals-MDGs)
pamoja na mikakati ya maendeleo ya
taifa, hususan Mpango wa Maende-
leo Makubwa Sasa (Big Results
Now-BRN), amesisitiza Kamishna
Ishengoma.
Amesema, Mradi husika
umelenga kuyafkia maeneo ya vijiji,
hususan ambavyo havijafkiwa na
miradi mbalimbali inayotekelezwa na
Wakala wa Nishati Vijijini (REA), na
kwamba dhamira ya Serikali baada ya
Mradi huo wa majaribio ni kusam-
baza makontena mengine 600 katika
vijiji mbalimbali nchini ili kuwafkia
wananchi wengi zaidi.
Akielezea maandalizi ya
Mradi husika, Kamishna Msaidizi
Ishengoma amesema tayari timu ya
wataalamu kutoka Wizara ya Nishati
na Madini imefanya ziara ya mafunzo
katika nchi ambazo zinatekeleza
Miradi ya aina hiyo na kuridhishwa
na ufanisi wake. Timu ya wataalamu
imeridhishwa na ufanisi wa miradi
husika katika nchi walizotembe-
lea. Taarifa yao imetupa nguvu sisi
kuanza utekelezaji wa Mradi huu
hivi karibuni kwani maandalizi yote
yamekamilika, amesisitiza.
Kwa upande wake, mmoja wa
wataalamu wa Wizara walioshiriki zi-
ara hiyo ya mafunzo, Mhandisi Isdory
Fitwangile amesifu ufanisi wa Mradi
husika katika nchi walizotembelea
na kuongeza kwamba ana uhakika
Mradi huo utakuwa wenye mafanikio
makubwa hapa nchini.
Tofauti na vifaa vya umeme-
jua (solar photovoltaic) tulivyozoea
kununua hapa nchini, ambavyo kwa
kawaida hutumika kuunganisha
umeme katika nyumba moja; ma-
kontena yatakayotumika katika mradi
husika yana uwezo mkubwa kwani
kila kontena moja linaweza kutoa hu-
duma ya umeme katika kaya/nyumba
60, amefafanua Mhandisi Fitwangile
na kuongeza kwamba uunganishwaji
wake hutumia distribution line kama
zinazotumiwa kuunganisha umeme
wa TANESCO (Shirika la Umeme
Tanzania.)
Nchi ambazo zimetekeleza
miradi ya aina hiyo mpaka sasa
barani Afrika ni pamoja na Senegal,
Mali, Cameroun na Gambia ambayo
imeelezwa kuonesha mafanikio
makubwa.
WATANZANIA VIJIJINI KUNUFAIKA
NA MIRADI YA UMEME
Moja ya Makontena ya kuunganisha umeme-jua
nZaidi ya Kaya 800 kuunganishwa
8 | MEM News Bulletin
NISHATI/MADINI
Katika ziara hiyo Waziri
Masele alikagua miradi ya
umeme katika vijiji vya
Kibara, Namibu, Kasahunga,
Nyamitwebili, Mahyolo, Ka-
suguti, Bulamba, Haruzare,
Karukekere na Buzimbwe.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wasiliana nasi kwa simu Namba +255 22 2110490 Fax 2110389 Mob: +255 732 999263
au Fika Ofsi ya Mawasiliano Ghorofa ya Tano (MEM) Barua pepe: badra77@yahoo.com
WIZARA YA NISHATI NA MADINI
Serikali yadhamiria
kufkisha umeme
vijiji vyote nchini
Na Greyson Mwase, Bunda
W
achimbaji
wadogo
wametakiwa
kuendesha
shughuli
zao za uchimbaji madini
kwa kuzingatia malengo
waliyojiwekea ili kupiga
hatua kubwa kimaendeleo
na kujikwamua kiuchumi.
Hayo yameelezwa na
mtaalamu kutoka Kitengo
cha Wachimbaji Wadogo,
Shirika la Madini la Taifa
(STAMICO) Mhandisi
Charles Mawala alipokuwa
akiwasilisha mada ya
ujasiriliamali katika semina
ya wachimbaji wadogo,
wakuu wa vijiji, viongozi
wa vyama na madiwani
iiliyofanyika Kibara,
wilayani Bunda mkoani
Mara.
Mhandisi Mawala
alisema kuwa ili mchimbaji
mdogo aweze kupiga
hatua katika shughuli
za uchimbaji madini
anatakiwa kubaini fursa
za mikopo na kuomba
kwa kuzingatia masharti
yaliyowekwa na kutumia
fedha hizo kulingana na
malengo aliyojiwekea.
Akizungumzia jinsi ya
kuweka mipango katika
uchimbaji madini Mhandisi
Mawala alieleza kuwa
wachimbaji wadogo
wanatakiwa kutengeneza
dhamira ya uchimbaji
madini pamoja na kuweka
malengo ya muda mfupi
na mrefu.
Aidha, aliwataka
kuhakikisha mipango
iliyopangwa inaleta
tija katika shughuli
za uchimbaji madini.
Akizungumzia changamoto
katika uombaji wa mikopo
kwenye mabenki, Mhandisi
Mawala alieleza kuwa
biashara nyingi ndogo za
uchimbaji madini zimejikita
katika sehemu ya chini
ya mnyororo wa thamani
na hazina mali nyingi
inayohitajika na mabenki
kama dhamana.
Mhandisi Mawala
alieleza kuwa mabenki
mengi inawawia vigumu
kupata taarifa za
biashara ndogo kuhusu
uwezo wa usimamizi
na fursa za uwekezaji
za wafanyabiashara
na kuongeza kuwa ni
gharama sana kwa
mabenki kukopesha
mikopo midogo
ikilinganishwa na mikopo
mikubwa.
Pamoja na
changamoto hizo Mhandisi
Mawala aliwataka
wachimbaji wadogo
kuunda vikundi vya ushirika
na kuomba mikopo kwa
ajili ya uendeshaji wa
uchimbaji madini huku
akiwahakikishia kuwa
mikopo hiyo inatumika
kulingana na malengo
waliyojiwekea.
Kama mnavyofahamu
ujasiriliamali unahitaji
kujiamini, na kujipanga
kabla ya kuomba mkopo
wowote, ni vyema
mkahakikisha mmejiwekea
malengo ya matumizi
ya mikopo mnayoomba
na kuhakikisha
kuwa matumizi yake
yanaendana na malengo
mliyojiwekea.
Mhandisi Mawala
alieleza njia nyingine
za kukabiliana na
changamoto za
upatikanaji wa mikopo
kwa wachimbaji wadogo
ni pamoja na uhamasishaji
wa mitaji ya ubia
na uhamasishaji wa
ushirikiano katika ununuzi
wa malighafi, uzalishaji
na uuzaji hasa kwa
wachimbaji walio katika
eneo moja wanaozalisha
madini yanayofanana.
Wakati huo huo
wachimbaji wadogo
waliomba mabenki
kulegeza masharti ya
dhamana kwa kutumia
leseni ya uchimbaji madini
au umiliki wa ardhi kama
mojawapo ya vielelezo
vinavyohitajika wakati wa
uombaji wa mikopo.
Na Greyson Mwase,
Bunda;

S
ERIKALI imesema kuwa
dhamira yake kubwa ni
kuhakikisha vijiji vyote
nchini vinapatiwa umeme,
ili wananchi waweze kujiletea
maendeleo kutokana na nishati
hiyo ya umeme.
Hayo yameelezwa na Naibu
Waziri wa Nishati na Madini
anayeshughulikia madini Mhe.
Stephen Masele, wakati akikagua
miradi ya umeme inayotekelezwa
katika jimbo la Mwibara, wilay-
ani Bunda.
Naibu Waziri Masele
alisema dhamira ya serikali ni
kuhakikisha vijiji vyote hapa
nchini vinapata nishati hiyo ya
umeme, hali ambayo itaharakisha
maendeleo ya wananchi katika
maeneo hayo.
Katika ziara hiyo Wa-
ziri Masele alikagua miradi ya
umeme katika vijiji vya Kibara,
Namibu, Kasahunga, Nyamit-
webili, Mahyolo, Kasuguti,
Bulamba, Haruzare, Karukekere
na Buzimbwe.
Aidha, aliangalia jinsi mradi
huo unavyotekelezwa katika
jimbo hilo, ambapo mkanda-
rasi tayari amekwisha peleka
nguzo katika vijiji mbalimbali
na kwamba mradi huo kupitia
Wakala wa Umeme Vijijini
(REA) unatekelezwa katika vijiji
48 vya jimbo hilo.
Alisema kuwa mkandarasi
aliyepewa kusambaza umeme
katika mkoa wa Mara, amepewa
muda wa kumaliza utekelezaji wa
mradi huo, ifkapo Juni mwakani.
Wachimbaji wadogo watakiwa kuendesha shughuli zao kwa malengo
Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia
masuala ya madini Mhe. Stephen Masele akiwa
katika picha ya pamoja na baadhi ya wachimbaji
wadogo mara baada ya ufunguzi wa mafunzo hayo.
MEM News Bulletin | 9
Imeelezwa kuwa kutokuzingatia kanuni za
uchimbaji salama wa madini migodini kunachangia
kwa kiasi kikubwa ajali nyingi nchini
Hayo yameelezwa na mtaalamu kutoka Wizara
ya Nishati na Madini Mhandisi Kungulu Kasongi
alipokuwa akiwasilisha mada kwenye semina
iliyoshirikisha wachimbaji wadogo na viongozi wa
serikali za vijiji, wilaya na viongozi wa vyama vya
siasa iliyofanyika Kibara, wilayani Bunda mkoani
Mara.
Mhandisi Kasongi amesema kutokuzingatia
kanuni za usalama migodini kumepelekea ajali
za mara kwa mara migodini katika kanda ya ziwa
kama vile kuangukiwa na vifusi, kugongwa na
magari ya vifusi na kukosa hewa.
Akielezea athari za ajali migodini kwa wamiliki
wa migodi, Mhandisi Kasongi alizitaja athari hizo
kuwa ni pamoja na kulipa fidia kwa waathirika,
kuharibika kwa mitambo na vifaa, kuharibika kwa
miundombinu ya mgodi, kupoteza uzalishaji na
kupoteza imani kwa umma na kwa watumishi
Mhandisi Kasongi aliendelea kutaja athari za
ajali migodini kwa wafanyakazi kuwa ni pamoja
na kupoteza kipato, kutumia kipato cha akiba
kwa matibabu, kuathirika kiakili na kisaikolojia,
kupoteza uwezo wa kufanya kazi kutokufurahia
maisha.
Akielezea kanuni za afya na usalama migodini
Mhandisi Kasongi alieleza kanuni hizo kuwa ni
pamoja na kuvaa vifaa maalumu vya kujikinga
kama vile kofia ngumu, viatu maalumu, miwani
maalumu, gloves; kuweka mgawanyo mzuri wa
kazi unaozingatia uwezo wa taaluma; kufanya
ukaguzi wa maeneo ya kazi kabla ya kuanza kazi;
kufukia mashimo yasiyohitajika na kuzungushia
wigo mashimo yanayotumika na kutofanya kazi
katika hali ya ulevi na njaa kali au matatizo ya
kiafya.
Mhandisi Kasongi aliendelea kuelezea kanuni
nyingine za usalama migodini ni pamoja na
kutofanya kazi katika sehemu zenye vumbi jingi
na hewa iliyochanganyika na sumu kwa kuvaa
vifaa vya kukinga vumbi na kuvaa vifaa maalumu
vya kuzuia makelele kwa sehemu zenye makelele
mengi.
Aidha, Mhandisi Kasongi aliwataka washiriki
hao kutokulundika vifusi vya udongo karibu na
mashimo pamoja na kudhibiti kiwango cha hewa
chafu au yenye sumu kwa kutumia mashine za
kutoa hewa chafu.
Pamoja na hayo inashauriwa kutoa taarifa
kwa mkaguzi wa migodi juu ya matukio ya hatari
au ajali zinazotokea migodini. Alisisitiza Mhandisi
Kasongi.
Mhandisi Kasongi aliendelea kueleza kuwa
kanuni nyingine za kuzingatia katika shughuli
za uchimbaji salama wa madini ni pamoja na
kutoshirikisha watoto walio chini ya umri wa miaka
18 katika shughuli za uchimbaji madini, vifaa vya
huduma ya kwanza kuwekwa mahali pa kazi na
kutokufanya kazi ngumu kwa muda mrefu sehemu
yenye joto kali.
Mhandisi Kasongi aliendela kuelezea kanuni
nyingine za usalama migodini ni pamoja na
kuepuka kufanya kazi migodini pasipo mwanga
kwa kutumia vibatari badala ya tochi maalumu na
kutumia njia sahihi kuingia katika mgodi.
Si njia sahihi kabisa kuingia au kutoka
mgodini bila kutumia ngazi au kamba maalumu.
Alisisitiza Mhandisi Kasongi.
Akielezea changamoto katika uzingatiaji wa kanuni
za usalama migodini Mhandisi Kasongi alieleza kuwa
ni pamoja na ukosefu wa vifaa madhubuti na salama
vya uchimbaji mdogo wa madini, wafanyakazi migodini
kutokuwa na utashi wa kutumia vifaa vya kinga ya mwili,
teknolojia duni katika uchimbaji mdogo wa madini,
uwezo duni katika kuchunguza matukio na ajali za
migodini na usiri katika kutoa taarifa za ajali migodini.
Akielezea mikakati ya kupunguza ajali migodini
Mhandisi Kasongi alisema ipo haja ya kuendelea
kutoa elimu ya uchimbaji salama migodini kupitia
semina na vipeperushi, kufanya ukaguzi wa mara kwa
mara migodini na wamiliki kuweka mazingira salama
ya utendaji kazi migodini na wafanyakazi migodini
kuzingatia kanuni za uchimbaji salama.
Mhandisi Kasongi aliwataka washiriki kuzingatia
usalama kwanza kabla ya kufanya jambo lolote
mgodini.
Ni imani yangu kuwa iwapo tutazingatia usalama
kwanza badala ya faida kwanza kama njia mojawapo
ya kuweka usalama kwanza badala ya maslahi basi ajali
migodini katika kanda ya Ziwa zitapungua kwa kiwango
kikubwa. Alisisitiza Mhandisi Kasongi.
Na Greyson Mwase, Bunda
Kutokuzingatia
kanuni za uchimbaji
migodini chanzo
cha ajali nyingi
Mhandisi Kungulu Kasongi akionesha moja ya vifaa vya
kujikinga wakati wa uchimbaji wa madini.
10 | MEM News Bulletin
W
ananchi wame-
aswa kuungana
na serikali katika
kukabiliana na
mabadiliko ya
tabianchi kwa kutumia nishati
mbadala kama vile jua, bayogesi,
upepo, makaa ya mawe, na gesi
asilia ikiwa ni pamoja na kutumia
majiko banifu yanayotumia kuni
au mkaa mchache ili kupunguza
utegemezi kwenye nishati itokan-
ayo na maji yaani Hydro power.
Hayo yameelezwa na Waziri
wa Nchi Ofsi ya Makamu wa Rais,
Mazingira, Mheshimiwa Dkt
Binilith Mahenge aliyekuwa Mgeni
rasmi wakati wa ufunguzi wa ma-
onesho ya Mazingira yaliyofungu-
liwa rasmi Juni mosi katika viwanja
vya Furahisha jijini Mwanza na
kufkia kikomo Juni 5, 2014.
Kaulimbiu ya maadhimisho ya
siku ya mazingira kimataifa kwa
mwaka huu ni Chukua hatua
kukabiliana na mabadiliko ya tabi-
anchi Ambapo kaulimbiu ya siku
hiyo kitaifa ni Tunza mazingira
ili kukabiliana na mabadiliko ya
Tabianchi.
Kaulimbiu hiyo ilibeba maud-
hui yenye lengo la kuelimisha na
kuhamasisha wananchi wote vijijini
na mijini kuendesha shughuli zao
za kiuchumi kwa kuzingatia tarati-
bu ambazo hazichangii kuongezeka
kwa gesi joto na hazina athari kwa
mazingira.
Akihojiana na Mwandishi wa
Habari hizi Bi Winnifrida Mrema,
Afsa Mazingira mwandamizi
alisema mwitikio wa wanan-
chi ulikuwa mzuri na wananchi
wameweza kuelewa madhara na
faida wanazoweza kuzipata endapo
watafuata taratibu elekezi za uhifa-
dhi wa mazingira.
Akieleza kuhusu madhara ya
mabadiliko ya tabia nchi mabadi-
liko ya tabianchi ameyataja kuwa ni
pamoja na kukosekana kwa mvua
na kuongezeka kwa hali ya ukame
yenye athari za moja kwa moja na
shughuli za uzalishaji wa umeme
unaotokana na uwepo wa maji
(Hydro Power).
Maonesho hayo ya Mazin-
gira yanayofanyika kila mwaka
mwezi Juni yamefkia mafanikio
makubwa kutokana na wananchi
wengi kupata nafasi ya kutembelea
mabanda ya maonesho na kujifunza
umuhimu wa kuhifadhi mazingira
ili waweze kuepukana na mad-
hara yatokanayo na uharibifu wa
mazingira.
Tunza mazingira ukabiliane
na mabadiliko ya tabianchi
Mtaalamu kotoka kitengo cha Mazingira, Emmanuel
shija akimkaribisha mgeni aliyetembelea banda la
Wizara katika maadhimisho ya siku ya mazingira jijini
Mwanza
Baadhi ya wananchi wakiwa katika viwanja vya
Furahisha katika maadhimisho ya siku ya mazingira
jijini Mwanza
Mtaalamu kutoka kitengo cha Mazingira, Winnifrida
Mrema akitoa elimu kwa wananchi waliotembelea
banda la Wizara katika maadhimisho ya siku ya
mazingira jijini Mwanza

You might also like