Professional Documents
Culture Documents
WIZARA YA UCHUKUZI
S.L.P. 3056
DAR ES SALAAM
31 Desemba, 2013
Katika kipindi cha msimu wa mvua za Vuli Oktoba hadi Desemba 2013, maeneo mengi ya
nchi yamepata mvua chini ya wastani isipokuwa katika maeneo ya magharibi na yale ya
ukanda wa Ziwa Victoria ambayo yalipata mvua za wastani na maeneo machache ya Mikoa
ya Mara na Shinyanga yalipata mvua za juu ya wastani.
Vifuatavyo ni viwango vya mvua pamoja na wastani wa muda mrefu katika baadhi ya vituo
hivyo:
Maeneo yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka:
Ukanda wa Ziwa Victoria:
Oktoba: Bukoba (64.7%), Mwanza (19.7%), Musoma (9.7%), Ukiriguru (36.9%) na
Shinyanga (38.1%); Novemba: Bukoba (76.0%), Mwanza (90.0%), Musoma (63.0%),
Ukiriguru (87.0%) na Shinyanga (60.0%); Disemba: Bukoba (1.7%), Mwanza (1.3%),
Musoma (199.1%), Ukiriguru (125.2%) na Shinyanga (229.4%).
Pwani ya Kaskazini pamoja naVisiwa vya Unguja na Pemba:
Oktoba: Zanzibar (53.4%), Amani (125.7%), Tanga (104.7%), Pemba (57.4%) na JNIA
(51.1%); Novemba: Zanzibar (64.0%), Amani (107.0%), Tanga (112.0%), Pemba (61.0%)
na JNIA (55.0%); Disemba: Zanzibar (43.7%), Amani (96.2%), Tanga (89.1%), Pemba
(97.4%) na JNIA (64.2%).
1
Mikoa ya Magharibi:
Novemba: Tabora (44.0%), Kibondo (92.0%) na Kigoma (98.0%); Desemba: Tabora
(126.8%), Kibondo (34.97%) na Kigoma (137.3%).
Pwani ya Kusini:
Novemba: Kilwa (30.0%)
(83.2%).
Mikoa ya Kati:
Novemba: Singida (0.0%), Dodoma (0.0%) na Hombolo (0.0%); Disemba: Singida
(197.7%), Dodoma (60.3%) na Hombolo (28.4%).
Ruvuma:
Novemba: Songea (m%); Desemba: Songea (49.5%).
Kielelezo: Viwango vya mvua chini ya asilimia 75 ya wastani kwa kipindi kirefu hutafsiriwa
kama chini ya wastani, wakati viwango vya kati ya asilimia 75 hadi 125 hutafsiriwa kama
mvua za wastani na vile vya zaidi ya asilimia 125 hutafsiriwa kama juu ya wastani.
2.0 MWELEKEO WA MVUA ZA MSIMU WA JANUARI HADI MACHI 2014.
2.1: Utangulizi
Wataalam wa Mamlaka ya Hali ya Hewa walishirikiana na wataalam wengine katika
mkutano wa kutoa uchambuzi wa mwelekeo wa Mvua za Msimu wa Januari-Machi, 2014
katika nchi za kusini mwa Afrika (SADC) mnamo mwezi Agosti, 2013. Mwezi wa
Disemba, 2013 wataalam na wachambuzi wa masuala ya hali ya hewa na klimatolojia katika
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) walifanya uchambuzi wa mrejeo wa msimu .
Katika mkutano huo, tathimini ya kina katika mifumo ya hali ya hewa na athari zake kwa
msimu ujao wa mvua. Viashiria vikuu vilivyotumika ni pamoja na Hali ya joto la Bahari
katika maeneo ya Bahari ya Hindi, tropikali ya Bahari ya Pasifiki na Bahari ya Atlantiki.
2
Mvua za Vuli zinazoendelea katika maeneo yanayopata mvua mara mbili kwa mwaka
(Mikoa ya Dar es salaam, Tanga, Pwani, Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Mwanza, Mara,
Geita, Shinyanga, Kagera na Simiyu) zinatarajiwa kuisha mwishoni mwa mwezi Disemba,
2013. Hata hivyo maeneo haya yanatarajiwa kupata mwendelezo wa mvua za nje ya msimu
(out of season rains) katika miezi ya Januari na Februari, 2014 katika maeneo ya kaskazini
hususan mwa mkoa wa Morogoro, kusini mwa mikoa ya Pwani na Manyara. Maeneo
mengine yanatarajiwa kuwa makavu kwa ujumla.
Utabiri wa mvua za masika katika maeneo haya utatolewa mwishoni mwa mwezi
Februari, 2014.
(ii)
Mvua za Msimu katika Maeneo yanayopata msimu mmoja wa mvua
Kipindi cha mvua za Msimu (Novemba hadi Aprili) zinaendelea na ni mahsusi kwa maeneo
yanayopata mvua mara moja kwa mwaka (Kanda ya Magharibi, Kanda ya kati, Nyanda za
juu kusini magharibi, mikoa ya kusini na pwani ya kusini). Mvua zinazoendelea kunyesha
kwa kipindi cha Januari hadi Machi, 2014 zinatarajiwa kuwa kama ifuatavyo:Kanda ya Magharibi (Mikoa ya Tabora, Rukwa, Katavi na kusini mwa Kigoma):
Mvua zinatarajiwa kuwa za wastani hadi chini ya wastani
3
Uwezekano wa kupata
mvua zilizo nje ya
msimu kwa mwezi
Januari na Februari
2014
Taarifa katika jedwali linaonyesha uwezekano (probability) kwa mfano maeneo ya kusini
uwezekano wa kupata mvua za juu ya wastani ni asilimia arobaini 40%, mvua za wastani
35% na mvua za chini ya wastani 25%.